Hakuna Mtanganyika (mtanzania bara) Anayemiliki Ardhi/Nyumba Zanzibar

eedoh05

JF-Expert Member
Apr 20, 2011
632
234
Nd.wana jf. Nasikia ati ni marufuku kwa mtu kutoka bara (tanganyika) kumiliki aridhi,nyumba au jengo huko Zanzibar. Je ni kweli?
Kama jibu ni NDIYO. Kwa nini huku Tanganyika hatujawa na sera kama hiyo kwa wazanzibar?

Wazanzibar hawapaswi kumiliki ardhi huku Tanganyika. Kwani katiba inasemaje? Si kwamba mtanzania ana uhuru wa kuishi popote ndani ya Jamhuri ya Muungano. Kwa nini watanganyika hawamiliki aridhi kule?

=========
June 2012:
ACTUALLY, NAANDIKA HII MADA KWA MAKUSUDI ILI TUJADILI...

Watz bara wanakatazwa kunujua ardhi kule visiwani, lakini wavisiwani wanaweza kununua ardhi kubwa kiasi wakipendacho hapa bara....swali langu ni, kuna haki hapo? pia, wazanzibari waliojenga bara (tukianza na mwinyi na familia yake wenye majumba mengi mikocheni na maeneo mengine dsm), wenye mashamba mengi hapa tz, siku muungano ukivunjika kama wazenji wanavyotaka, wataendelea kumiliki au ndo watavirudisha kwa wazanzibari...

Wapemba wenye maduka kila kona dsm watafungasha virago au watabadilisha kuwa wawekezaji kupitia kituo cha uwekezaji TIC.....wawe na mtaji si chini ya milioni 300 ambazo nina uhakika hawana......wataondoka wote kurudi makwao wakarundikane kwenye mitaa?...

Mbona viongozi kama mwinyi na wengine wamenyamaza kimyaaa, au ukivunjika wao wataomba uraia wa tz....
July 2013:
Wapendwa Watanzania wenzangu,

Zanzibar tangu enzi Dr Amani Karume alibadilisha katiba ili Watu wenye Asili ya Tanganyika wasimiliki Ardhi Zanzibar, badala yake wakodishwe na serikali kwa masharti ya uwekezaji sawa na wawekezaji we Nchi nyingine duniani.

Je, katiba ijayo itawarudishia Watanzania haki sawa? Au ndio na Wazanzibari walio wengi Tanganyika walipie kama kodi mahekalu, mashamba na Viwanda wanavyomiliki?

Ardhi si mali ya Muungano:

"Mwanasheria anena na JAMHURI"

"Sheria ya Ardhi ya Zanzibar ya mwaka 1992 hairuhusu mtu asiye Mzanzibari (wakiwamo Watanganyika) kumiliki ardhi Zanzibar."


Wazanzibari wanajidanganya kama wanakimbia kununua ardhi katika maeneo mbalimbali ya Tanganyika , kwani watapoteza fedha zao bure.
¡°Bila hata kubadili sheria ya sasa, kitakachobadilika katika sheria za ardhi Na. 4 na Na. 5 za mwaka 1999 ni jina kutoka Tanzania kwenda Tanganyika.


Sheria iko wazi, kuwa mtu ambaye si Mtanganyika ataruhusiwa kupewa ardhi ya Tanganyika iwapo tu anafanya kazi ya uwekezaji.
¡°Inatamka wazi kuwa ardhi ya Tanganyika si kwa ajili ya watu kuja kujenga makazi, bali uwekezaji. Hivyo kama kuna Mzanzibari anayejidanganya kuwa akinunua ardhi Tanganyika atajenga na kuishi hapa kama si mwekezaji anapoteza kuda na fedha zake.



Ardhi hiyo itachukuliwa na Rais wa Tanganyika bila kulipwa fidia. Wazanzibari wameyataka haya, lazima tuelezane ukweli mgumu,¡±


¡°Umiliki wa ardhi, haki za wenyeji na mipaka ya matumizi ya ardhi kwa wageni utawekwa wazi."

Na sasa wageni ni pamoja na Wazanzibari. Nasema Tanganyika wana haki ya kutunga sheria yao na wana haki ya kuweka mipaka kwa walio wageni.

¡°Wageni hawatapewa haki ya kumiliki ardhi ila watakuwa na haki ya kutumia ardhi. Zanzibar kilichowapa access (umiliki) wa ardhi ya Tanganyika awali ni kwa sababu sisi Tanzania Bara imo ndani ya Muungano. Itabidi Wazanzibari wajue kuwa nao ni wageni wakija Tanganyika."

