Elections 2010 Hali halisi vituoni siku ya kupiga kura

Nimefika Mapambano A Sinza, kuna tatizo la upungufu wa wasimamizi waelekezaji wa wapiga kura. Walibandika huko siku za nyuma list ya wapiga kura, leo wametoa pale yalipokuwa na kuyahamishia kwenye madarasa mbali mbali, lakini hakuna mtu wa kuelekeza wapiga kura hili jambo, hivyo watu wanafika na kusumbuka kutafuta majina yao, na wengine kukata tamaa, nimefanikiwa kujaribu kuelekeza watu kama kumi hivi, lakini sioni msimamizi wa kituo, askari na hao wasimamizi wa tume hawana usaidizi wowote wamekaa, kwa sasa watu ni wachache sijui itakuwaje pale kutakapokuwa na watu wengi.
Kama kuna mtu anamjua mtu wa tume anayeweza kusaidia hili ataarifiwe.
 
Nimemaliza kupiga kura yangu hapa Ilkiurei nje kidogo ya mji wa Arusha, watu ni wengi sana, kuna utata wa baadhi ya majina ya watu kutoonekana lakini waangalizi wako makini sana kuwaelekeza wapiga kura namna wanavyoweza kutambua vituo vyao kwani wengine majina yao yamehamishiwa vituo vingine tofauti na walipojiandikishia. Inatia moyo sana jinsi upigaji kura unavyosimamiwa hapa.
Nimejaribu kudodosa kidogo kujua msomamo wa watanzania, kwa kweli CCM mnakazi kwani kila niliemuuliza nini hasa kilimsukuma kuwahi kiasi hicho kuja kupiga kura, jibu lilikuja tofauti na nilivyotegemea. Mzee mmoja kaniambia amechoshwa na uongozi usio na maslahi kwa wananchi na sasa kawahi ili aitumie haki yake vizuri kumchagua Dr. Slaa kwa mabadiliko ya kweli, anasema "pamoja na uzee wangu naamini Dr. Slaa ataniwezesha kufanikisha ujenzi wa kibanda changu" inatia moyo sana!

Wakati wa Ushabiki umepita subiri ndugu, jiandae kupokea matokeo hasi. Lakini kama Arusha yenyewe inaweza kutoa Rais basi kuwa na Furaha Rais munae tayari.
 
Mwaka huu wa uchaguzi tunasikia vituko vingi sana vyenye kuleta burudani ndani ya chumba cha kupigia kura.
Hii inaonyesha jinsi vijana wa kitanzania walivyochoka kabisa kabisa kuburuzwa na watu wazembe kutoka chama kijiitacho CCM.

Mara ya kwanza kabisa kupiga kura hapa duniani ilikuwa ni mwaka 1985. Vijana wa Tosa Sec tulipigwa mkwara mzito sana tukashindwa kupiga kura kwa vurugu za kijinga tu.
Kisa kilikuwa ni njama za kutuzuia tusimpigie mpinzania wa General Luhanga, Marehemu Kirangi, wote wa CCM ili Generali ashinde.Shule ya Tosa wakati ule ilikuwa na jumla ya wanafunzi 750 wote tukiwa tunasoma bure kabisa.
Nadhani walimu wetu pale Tosamaganga walivuta kitu kidogo ili wavuruge uchaguzi ule, sina uhakika.
Mwaka mwingine nilikuwa Manzese Midizini nadhani ilikuwa 1995 tulipiga kura kwa taabu sana tena kwa kuchelewa huku wanajeshi kadhaa wa JWTZ wakipga watu mateke na makofi.

Mizengwe ya CCM na NEC yao wakati wa kupiga kura huwa inaudhi sana.
Kwa uzoefu nilionao nashauri watu wawe na subra hadi mwisho.

Dr Slaa ukiingia hapo ikulu usisahau kwamba kuna WaTz wakaao ughaibuni ambao nao wana haki ya kupiga kura.Every vote counts
Vile vile usisahau kwamba huku ughaibuni kuna watu wenye akili sana wafanyao kazi katika vitengo mbali mbali ambao hata wazungu hawako tayari kuwaona wakiondoka na kurudi kwao kwani ukali wa vipaji vyao, makali ya wembe chapa Mamba yamesingiziwa.

