Lupweko
JF-Expert Member
- Mar 26, 2009
- 20,604
- 20,336
Inawezekana kuna watu hawajajua bado kuwa hakuna hata klabu moja ya Sudan iliyowahi kupata ushindi kwa Simba. Kama nimekosea, aje mtu anisahihishe hapa. Hata mwaka ule El-Mereikh walipovunja pambano la CECAFA, walikuwa nyuma kwa mabao 2-1 hadi dakika ya 89, na wakawapiga sana wachezaji wa Simba. Bahati nzuri Simba na El-Mereikh zikapangwa kucheza raundi ya kwanza klabu bingwa Africa, ambapo Simba ilishinda 1-0 Dar na ikashinda tena 1-0 Khartoum. El-Mereikh hawatamsahau Nteze John hata siku moja Timu ya El Hilal (ambayo ilijenga urafiki na Simba baada ya kuona Simba inawafunga mara kwa mara El-Mereikh watani wao), nayo pia imeshapigwa mara kadhaa na Simba. Kwa hiyo hii Al Ahly Shandy itakuwa klabu ya kwanza kuifunga Simba kama itafanya hivyo mjini Shandy, Sudan, jambo ambalo si rahisi hivi hivi.