Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,884
- 6,885
Tumekuwa na kawaida ya kulaumu tu bila kuangalia sheria ambazo huongozwa na sheriamama ambayo ni katiba ya nchi. Katiba ya nchi haikatazi ushoga, bali inakazia haki za msingi za uhuru wa kila binadamu.
Mashoga wapo wengi tu gays/lesbians na tunawaona kila siku na sheria inawalinda kama raia wenye haki ya kupata maisha, ajira na haki nyingine kwa msingi wa haki za binadamu.
Wanaopinga baadhi tumewaendekeza binti kujinafsisha kama lesbians kwa ajili ya kulinda ubikira wao ili waolewapo waonekana wako fresh. Hayo yako karibu mabara yote duniani.
Leo mambo haya huongelea na kuonekana hadharani na kwa uwazi sababu ya mawasiliano kuwa rahisi, lakini wakati huo yatokeayo kijiji fulani waliokuwa wanayafahamu na hao na yaliishia kwao. Ni dalili wazi mambo haya yapo.
Tunachopaswa kukemea ni kuwalea vijana kujiepusha na vitendo hivyo na kukemea kwamba utamaduni huo sio mzuri kwa vile si mpango wa Mungu katika kushiriki uumbaji wake. Kwa waliokwisha athirika na mfumo huo hakuna njia nyingine ya kuwatema katika jamii kwa vile wana haki za msingi kama binadamu na hata haki ya kupata huduma za kijamii na ajira ni halali yao.
Gay and Lesbian Rights
Mashoga wapo wengi tu gays/lesbians na tunawaona kila siku na sheria inawalinda kama raia wenye haki ya kupata maisha, ajira na haki nyingine kwa msingi wa haki za binadamu.
Wanaopinga baadhi tumewaendekeza binti kujinafsisha kama lesbians kwa ajili ya kulinda ubikira wao ili waolewapo waonekana wako fresh. Hayo yako karibu mabara yote duniani.
Leo mambo haya huongelea na kuonekana hadharani na kwa uwazi sababu ya mawasiliano kuwa rahisi, lakini wakati huo yatokeayo kijiji fulani waliokuwa wanayafahamu na hao na yaliishia kwao. Ni dalili wazi mambo haya yapo.
Tunachopaswa kukemea ni kuwalea vijana kujiepusha na vitendo hivyo na kukemea kwamba utamaduni huo sio mzuri kwa vile si mpango wa Mungu katika kushiriki uumbaji wake. Kwa waliokwisha athirika na mfumo huo hakuna njia nyingine ya kuwatema katika jamii kwa vile wana haki za msingi kama binadamu na hata haki ya kupata huduma za kijamii na ajira ni halali yao.
Gay and Lesbian Rights