¡°Tuliwatahadhalisha na tunaendelea kuwatahadharisha kuwa hata ukinunua ardhi Katiba ya Tanzania Bara (Tanganyika) itakuwa na haki ya kufuta umiliki wa ardhi."



"Mzanzibari atatumia ardhi kama mwekezaji ila si makazi, au kilimo cha kujikimu."

¡°Ni kama ambavyo Wakenya wanakuja wananunua ardhi na nyumba kumbe wanapoteza fedha zao, hata wakikimbilia kununua wanapoteza hela zao bure,¡±

Sheria ya Ardhi ya Zanzibar ya mwaka 1992 hairuhusu mtu asiye Mzanzibari (wakiwamo Watanganyika) kumiliki ardhi Zanzibar.


Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Profesa Palamagamba Kabudi, alipoulizwa na JAMHURI juu ya mshikemshike wa ardhi na kuhamishwa kwa makao makuu ya Serikali ya Tanzania kutoka Dodoma kwenda Dar es Salaam, alisema kwa ufupi, ¡°Mawazo haya yalikuwapo na yalizungumzwa, ila tusubiri wananchi ndiyo waamue.¡±
Tafsiri rahisi juu ya mabadiliko haya ina maana Wazanzibari waliojenga Tanganyika wanaokadiriwa kufikia 600,000 wanaweza kulazimika kurejea Zanzibar kwanza na kurudi Tanganyika baada ya kuomba, ama kibali cha ukaazi, au uwekezaji kupitia Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) na kukubaliwa kupewa ardhi baada ya kutimiza masharti.
Moja ya masharti ya uwekezaji watakayopaswa kuyatimiza kupitia TIC ni kwamba lazima mwekezaji kama anataka kwenda kuwekeza Tanganyika awe na mtaji usiopungua dola 100,000 sawa na Sh milioni 160 za Tanzania ndipo apewe vibali vya kuishi. Wazanzibari wanaweza kutakiwa kutekeleza sharti hilo la kisheria.



JAMHURI
 
Nd.wana jf. Nasikia ati ni marufuku kwa mtu kutoka bara (tanganyika) kumiliki aridhi,nyumba au jengo huko Zanzibar. Je ni kweli?
Kama jibu ni NDIYO. Kwa nini huku Tanganyika hatujawa na sera kama hiyo kwa wazanzibar?

Wazanzibar hawapaswi kumiliki ardhi huku Tanganyika. Kwani katiba inasemaje? Si kwamba mtanzania ana uhuru wa kuishi popote ndani ya Jamhuri ya Muungano. Kwa nini watanganyika hawamiliki aridhi kule?

Hii tetesi yako ni hatari kama ni ya kweli au ya uongo
 
Mkuu hii nadhani itakuwa uongo mkubwa..., mtu kutoka bara?, je wali ambao wanatoka nje ya Tanzania?
 
Yani nataman aje atokee rais kichaa huku bara..aamue kuuvunja 2 huo muungano..hauna faida kwa watanganyika kabisa.
 
Msikurupuke kusema uongo wakati jambo hili la ubaguzi linafanyika. Nina rafiki yangu mfanyabiashara Kariakoo, pia amefanya/anafanya biashara zake Pemba. Aliona shamba akataka kununua ili alime karafuu. Mwenye eneo alikubali, walipokwenda kwa Sheha ili waandikishiane Sheha akaleta kauzibe. Ukatokea mvutano kati ya Sheha na mwenye shamba. Ndipo Sheha akapasua, " Huyu mtu wa bara hawezi kununua ardhi huku kwetu wao wanamapori mengi". Hadi leo rafiki yangu hajapata eneo sehemu yoyote, si Unguja wala Pemba.

Kama haitoshi mwaka jana Novemba nilimwuuliza muunguja,"Hivi Unguja yote imejaa kiasi cha kwamba wazanzibari hawawezi kupata viwanja?" akasema "Haijajaa, viwanja na mashamba yapo. Watu mbona wanauziana kila uchao? Ni pesa yake mtu na maelewano na mwenye mali" Nikamuuliza "Na mimi naweza kupata nikiwa na hela ya kutosha?" Akajibu "Huwezi kupata." Nilipomdadisi zaidi kwanini siwezipata na yeye anawezakupata. Jibu lilikuwa, "Mbona wewe unatokea Bara, huwezi kupata." And I concluded on how racist are they.
 
