kakakuona40
JF-Expert Member
- Oct 3, 2011
- 300
- 52
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) mkoani Kilimanjaro kimevunja ngome ya Chadema katika Kata ya Mji Mpya katika Manispaa ya Moshi, baada ya kuvuna wanachama 75 akiwemo Katibu Mwenezi wa kata hiyo, Ludy Mlaki.
Akipokea wanachama hao, Katibu wa CCM mkoani humo, Stephen Kazidi alisema wanachama hao wapya pamoja na ugeni wao ndani ya chama lakini pia wana haki za kuomba nafasi yoyote ya uongozi ndani ya uchaguzi wa chama.
Akizungumza katika mkutano wa hadhara katika kata hiyo baada ya kufungua mashina matatu ya wakereketwa wa CCM na kushusha bendera za Chadema katika kata hiyo, Kazidi aliwataka wanachama hao wapya wasitishwe na viongozi wa chama walichotoka.
Nimepata taarifa kuwa waliojiunga na CCM wameanza kupokea vitisho kutoka katika vyama walivyotoka, ninyi kuweni na amani, mkipata vitisho vyovyote toeni taarifa katika vyombo vya dola siasa siyo vita, lakini mtu halazimishwi kuwa mwanachama, alisema.
Alisema chama kitawezesha matawi hayo kuwa na miradi ya kiuchumi katika kipindi kifupi kijacho kwani wanatambua kwamba vijana wanahitaji ajira na uanzishwaji wa miradi ndiyo ukombozi wao.
Katibu huyo aliwataka wana CCM kuchukua fomu za kugombea nafasi mbalimbali za uongozi katika uchaguzi mkuu ndani ya chama ili kuweka safu imara itakayokisaidia chama kushinda katika uchaguzi wa mwaka 2015.
Akizungumza baada ya kupokea kadi ya CCM, Mlaki alisema amejitoa Chadema kutokana na ubabaishaji unaofanyika ikiwemo ahadi hewa na unyanyasaji dhidi ya wananchi.
Alidai kwa kipindi chote akiwa Chadema, amekuwa akihamasishwa kufanya maandamano na kugomea shughuli mbalimbali za maendeleo bila kujali kuwa wanaoathirika ni wao wenyewe.
Source: HabariLeo | CCM yainyanyasa Chadema Moshi
Akipokea wanachama hao, Katibu wa CCM mkoani humo, Stephen Kazidi alisema wanachama hao wapya pamoja na ugeni wao ndani ya chama lakini pia wana haki za kuomba nafasi yoyote ya uongozi ndani ya uchaguzi wa chama.
Akizungumza katika mkutano wa hadhara katika kata hiyo baada ya kufungua mashina matatu ya wakereketwa wa CCM na kushusha bendera za Chadema katika kata hiyo, Kazidi aliwataka wanachama hao wapya wasitishwe na viongozi wa chama walichotoka.
Nimepata taarifa kuwa waliojiunga na CCM wameanza kupokea vitisho kutoka katika vyama walivyotoka, ninyi kuweni na amani, mkipata vitisho vyovyote toeni taarifa katika vyombo vya dola siasa siyo vita, lakini mtu halazimishwi kuwa mwanachama, alisema.
Alisema chama kitawezesha matawi hayo kuwa na miradi ya kiuchumi katika kipindi kifupi kijacho kwani wanatambua kwamba vijana wanahitaji ajira na uanzishwaji wa miradi ndiyo ukombozi wao.
Katibu huyo aliwataka wana CCM kuchukua fomu za kugombea nafasi mbalimbali za uongozi katika uchaguzi mkuu ndani ya chama ili kuweka safu imara itakayokisaidia chama kushinda katika uchaguzi wa mwaka 2015.
Akizungumza baada ya kupokea kadi ya CCM, Mlaki alisema amejitoa Chadema kutokana na ubabaishaji unaofanyika ikiwemo ahadi hewa na unyanyasaji dhidi ya wananchi.
Alidai kwa kipindi chote akiwa Chadema, amekuwa akihamasishwa kufanya maandamano na kugomea shughuli mbalimbali za maendeleo bila kujali kuwa wanaoathirika ni wao wenyewe.
Source: HabariLeo | CCM yainyanyasa Chadema Moshi