Habari za afya ya Dr. Harrison Mwakyembe

Mshama wa SIKONGE?....


Wee Mkandara, imesemwa "ULIMI HAUNA MFUPA." Aja*u iko wapi?

Wengine hatuna mikononi herufi *. Kama Wafaransa vile. Ndiyo maana unaona mtu *a*ala ya kuitwa Yahya, anaamua hata kuiandika aache na kusema yeye ni YAYA TOURE.
Nimeshareke*isha, Asante.
 
Nsesi,

Sitaki kuendeleza malumbano. Ni ukweli mtupu kwamba Prof. alimuunga mkono Dr. Mwakyembe 2005. Lakini pia ni ukweli mtupu kwamba prof. sio mjinga hakutumbukiza kichwa kichwa kwenye siasa za Kyela kama ambavyo hakufanya kwenye siasa za Mbeya. Pia ni ukweli mtupu kwamba Prof. Mwandosya ni kingmaker wa siasa za mkoa wa Mbeya.

Pia ni ukwelui mtupu kwamba Kyela inategemea baadhi ya mambo toka Rungwe wakati ilitakiwa kuwa kinyume. Hali ya hewa ya Kyela ni nzuri zaidi lakini hata mboga za majani zinaletwa toka Rungwe.

Hapo mjini penyewe, biashara zimeshikwa na wageni wakati sisi wenyeji tunapiga domo. Hayo ndio mambo ya kushughulikia na sio kuelezea mapato ya halmashauri. Hayo mapato si yanaletwa na watu wanaochapa kazi wakiwemo wengi kutoka nje ya Kyela?

Unaweza kuukataa ukweli lakini ndio hivyo. Kyela tuko nyuma sana mkuu. Mimi naijua Kyela kuliko unavyodhani na inanisikitisha sana kuona huo umaskini wa kutisha huko vijijini wakati resources zipo kibao. Ninawaelewa vijana wa Kyela hapo mjini, ni maneno tu na majungu mengi ya kisiasa badala ya kuchangamkia kazi. Afadhali hata dada zetu angalau wameanza kuamka na kujifunza toka kwa wenzao wa Rungwe na kuanza kufanya vibiashara vyao.

Concern yangu Kyela ni maendeleo na wala sio mwanasiasa mmoja mmoja. Sio rafiki wa mwanasiasa yeyote lakini pia si adui wa mwanasiasa yeyote. Kwangu mimi Kyela ni kubwa kuliko mimi au kuliko mtu mwingine yeyote. Yeyote ambaye yuko tayari kukemea ujinga huo, mimi nitamuunga mkono.

hapo umesema. safi sana. japo ulivyoandika tangia mwanzo wa hii thread sikuungi mkono sana.
 
Raia Mwema,

...... Hivi mimi Mtanzania leo nikiandaa maandamano ya wahuni pale mjini na kuwapa pesa za soda kisha nikawaambia waseme ninachokitaka, mwandishi makini utachukulia hiyo kama wananchi wa Kyela wanaamini kwamba?

Mbona Raia Mwema ilikuja kwa nguvu zote na kupinga matatizo ya RAI, wakati na nyie mnaandika habari bila hata kufanya analysis? .............

ulivyoandika hapo juu ni wazi unapinga kuwa wananchi wa kyela walisema kilichoandikwa walisema.

kwa mujibu wa raia mwema source ya habari hiyo ni wananchi wa kyela. umejuaje kama ni uongo? umejuaje kama wahuni ndio walikusanywa na kusema kilichotakiwa kusemwa? we chanzo cha habari yako ni nani/nini?

unataka vichwani mwetu tujenge picha kuwa watu wa mwakyembe waliwaambia wahun waseme yaliyoandikwa. lakin for sure watu wasio wahuni wanaweza kutoa habari kama hizo kwa vyombo vya habari

au unataka kutuaminisha kuwa hamna watu wasio wahuni kyela wanaweza kutoa taarifa kama ile kwa vyombo vya habari?

