O-man
JF-Expert Member
- Nov 17, 2011
- 323
- 65
Katika hali ya kusikitisha na kukatisha tamaa, maisha, ambayo nayaita ya kawaida, katika jiji letu, yameota mbawa. Hata bamia limekuwa ni anasa - kilo moja ni shilingi 3,000. Najiuliza maswali lakini nachelea kutoa majibu. Hivi wapo viongozi ambao wanaguswa na hali hii? Huyu mtu ambaye katika kukuru kakara zake amefanikiwa kupata unga kwa ajili ya ugali, mboga ya rahisi na ambayo wengi wetu imetutoa mbali imekuwa tunu? Nyama, maharage na samaki ni mboga za siku za mshiko tu. Mtu huyu ana akili timamu na siku akisema hii inatosha, sikubali, lazima hali ibadilike, lolote na liwe. . . Atalaumiwa kweli? Najuwa fika likitokea hili vipo vyama vitabebeshwa mzigo wa lawama. Ukweli utabakia pale pale - viongozi wetu, kwa sababu wameshiba, wamesahau waliowaweka madarakani. Kama kipo kidogo basi tugawane ili atakayelalamika tumuone mlafi. Inauma sana.