Wakuu,wiki iliyopita nilipost thread hapa ya baadhi ya mambo yanayotufanye tuwe dhalili na kuonekana duni mbele ya wageni wanaoishi ndani na nje ya Nchi.
Kwa bahati mbaya sana thread hiyo haikukaa hata dk 5 hapa JF.
Nilikuwa na nia njema tu, tuangalie, tujitafakari na kujipanga upya ili tusonge mbele.
Leo, langu ni dogo tu. Ingekuwa vema iwapo wanaotunza diary za wakubwa na wana nafasi za kushauri waangalie uwezekano wa kufanya ziara za kimkakati Nje ya Nchi na sio ziara za kuhudhuria hafla, parties, birthdays na nyinginezo eti kwa sababu tu umepata mualiko!
Huku ni kujidhalilisha na kupunguza nguvu uzito wa ofisi tulizopewa dhamana ya kuziongoza.
Ziara za kimkakati zinakuwa na malengo mahsusi ya kitu unachoenda kufanya na zinalenga kuvuta uwekezaji wa kudumu wa kimaendeleo katika nyanja mbalimbali kama vile elimu, afya, barabara, maji, n.k.
Ziara za namna hii, zinakwenda kwa mpangilio maalum na mapitio kila baada ya muda fulani. Tuentendee haki Nchi yetu!
Kwa bahati mbaya sana thread hiyo haikukaa hata dk 5 hapa JF.
Nilikuwa na nia njema tu, tuangalie, tujitafakari na kujipanga upya ili tusonge mbele.
Leo, langu ni dogo tu. Ingekuwa vema iwapo wanaotunza diary za wakubwa na wana nafasi za kushauri waangalie uwezekano wa kufanya ziara za kimkakati Nje ya Nchi na sio ziara za kuhudhuria hafla, parties, birthdays na nyinginezo eti kwa sababu tu umepata mualiko!
Huku ni kujidhalilisha na kupunguza nguvu uzito wa ofisi tulizopewa dhamana ya kuziongoza.
Ziara za kimkakati zinakuwa na malengo mahsusi ya kitu unachoenda kufanya na zinalenga kuvuta uwekezaji wa kudumu wa kimaendeleo katika nyanja mbalimbali kama vile elimu, afya, barabara, maji, n.k.
Ziara za namna hii, zinakwenda kwa mpangilio maalum na mapitio kila baada ya muda fulani. Tuentendee haki Nchi yetu!