Mimi si miongoni mwa watu ambao nimepata kutokukubaliana na tangazo lolote la HakiElimu! Hata hivyo, lazima nikiri wazi kwamba wadau wa Elimu Lindi wamenena, na sasa kazi kwenu HakiElimu kuifanyia kazi kauli yao! Kwa mujibu wa wadau wa Elimu Mjini Lindi, ni kwamba matangazo ya HakiElimu inaangalia upande mmoja na kusahau upande mwingine wa shilingi! Madai mara kwa mara yamekuwa yakitolewa na wadau wa kila aina kwa nyakati tofauti kulingana na dhima ya tangazo husika! Mathalani, serikali imeshawahi kuyalalamikia matangazo hayo pale yanapoonekana kuisakama zaidi serikali! Lakini wadau wa Elimu Mjini Lindi wanauliza kulikoni HakiElimu kusahau upande wa pili wa shilingi ambao ni WANAFUNZI WENYEWE?! Wadau hawa wanauliza, je ni kweli WANAFUNZI/VIJANA WETU wanafahamu wajibu wao wa kuwa wanafunzi? Je, HakiElimu wanafahamu kwamba kuna wanafunzi kibao wanatoka home wakielekea shule lakini wanaishia chimbo( hawaingii darasani)! Unaweza kumlamu, lakini what abt mzazi sawa na wazazi wetu wengi?! Kuna mtoto wa kaka yangu ambae ni miongoni mwa wanafunzi ambao bado hawajui wajibu wao!! Baada ya kumuona kazidisha usela, nikamlazimisha anioneshe matokeo yake shule. Ktk matokeo ya Form II, dogo kakunguta C moja na zilizobaki ni D chache na F!!!!! Ni form II huyo!! Mimi sikai pamoja na familia hii, lakini nilipohulizia pale kwao nikakuta kumbe mama mtu anafuatilia sana maendeleo ya mwanae- na kwa kauli yake mwenyewe shemeji yangu akaniambia mimi mara kwa mara huwa naenda shuleni kwao kuulizia maendeleo yake na wananiambia kwamba hakosi shule na maendeleo yake darasani ni mazuri! Shemeji yangu anaamini kwamba maendeleo ya kijana wake ni mazuri-ni mbaya zaidi hata akiyaona hayo matokeao hawezi kuelewa what is all about C, D, or F! Hawa ndio wazazi wengi wa wanafunzi wetu wa mjini na vijijini!Wazazi wengi wa aina hii wanachojali ni mwanafunzi kwenda shuleni; hiyo ndio kusema mtoto anaendelea vizuri! Je, HakiElimu mnaliangalia vp suala hili?! Serikali ishakumbushwa sana, kama wana masikio wamesikia na kama hawana basi mtaendelea kupoteza resources bure ingawaje ni wajibu kukumbushana. Ni wakati umefika sasa kuwakumbusha na wanafunzi kufahamu wajibu wao wa kuwa shule. Kila penye haki, lazima pawe na wajibu. Mmejitahidi kutetea haki za wanafunzi, sasa wakumbusheni wajibu wao ili badala ya kuwaona ni WATETEZI WAO sasa wawaone ni WAPIGANAJI WA MAENDELEO YAO YA ELIMU. Hata kama tutakuwa na maabara kama za New York au Tokyo! Hata kama tukipata best teachers kuliko wengine wowote duniani! Hata kama kila mwanafunzi atapatiwa Helikopta ya kumpeleka shuleni! Hata kama kila mwalimu atajengewa kasri lake na kupewa Benzi la kumfikisha shuleni! Hata kama akina Issack Newton, Archimedes, Einstein wakifufuka na kuja kufundisha shule zetu; bado itakuwa ni sawa na hakuna endapo bado wanafunzi hawafahamu wajibu wao!