Sitta alisema jana, ka mbuai mbuai bwana! Mambo yawekwe hadharani na kama Muungano uvunjwe na ijulikane hivyo, sio kujishaua tuu!!
 
Msikurupuke kusema uongo wakati jambo hili la ubaguzi linafanyika. Nina rafiki yangu mfanyabiashara Kariakoo, pia amefanya/anafanya biashara zake Pemba. Aliona shamba akataka kununua ili alime karafuu. Mwenye eneo alikubali, walipokwenda kwa Sheha ili waandikishiane Sheha akaleta kauzibe. Ukatokea mvutano kati ya Sheha na mwenye shamba. Ndipo Sheha akapasua, " Huyu mtu wa bara hawezi kununua ardhi huku kwetu wao wanamapori mengi". Hadi leo rafiki yangu hajapata eneo sehemu yoyote, si Unguja wala Pemba.

Kama haitoshi mwaka jana Novemba nilimwuuliza muunguja,"Hivi Unguja yote imejaa kiasi cha kwamba wazanzibari hawawezi kupata viwanja?" akasema "Haijajaa, viwanja na mashamba yapo. Watu mbona wanauziana kila uchao? Ni pesa yake mtu na maelewano na mwenye mali" Nikamuuliza "Na mimi naweza kupata nikiwa na hela ya kutosha?" Akajibu "Huwezi kupata." Nilipomdadisi zaidi kwanini siwezipata na yeye anawezakupata. Jibu lilikuwa, "Mbona wewe unatokea Bara, huwezi kupata." And I concluded on how racist are they.


Huu ni uongo uliokithiri na kushtadi.

Mfano mzuri ni maeneo ya Chake-Chake, Kusini, Pemba ambako Kanisa la Roman Catholic wanamiliki kiwanja na wamejenga kindergarten

Hapa hapa Chake-Chake, Kanisa la SDA wanamiliki kiwanja na wamejenga hospitali.

Unguja, maeneo ya Cheju, Kanisa la Roman Catholic wanajenga high school.

Lakini kubwa ni kwamba karibu mtaondoka, viwanja vya nini?

Nyie huku mje mlime tu mpaka "muungano" utakapo kata roho.
 
Zanzibar, ardhi yote ni mali ya Serikali, yenu wapeni magabachori tu.

Mtakufa kwa pombe na ufisadi.
kwahiyo mzanzibar na yeye aruhusiwi kupata ardhi, zanzibar????, pia kuna wanzanzibar wengi tu (kina Ali Hassan Mwinyi n.k.) wana ardhi bara je na wenyewe ni magabachori?
 
Yani nataman aje atokee rais kichaa huku bara..aamue kuuvunja 2 huo muungano..hauna faida kwa watanganyika kabisa.

'The man shall rise from the hills and save the people at their hour of need'.

Kukiwa na mgombea Urais atakayesema atavunja Muungano kura yangu anayo hata kama ni Fisadi kama EL, nitamchagua tu kuondoa hii kero ya miaka mingi. Ee Mwenyezi Mungu inua kiongozi thabiti atakayefanya maamuzi magumu ambayo wengine wameshindwa.
 
Hizi ni fitna na choko choko kuna mimi mtanganyika, mbona nina nyumba nimejenga na nimepangisha Zanzibar!!!!. Acheni fitina zisizokuwa na mpango
 
Huu ni uongo uliokithiri na kushtadi.

Mfano mzuri ni maeneo ya Chake-Chake, Kusini, Pemba ambako Kanisa la Roman Catholic wanamiliki kiwanja na wamejenga kindergarten

Hapa hapa Chake-Chake, Kanisa la SDA wanamiliki kiwanja na wamejenga hospitali.

Unguja, maeneo ya Cheju, Kanisa la Roman Catholic wanajenga high school.

Lakini kubwa ni kwamba karibu mtaondoka, viwanja vya nini?

Nyie huku mje mlime tu mpaka "muungano" utakapo kata roho.

Sina uhakika na watanganyika kutomiliki ardhi Zanzibar ila makanisa na taasisi za kidini ni tofauti sana na mtu binafsi, na hata hivyo, kanisa kama RC, SDA, KKKT, TAG na mengineyo kutoka tanganyika pamoja na kuwa na usajili wa kanisa huku tanganyika, bado wanapoenda kuanzisha makanisa zanzibar lazima tena watume maombi na wapewe usajili wa makanisa yao. Huwezi toka hapa tanganyika na usajili wa hapa ukanzisha kanisa zanzibar, usajili wa bara hautambiliki zanzibar...huu muungano una matatizo kibao
 
kwahiyo mzanzibar na yeye aruhusiwi kupata ardhi, zanzibar????, pia kuna wanzanzibar wengi tu (kina Ali Hassan Mwinyi n.k.) wana ardhi bara je na wenyewe ni magabachori?