mwakyembe anaweza kuwa na weaknesses nyingi sana. lakin usitake kutuaminisha kuwa ni wahuni tu ndio waliotoa habari kwa raia mwema (japo inawezekana)

kama ulivyosema somewhere - maendeleo ya watu kwanza
 
ulivyoandika hapo juu ni wazi unapinga kuwa wananchi wa kyela walisema kilichoandikwa walisema.

kwa mujibu wa raia mwema source ya habari hiyo ni wananchi wa kyela. umejuaje kama ni uongo? umejuaje kama wahuni ndio walikusanywa na kusema kilichotakiwa kusemwa? we chanzo cha habari yako ni nani/nini?

unataka vichwani mwetu tujenge picha kuwa watu wa mwakyembe waliwaambia wahun waseme yaliyoandikwa. lakin for sure watu wasio wahuni wanaweza kutoa habari kama hizo kwa vyombo vya habari

au unataka kutuaminisha kuwa hamna watu wasio wahuni kyela wanaweza kutoa taarifa kama ile kwa vyombo vya habari?

mwakyembe anaweza kuwa na weaknesses nyingi sana. lakin usitake kutuaminisha kuwa ni wahuni tu ndio waliotoa habari kwa raia mwema (japo inawezekana)

kama ulivyosema somewhere - maendeleo ya watu kwanza


Mwaka,
Naona wee hujambo kwa kuchukua mapande ya nyama mazima mazima na kuyameza bila kutafuna. Kama simba vile, unayabugia tu Mnyakyusa wee. Na wewe uko kwenye PAYROLL ya Mwakyembe? Naona huko Kyela mwakani kutawaka moto. Heri sisi Sikonge watu bado wamelala na watampa Kikwete kura asilimia 100%. Na mwisho Wakwere si watoto wetu?

Amesema kuwa mtu unaweza kuchukua watoto wa kihuni kadhaa na kuwapa hela ya soda. Wakakusanya watu kadhaa na kutoa risala. Ikiandikwa imesemwa na Wakyela, si itakuwa sawa? Hata kama wangelikuwa ni ndugu wa Mwakyembe tu na jirani zake, bado ni Wakyela. Sijui kama unaiona tofauti au nyie Wanyakyusa ni mbuzi fulani mnaopigiwa gitaa? Wanyakyusa bana. Njooni Sikonge mfundishwe kuwa wapole kama mnanyolewa.

Nakubaliana na kuwaonea wivu sana wenzetu kuwa hata mnagombana, mwisho mnasema "Naweka Kyela yangu mbele...." Sikonge hatujaanza kugombana bado. Tupo tu na ka-Uarabu ketu hatuna noma. Sijui nichukue tu SMG siku moja niwarushie watu angani waamke kutoka usingizini? Kila la kheri Kyela, tangulieni na sisi tupo nyum...... ahhh bega kwa bega.
 
Napenda sana watu wenye misimamo na maamuzi sahihi heko wana kyelana tarime...wengine je??unafiki tupu...mtaburuzwa hata mwisho wa dunia...
 
Nsesi na Ijabu Issa
Naona ubishi wenu hauna manufaa yeyote.Kila mmoja wenu anaongelea ushabiki tu.
Hapa kyela kuna waandishi wawili.Richad na Israel. Siku ya mkutano wa Mwakyembe, walikuwa pale kwenye Intenet cafe moja hapa kyela inaitwa DEMATE.Walikuwa pamoja na wandishi wa habari kutoka mbeya,ambao walialikwa na kamati ya huo mkutano wa mwakyembe

Moja ya mazungumzo yao ilikuwa wale waliotoka mkoani wakiwalazimisha wenzao wa kyela kwenda kwenye mkutano.
Hawa wa kyela walisema wamepata taarifa kutoka kwenye kamati ya maandalizi kuwa wao wasihudhulie huo mkutano.