Serikali ya CCM hata haijui uwepo wa vijana wake hao.

Mimi nawatakia kila la kheri muwapo ndani ya vyumba vya kupigia kura. Safari hii muueni Nyani huku mmemkazia macho yote mawili.
 
Nimetoka kutumia haki yangu kikatiba kuleta mabadiliko hapa kituo cha kimara baruti hali ni shwari watu wengi wamejitokeza wazee kwa vijana kuna vituo takriban sita hivi kwa hiyo mistari ni mifupi mifupi unapiga kura kwa raha mustarehe.
 
Nimetoka kupiga kura maeneo ya mbezi beach na kuna vituo 6. Kituoni nimeona kasoro hizi
  • Vituo vimefunguliwa saa 12 asubuhi lakini kupiga kura tumeanza saa 1 asubuhi tumeambiwa mtu wa mwisho kuruhusiwa kupiga kura ni atakae fika saa 10 jioni, na kila kituo kitahudumia watu 500, hesabu za haraka kila saa moja watu 55. Lakini kwa saa moja kituo kimoja kimehidumia watu 9 tu. Kuna uwezekano watu wengi wasiweze kupiga kura
  • Kuna watu watano ambao nimeshuhudia majina yao hayapo kwenye orodha ya wapiga kura wakati daftari lina majina na picha zao.
  • Mtu mmoja kakuta majina yake yamekosewa ingawa namba ya mpiga kura kwenye kitambulisho ni sawa daftari
  • Vituo vina mawakala wachache watatu hadi wanne, baadhi ya vyama havina mawakala
  • Kati ya mawakala hao waliopo wa vyama wengine wamekuja baada ya upigaji kura kuanza
  • Mawakala wa nec wako slow na hii ni asubuhi, ikifika mchana jua kali itakuwaje?
Tungepata na vituo vingine hali ilivyo

Mkuu yote usemayo ni ya kweli na mimi ninaishi mbezi beach nimepiga kura yangu kituo cha shule ya msingi. Mstari wetu mawakala wa NEC wapo very slow nilifika pale saa 1 nometoka saa 3..15.
 
Nilipopigia kura mimi nimekutana na msimamizi kichwa maji.Kwa wale ambao hawakuwahi kuangalia majina yao lazima ashike yeye kadi na kulitafuta jina.Hii ni kwa vile foleni zilivyopangwa watu hawawezi kuiona hiyo orodha.Hili lilipelekea wapiga kura kusongamana bila sababu na tofauti na vibanda vyengine jirani ambapo kuangalia ni jukumu la mpiga kura mwenyewe.
Nimewaona wapiga kura si chini ya watatu wamefika mwisho majina yao hayakuonekana na kutakiwa waende wakaangalia vibanda vyengine.
Tume ya Uchaguzi walione hili mapema kwani ikifika saa 9 alasiri itasababisha kudorora zaidi na pengine mabishano.
 
Mimi nimepigia Kivukoni, Watu wamejitokeza, na nimebahtika kufanya mahojiano kadhaa na wapiga kura baadhi wametoka Kilimanjaro, Tanga, Arusha na mikoa mingine jirani kuja kupiga kura kituo hicho (Most ni former students wa IFM). Vijana ni wengi sana jambo ambalo kimsingi linaashilia ushindi kwa Dr. wa Ukweli.....Tahadhari kubwa sana naomba mwenye contact ya moja kwa moja Dr. Slaa, John Mnyika, Freeman Mbowe au kiongozi yeyote anayeweza kuchukua hatua za haraka kulifanyia kazi hili. Nimekuta na rafiki yangu, roommate wangu chuo, najua kabisa ni kada wa sisiem na mnazi wa kufa, Ni mtu wa karibu sana na Mbunge mmoja wa Bunge la Afrika Mashariki na mmiliki wa chuo fulani huko Chanika kilichonistusha ni kwamba yupo na nyaraka za CHADEMA anadai yeye ndiye kapewa jukumu la kusimamia vituo vyote Maeneo ya Kivukoni, ili kura zetu zisiibiwe na madai yake ni kwamba yupo upande wa kijani kimaslahi zaidi na si kizalendo.....Naomba hizi habari zifike huko na tujiridhishe juu ya mtu huyu isije kuwa tunachezewa mchezo mchafu kwa kuweka imani kwa watu wasiokuwa wenzetu...... i have all his contacts.
 
