Hali tete serikalini, mafungu ya matumizi chini 40% ulinzi na polisi juu

Profesa

JF-Expert Member
Oct 28, 2010
905
624
Wakulu jana nilichelewa kuwaletea habari hii kwakuwa nilibanwa na shughuli nyingi na vikao kemkem. Kuna taarifa nilizozipata kutoka chanzo cha kuaminika kuwa sasa pesa zilizopitishwa serikalini kwa Ministries, Departmentas and Agencies zinazotegemea serikali kuu kiwango kimeshuka kwa zaidi ya asilimia 40. Wizara zenye fungu lililooongezeka nji Wizara Ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga taifa na Wizara ya mambo ya Ndani. Hii maana yake nini? Ukizingatia hivi majuzi Serikali imedai kuvuka lengo la makusan yo. Mwenye kulijua hili kiundani atujuze mana ninahofu na mwelekeo wa Taifa hili kama hali ndiyo hii.
 
Profesa,
Usalama wa raia ni muhimu sana kwa taifa lolote! so ondoa shaka kabisa ni uhakika wa ulinzi kaka!
Sema kwenye report ya CAG imeonyesha miongoni wa sehemu kuna ubadhirifu wa kutisha ni huko kwenye majeshi hao ndio naona utata! labda huenda ni technique ya kukwapua maana kule kwenye ulinzi na usalama maswali sio mwengi, tunaambiwa ni kwa kwa "usalama wa taifa"
 
Kwani hujui tumeshakuwa Ugiriki na hatukopesheki tushavuka kiwango cha kukopesheka. Makusanyo ya TRA yanaenda kununua vuatafunwa vya ikulu
 
Namuona pia EMT aliipata hii habari kutoka Bungeni kupitia gazeti moja: https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...rikali-inakabiliwa-na-hali-mbaya-kifedha.html

Ila mimi nilikuwa na mkuu wa idara moja na akanionyesha nyaraka zinazowataka ku-cut down expenditures na hata budget, tofauti na miaka ya nyuma kipindi hiki fedha zinakuwa zimeebaki basi vi-workshop vya kumwaga. Ila sasa, tunajivunia nini kuvuka malengo ya ukusanyaji kodi kama hali yetu ni hii? Je kuna tatizo la uwiano wa kodi na mahitaji halisi? au ni kuweka malengo feki yasiyokidhio haja za serikali? Au kuna mahali wanahifadhi hizo fedha kwa ajili ya nini kijacho? Uchaguzi? Sensa? Au ni mwanya unaovuja na srikali haijaujua au inaujua na wameutengeneza wenyewe?
 
tra ni wanasiasa, thamani ya Tsh imeporomoka, inflation juu.. na kodi nazo zinafuata inflation that's why unaona mapato yameongezeka lkn serikali inalia njaa
 
Wakulu jana nilichelewa kuwaletea habari hii kwakuwa nilibanwa na shughuli nyingi na vikao kemkem. Kuna taarifa nilizozipata kutoka chanzo cha kuaminika kuwa sasa pesa zilizopitishwa serikalini kwa Ministries, Departmentas and Agencies zinazotegemea serikali kuu kiwango kimeshuka kwa zaidi ya asilimia 40. Wizara zenye fungu lililooongezeka nji Wizara Ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga taifa na Wizara ya mambo ya Ndani. Hii maana yake nini? Ukizingatia hivi majuzi Serikali imedai kuvuka lengo la makusan yo. Mwenye kulijua hili kiundani atujuze mana ninahofu na mwelekeo wa Taifa hili kama hali ndiyo hii.
Wewe ni kama nani sasa mpaka utuombe radhi kwa kuchelewesha tarifa hii? ni msemaji wa Serikali au?
 
Taifa lisilo control nakisi ni mfu kiuchumi. Waulizeni Argentina

kama polisi wamezidishiwa maana nyingine maslahi yao ni mazuri mbona hawaridhiki wanaendekeza rushwa yaani hata jero hawaaachi? halafu kwaani budget si ilishapitishwa sasa haya mabadiliko ya ugawaji mafungu yanafanywa na nani aliye juu ya bunge lililopisha budget??
 
