Siku za karibuni mume wangu kipenzi, al aziz, nuru ya macho yangu kwa siku tofauti amekuwa akisumbuliwa na magonjwa kama vile tumbo, homa, kichwa, malaria na siku nyingine uchovu uliopindukia. Haya yote yalisababisha dia wangu arudi nyumbani kupumzika. Pamoja na hayo ufanisi wake kiunyumba ulikuwa umelegalega. Pia amebadilika tabia na kuwa mtulivu nyumbani, hata kutoka toka weekends au nyakati za jioni anapokuwa fit, amepunguza kama sio kuacha kabisaaa. Nilimshukuru Mungu kwa kumtuliza mwenzangu huyu nyumbani, kwani kutokatoka nako kuna mengi.
Jana majira ya saa saba mchana nilipokea simu toka kwa mume wangu, barafu wa moyo wangu kuniarifu kuwa anaumwa sana, na amekwenda hospitali kapimwa na kugundulika ana malaria. Kwa jinsi anavyojisikia vibaya inambidi arudi nyumbani mida ile ile nyumbani kupumzika. Aliniambia nipitie duka la dawa nimnunulie dawa alizonitajia. Nilisikitika sana na hizi homa zinazomsumbua baba watoto wangu, ikanibidi niondoke kazini muda ule ule, nipitie duka la dawa na kuanza safari ya kurudi nyumbani kumliwaza.
Nilipofika nyumbani, niligonga sana geti, halikufunguliwa. Niliomba msaada kwa kijana wa jirani akapanda ukuta na kunisaidia kufungua geti kwa ndani. Nyumbani palikuwa kimya mno, gari ya mwenzangu ilikuwepo, na msaidizi wa kike wa kazi za nyumbani sikumuona kama nilivyotarajia na nyumba ilikuwa imefugwa. Jasho lilinitoka kuwa labda mpenzi baba wa watoto wangu kazidiwa na kupelekwa hospitali au hata ameshaaga dunia nikirejea alivyokuwa akilalamika kuumwa sana. Nilipiga simu yake ya mkononi haikupokelewa, ya msichana wa kazi haikupokelewa pia.
Nikazidi kuchanganyikiwa nianze kufanya nini na nianzie wapi. Nifungua nyumba kwa funguo zangu, nikaenda chumbani kwa binti hayupo, kwa watoto hakuna mtu. Mwisho nikaingia chumbani kwangu. Nikaingia chumbani kwangu......nilichokiona sikuamini. Nikatoka na kwenda kumwita jirani yangu alisaidie kuangalia pengine angeelewa. Jirani yangu kidogo azimie.... mume wangu na msaidizi wangu wa nyumbani walikuwa wamelala fofofo kitandani kwetu, wakiwa kama walivyozaliwa!
Naomba niishie hapa.
Jana majira ya saa saba mchana nilipokea simu toka kwa mume wangu, barafu wa moyo wangu kuniarifu kuwa anaumwa sana, na amekwenda hospitali kapimwa na kugundulika ana malaria. Kwa jinsi anavyojisikia vibaya inambidi arudi nyumbani mida ile ile nyumbani kupumzika. Aliniambia nipitie duka la dawa nimnunulie dawa alizonitajia. Nilisikitika sana na hizi homa zinazomsumbua baba watoto wangu, ikanibidi niondoke kazini muda ule ule, nipitie duka la dawa na kuanza safari ya kurudi nyumbani kumliwaza.
Nilipofika nyumbani, niligonga sana geti, halikufunguliwa. Niliomba msaada kwa kijana wa jirani akapanda ukuta na kunisaidia kufungua geti kwa ndani. Nyumbani palikuwa kimya mno, gari ya mwenzangu ilikuwepo, na msaidizi wa kike wa kazi za nyumbani sikumuona kama nilivyotarajia na nyumba ilikuwa imefugwa. Jasho lilinitoka kuwa labda mpenzi baba wa watoto wangu kazidiwa na kupelekwa hospitali au hata ameshaaga dunia nikirejea alivyokuwa akilalamika kuumwa sana. Nilipiga simu yake ya mkononi haikupokelewa, ya msichana wa kazi haikupokelewa pia.
Nikazidi kuchanganyikiwa nianze kufanya nini na nianzie wapi. Nifungua nyumba kwa funguo zangu, nikaenda chumbani kwa binti hayupo, kwa watoto hakuna mtu. Mwisho nikaingia chumbani kwangu. Nikaingia chumbani kwangu......nilichokiona sikuamini. Nikatoka na kwenda kumwita jirani yangu alisaidie kuangalia pengine angeelewa. Jirani yangu kidogo azimie.... mume wangu na msaidizi wangu wa nyumbani walikuwa wamelala fofofo kitandani kwetu, wakiwa kama walivyozaliwa!
Naomba niishie hapa.