Walisema watakwenda kama watazamaji wengine.Jamani ubishi wa nini?.Kama kuna mtu anataka kujua ukweli basi piga simu hii hapa ya mwandishi mmoja wao 0784431748.

Kwa mtazamo wangu mimi, nikiwa kama mwana kyela ni kwamba magazeti ya mengi yanampigia debe Mwakyembe.mfono ni siku ya jumatatu yake baada ya mkutano.Nipashe iliandika kuwa mwakyembe abebwa jimboni kwake.Hakuna aliye mbeba mwakyembe .Na hakukua na kiongozi yeyote wa ngazi za juu wilaya wa ccm aliyehudhulia mkutano huo.

Mwakyembe wakati yeye analaumu magazeti ya RA,Lakini yeye anatumia magazeti ya mengi kumfikishia taarifa za uongo.Hao wenye Richmond,wananchi wao wana unafuu kuliko huku kyela.Sasa hivi Hawezi kwenda Ipinda na Gari dogo.

Ni rahisi kwa mwakyembe kushinda ubunge wilaya yeyote kwa Dar kulikoni kushinda hapa kyela.Mwayembe anagawa watu,Mwakyembe anadharau watu,Mwayembe sio mkazi wa kyela.Hapa ni kama mtalii tu.Haishi hapa.

Ukiuliza,leo hii mwakyembe amefanya nini kyela,Utaambiwa kajenga daraja la Lusongo na hataki mafisadi.

Juzi hapa kwenye kikao cha halmashauri ya ccm wilaya ya kyela,Aliwatukana wajumbe kwa kuwaita wao ni kama mbuzi wanaosubiri awapeleke malishoni.Mwayembe hana groupwork.Alisema wamekuwa wakimuomba pesa mitaani na huku wanataka kumsaliti.

Hao anaowaita mafisadi,kule jimboni kwao,wananchi wao wanakula vizuri na wanakunywa maji safi na salama.

Hakuna siku unakuta ofisi ya mwakyembe imefunguliwa hapa kyela.Muda wote yuko Dar kwenye ofisi yake ya Uwakili.
Hapa kyela hana pa kuishi na hivyo anaishi GUEST HOUSE.Mara Stiva mara Pataya.

Jamaani acheni unafiki.Mwakyembe angeanzia wilayani na kwenda kitaifa.Kyela inakabiliwa na matitizo mengi sana na sio Ukimye tu.Huo mpunga wanakula miezi miwili tu umekwisha.Uwezi kulinganisha na Rungwe ata siku mmoja.Nafikiri ndiyo maana kila mara mawaziri wanatoka Rungwe na sio kyela.
 
Tunataka damu mpya.
Hawa akina Mwakyembe ningependa sana watupwe nje ya ulingo,mwanasiasa mzuri haendekezi malumbano ama chuki huwatakia maisha marefu adui zake.

Mimi nadhani hizi wanasiasa wanaodakia tuhuma za wenzao bila kuwafikisha wanaowatuhumu ktk vyombo vya sheria hao ni wahuni wanataka umaarufu na huruma kutoka kwa wananchi hawa wanahadaa hadhira yani wananchi kwa staili hiyo.

Kama Kweli Mwakyembe amepeleka maendeleo huko Kyela watuambie ni ktk maeneo yepi? kama sio maendeleo ya siasa majukwaaani.

Mimi naonelea hawa jamaa ni wakutupwa nje kabisa kuanzia Rais wabunge wote wa upinzani na ccm .
Mwakyembe naye nje siasa ktk njaa hatutaki sisi tunahitaji maendeleo mambo ya ufisadi wapelekee Takuru na mahakama pia uutoe huo ushaidi huko.
 
Mwakyembe hapa kyela hana pa kuishi na hivyo anaishi GUEST HOUSE.Mara Stiva mara Pataya.

