Sijasimuliwa nimetoka sasa hivi muhimbili, hali ni ya kuhuzunisha sana wagojwa ambao wanahitaji msaada wa daktari hawana la kufanya hakuna Daktari yeyote zaidi ya manesi ambao wapo wodini tu nafikiri kulinda usalama wa mashuka. Viongozi wanaohusika wakae na hawa madaktari ili kuokoa maisha ya watu wasio na hatia, hakuna sababu kabisa ya kuvutana, suluhu ni kufikia muafaka. inasikitisha sana. Uuungwana ni kusikiliza na kufanya maelewano kuokoa maisha ya watanzania wasio na hatia. hii ni laana kwa taifa damu hii itakuwa juu ya wahusika!!!