Hali ya Hospitali ya Taifa Muhimbili

think BIG

JF-Expert Member
Mar 24, 2008
236
40
attachment.php


Baadhi ya wagonjwa wakiwa wamelala chini katika hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), wodi namba 17 Sewa Haji kunakosababishwa na upungufu wa vitanda katika hospitali hiyo. (Picha na Peter Twite, Majira)

vitanda hakuna!
madawa je?
wauguzi je?
 

Attachments

  • mnh.JPG
    mnh.JPG
    45.3 KB · Views: 267
Think big
Hiyo ndiyo tanzania baba,

IsayaMwita,

inawezekana kweli hiyo ndiyo Tanzania, lakini Je ni kweli hiyo ndio Tanzania yenye mTanzania anayeitwa Andrew Chenge? .. anayeitwa Yusuf Manji? .. Rostam Aziz? .. mtanashati JK? Kweli? au ndio Tanzania ya wale walalahoi tu!

Ukae ukijua Muhimbili ndio hospital yetu ya Taifa, yaani kiufanisi ndio kubwa kuliko zote! Sasa tujiulize za uko mikoani je? wilayani? ..
 
Mafisadi wao wanatibiwa nchi za nje UK, US, SA, Kenya na India hivyo hawaoni umuhimu wowote wa kuipatia Muhimbili na hospitali zetu nyingine vitanda vya kutosha na vitendea kazi muhimu.
 
Mafisadi wangekuwa na huruma jamani maana yote yanasababishwa na wao

Ndugu Asha,

Siwezi kukuita Bibie kwa kuwa sina uhakika. Naomba nipingane na kauli yako ya kwamba hali mbaya katika Hospitali ya Muhimbili na Hospitali nyengine hapa Tanzania imesababishwa na Mafisadi. Hilo nadhani mimi ntalipinga.

Ni kweli ya kwamba hawa Mafisadi wamekwamisha kwa kiasi fulani maendeleo ya Taifa hususani katika kuboresha huduma za jamii na kufanya maisha yakawa rahisi kwa Mtanzania wa kawaida. Lakini tunaporudi katika Sekta ya Afya nadhani hapa Lawama haziwezi pelekwa kwa ile "List of Shame" na Mafisadi wengine ambao hawapo katika i le list, bali ni katika mipango mibovu ya Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya Mh. Jakaya Mrisho Kikwete kuboreasha huduma zote.

Ari Mpya, Kasi Mpya, Nguvu Mpya... Maisha bora kwa kila Mtanzania. Ni kwamba akiwa kama mwanasiasa, JK amehadaa na ameshindwa yatimiza yale ambayo amewaahidi Wapiga kura wake kuboresha maisha yao. Hapa hakuzuiwa na Mafisadi bali ni mipango yake mibovu katika kutekeleza Ilani iliyomuingiza madarakani mwaka 2005.

Mfumo mbovu wa Afya na Administration ya Kikwete kushindwa kusimamia hilo nadhani ni moja ya mambo ambayo yamesababisha hali kuwa mbaya sana katika Hospitali zetu na sehemu nyengine zinazotoa Huduma kwa Jamii.

Imekuwa kama Watanzania tumepata sehemu ya kulalamikia kwa hiyo inakuwa kila kitu ni Mafisadi, given a chance mimi ningeshauri tuwaponde mawe mpaka wafe lakini katika mambo mengine hatutakiwi kutafuta nani wa kumlaumu ila kujua nini sababu ya kushindwa kwetu na ufumbuzi unaweza kupatikana vipi!!! Kuna siku mvua haitanyesha kwa kipindi kirefu ama jua kuwa kali mno tutawalalamikia mafisadi!!!
 
IsayaMwita,

inawezekana kweli hiyo ndiyo Tanzania, lakini Je ni kweli hiyo ndio Tanzania yenye mTanzania anayeitwa Andrew Chenge? .. anayeitwa Yusuf Manji? .. Rostam Aziz? .. mtanashati JK? Kweli? au ndio Tanzania ya wale walalahoi tu!