Dr. Mwakyembe ana nyumba nzuri tu pale kijijini kwao Ikolo. Alijenga mwaka 2004/05 nafikiri wakati anajiandaa kugombea maana watu wangemwuliza kama walivyomwuliza Mpangala kule Mbeya kwamba utakuwa unakaa guest?

Nyumba hiyo iko kama km 5 toka mjini. Sijui kwanini anapendelea kukaa guest wakati ana nyumba yake ya maana kuliko hata baadhi ya hizo guests.

Niliona nisahihishe hilo la kwamba hana pa kuishi hapo Kyela.
 
Haya Samwel tumekusikia, Mwakyembe kweli hana nyumba maana ile ya pale muungano kijijini ulimjengea wewe. Kwako nyumba lazima ujenge mjini, acha hizo.

Natudia mwandishi haalikwi kwenye matukio ya hadhara kama mikutano, niliuliza kuhusu matukio machafu yanayotokea Kyela lakini waandishi wa kyela hawaandiki kwa sababu tu yanawahusu, tuite maswahiba. Kwa mfano wakati wanafunzi wa Shule ya Msingi Kyela wanalawitiwa na wafanyabiashara walimezea pamoja na uwt kuwapa taarifa, wenzao walitoka mbeya wakafichua wahalifu wakapelekwa mahakamani, hivi napo walipelekwa na Mwakyembe! Inapofikia mpaka mzazi analia na kueleza wazi kwamba "mtoto wangu anaf..." bado mwandishi unafumba macho lakini kila siku wanakuona umeganda kwenye gari la DC kama wewe ndo dereva, unadhani wananchi watakuhitaji tena!!!!

Kuelezea kwamba nyumba ya wageni ya diwani wa mjini ilitumika kulawitia watoto hao, mtu anakimbilia hoja dhaifu eti Nsesi mkabila, hata katika uchafu kama huo tena ulioripotiwa kwenye magazeti hadi watuhumiwa kufikishwa mahakamani tunataka kupotosha umma kwa kisingizio cha ukabila, ajabu sana.

Wafanyakazi kiwira wanadhulumiwa na wawekezaji feki, hao hao waandishi wa kyela wako kimya, wanaofuatilia na kuripoti kila siku ni hao hao wa kutoka mbeya, jee huko nako wanaongozana na Mwakyembe! Wakati wananchi wanakabiliwa na matatizo hayo mazito na wanawapelekea taarifa wako kimya ila wanawaona muda wote wako kwenye gari la DC, unategemea wananchi watawakimbilia nani!!!!.

Jamani mwandishi wa habari ni sauti ya wasio na sauti, kama hutekelezi hilo wananchi watakaa mbali na wewe, suala hapa sio jina tu mimi mwandishi. Kama kweli mko karibu na mambo ya kweli basi elezeni wanachokisema watu wa kawaida kuhusu hao waandishi. Katika maandamano yale waseme hawakualikwa na ni masuala mengi tu ya wananchi hawaelezwi.

Kyela hivi sasa kuna mafuriko, mbona hatusomi habari zao zinazoelezea kinachoendelea kila siku, na badala yake ni waandishi hao hao wa mbeya ndio wenye kuziandika, hivi napo walipelekwa na Mwakyembe! Hivi kwao habari ni za Dr. Mwakyembe tuu! Hizo za wananchi ndio sio habari!

Kama kweli mnaojadili humu mna uchungu na Kyela tuepuke kila jambo kulifanya la kisiasa, twende kwenye issues badala ya majungu.

Litakuwa jambo la msingi iwapo kutakuwa na michango yenye kuonyesha ufumbuzi wa matatizo yetu, kuliko kijifanya kila mmoja bingwa wa kukosoa.

Ombi langu ka JF ni kuwatupia jicho pia waandishi wetu hapa nchini, hivi kweli wanajishughulisha na matatizo ya wananchi au kwao habari ni wanasiasa, habari zao kubwa ni zipi, za wananchi au propaganda za siasa!

