Waziri mkuu alitangaza bungeni serikali kukabiliwa na ukata wa hela!Amezitaka Wizara na taasisi mbalimbali kubana matumizi kwa chochote watakachopata(kama wakibahatika kupata)
- Zito aliwahi kusema serikali imeishiwa na Waziri wa fedha Mustafa Mkulo kumkatalia na kumwambia ni muongo! NAFIKIRI NI WAKATI MUAFAKA WA MKULO KUWAJIBIKA NA KUJIUZULU KATIKA HILI.
- Kila mfanyakazi iwe wa UMMA au sekta binafsi anakatwa kodi kulingana na mshahara wake."THE HIGHER THE SALARY THE HIGHER THE TAX"Ni hela nyingi sanaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa!
- Kila mkulima na mfanyakazi analipa kodi katika kila bidhaa anayoinunua apende asipende. Ni hela Nyingi sanaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa
- TRA imekuwa ikisifika kwa makusanyo makubwa hivi karibuni. Zinakwenda wapi?
- Vipi kuhusu vyanzo vingine vya mapato kama madini mbalimbali,mbuga za wanyama,ardhi kubwa na yenye rutuba pamoja rasilimali zingine nyingi...............
- Wakati huo huo watu wenye kipato kidogo kama walimu,manesi,maaskari na nk wanakatwa kodi wakati kuna mijitu yenye kipato kikubwa na inakwepa huku huku walikindwa na kukumbatiwa na serikali.........?
- Ripoti ya mkaguzi mkuu wa serikali imethitisha matumizi mabaya ya fedha katika halmashauri nyingi nchini.HELA ZA KUTOA RUSHWA KATIKA CHAGUZI MBALIMBALI ZINAPATIKANA,MAFISADI WANAKUMBATIWA!KWA KWELI SIELEWI!
- NATAMANI MSHAHARA WANGU USIKWATWE KODI TENA MAANA SIONI UMUHIMU WAKE
- TUACHE USHABIKI NA TUTANGULIZE UZALENDO.TUFANYE MABADILIKO YA DHATI.