Ukae ukijua Muhimbili ndio hospital yetu ya Taifa, yaani kiufanisi ndio kubwa kuliko zote! Sasa tujiulize za uko mikoani je? wilayani? ..

Hilo usitake jua kaka...

Lakini je hali mbaya katika hizi Hospitali ni matunda ya hawa Mafisadi ama? Mimi hilo ndio linaniumiza kichwa... Walioshindwa tunawaacha na tunakaa kuwalalamikia Watuhumiwa wa Ufisadi.

Ndio bado ni Watuhumiwa ambao mpaka sasa wapo juu ya Sheria. Kabla ya kufikiria Mafisadi ni kuweka wazi kwamba hii hali inatokana na kushindwa kwa Kikwete's Administration!!!!

Sitegemei kupata kisingizio kwamba ati aliikuta hali kama hivo toka awamu ya tatu. Wao wameshindwa sasa ni kwamba wanatakiwa wawajibike kama Watawala kisha issue ya Mafisadi itafata baaaaaddaaaaae!!!
 
Mafisadi wao wanatibiwa nchi za nje UK, US, SA, Kenya na India hivyo hawaoni umuhimu wowote wa kuipatia Muhimbili na hospitali zetu nyingine vitanda vya kutosha na vitendea kazi muhimu.

Hivi Mafisadi ndio walitakiwa kutoa yote haya katika Hospitali zetu kama ambavyo Bubu ameainisha...

Naomba Ufafanuzi.
 
Kulikuwa kuwe na mkutano wa waandishi wa habari kuhusu malalamiko ya madaktari pale leo hii.. sijui kuna mtu anajua kilichojiri?
 
Kulikuwa kuwe na mkutano wa waandishi wa habari kuhusu malalamiko ya madaktari pale leo hii.. sijui kuna mtu anajua kilichojiri?

Naomba mtupatie taarifa husiana na hili kwa wale ambao wanaweza kuwa wamesikia lolote. Natumaini ntakesha na hii Thread kwa usiku wa leo maana natumaini ntapata mwanga na kufanikiwa kupanua uwanja wangu wa mawazo.

Kwa sasa naenda pambana na na usafiri wa Bongo kurudi sehemu yangu ya Kujificha kwa Usiku na nikifika huko tutaungana tena tuendelee na Huu Mjadala.

Heshima Mbele.
 
wennyewe wanapenda kupanga haya magari na sasa wameamua kunu v8 ili wakabiliane na mfgumuko wa bei..yaani ukiangalia vipaumbele za watu walioko serikalini bwana..yote hii inachangiwa n RUSHWA na wazee wa ovyo watumishi wa serikali.Yes wengi wao Wachaga..Ni bora nionekana hivyo ila habari ndiyo.

toyl20002.jpg


Hawana pesa za kununulia vitanda sababu ten per cent zao ni ndogo
 
Umasikini wa akili, roho mbaya na kujizoelesha vinaondoa hata empathy.

Umasikini wa akili unatupa justification kwamba tuko hivi kutokana na umasikini wetu wa mali.

Roho mbaya ina downplay mateso ya wenzetu, tunasema "utasadia utasaidia wangapi?" halafu tunaongezea hilo hapo juu "nchi yenyewe masikini".

Watu wanawaangalia wagonjwa hao miaka nenda rudi, wanakubali kukubali hali hiyo kutokana na mazoea tu.

Wengi hatuchukui challenge, hata sisi hapa.Nakumbuka Mwanakijiji -bless his soul- alionyesha mfano kufanya mchango au something like that kwa watoto yatima if I am not mistaken. Lakini Mwanakijiji ni mmoja tu, tunahitaji wengi zaidi.

Not to blame the victim, to make matters worse, hata wanaoumia nao wako katika apathy na ndio kwanza majority wanawapigia kura CCM against their own interests kama katika "What's the Matter with Kansas", upinzani nao unashindwa ku capitalize on this na ku translate into election victories.Kuna mtu alishatangaza msaada wa scholarship (personal funds) watu wamelala!
 
Kulikuwa kuwe na mkutano wa waandishi wa habari kuhusu malalamiko ya madaktari pale leo hii.. sijui kuna mtu anajua kilichojiri?