Niko Moro. Hali ya hapa pamoja kuwa ni shwari lakini mawakala hawajishughulishi kabisa kuhakiki taarifa za wapiga kura. Wamewekewa viti mbali na maofisa wanaohakiki na hawana copy za orodha za wapiga kura. Nahisi wakija mamluki hawatagundulika kabisa...
 
Acha upuuzi, vituo vyote vimepewa watu ambao sio zaidi ya 450!!! Wabongo mna matatizo sana... Mumeambiwa usome majina kwenye sehemy ujue umewekwa kwenye kituo kipi? Mimi nimeona kila kitu kilikuwa poa... watu kulalamika kawaida tu Tanzania.

Kasheshe
Tatizo si kuwa watu hawakusoma majina, umesoma kabisa na kuona jina na kituo chako, ukija unakuta wamebadirisha kwa kupanga wao tena na wameng'oa ile list ya mwanzo, tatizo hakuna mtu wa kueleza kuwa sasa wamepanga vipi hivyo vituo - Mfano Mapambano A Sinza, binafsi imebidi nijitolee kuanza kuelekeza watu maana wengi wanahangaika na kukata tamaa.
 
tarakea mambo yameenda poa, vijana ni wengi wamejitokeza, kuliko wazee

Nawatakia kila la heri. ngaishwa mfele ya mhindi hali ni ngvishwa. Kumbireni mramba fo yoruni mtale mwanakesho wa chadema...
 
Tunashukuru sana kwa taarifa. Maana hata tulio mbali tunajiona kama vile tuko nyumbani jinsi mtandao unavyokwenda. Keep it up!!
 
Mimi nimepigia Kivukoni, Watu wamejitokeza, na nimebahtika kufanya mahojiano kadhaa na wapiga kura baadhi wametoka Kilimanjaro, Tanga, Arusha na mikoa mingine jirani kuja kupiga kura kituo hicho (Most ni former students wa IFM). Vijana ni wengi sana jambo ambalo kimsingi linaashilia ushindi kwa Dr. wa Ukweli.....Tahadhari kubwa sana naomba mwenye contact ya moja kwa moja Dr. Slaa, John Mnyika, Freeman Mbowe au kiongozi yeyote anayeweza kuchukua hatua za haraka kulifanyia kazi hili. Nimekuta na rafiki yangu, roommate wangu chuo, najua kabisa ni kada wa sisiem na mnazi wa kufa, Ni mtu wa karibu sana na Mbunge mmoja wa Bunge la Afrika Mashariki na mmiliki wa chuo fulani huko Chanika kilichonistusha ni kwamba yupo na nyaraka za CHADEMA anadai yeye ndiye kapewa jukumu la kusimamia vituo vyote Maeneo ya Kivukoni, ili kura zetu zisiibiwe na madai yake ni kwamba yupo upande wa kijani kimaslahi zaidi na si kizalendo.....Naomba hizi habari zifike huko na tujiridhishe juu ya mtu huyu isije kuwa tunachezewa mchezo mchafu kwa kuweka imani kwa watu wasiokuwa wenzetu...... i have all his contacts.

Jamani hili lisipuuziwe, naomba habari hii ifikishwe kunakohusika ....
 
Nimetoka kupiga Kura Kijitonyama Kituo cha Kentoni A.
Kwa kweli watu pale walikuwa wanaongea waziwazi kuwa wanaenda kupigia kura Dr. Slaa, sasa sijui kama hali ndo iko ivi CCM wataenda wapi.....
Labda kuiba.
 
Kwa kweli inatia moyo sana. Mimi familia yangu yote imeshawai asubuhi na mapema kupiga kura na tayari wote ni kwa DR wa matumaini. Mwaka huu nililazimika kutumia muda mwingi home kutoa semina kwa familia na ukoo juu ya kufanya mapinduzi. Nashukru wengi wamenielewa. CHADEMA juu
 
Kwa kweli hili ni la kulishughulikia. Chukua tahadahari mapema. Ndo maana Dr alisema tulinde kura zetu. wenye mawasiliano ya moja kwa moja washughulikie hili suala
 
Image0967.jpg
 
Back
Top Bottom