Si siri tena kwamba Lowassa ana mkakati mkubwa wa kugombea urais kwa tiketi ya CCM. Na wale Thomases wajue kwamba hakuna atakayeweza kumzuia Lowassa kwa sasa. Malecela alikuwa na mikakati kama hii ila Nyerere alimwangalia machoni na kumwambia hafai. Je, ni nani katika CCM leo anaweza kumkemea Lowassa? Mashaka yangu ni kuwa kama alivyosema Mwalimu, mtu anayeitafuta sana ikulu kama alivyo Lowassa, atakuwa anatafuta maslahi binafsi na hivyo hatufai. Ila kwa upande mwingine angashinda Lowassa kwa tiketi ya CCM ningefurahi ili iwe rahisi zaidi kwa CDM kushinda maana itakuwa ngumu sana kumuuza!