Ali Hassan Mwinyi kwao Mkuranga, Unguja alikuja kusoma Quran tu na hakutoka tena. Yeye na wenzake kibao.
 
Huu ni uongo uliokithiri na kushtadi.

Mfano mzuri ni maeneo ya Chake-Chake, Kusini, Pemba ambako Kanisa la Roman Catholic wanamiliki kiwanja na wamejenga kindergarten

Hapa hapa Chake-Chake, Kanisa la SDA wanamiliki kiwanja na wamejenga hospitali.

Unguja, maeneo ya Cheju, Kanisa la Roman Catholic wanajenga high school.

Lakini kubwa ni kwamba karibu mtaondoka, viwanja vya nini?

Nyie huku mje mlime tu mpaka "muungano" utakapo kata roho.

Wakuu,
Naomba kufahamishwa endapo kanisa katoliki, sabato/SDA wanapo milikishwa ardhi wanaiwakilisha Tanzania Bara?
maana nimeshindwa kuelewa jibu hili.
 
Sina uhakika na watanganyika kutomiliki ardhi Zanzibar ila makanisa na taasisi za kidini ni tofauti sana na mtu binafsi, na hata hivyo, kanisa kama RC, SDA, KKKT, TAG na mengineyo kutoka tanganyika pamoja na kuwa na usajili wa kanisa huku tanganyika, bado wanapoenda kuanzisha makanisa zanzibar lazima tena watume maombi na wapewe usajili wa makanisa yao. Huwezi toka hapa tanganyika na usajili wa hapa ukanzisha kanisa zanzibar, usajili wa bara hautambiliki zanzibar...huu muungano una matatizo kibao

Ndio. Kwa sababu Zanzibar ni nchi yenye Sheria zake tofauti na Bara.
 
Acheni upotoshaji mimi mwenyewe na nyumba Zanzibar nimejenga nimepangisha, na mimi ni Mtanganyika safi naishi bara

Ritz,

Watu wengine wa ajabu sana majungu na fitina zisizo na mpango ndio jadi, kama umeingizwa mjini ulipotaka kununua kiwanja au nyumba na wajanja zanzibar bora useme ukasaidiwa na sio kutoa visingizio visivyo na mpango
 
Katika orodha ya mambo ya muungano suala la ardhi halimo. Wenzetu zanzibar wapo makini kulinda ardhi yao kuliko bara.
Kama yanavyoonekana hapa chini:
NYONGEZA YA KWANZA_________(Imetajwa katika ibara ya 4)Mambo ya Muungano​
1. Katiba ya Tanzania na Serikali ya Jamhuri ya Muungano.2. Mambo ya Nchi za Nje.3. Ulinzi na Usalama.4. Polisi.5. Mamlaka juu ya mambo yanayohusika na hali ya hatari.6. Uraia.7. Uhamiaji.8. Mikopo na baiashara ya Nchi za Nje.9. Utumishi katika Serikali ya Jamhuri ya Muungano.10.Kodi ya Mapato inayolipwa na watu binafsi na mashirika,ushuru wa forodha na ushuru wa bidhaa zinazotengenezwanchini Tanzania unaosimamiwa na Idara ya Forodha.11.Bandari, mambo yanayohusika na usafiri wa anga, posta nasimu.12.Mambo yote yanayohusika na sarafu na fedha kwa ajili yamalipo yote halali (pamoja na noti); mabenki (pamojamabenki ya kuweka akiba) na shughuli zote za mabenki;fedha za kigeni na usimamizi juu ya mambo yanayohusikana fedha za kigeni.13.Leseni ya viwanda na takwimu.14.Elimu ya juu.15.Maliasili ya mafuta, pamoja na mafuta yasiyochujwa yamotokaa na mafuata ya aina ya petroli na aina nyinginezo zamafuta au bidhaa, na gesi asilia.16.Baraza la Taifa la Mitihani la Tanzania na mambo yoteyanayohusika na kazi za Baraza hilo.17.Usafiri na usafirishaji wa anga.18.Utafiti.19.Utafiti wa hali ya hewa.20.Takwimu.21.Mahakama ya Rufani ya Jamhuri ya Muungano.22.Uandikishaji wa Vyama vya siasa na Mambo mengine​
yanayohusiana navyo.
 
Back
Top Bottom