Ukisikia madaktari wa Tanzania wanalalamika ujue hawalalamikii huduma duni bali mapato yao tu. Madaktari wetu nao ni some kind of disappointment.
 
Mimi siamini hizi picha...siyo Muhimbili hapo. Tanzania hakuna wagonjwa wanaolala chini bana.....watu watalalaje chini wakati tuna mafundi seremala kibao ambao wanaweza kutengeneza vitanda....ukisema mbao nitakwambia miti tunayo kibao.....ukisema magodoro nitakwambia mbona kiwanda cha kutengeneza magodoro tunacho....sasa iweje watu (wagonjwa au la) walale chini? Hapana....hizi picha ni propaganda za nchi za Magharibi........
 
Ndugu Asha,

Naomba nipingane na kauli yako ya kwamba hali mbaya katika Hospitali ya Muhimbili na Hospitali nyengine hapa Tanzania imesababishwa na Mafisadi. Hilo nadhani mimi ntalipinga.

Ni kweli ya kwamba hawa Mafisadi wamekwamisha kwa kiasi fulani maendeleo ya Taifa hususani katika kuboresha huduma za jamii na kufanya maisha yakawa rahisi kwa Mtanzania wa kawaida. Lakini tunaporudi katika Sekta ya Afya nadhani hapa Lawama haziwezi pelekwa kwa ile "List of Shame" na Mafisadi wengine ambao hawapo katika i le list, bali ni katika mipango mibovu ya Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya Mh. Jakaya Mrisho Kikwete kuboreasha huduma zote.

Ari Mpya, Kasi Mpya, Nguvu Mpya... Maisha bora kwa kila Mtanzania. Ni kwamba akiwa kama mwanasiasa, JK amehadaa na ameshindwa yatimiza yale ambayo amewaahidi Wapiga kura wake kuboresha maisha yao. Hapa hakuzuiwa na Mafisadi bali ni mipango yake mibovu katika kutekeleza Ilani iliyomuingiza madarakani mwaka 2005.

Mfumo mbovu wa Afya na Administration ya Kikwete kushindwa kusimamia hilo nadhani ni moja ya mambo ambayo yamesababisha hali kuwa mbaya sana katika Hospitali zetu na sehemu nyengine zinazotoa Huduma kwa Jamii.

Imekuwa kama Watanzania tumepata sehemu ya kulalamikia kwa hiyo inakuwa kila kitu ni Mafisadi, given a chance mimi ningeshauri tuwaponde mawe mpaka wafe lakini katika mambo mengine hatutakiwi kutafuta nani wa kumlaumu ila kujua nini sababu ya kushindwa kwetu na ufumbuzi unaweza kupatikana vipi!!! Kuna siku mvua haitanyesha kwa kipindi kirefu ama jua kuwa kali mno tutawalalamikia mafisadi!!!

Unasema maendeleo katika nyanja ya afya hayazuiwi na ufisadi. Ni mifumo na mipango na ufuatiliaji mbaya wa Kikwete administration.

Nakataa.

Definition yako ya fisadi inajumuisha wizi wa kina Chenge tu, wakati kuna ufisadi mwingine mbaya kama, au kupita, wa Chenge.

Rais, Mawaziri na tabaka tawala zima linapoenda India kutibiwa na hela yetu wakati sisi tunakufa kwa kuumwa na mbu hospitali, huo ni ufisadi. Hujali.

Utajali vipi kufuatilia mipango ya maendeleo ya afya kama wewe hilo kwako sio tatizo: ukiugua unatibiwa India.

Kama mtu anaamini kwamba kuna madaraja mawili ya binadamu, yule anaestahili huduma bora ya afya, Waziri na Rais, na yule asiyestahili, Kalagabaho mlima kunde wa Gezaulole na Kuhani mpita njia, huyo mtu ni evil. Na hawa watu hiki kitu cha madaraja mawili ya binadamu, hii hulka evil, wanaiamini kwa vitendo: wakiugua wanaenda kutibiwa India kwa hela zetu!

Fisadi maana yake pia ni kiongozi evil.

Yusuph Makamba amepotosha watoto wa shule juzi aliposema maana ya fisadi kwenye kamusi ni mzinzi peke yake.