Ushauri kwa mnaowatete hao waandishi kwamba walizuiwa, waelemisheni, watoe kipaumbele kwa matatizo ya wananchi, kwamba waelewe kuwa wao sio waheshimiwa bali ni "Voice of the Voiceless." Wajifunze kwa wanzao wa Mbozi.
 
Nadhani haya ndiyo muhimu kujadili kwa sasa,

Mvua kubwa yabomoa nyumba wilayani Kyela

MVUA inayoendelea kunyesha katika Wilaya za Rungwe, Ileje na Kyela mkoani Mbeya hivi sasa imesababisha zaidi ya kaya 40 kukosa makazi ya kuishi wilayani Kyela baada ya nyumba zao kuzama na maji.

Mbali ya kuzamisha makazi ya kaya hizo, mvua hiyo vile vile imebomoa jengo kubwa la Msikiti linalojengwa mjini Kyela na kusababisha hasara ya zaidi ya milioni tisa.

Mvua hiyo ilianza kunyesha kwa nguvu katika wilaya hizo Machi 31, mwaka huu na maji yake kujaza mito ya Songwe na Kiwira wilayani humo ambapo ilifurika na kusababisha mafuriko yaliyozamisha nyumba za wakazi wa kata mbili za Katumba Songwe na Ngonga.

Kufuatia mvua hiyo kuzidi kunyesha kwa nguvu mfululizo, zaidi ya kaya 40 katika vijiji vya Katumba, Kabanga, Mpunguti pamoja na Ndwanga katika kata ya Katumba Songwe zimekosa makaazi na hivyo kupatiwa hifadhi katika Shule ya Sekondari ya kutwa Katumba Songwe baada ya makazi yao kujaa maji.

Chanzo Mtanzania Jumamosi Aprili 4, 2009
 
Mkama P.
Hawa jamaa wa ajabu kweli kweli.
Mimi baba yao ninasema ushabiki na maendeleo ni kitu tofauti kabisa.

Hawa Ippmedia wanapotosha sana wananchi tena sana.

Mwakyembe tangu akiwa mwalimu chuo kikuu pale Mlima.Kaifanyia nini Kyela?.

Wewe uliona wapi mbunge anakaa Guest house anapotembelea Jimbo Lake.Muda wote huo alishindwa ata kujenga kibanda cha kukaa na leo hii unasema eti kaleta maendeleo?

Maji ambayo yalikuwa yanatoka kila kijiji kwa sasa hayotoki tena.Watu wanachota kisimani.Kweli hayo ni maendeleo wanangu?

NSESI tueleze mwakyembe anakaa wapi akija hapa kyela?Ikolo?Usanii mtupu.Acheni ushabiki wa kijinga bwana.Ushabiki wa kijinga nao ni Ufisadi.

Yeye alikuwa na ndoto za uwaziri na jaziba zake zinaishia kwa wenzie.

Hana pa kuishi hapa jimboni kwake.Kama hamtaki mafisadi,iweje mnamshabikia mtu ambaye anagawa watu?Tuna kwenda wapi ninyi wanangu.

Wewe NSESI,BABU ATAKA KUSEMA NA NDUGU YANGU IJABU ISSA,Maendeleo aliyoleta Mwakyemba hapa ni yapi?.Mtu unashangaa kushangiliwa na watoto wa mjini?Kweli wewe una akili timamu?Nenda pale manzese.Ata ukilewa pombe utashangiliwa.Kweli kushangiliwa mjini nikipimo cha kupendwa na wananchi?

