Haki Inadaiwa Bila Kujua Wajibu?

Haika

JF-Expert Member
Mar 3, 2008
2,348
559
Naomba msaada,

Kila mara nasikia wanaharakati wa watoto wanadai haki za hao watoto. Wanatumia hela nyingi sana za wafadhili kuzitetea.

Mimi nilivyolelewa nilifundishwa wajibu wangu kwangu, kwa familia na kwa jumuiya nzima kwa ujumla. Pamoja na hayo pia lilikuwa jukumu la mzazi wangu kuilinda haki yangu. sina uhakika kama alifanya kama inavyotakiwa, ila namshukuru sana.

Sasa hawa wenzetu mimi wananikwaza pale wanapotumia muda mwingi na kupoteza miaka ya watot kuacha kuwahimiza wajibu wao.

Kizazi kijacho kitakuwa cha watu wazima wenye kudai kufanyiwa tu? kufanya atafanya nani?

mfano kusha vyombo nyumbani, inakuwaje vyombo vioshwe na nani? Huyo binti atafundishwa kusha vyombo wakati wa likizo tu? (kama haendi tuisheni)
 
Back
Top Bottom