Huwezi kuwasafisha mafisadi wanaotibiwa nje huku sisi twafa kwa kutokujali kwao kwa kusema eti ni tatizo la mipango ya afya. Hawajali. Ni evil.

Kiongozi evil ni fisadi.
 
Unasema maendeleo katika nyanja ya afya hayazuiwi na ufisadi. Ni mifumo na mipango na ufuatiliaji mbaya wa Kikwete administration.

Nakataa.

Definition yako ya fisadi inajumuisha wizi wa kina Chenge tu, wakati kuna ufisadi mwingine mbaya kama, au kupita, wa Chenge.

Rais, Mawaziri na tabaka tawala zima linapoenda India kutibiwa na hela yetu wakati sisi tunukufa kwa kuumbwa na mbu hospitali, huo ni ufisadi. Hujali.

Utajali vipi kufuatilia mipango ya maendeleo ya afya kama wewe hilo kwako sio tatizo: ukiugua unatibiwa India.

Kama mtu anaamini kwamba kuna madaraja mawili ya binadamu, yule anaestahili huduma bora ya afya, Waziri na Rais, na yule asiyestahili, Kalagabaho mlima kunde wa Gezaulole na Kuhani mpita njia, huyo mtu ni evil. Na hawa watu hiki kitu cha madaraja mawili ya binadamu, hii hulka evil, wanaiamini kwa vitendo: wakiugua wanaenda kutibiwa India kwa hela zetu!

Fisadi maana yake pia ni kiongozi evil.

Yusuph Makamba amepotosha watoto wa shule juzi aliposema maana ya fisadi kwenye kamusi ni mzinzi peke yake.

Huwezi kuwasafisha mafisadi wanaotibiwa nje huku sisi twafa kwa kutokujali kwao kwa kusema eti ni tatizo la mipango ya afya. Hawajali. Ni evil.

Kiongozi evil ni fisadi.

Sijasema ya kwamba maendeleo katika huduma ya afya na huduma nyenginezo hayazuiwi na ufisadi... kitu ambacho hapa nimekisema ni kwamba hii hali yooote imesababishwa na Uongozi Butu wa Serikali ya Awamu ya Nne ya Muungwana.

Na husiana na mafisadi, sijajaribu ongelea chukua chukua kama za EPA....na Ufisadi wa akina Chenge. uko sawa husiana na viongozi wetu watukufu ku imbilia nje kutibiwa na kuacha sisi tulio na bahati mbaya ya kuwachagua tukihenyeka na huduma mbovu za kiafya... hata Lyatonga Mrema ali ngea hili alipokuwa amelazwa pale KCMC.

jaribu kuangalia kiini na chimbuko la mafisadi ni wapi...ni kitu gani ambacho kinawapa jeuri hao mafisadi? na je serikali imeundwa na watu gani? ukiangalia yote nadhani utafahamu kwa nini sijataka kuwalenga Mafisadi bali serikali ambayo imewageuza hawa Mafisadi mifugo yake...na kuwalinda....

authorization ya safari zote hizo za india na kwengineko kwa ajili ya matibabu zinatoka wapi? na wanapochota pesa kwa ajili ya hilo serikali ikawa inafumba macho ni yupi wa kubeba lawama.?

kumaliza kabisa ufisadi tunatakiwa shughulika na matawi, shina au mizizi ya ufisadi?
 
Hivi Mafisadi ndio walitakiwa kutoa yote haya katika Hospitali zetu kama ambavyo Bubu ameainisha...

Naomba Ufafanuzi.

Wanatuibia mabilioni kwenye rasilimali zetu na makusanyo ya kodi. Kwa mwaka mmoja tu 2005/2006 pale BOT wamekwapua billioni 288 na hapa hatujaweka wizi wa rasilimali zetu dhahabu, Almasi, Tanzanet n.k. kutokana na mikataba isiyo na maslahi kwa Watanzania . Fikiria kama mapesa yote hayo yangeelekezwa katika kuboresha mahospitali yetu basi hata mafisadi wasingezikimbia hospitali zetu
 
Back
Top Bottom