Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,266
- 33,039
Wakati Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limeunda kamati ya kufanya uchunguzi wa suala la kutekwa, kupigwa na kuumizwa vibaya Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari, Dk. Stephen Ulimboka, makundi mbalimbali katika jamii yameibuka na kueleza kutokuridhishwa kwao na polisi pekee kufanya kazi hiyo.
Makundi hayo yanajenga hoja mbalimbali zinazolenga uhalali wa kutaka kuweko na tume huru ya kufanya kazi hiyo kwa sababu hadi sasa hisia ambazo zimetanda juu ya mateso yaliyomkuta Dk. Ulimboka, ni kwamba inawezekana serikali ikawa na mkono wake katika hilo.
Tunajua na tumesikia serikali kupitia kwa viongozi wakuu, kwanza Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi na baadaye Waziri Mkuu kwamba serikali haina mkono katika suala hilo, lakini pia tumeshuhudia maoni ya watu mbalimbali wakiwamo madaktari wenyewe ambao ndiyo chimbuko la kadhia hii, kila upande ukionyesha kuwa kuna nguvu kutoka mahali fulani ya utekelezaji wa uhalifu huu.
Kwa kifupi, katika suala la kutekwa, kupigwa na kuumizwa mno kwa Dk. Ulimboka ambaye kwa sasa amelazwa Taasisi ya Mifupa Muhimbili (MOI), akitibiwa chini ya uangalizi maalum, ni vigumu sana watu kuaminiana hata kama wataapa kwa miungu yao kama uchunguzi huru utakaohusisha makundi mbalimbali katika jamii hautafanyika.
Kwa bahati mbaya, anayenyooshewa kidole katika kadhia hii ya kuudhi, kukasirisha na kwa kweli kuamsha hasira ya umma, ni serikali. Serikali inanyooshewa kidole kwa sababu za wazi kabisa, ndiyo ilikuwa katika mvutano na madaktari na Dk. Ulimboka ndiye alikuwa kiongozi wa madaktari hao.
Hili ni suala nyeti, tata na ambalo limekuwa vigumu kueleweka kwa maelezo ya kawaida ama ya vyombo vya usalama kama polisi na hata vya wasemaji wengine wa serikali; hisia za wananchi kwa ujumla wake zimekuwa kali mno. Ni kali kuliko inavyoweza kuelezwa.
Kwa maana hiyo inahitaji kutazamwa kwa njia ya kipekee ili kwanza kujenga imani kuwa haki itapatikana katika jambo hilo.
Tunajua taifa hili pia lina historia yake, kwamba siyo mara ya kwanza kuundwa kwa tume huru kufanya uchunguzi wa jambo ambalo limetatiza jamii na kwa kweli ambalo linaiweka serikali katika muonekano wa kuwa mtuhumiwa wa hilo lililotendeka; katika mazingira kama hayo serikali au vyombo au chombo chake kimojawapo kujiteua tu haraka haraka kufanya uchunguzi, kwa kweli haiwaletei wananchi amani na kwa hali hiyo matokeo ya uchunguzi wake yanakuwa tayari yamekwisha kupingwa hata kabla ya uchunguzi wenyewe kuanza kufanywa.
Ni vema ikaeleweka mapema kuwa taifa hili sasa limepiga hatua kubwa sana, kwanza kutambua na kuheshimu haki za binadamu, kuna vyomvyo ambavyo serikali imeviunda vya kulinda haki hizo, kuna sheria na katiba katika kulinda haki hizo pia, lakini zaidi sana makundi mbalimbali ya kijamii yamejipa wajibu wa kuwa waangalizi wa haki za binadamu; kila kundi katika wadau wote hawa linakubalika na kutambulika katika jamii.
Itakuwa ni makosa makubwa kwa serikali kujiaminisha kwamba inaweza tu kupuuza makundi mengine yenye dhima ya kutetea haki za binadamu na kujifanyia mambo kama itakavyo.
Ni kwa kutambua ukweli huu na kwa kweli tukijua fika kwamba serikali yoyote ambayo imeingia madarakani kwa njia ya sanduku la kura, inawajibika kusikiliza na kuzifanyia kazi hisia za wananchi wake, kwa kuwa wao ndiyo chimbuko la madaraka ya serikali, iunde tume huru. Hata hivyo, inawezekana ikapuuza, lakini ni uhakika pia kuwa gharama yake nayo ni kubwa baada ya kitambo kidogo.
Ndiyo maana nasi tunasisitiza kuishauri serikali kuwa isikilize vilio na hisia hizi juu ya janga lililomkuta Dk. Ulimboka; iunde tume huru ambayo itajumuisha watu wenye uadilifu usiotiwa shaka ili ripoti itakayopatikana ikubaliwe na umma juu janga lililomkuta Dk. Ulimboka.
Ni vema serikali ikashughulika na janga lililomkuta Dk. Ulimboka kwa kutambua wazi kwamba inashughulikia kadhia nzima ya mgomo wa madaktari, kwa hiyo ni lazima ifanye bidii ili kwanza kuokoa maisha ya wananchi wake kwa kuwashawishi madaktari warejee kazini, lakini la umuhimu zaidi ionyeshe kwa vitendo halisi inafanyia kazi changamoto hizi zilizombele yake kwa uhuru na uwazi ambavyo vitaisafisha dhidi ya tuhuma hizi.