Ninyi watoto, mmesomea wapi shule zetu?Kama ndivyo hivyo,basi Mrema angekuwa Rais siku nyingi sana.Au Dar majimbo yote yangechukuliwa na CUF.Kwa sababu ndiyo wanaoshangiliwa sana mjini.Au CHADEMA wangechaguliwa na Helikopta yao.Mimi nilikuwepo Mkamba alipokuja hapa kyela.Atuhutubia ccm kyela na kule Ipinda.Sasa ni wapi alibebwa?Acheni upuuzi bwana.Mnani kera kweli kweli.

Kama unashabikia Richmond,sawa,Lakini kyela pamoja na kuwa na ule mgodi wa makaa ya mawe,baado ni giza tupu.

Mimi babayenu ni siwadanganye,Siwezi kuweka utaifa mbele wakati mama yangu hana maji ya kunywa,hana pa kupitishia baiskeli yake,Mpunga wake anauza kwa mpemba kwa bei ya dhuluma.

Siwezi nikaweka utaifa mbele wakati kyela hakuna mshikamano wowote,Watu wanaangamia kwa ukimwi na uku viongozi hawaoni kama hilo ni Tatizo.Kyela hatuna ata Private hospita,zaidi zaidi ukizidiwa utapelekwa Igogwe au Ilembula Tukuyu.Siwezi kushangilia Richmond wakati ninashindwa kwenda Ipinda kunywa Ulanzi niliozoea.Siwezi kushangilia Utaifa wakati Nimekosana na rafiki yangu kutona na kuwa yeye anampenda mwayembe na mimi simpendi na mwakyembe ameshindwa kutuunganisha.

Mimi ninasema kyela kwanza na ndiyo Utaifa.sijakaa ulaya sijui wanafanyeje?.
Uwezi ukaongoza nyumba kumi wakati matatizo ya nyumbani kwako umeyashindwa.sijajua ninyi bongo Flava mnafanya nini?.Waache wana kyela waamue wenyewe.Ninyi IPP Mnatuchafulia mipango yetu.
Mwakyembe hakubebwa na mtu yeyote hapa.

Mtu anapewa miaka mitano.Kama amechemsha,basi akafanye shuguli zingine.Kama ninyi mama zenu wanaishi vizuri,Bomba zao zinatoa maji sawa.

Miaka mitano tungekaa naye hapa,halafu baadaye angekwenda kugombana na RA na ED.Hao wenzake wana chakujivunia kule kwao.Yeye huku nyumbani ni mtu tena ni mtupu kweli.

Basi njoja niwape ukweli.

Huyu Bwana anapata pesa nyingi sana kwa ajili ya Misaada ya kyela.Kutoka kwa mkuu wa majeshi na kwingineko.Lakini hatuelewi anapeleka wapi.

Ipp media, tuacheni sisi wenyewe tufanye mabadiliko na mbunge wetu mpya.atukumtuma sisi kwenda kugombana na wenzie huko bungeni.Tunataka kwanza kyela ndiyo taifa.

Wewe IJABU ISSA.ulitegemea Makamba alipokuja hapa,amtukane Mwakyembe?wewe kweli hauwajui wana siasa?
 
Nsesi,
wewe unaushabiki wa kitoto.
Sawa hao waandishi hawaandiki mambo uliyo yasema.Je unawatenga watu kutokana na kuwa Taarifa zao hazikutoka gazetini?Ujinga huo sasa.Wao sio wahariri wakuu ndugu yangu.





Swali liko pale pale.

Mwayembe kaifanyia nini Kyela?
 
Nadhani haya ndiyo muhimu kujadili kwa sasa,

Mvua kubwa yabomoa nyumba wilayani Kyela

MVUA inayoendelea kunyesha katika Wilaya za Rungwe, Ileje na Kyela mkoani Mbeya hivi sasa imesababisha zaidi ya kaya 40 kukosa makazi ya kuishi wilayani Kyela baada ya nyumba zao kuzama na maji.

Mbali ya kuzamisha makazi ya kaya hizo, mvua hiyo vile vile imebomoa jengo kubwa la Msikiti linalojengwa mjini Kyela na kusababisha hasara ya zaidi ya milioni tisa.

