figganigga
JF-Expert Member
- Oct 17, 2010
- 25,492
- 54,890
Hapo zamani kuku na mwewe walikuwa marafiki. Siku moja kuku akaenda kuazima sindano ya kushona nguo kwa mwewe iliyokuwa ikitumiwa na ukoo mzima wa mwewe.
Kwa bahati mbaya ile sindano ikapotea. Mwewe alikasirika sana akataka alipwe sindano yake ya ukoo la sivyo atajilipiza kwa kuchukua vifaranga vya kuku na kupeleka kwenye ukoo wake hadi sindano itakapo patikana. Ndo maana hadi leo kuku anatafuta sindano kwa kufukua fukua kila sehemu ili kuokoa kizazi chake.
Hadithi yangu inaishia hapo. Mia
Kwa bahati mbaya ile sindano ikapotea. Mwewe alikasirika sana akataka alipwe sindano yake ya ukoo la sivyo atajilipiza kwa kuchukua vifaranga vya kuku na kupeleka kwenye ukoo wake hadi sindano itakapo patikana. Ndo maana hadi leo kuku anatafuta sindano kwa kufukua fukua kila sehemu ili kuokoa kizazi chake.
Hadithi yangu inaishia hapo. Mia