Wewe ni kama nani sasa mpaka utuombe radhi kwa kuchelewesha tarifa hii? ni msemaji wa Serikali au?
Kengemumaji inategemea kama Kiswahili unakifahamu au ndio unajifunza, jana ni Ijumaa ndio siku ya kazi unapoweza kuwa na timely news na leo ni jumamosi sio siku ya kazi kiserikali, na source yangu ni ndani ya serikali. Unajaza thread na unaipotezea JF sifa, kama huna ishu piga kimya waache wenye uchungu na nchi hii na hoja watete
 
mkuu unasema ulichelewa kuleta habari jana....mwishoni unatuuliza mwenye taarifa.!
Kama nilivyosema Chanzo changu ni ndani ya Srikali, ukitoa taarifa ni vema ziwe kwa wakati na chanzo, chanzo changu ni ndani ya serikali na jana ni siku ya kazi leo sio siku ya kazi kiserikali ndiyo maana ya kuchelewa... Mwenye taarifa ni yule mwenye evidence in writing ya taarifa hii, Post yangu ina prefix ya "Tetesi" inasubiri kuthibitishwa, kama huna ukweli wa jambo hili unachohoji ni kupoteza maana, jamani ukiachia Nipashe ambapo nimeona post ya EMT akimnukuu waziri mkuu Bungeni (mimi sikuona kipindi hicho) basi atujuze, au hata kuongezea hoja kwa wale wanaofanya kazi serikalini nafasi za juu wenye uchungu na nchi hii. Hoja yangu ni kuwa Mkapa alipoimarisha Kodi kipindi chake cha pili cha uraisi tuliona matunda, jamaa data za kodi ziko juu lakini matokeo duni inakuwaje....
 
kama polisi wamezidishiwa maana nyingine maslahi yao ni mazuri mbona hawaridhiki wanaendekeza rushwa yaani hata jero hawaaachi? halafu kwaani budget si ilishapitishwa sasa haya mabadiliko ya ugawaji mafungu yanafanywa na nani aliye juu ya bunge lililopisha budget??

Mukulu, kupitisha budget (yenye bubles au hewa nyingi zaidi ya solid matters) ni tofauti na uwepo wa pesa na matumizi ni jambo lingine hasa kwa nchi kama Tanzania ambayo budget yake ina deficit ya karibu 30% (tunabudget tukiwa na 70% tu ya pesa au mapato tarajiwa 30% hatujui itatoka wapi sanasana tuantegemea kuiomba tupewe bure au kwa mashartina wenye "kutunyonya") wakati Kenya wanazungumzia surplus (ziada ya akiba) ya reserve ile stori ya BM ya "tumejenga... kwa pesa zetu wenyewe" haipo tena ila "tumekusanya misaada mingi sana na tumejenga imani kwa wanaotufadhili..." ndiyo iliyoshamiri ikimaanisha tumetokomeza kujitegemea na tumeimarisha ukoloni mambo leo na uchumi tegemezi au????
 
Inflatuin siyo kigezo, mapato yalikuwa 160bil hela ilikuwa inabaki sasa 600bil, hamna hela! Inflation c kwa hivyo!
 
Wakulu jana nilichelewa kuwaletea habari hii kwakuwa nilibanwa na shughuli nyingi na vikao kemkem. Kuna taarifa nilizozipata kutoka chanzo cha kuaminika kuwa sasa pesa zilizopitishwa serikalini kwa Ministries, Departmentas and Agencies zinazotegemea serikali kuu kiwango kimeshuka kwa zaidi ya asilimia 40. Wizara zenye fungu lililooongezeka nji Wizara Ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga taifa na Wizara ya mambo ya Ndani. Hii maana yake nini? Ukizingatia hivi majuzi Serikali imedai kuvuka lengo la makusan yo. Mwenye kulijua hili kiundani atujuze mana ninahofu na mwelekeo wa Taifa hili kama hali ndiyo hii.

Mbona jibu liko wazi, ili wadhibiti maandamano ya wana CDM nchi nzima, kudidimiza demokrasia. kwani umesahau igunga na arumeru mashariki walipelekwa askari wangapi?
 
Back
Top Bottom