Haki Nyimifu Katika Katiba-Kigoma Kusini waungana Kufungua kesi

Amavubi

JF-Expert Member
Dec 9, 2010
30,145
13,216
Wapiga kura wa jimbo la Kigoma Kusini, ambalo mbunge wake ni David Kafulila wamefungua kesi ya Kikatiba Mahakama Kuu, Dar es Salaam wakipinga kifungu kwenye Katiba kinachotamka mbunge anapovuliwa uanachama anakoma kuwa mbunge.

Watu hao watatu walifungua kesi hiyo leo na kupewa namba 1/2012 wanakilalamikia matumi ya Ibara ya 71 (1) (f) kinachosema Mbunge atakoma kuwa mbunge iwapo ataacha kuwa mwanachama wa chama alichokuwamo wakati alipochaguliwa au alipoteuliwa kuwa mbunge .

Aidha wanaiomba mahakama hiyo iamuru Bunge litunge sheria inayoruhusu mbunge aliyefukuzwa uanachama katika chama chake awe huru aruhusiwe kuhamia chama chochote atakacho bila kuvuliwa ubunge.

Kesi hiyo imefunguliwa zikiwa ni siku chache baada ya Mbunge wa Kigoma Kusini David Kafulila kuvuliwa uanachama katika chama NCCR-Mageuzi na hivyo kupoteza ubunge wake.

Kafulia alivuliwa uanachama wa chama hicho Novemba 20, mwaka jana, lakini amefungua kesi mahakamani hapo kupinga hatua hiyo ya kuvuliwa uanachama.

Kesi hiyo ya kikatiba imefunguliwa leo na wapiga kura watatu wa jimbo ambao ni wanachama wa tofauti kwa niaba ya wananchi wengine wa jimbo hilo dhidi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Walalamikaji wanaowakilishwa na Kampuni ya uwakili ya Mpoki & Associates, ni Juma Shaban Nzengula (CCM), Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM Kigoma kata ya Nguruka, Patrick Haruna Rubilo (NCCR-Mageuzi), mjumbe wa Kata ya Itebula na Mwenyekiti wa Kijiji cha Bweru na Fanueli Misigalo Bihole ambaye ni mwanachama wa Chama cha Wananchi (CUF) ni Katibu wa wazazi wa Kata ya Mtegowanoti.

Wanalalamikia kifungu hicho kinakiuka haki za msingi katika Ibara ya 21 ya Katiba inayotoa uhuru wa kushiriki katika shughuli za umma kupitia wawakilishi waliochaguliwa na wananchi kwa mujibu wa sheria.

Aidha Ibara hiyo inakiuka Mkataba wa Kimataifa wa Haki za Binadamu ambao Tanzania imeuridhia na kuusaini.

Mbali na hayo inakiuka Ibara ya 201 (1) ya Katiba ya Nchi inayotoa uhuru kwa wananchi kushiriki na kutoa maoni yao kwa uwazi. Nje ya mahakama walidai kuwa kesi hiyo wamefungua kwa niaba ya wapiga kura wa jimbo la Kigoma Kusini baada ya kuona wimbi la kufukuzwa uanachama wabunge lililoingia sasahivi baada ya mbunge wao, Kafulila kufukuzwa NCCR na sasa mbunge wa Wawi Zanzibar (CUF), Hamad Rashid kufukuzwa.

Wakizungumza baada ya kufungua kesi hiyo, walalamikaji hao walisema kwamba wameamua kufungua kesi hiyo liocha ya kwamba wanatoka vyama tofauti kwa kuwa mbunge huo hakuchaguliwa na wanachama wa NCCR-Mageuzi tu bali na wa vyama vingine pia.

Walisema mbunge anakuwa ametoa ahadi nyingi baada ya kuchaguliwa, na sasa ni kipindi cha kutekeleza ikiwa ni pamoja na shunguli mbalimbali za maendeleo na hivyo ni kurudisha maendeleo nyuma.

Kwa upande wake Rubilo alisema kuwa mbunge anafunga mkataba na wananchi na kwamba huwa wanatoa ahadi nyingi katika kutekeleza mkataba huo kama vile kusomesha watoto na shughuli nyingine za maendeleo.
 
​mbona wanongelea mbunge tu waseme ata rais akifukuzwa chamani kwake awe huru kuendelea na urais wake bila kuupoteza
 
Nina wasiwasi na hawa wa sisiem.....ni kweli inatoka rohoni au wametumwa?
 