Mvua hiyo ilianza kunyesha kwa nguvu katika wilaya hizo Machi 31, mwaka huu na maji yake kujaza mito ya Songwe na Kiwira wilayani humo ambapo ilifurika na kusababisha mafuriko yaliyozamisha nyumba za wakazi wa kata mbili za Katumba Songwe na Ngonga.

Kufuatia mvua hiyo kuzidi kunyesha kwa nguvu mfululizo, zaidi ya kaya 40 katika vijiji vya Katumba, Kabanga, Mpunguti pamoja na Ndwanga katika kata ya Katumba Songwe zimekosa makaazi na hivyo kupatiwa hifadhi katika Shule ya Sekondari ya kutwa Katumba Songwe baada ya makazi yao kujaa maji.

Chanzo Mtanzania Jumamosi Aprili 4, 2009

Mkuu wangu Nsesi,

Asante kwa taarifa. Hivi hizi habari mnaziandika kwa kuona kinachotokea au zinapikwa maofisini?

Kweli kama unaijua Kyela, mtu wa katumba akapate hifadhi kwenye shule ya secondary Katumba Songwe? Kweli inaingia akilini kwamba taarifa kama hiyo inaweza kuwa sahihi?

Isije ikawa hizi taarifa zingine zinatolewa kama njia ya kutafuta misaada tu.

Ni rahisi kwa mtu wa Katumba kwenda Itete kuliko kwenda iliko secondary.

Ni kweli maeneo hayo yaliyotajwa kuna mafuriko ila mambo mengine naona kama sio sahihi.

Ebu angalia kaya 40, iweje maeneo yenye kaya zaidi ya 500, kaya 40 tu ziwe affected? Hizo sehemu maeneo yamepakana na hakuna viwanja vikubwa, kama mmoja yuko affected ni wazi hata majirani watakuwa affected.

Ni vizuri waandishi mkiwa mnaenda sehemu husika na kuandika mambo kama yalivyo. Suala la mafuriko eneo hilo linajulikana na ni tatizo karibu kila mwaka. Inatakiwa ifike mahali wananchi tuamue kushirikiana kuondoa tatizo hili. Kuna haja ya kupanda miti kando kando ya mto Songwe na pia kutengeneza mabwawa ya kuhifadhia maji wakati wa mafuriko na hayo mabwawa pia yanaweza kutumika kwenye kilimo cha umwagiliaji. Hapa wote ni wahusika na badala ya kugombana bora tufikirie mambo kama hayo kwa ajili ya wilaya yetu.
 
Nsesi,
Kuelezea kwamba nyumba ya wageni ya diwani wa mjini ilitumika kulawitia watoto hao, mtu anakimbilia hoja dhaifu eti Nsesi mkabila, hata katika uchafu kama huo tena ulioripotiwa kwenye magazeti hadi watuhumiwa kufikishwa mahakamani tunataka kupotosha umma kwa kisingizio cha ukabila, ajabu sana.
Mkuu haya maneno kweli au?.. mbona unatisha mkuu wangu, yaani kweli haya maswala yametokea nyumbani kwa Diwani!...
Duh, jamani mwee nyie acheni ujinga hili swala zito sana kuliko huyo Mwakyembe mara 1000..Hata kama ni swala la Mhariri wa habari kuichapisha gazetini, lakini kama atakataa kuichapisha bado itauzika tena kwa bei kubwa kuliko mshahara wa mwezi -Kuwatahadharisha wananchi!
 
Nsesi,

Mkuu haya maneno kweli au?.. mbona unatisha mkuu wangu, yaani kweli haya maswala yametokea nyumbani kwa Diwani!...
Duh, jamani mwee nyie acheni ujinga hili swala zito sana kuliko huyo Mwakyembe mara 1000..Hata kama ni swala la Mhariri wa habari kuichapisha gazetini, lakini kama atakataa kuichapisha bado itauzika tena kwa bei kubwa kuliko mshahara wa mwezi -Kuwatahadharisha wananchi!

