Haki nisaidieni hapa! Huyu binti yangu..............

Eeka Mangi

JF-Expert Member
Jul 27, 2008
3,173
481
Jambo wote JF,
Msichoke kusoma! Nahitaji msaada!
Ndugu naombeni msaada wenu. Wakati fulani huko miaka ya nyuma, niliwahi kuoa mdada mmoja mkenya. Tuliishi kwa miaka 7.

Katika ndoa yetu ambayo haikuwahi kuwa na baraka za Paroko tulibahatika kupata mabinti 2. Wa kwanza alizaliwa 1990 na wa pili 1995. Tulikorofishana naye 1996. Kipato changu hakikuwa kinatosha. Nilikuwa najilipia shule na wakati huo huo kuhudumia familia. aliondoka na kurudi kwao kwa madai hakuzoea shida. Wakati huo nilikuwa naishi Dar. Aliondoka na watoto wote. Yule wa kwanza alipofika darasa la 7 akaleta ukorofi (kwa madai ya mama yake) ikabidi niende kwao Nairobi na kwa kuongea na binti ilibidi niondoke naye na kumtafutia shule huku.

Alipata shule na sasa yuko high school. Shida sasa! Huyu mdogo naye kamaliza 8, hakupata alama za kutosha kujiunga na form 1. Mama yake kanipigia simu kuwa mtoto hakufanya vizuri. Tukakubaliana atafute shule huko na mimi nitafute atakayefanikiwa basi aende shule.

Taarifa hizi ni tangu 28th Dec 10. Nilihangaika kwa kweli, sijui yeye kama alikuwa anahangaika! Last week nikapata shule fulani ya kanisa katoliki. Nikamwambia, kwanza hakutaka aende lakini baada ya kuhimiza sana akasema hana muda wa kumpeleka. Ikabidi nikatize safari yangu na kwenda NRB kumchukua.

Nikampeleka shuleni na kwa bahati akafanya vizuri. Wale masista wa pale wakanambia nikalipe ada na ikifika J2 nihakikishe nampeleka mtoto shule. Nilikiwa njiani nikamjulisha huyu mama kuwa mtoto anatakiwa shule jumapili. Akaanza oooh ni mapema sana na mimi nilikuwa na mipango ya shule, mara sijui huyu mtoto kakulia kwenye maadili ya kiislamu umempeleka shule ya kikristu. Nilikasirika na kukata simu.

Binti alikubali kusoma pale. Kesho yake nikampigia simu kuwa naenda kulipa ada akanung'unika sana mwisho akanambia sawa nenda kalipe. Nikaenda kulipa shs 1,438,000/= acha mahitaji mengine. Kumbe huku nyuma akampigia simu mtoto aombe kwenda kuchukua baadhi ya vitu vyake. Kwa nia njema kabisa nikamkubalia.

Kufika jioni akanipigia simu kuwa amepata shule huko kenya na ada ni shs 55,000/= kwa muhula. Kwanza niliduwaa halafu nikamuuliza zile ambazo nimeshalipa inakuwaje? Alichonambia hiyo itabidi iwe hasara. Nikamwambia kuwa hayo ni masihara.

Nilimtaka ahakikishe kuwa leo Jumamosi tarehe 22/1/11 kuwa mtoto anakuwa hapa kwangu ili nimpeleke shule Kesho. Niandikapo ujumbe huu SIJAONA HATA ALAMA YA HUYU BINTI YANGU KUJA. Na mbaya zaidi hata simu zao hazipatikani.

Nifanyeje jamani, shida sio hasara ila ile munkari alokuwa naye ya kusoma hapa kwetu Tanzania na ndoto alizokuwa nazo kwa kipindi kifupi nilichokaa nacho ndo kinanitesa.

Jamani nisaidieni ushauri.
 
Pole sana kaka yangu, mimi sio mtaalam wa kushauri, lakini nakusii usikate tamaa. Endelea kusisitiza tu mtoto arejeshwe TZ.

Sometimes maisha yanaweza kwenda kinyume kabisa na matarajio yetu.
 
Kha pole sana mkuu, ukweli imenihuzunisha sana, lakini mbona huyo mzazi mwenzio anafanya mambo ya kigaidi sana?
 
Pole saana,Hakika yahuzunisha saana.
Imenihuzunisha ila am sure subiri wataalamu hapa jamvini utashaurika na kupewa njia bora za utatuzi wa jambo hili kiujumla bali pia kukuweka sawa KISAIKOLOJIA.
Pole mkuu.
 
Kaka huyo mama anataka kukutumia, maana anajua hana nafasi nyingine zaidi ya hiyo, pia anajua baada ya kuwachukua watoto wote hutakuwa na habari nae tena, au anaweza asiwaone tena.

Kubaliana nae, then sasa na yeye atoe mchango katika kumsomesha huyo mdogo, maana ye sikaona uliyotafuta wewe haifai, mwache amsomeshe kama anaweza.
 
mmmh inasikitisha,na pole sana.ingawa simu haipatikani,jee huwafahamu ndugu zake?ipo siku atakutafuta tena tu,ni kama ana ku use tu huyo mama.mara nyingi w.ume huwa na matatizo,lakini na w.ke nasi tuna mapungufu yetu.
 
Pole mkuu. Hiyo ada ya shs 55,000/= kwa muhula pesa ya Kitanzania au ya Kikenya? Whether or not mama anamtumia mtoto as a "battlefield" and "ammunition" cha muhimu hapo ni kuangalia future ya mtoto. Her mother may simply do not realise the damage she is doing to her child. Or may be she is worried that she might loose both of her children. But this is merely my assumption because we don't know her story yet. Hata hivyo, a child is not a piece of property which can be parcelled up and moved around at will. For the best interests of the child, mnabidi mkae chini mjadili na kufikia makubaliano.