CHANZO: NIPASHE
Makundi hayo yanajenga hoja mbalimbali zinazolenga uhalali wa kutaka kuweko na tume huru ya kufanya kazi hiyo kwa sababu hadi sasa hisia ambazo zimetanda juu ya mateso yaliyomkuta Dk. Ulimboka, ni kwamba inawezekana serikali ikawa na mkono wake katika hilo.
Tunajua na tumesikia serikali kupitia kwa viongozi wakuu, kwanza Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi na baadaye Waziri Mkuu kwamba serikali haina mkono katika suala hilo, lakini pia tumeshuhudia maoni ya watu mbalimbali wakiwamo madaktari wenyewe ambao ndiyo chimbuko la kadhia hii, kila upande ukionyesha kuwa kuna nguvu kutoka mahali fulani ya utekelezaji wa uhalifu huu.
Kwa kifupi, katika suala la kutekwa, kupigwa na kuumizwa mno kwa Dk. Ulimboka ambaye kwa sasa amelazwa Taasisi ya Mifupa Muhimbili (MOI), akitibiwa chini ya uangalizi maalum, ni vigumu sana watu kuaminiana hata kama wataapa kwa miungu yao kama uchunguzi huru utakaohusisha makundi mbalimbali katika jamii hautafanyika.
Kwa bahati mbaya, anayenyooshewa kidole katika kadhia hii ya kuudhi, kukasirisha na kwa kweli kuamsha hasira ya umma, ni serikali. Serikali inanyooshewa kidole kwa sababu za wazi kabisa, ndiyo ilikuwa katika mvutano na madaktari na Dk. Ulimboka ndiye alikuwa kiongozi wa madaktari hao.
Hili ni suala nyeti, tata na ambalo limekuwa vigumu kueleweka kwa maelezo ya kawaida ama ya vyombo vya usalama kama polisi na hata vya wasemaji wengine wa serikali; hisia za wananchi kwa ujumla wake zimekuwa kali mno. Ni kali kuliko inavyoweza kuelezwa.
Kwa maana hiyo inahitaji kutazamwa kwa njia ya kipekee ili kwanza kujenga imani kuwa haki itapatikana katika jambo hilo.
Tunajua taifa hili pia lina historia yake, kwamba siyo mara ya kwanza kuundwa kwa tume huru kufanya uchunguzi wa jambo ambalo limetatiza jamii na kwa kweli ambalo linaiweka serikali katika muonekano wa kuwa mtuhumiwa wa hilo lililotendeka; katika mazingira kama hayo serikali au vyombo au chombo chake kimojawapo kujiteua tu haraka haraka kufanya uchunguzi, kwa kweli haiwaletei wananchi amani na kwa hali hiyo matokeo ya uchunguzi wake yanakuwa tayari yamekwisha kupingwa hata kabla ya uchunguzi wenyewe kuanza kufanywa.
Ni vema ikaeleweka mapema kuwa taifa hili sasa limepiga hatua kubwa sana, kwanza kutambua na kuheshimu haki za binadamu, kuna vyomvyo ambavyo serikali imeviunda vya kulinda haki hizo, kuna sheria na katiba katika kulinda haki hizo pia, lakini zaidi sana makundi mbalimbali ya kijamii yamejipa wajibu wa kuwa waangalizi wa haki za binadamu; kila kundi katika wadau wote hawa linakubalika na kutambulika katika jamii.
Itakuwa ni makosa makubwa kwa serikali kujiaminisha kwamba inaweza tu kupuuza makundi mengine yenye dhima ya kutetea haki za binadamu na kujifanyia mambo kama itakavyo.
Ni kwa kutambua ukweli huu na kwa kweli tukijua fika kwamba serikali yoyote ambayo imeingia madarakani kwa njia ya sanduku la kura, inawajibika kusikiliza na kuzifanyia kazi hisia za wananchi wake, kwa kuwa wao ndiyo chimbuko la madaraka ya serikali, iunde tume huru. Hata hivyo, inawezekana ikapuuza, lakini ni uhakika pia kuwa gharama yake nayo ni kubwa baada ya kitambo kidogo.
Ndiyo maana nasi tunasisitiza kuishauri serikali kuwa isikilize vilio na hisia hizi juu ya janga lililomkuta Dk. Ulimboka; iunde tume huru ambayo itajumuisha watu wenye uadilifu usiotiwa shaka ili ripoti itakayopatikana ikubaliwe na umma juu janga lililomkuta Dk. Ulimboka.
Ni vema serikali ikashughulika na janga lililomkuta Dk. Ulimboka kwa kutambua wazi kwamba inashughulikia kadhia nzima ya mgomo wa madaktari, kwa hiyo ni lazima ifanye bidii ili kwanza kuokoa maisha ya wananchi wake kwa kuwashawishi madaktari warejee kazini, lakini la umuhimu zaidi ionyeshe kwa vitendo halisi inafanyia kazi changamoto hizi zilizombele yake kwa uhuru na uwazi ambavyo vitaisafisha dhidi ya tuhuma hizi.
CHANZO: NIPASHE