Wapiga kura wa jimbo la Kigoma Kusini, ambalo mbunge wake ni David Kafulila wamefungua kesi ya Kikatiba Mahakama Kuu, Dar es Salaam wakipinga kifungu kwenye Katiba kinachotamka mbunge anapovuliwa uanachama anakoma kuwa mbunge.

Watu hao watatu walifungua kesi hiyo leo na kupewa namba 1/2012 wanakilalamikia matumi ya Ibara ya 71 (1) (f) kinachosema Mbunge atakoma kuwa mbunge iwapo ataacha kuwa mwanachama wa chama alichokuwamo wakati alipochaguliwa au alipoteuliwa kuwa mbunge .

Aidha wanaiomba mahakama hiyo iamuru Bunge litunge sheria inayoruhusu mbunge aliyefukuzwa uanachama katika chama chake awe huru aruhusiwe kuhamia chama chochote atakacho bila kuvuliwa ubunge.

Kesi hiyo imefunguliwa zikiwa ni siku chache baada ya Mbunge wa Kigoma Kusini David Kafulila kuvuliwa uanachama katika chama NCCR-Mageuzi na hivyo kupoteza ubunge wake.

Kafulia alivuliwa uanachama wa chama hicho Novemba 20, mwaka jana, lakini amefungua kesi mahakamani hapo kupinga hatua hiyo ya kuvuliwa uanachama.

Kesi hiyo ya kikatiba imefunguliwa leo na wapiga kura watatu wa jimbo ambao ni wanachama wa tofauti kwa niaba ya wananchi wengine wa jimbo hilo dhidi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Walalamikaji wanaowakilishwa na Kampuni ya uwakili ya Mpoki & Associates, ni Juma Shaban Nzengula (CCM), Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM Kigoma kata ya Nguruka, Patrick Haruna Rubilo (NCCR-Mageuzi), mjumbe wa Kata ya Itebula na Mwenyekiti wa Kijiji cha Bweru na Fanueli Misigalo Bihole ambaye ni mwanachama wa Chama cha Wananchi (CUF) ni Katibu wa wazazi wa Kata ya Mtegowanoti.

Wanalalamikia kifungu hicho kinakiuka haki za msingi katika Ibara ya 21 ya Katiba inayotoa uhuru wa kushiriki katika shughuli za umma kupitia wawakilishi waliochaguliwa na wananchi kwa mujibu wa sheria.

Aidha Ibara hiyo inakiuka Mkataba wa Kimataifa wa Haki za Binadamu ambao Tanzania imeuridhia na kuusaini.

Mbali na hayo inakiuka Ibara ya 201 (1) ya Katiba ya Nchi inayotoa uhuru kwa wananchi kushiriki na kutoa maoni yao kwa uwazi. Nje ya mahakama walidai kuwa kesi hiyo wamefungua kwa niaba ya wapiga kura wa jimbo la Kigoma Kusini baada ya kuona wimbi la kufukuzwa uanachama wabunge lililoingia sasahivi baada ya mbunge wao, Kafulila kufukuzwa NCCR na sasa mbunge wa Wawi Zanzibar (CUF), Hamad Rashid kufukuzwa.

Wakizungumza baada ya kufungua kesi hiyo, walalamikaji hao walisema kwamba wameamua kufungua kesi hiyo liocha ya kwamba wanatoka vyama tofauti kwa kuwa mbunge huo hakuchaguliwa na wanachama wa NCCR-Mageuzi tu bali na wa vyama vingine pia.

Walisema mbunge anakuwa ametoa ahadi nyingi baada ya kuchaguliwa, na sasa ni kipindi cha kutekeleza ikiwa ni pamoja na shunguli mbalimbali za maendeleo na hivyo ni kurudisha maendeleo nyuma.

Kwa upande wake Rubilo alisema kuwa mbunge anafunga mkataba na wananchi na kwamba huwa wanatoa ahadi nyingi katika kutekeleza mkataba huo kama vile kusomesha watoto na shughuli nyingine za maendeleo.

Tatizo hapa ni siasa za mikakati na mbinu za kila namna kuhakikisha mwisho wa siku mtu wa mikakati toka ndani ya system anabaki kuwa mbunge ili PLAN 'A' iendelee kama ilivyokwisha semwa hapo awali.

Kama suala ni mgogoro wa vifungu tajwa kikatiba,je kwa nini tatizo hili halikuonekana hapo awali japo si mara ya kwanza jambo hili kutokea.
Mchungaji mtikila alikwisha liona hili na akachukuwa hatua husika kama mzalendo a nchi hii lakini alipuuzwa sasa leo linarudi tena.
Nafikiri ni mtihani mwingine kwa mhimili wa kisheria nchini.
 
Back
Top Bottom