Nina imani kuna wadau hapa watakuwa na ushauri mzuri juu ya nini cha kufanya. Ila mkuu punguza jazba na hasira wakati ukideal na hili jambo. It is not your fault. You did all the best you could.
 
Cha Muhimu ni kukazana na kuhakikisha watoto wako wanasoma hata afanye nini ajue watoto Baba yao ni wewe na wewe unesha mchango wako kama baba hiyo uliyolipa usijali ila hakikisha kweli amepata shule?

Maana hapo alitaka labda utume pesa ili nae zimsaidie. Pole sana
 
hao ndo wakenya bana wana roho ka wanafanya kazi kiwanda cha sumu......kaka fanya nenda nrb ukajue mbichi na mbivu
 
Hakikisha watoto wanarudi kwako na kuwalea mwenyewe, otherwise atakuingiza mjini tu, maana hana uchungu na maisha yako!
 
Kaka huyo mama anataka kukutumia, maana anajua hana nafasi nyingine zaidi ya hiyo, pia anajua baada ya kuwachukua watoto wote hutakuwa na habari nae tena, au anaweza asiwaone tena.

Kubaliana nae, then sasa na yeye atoe mchango katika kumsomesha huyo mdogo, maana ye sikaona uliyotafuta wewe haifai, mwache amsomeshe kama anaweza.

Hili ni wazo la busara kabisa, najua anamg'ang'ania huyo mtoto ili aendelee kuchuma noti zako... mpe masharti ili muende sawa, akija kusoma shule ulomtafutia majukumu yote yatakuwa juu yako akimng'ang'ania ampe kila kitu yeye.... ninauhakika akijua kuwa hatopata tena minoti kutoka kwako atamrejesha mtoto asome huko ulikomtafutia.....
 
Wakenya Wana roho za kinyama sana, labda kutokana na maisha yao ya kikatili. Wengi sana wanaolewa tz ili wapate kupata ajira au maisha mazuri na siyo mapenzi.

Nadhani alipoona mambo yako hayajatulia kwa wakati huo akaona siyo bahati yake. Inawezekana kitendo cha hali yako kuimarika sasa anataka kurejea. Amegundua akiachia watoto wote uwezekano wa kurudi haupo. Hebu jaribu kumwita aje na mtoto uone.

Pole pia
 
kwa ujumla huyo mama anataka kumtumia binti kupata pesa kutoka kwako. Kwanza usiseme hasara ya 1.4 m na nafasi ya shule eti sio shida, nooo! We usichoke, nenda waombe radhi shuleni ili wakuvumilie kwa muda atakao kuwa hajaripoti halafu nenda kenya ongea nao wote kwa upole uwashawishi.

Kama mama na mtoto watakataa kuja kusoma tz, basi mwachie mama asomeshe mwenyewe! Amini usiamini mtoto ambae hujamlea wala kumgharamia malezi hawezi kukuthamini wala hawezi kuwa na faida kwako!

Akisoma kenya hatajua umuhimu wako kama baba! Komaaa aje TZ ikishindikana kabisa potezea usife kwa presha!
 
Kwa jinsi nilivyoisma hii habari nimehisi kuwa unatumia hasira sana wakati wa kujadiliana na huyo mkeo, pia nimehisi kuwa bado mna bifu naye na kuna kudharauliana baina yenu. Inawezekana kwa sababu hiyo basi anaamua kukukomoa kwa kutothamini mawazo yake..

Ushauri wangu ni: usikate tamaa na wala usi-panic wakati unafuatilia hili suala, fanya uchunguzi ili ujue kuhusu shule aliyopelekwa huyo binti na mama yake, kama unaona ina sifa nzuri basi unaweza kumwacha aendelee kubakia huko na uwe unamsapoti direct bila kupitia kwa mama yake, ikiwezekana mfungulie akaunti na uwe unamwekea pesa za matumizi bila kuzipitisha kwa mama yake. Ukiridhishwa na hiyo shule basi unaweza kwenda kudai ada yako kwenye hiy sule ya nyumbani ambayo nina matumaini kuwa watakuelewa na watakurejeshea pesa yako...

Pia jaribu kukaa chini na huyo mama watoto wako na mjaribu kuziondoa tofauti zenu, hii ni kwa mustakabali wa hao watoto wenu ili wasije kuathirika kutokana na ugomvi wa wazazi wao.
 
Kaka pole sana, ila tumia taratibu za kisheria coz the girl z over 7yrs. But the woman seem she dont know the negative impacts of her parenting style . The best thing you can do is to apply dictatorship so that she wont keep playing with you. I think your too polite bro.

Tuliusiwa tukae nao kwao akili. Lakin haijafafanuliwa kuwa ni akili ya namna gani.! Mbona anachezea hela yako? By the way, what is she doing in Nairobi? But don gv up, ask God if you have a FAITH on him, all the best Mkuu
 
Sio wakenya Tu wapo hata Watanzania wenye roho hizo pia

Unamfahamu mwanamke wa kikenya aliyebahatika kulazimisha ndoa na mtz? Kama hayajakukuta basi fanya utafiti bwana. Hawana mapenzi ya ngono Bali ya mali. Akishaolewa anawaunganisha ndugu na rafiki zake kuja tz kutafuta kazi na maslahi. Wengi hujifanya ni wajaluo wa tz, hufoji vyeti vya kuzaliwa na kuchukua Pasport za tz haraka.

Wapo wengi mno, serikali yetu inachekacheka tu
 
Back
Top Bottom