Sir R
JF-Expert Member
- Oct 23, 2009
- 2,175
- 298
CCM inapata wakati mgumu sana katika jimbo la Mbulu,
Wananchi kutoka vijiji mbalimbali hawataki kumwona Mgombea wa CCM Marmo, anazomewa sana sehemu mbalimbali mfano maeneo ya Haydom siku anazindua kampeni, Masyeda wiki hii, Pia alipigiwa miluzi katika eneo la Maghangw, watu katika eneo hilo watu wanadai ahadi ya umeme, siku ya pili yake kawapelekea nguzo za umeme.
Kwa kweli hali kwa upande wa CHADEMA ni nzuri sana, wairaqw wamekasirishwa sana na kitendo cha CCM kutoa ahadi mara kwa mara bila kutekeleza. Pia kitendo cha Marmo kumrubuni Bwana Lori aliyegombea wakati wa kura za maoni, wengi walimtaraji Lori kushinda katika kura za maoni cha ajabu Marmo kawa mshindi kitendo hicho kiliwaudhi watu wengi kiasi cha kukigeukia CHADEMA;
Wana CCM wengi ni kama yatima kwani ni aibu kuvaa Tshirt, kofia ya CCM, wavaao wanakejeliwa sana, hakuna anayetetea CCM. Washabiki wa chache wa CCM hawathubutu kusifia CCM hadharani kwani kejeli nyingi sana.
Wazee wa mila wanamwombea Dr Slaa kwa ibada ya kimila,
Watu wanahamasishana ndani ya mabasi kila wakati. Marmo anahangaika kujenga barabara sehemu mbalimbali.
JK sitegemei kama atapata zaidi ya asilimia moja katika jimbo la Mbulu maana hata washabiki wachache wa CCM wameapa kura ya urais ni kwa Dr Slaa ila ya ubunge watampa Marmo, miongoni wa hao wachache ni walimu wakuu wachache.
Wananchi kutoka vijiji mbalimbali hawataki kumwona Mgombea wa CCM Marmo, anazomewa sana sehemu mbalimbali mfano maeneo ya Haydom siku anazindua kampeni, Masyeda wiki hii, Pia alipigiwa miluzi katika eneo la Maghangw, watu katika eneo hilo watu wanadai ahadi ya umeme, siku ya pili yake kawapelekea nguzo za umeme.
Kwa kweli hali kwa upande wa CHADEMA ni nzuri sana, wairaqw wamekasirishwa sana na kitendo cha CCM kutoa ahadi mara kwa mara bila kutekeleza. Pia kitendo cha Marmo kumrubuni Bwana Lori aliyegombea wakati wa kura za maoni, wengi walimtaraji Lori kushinda katika kura za maoni cha ajabu Marmo kawa mshindi kitendo hicho kiliwaudhi watu wengi kiasi cha kukigeukia CHADEMA;
Wana CCM wengi ni kama yatima kwani ni aibu kuvaa Tshirt, kofia ya CCM, wavaao wanakejeliwa sana, hakuna anayetetea CCM. Washabiki wa chache wa CCM hawathubutu kusifia CCM hadharani kwani kejeli nyingi sana.
Wazee wa mila wanamwombea Dr Slaa kwa ibada ya kimila,
Watu wanahamasishana ndani ya mabasi kila wakati. Marmo anahangaika kujenga barabara sehemu mbalimbali.
JK sitegemei kama atapata zaidi ya asilimia moja katika jimbo la Mbulu maana hata washabiki wachache wa CCM wameapa kura ya urais ni kwa Dr Slaa ila ya ubunge watampa Marmo, miongoni wa hao wachache ni walimu wakuu wachache.