Mkuu Mkandara,

Madai ni kwamba kuna wanafunzi walifanyiwa hivyo vitendo kwenye guest house ambayo mmiliki wake ndiye diwani wa Kyela mjini.

Sasa hapo mwenye kosa ni mmiliki wa guest au hao waliofanya kosa na kukamatwa?

Huyo jamaa ni Mkinga na pia haelewani na mheshimiwa. Ghafla kuna vita kibao juu yake na madai kama haya ya akina Nsesi. Juzi kwenye kura za Albino, wametuma vijana wao wakaandika jina la huyo diwani kama ni jambazi. Kuna maneno kibao ya kibaguzi yanaendeshwa. Ukienda kuangalia, huyo diwani anajituma kwenye maendeleo kuliko hata madiwani wengine. Lakini kwasababu sio Mnyakyusa tayari maneno, kwani waliomchagua mbona walijua hilo?

Ni siasa za Kyela tu na ujinga wa watu kutumia elimu zao, magazeti yao kuendeleza chuki badala ya umoja.

Tulikuwa na DC wa maana sana pale Kyela kwa ufuatiliaji na kafanya kazi kubwa kweli kwenye ujenzi wa shule. Kawabana watendaji, kafuatilia maendeleo lakini nasikia majungu yamepigwa mpaka jamaa kaondolewa. Nsesi alikuja hapa akaandika kahongwa gari na Kiwira Coal Mine, hivi hata anaijua Kiwira? Wafanyakazi wa Kiwira Coal Mine wako hoi mno, hata hizo pesa za kumnunulia gari mkuu wa wilaya watatoa wapi? Watu wanashindwa hata kutoa 70,000 ya kulipia ada za watoto wao kwa mwaka, kweli watamnunulia gari DC?

Kule kwetu nafikiri ifike mahali tupigane viboko, ujinga umekuwa mwingi sana.
 
Nsesi,
wewe unaushabiki wa kitoto.
Sawa hao waandishi hawaandiki mambo uliyo yasema.Je unawatenga watu kutokana na kuwa Taarifa zao hazikutoka gazetini?Ujinga huo sasa.Wao sio wahariri wakuu ndugu yangu.





Swali liko pale pale.

Mwayembe kaifanyia nini Kyela?[/QUOTE]

Nijuavyo aliwajengea au ana mpango wa kujenga shule maana kwenye fundraising hata mie niliwachangieni tena si kitoto!
Au hiyo shule nayo ni hewa?
 
Mtanzania,
Madai ni kwamba kuna wanafunzi walifanyiwa hivyo vitendo kwenye guest house ambayo mmiliki wake ndiye diwani wa Kyela mjini.
Sasa hapo mwenye kosa ni mmiliki wa guest au hao waliofanya kosa na kukamatwa?
Mkuu wangu kulingana na habari hiyo, mwenye Guest na hao waliowaliwiti watoto wa shule ya msingi wote wana makosa!..
 
Mtanzania,

Mkuu wangu kulingana na habari hiyo, mwenye Guest na hao waliowaliwiti watoto wa shule ya msingi wote wana makosa!..

Nakuunga mkono Mkuu na kwa kuongezea ni kuwa hao wanaosimamia hiyo guest house hawakuwa wamefumba macho hadi watoto wanaingizwa humo kufanyiwa vitendo viovu.Wafanyakazi hao ambao wanafanya hiyo kazi ya kuendesha biashara ya guest house wana makosa maana kuna sheria ya kuendesha nyumba za wageni.Kinachotendeka ni kuwa badala ya kulaza wageni haswa, wao wanaendesha kama madanguro.Ileweke hili ni kosa pia kisheria.
 
Back
Top Bottom