Haiti Ex-President Aristide afanya promotion ya Kiswahili

Tiba

JF-Expert Member
Jul 15, 2008
4,604
3,163
Wana JF,

Naomba mniruhusu niwashirikishe kitu kimoja kilichonifurahisha jioni ya leo. Nimepata bahati ya kupelekwa Haiti na moja ya mashirika yasiyokuwa ya kiserikali kwa ajili ya kuangalia mwenendo wa uchaguzi. Uchaguzi huo umefanyika leo tarehe 20 March 2011 na mimi niko hapa Port-Au-Prince Haiti kuanzia tarehe 15 March 2011. Juzi tarehe 18 Rais wa zamani Jean Betrand Aristide alirudi Haiti baada ya kukaa uhamishoni kwa muda wa takribani miaka 7. Alipoingia mjini Port-Au-Prince kila kitu kilisimama kwani trafiki jam ilikuwa kubwa na watu walishindwa kuwahi kwenye shughuli zao.

Jioni ya leo baada ya kushuhudia uchaguzi ulivyokwenda, nilirudi hotelini kwangu na nikiwa chumbani nilifungulia TV channel 18 ambako walikuwa wanaonyesha mapokezi ya kiongozi huyu wa nchi wa wazamani. Akiwa pale airport alipewa nafasi ya kuzungumza na waandishi wa habari na kwenye hotuba yake alitumia lugha mchanganyiko kama kifaransa, kiingereza, kispanish, creory na cha kufurahisha zaidi alitumia pia kiswahili. Alisema "umoja ni nguvu na utengano ni udhaifu na mtu ni watu" kwa kweli nilikunwa sana na maneno yake haya ya kiswahili na nilijikuta napiga makofi kabla ya kugundua kwamba niko peke yangu chumbani.

Mkubwa huyu amepromote kiswahili, je sisi kama watanzania tunachukua hatua gani kuhakikisha lugha hii inaendelea kutambuliwa kimataifa?

Tujadili.

Tiba
 
Very Good alijifunza alipokuwa Padre, ni mzuri sana na watu wanampenda Marekani tu ndiyo inamchukia. Tanzania imepata nafasi ya kuendeleza kiswahili bure na tumeshindwa.
1. Wakimbizi walikuwa hapa na hatukuwafundisha
2. Redio za nje nyingi zimejitahidi sana lakini viongozi wetu wanaziona wakati wa uchaguzi
3.Mashirika ya dini ynafanya kazi kubwa lakini viongozi wa serikali wanawabeza.
5.
6.
7.
 
Kiswahili kina soko sana ni sisi tu ndio tunakidharau. Kenya wenzetu hawakijui vizuri lakini wamekigeuza mtaji huko ughaibuni.
 
Lugha ya Kiswahili kwa Taifa letu si tuu ni alama yetu bali pia kwa National security ni njia nzuri sana. Kwa mfano nilitarajia waziri wa mambo ya nje aishauri serikali itoe scholarship kuanzia hata 500 kila mwaka kwa wanafunzi wanaotaka kusoma kiswahili UDSM na vyuo vingine nchini kutoka mataifa jirani kama Rwanda,Burundi,DRC,Kenya na Uganda bila kuwasahau na akina Zambia,Zimbabwe,Malawi na South Afrika.

Ingekuwa bonge ya goal na sio upuuzi wa kila siku mambo ya nje wazirii kulaumu mataifa ya magharibi kufadhili chama asichokitajaaa..na dual citzenship..cheap issue!! Lol
 
Very Good alijifunza alipokuwa Padre, ni mzuri sana na watu wanampenda Marekani tu ndiyo inamchukia. Tanzania imepata nafasi ya kuendeleza kiswahili bure na tumeshindwa.
1. Wakimbizi walikuwa hapa na hatukuwafundisha
2. Redio za nje nyingi zimejitahidi sana lakini viongozi wetu wanaziona wakati wa uchaguzi
3.Mashirika ya dini ynafanya kazi kubwa lakini viongozi wa serikali wanawabeza.
5.
6.
7.

Yes huyu Bwana ni muasi wa kanisa katoliki kama alivyo Dr.Slaa. Aliasi kazi ya upadri na kuingia kwenye siasa. Kwa sasa ana watoto wawili mabinti wazuri tu. Ni kweli raia wa hapa wanampenda na wengi hawajui mpaka leo kwanini Marekani ikishirikiana na ufaransa walimwondoa madarakani.

Tiba
 
Lugha ya Kiswahili kwa Taifa letu si tuu ni alama yetu bali pia kwa National security ni njia nzuri sana. Kwa mfano nilitarajia waziri wa mambo ya nje aishauri serikali itoe scholarship kuanzia hata 500 kila mwaka kwa wanafunzi wanaotaka kusoma kiswahili UDSM na vyuo vingine nchini kutoka mataifa jirani kama Rwanda,Burundi,DRC,Kenya na Uganda bila kuwasahau na akina Zambia,Zimbabwe,Malawi na South Afrika.

Ingekuwa bonge ya goal na sio upuuzi wa kila siku mambo ya nje wazirii kulaumu mataifa ya magharibi kufadhili chama asichokitajaaa..na dual citzenship..cheap issue!! Lol

Mkuu hapa tuko pamoja. Kuna haja ya kufanya juhudi za makusudi serikali kutoa scholarship kwa wazungu waje kujifunza kiswahili kama sisi tunavyojifunza kiingereza, kifaransa, kireno na lugha nyinginezo. Matunda ya mpango huu tunaweza kuja kuyafaidi baadae!!!

Tiba
 
Back
Top Bottom