Habari za afya ya Dr. Harrison Mwakyembe

Wananchi hao, wakiongozwa na viongozi wao wa jadi na wazee waliandaa maandamano makubwa mjini Kyela, Jumapili iliyopita, maandamano ambayo katika dakika zake za mwisho yalizuiwa kwa amri ya Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mbeya, Zelothe Stephen. Hatua hiyo imeacha maswali mengi yasiyo na majibu.

Katika hili Rais Jakaya Kikwete anapaswa kuelewa kwamba anapolea uozo kama huo wa kudumaza demokrasia na kuwanyima wananchi haki yao ya msingi na kikatiba, anazidisha hasira ya wananchi dhidi yake yeye na wala si hao wasaidizi wake.

Wananchi wa Kyela wanaamini kwamba Rais wao ndiye chanzo cha matatizo yote ya kisiasa yanayowasibu wilayani humo pamoja na mbunge wao.[/COLOR][/font][/size]

Raia Mwema,

Hivi kumbe Kyela kuna viongozi wa jadi? Wamechaguliwa na nani? Najua kuna wazee lakini viongozi wa jadi tena inatoka wapi?

Pia kusema wananchi wa Kyela wanaamini kwamba: utafikiri hata kuna kura ya maoni yoyote umefanya?

Hivi mimi Mtanzania leo nikiandaa maandamano ya wahuni pale mjini na kuwapa pesa za soda kisha nikawaambia waseme ninachokitaka, mwandishi makini utachukulia hiyo kama wananchi wa Kyela wanaamini kwamba?

Mbona Raia Mwema ilikuja kwa nguvu zote na kupinga matatizo ya RAI, wakati na nyie mnaandika habari bila hata kufanya analysis?

Matatizo ya Kyela sio JK wala sio prof. Mwandosya. Matatizo ya Kyela ni ubinafsi wa watu wawili ambao baada ya kushindana mwaka 2005, mpaka leo wameshindwa kabisa kuweka tofauti zao pembeni na kazi zao ni kulalamika kila siku. Wanatumia vijana wasio na kazi na wazee wenye njaa ili kuchochea maugomvi yasiyoisha. Badala ya kutumia resources hiyo ya wananchi ili kusaidia kusukuma maendeleo ya wilaya, viongozi wetu ni majungu tupu usiku na mchana na kuendelea kuwachanganya wananchi.

Kama maandamano yalizuiwa, mbona wafuasi wa mbunge nao walizuia hao waandishi wa Kyela wasiende kwenye mkutano huo. Mimi naona kama ni kitu kile kile cha kutumia mabavu na kutaka kuwalazimisha wananchi wafuate upande mmoja. Kama wananchi wanataka kuandamana, wache waandamane ili mradi hawavunji sheria. Kama kuna mkutano wacha waandishi waje na waandike wanachokijua. Sisi wananchi tuna uwezo wa kuchambua pumba na mchele.
 
Bubu Ataka Kusema said:
Tuliambiwa hapa kwamba Mwakyembe katika mkutano ule alitumia muda mwingi kumtukana fisadi Rostam na mpaka sasa hivi sijaona pengine popote pale matusi hayo kama ilivyodaiwa na engineer. Kwa maoni yangu kama Mwakyembe angekuwa ametumia matusi basi wabaya wake ndani ya CCM wangeshalizungumza hilo la uvurumishaji matusi, lakini hadi hii leo hatujasikia lolote. Je, kulikuwa na matusi kweli yaliyotolewa na Mwakyembe ama engineer aliandika kishabiki ili kumpaka matope Mwakyembe?[/B]

Bubu,

Labda tuambie nini maana ya matusi. Wengine watu wa bara, neno matusi lina maana nyingi sana. Je maneno kama haya kwa mawazo yako sio matusi?

Rostam ni fisadi namba moja
Rostam ni mbumbumbu na hajui kitu
Rostam ni mchafu
Rostam ni bubu hata bungeni hawezi kufungua mdomo wake nk.

Sija quote exactly, lakini maneno karibu na hayo kama sio matusi utaita ni nini?

Maana ya tusi kwa kiingereza imetafsiriwa kama insult, swear word, abusive behaviour.

Unamwita mtu fisadi ambaye hajahukumiwa na mahakama, kama sio insult ni nini?

Nafikiri taarifa ya engineer ilikuwa sahihi kabisa. Labda kama watu mnaona matusi ni mpaka ya nguoni.

Kwa habari mimi nilizozipata Kyela, taarifa ya Engineer ilikuwa sahihi kwa asilimia kubwa sana. Of course kila mtu anaandika kwa namna anayoijua yeye hivyo kunaweza kuwa na tofauti ya tafsiri ya hapa na pale, lakini karibu kila alichoandika Engineer kilitokea siku hiyo.
 
Mtanzani, umeongea mengi kuhusu siasa za kyela. Ninachokiona katika maelezo yako mengi ni uegemezi wako upande usiokubaliana na Dr Mwakyembe. Hilo ni jambo la kawaida, lakini tatizo nilionalo ni kuegemea habari za kuelezwa na upande mmoja, hivi nani alikweleza kwamba Prof Mwandosya ni miongoni mwa kingmakers wa siasa za Kyela, na kwamba Dr. Mwakyembe anaitegemea nguvu ya Profesa kushinda jimboni kwake?

Kama ulikuwa huelewi Profesa hakumuunga mkono Dr Mwakyembe 2005, yeye aliegemea kwa Mwakipesile pamoja na kusaidiwa sana na Mwakyembe kwenye harakati zake za kugombea Urais. Hata Mbeya Mjini Profesa alimpigania sana Thom na kumshughulikia Mpesya. Sababu kubwa aliamini Mwang'onda na kundi lake la kina Mwakipesile walikuwa upande wake kwenye Urais. Uteuzi wa JK ndio uliomfadhaisha Profesa kwani ndipo alipobaini kuwa jamaa hawakuwa upande wake na walimchuuza.

Kwenye kinyang'anyoro cha NEC kilichomuokoa ni wabunge wa mkoa huo wakiwemo alowapiga vita, kina Mwakyembe na Mpesya, kupigania heshima ya mkoa wao kwa kutoruhusu watu wa nje kuwaamulia mambo yao, na hiyo ndiyo inayoelezwa kuwa moja ya sababu za Dr Siame kutemwa kwenye uwaziri kwa sababu alieleza wazi msimamo wake.

Dr Mkwayembe amefanya kazi jimboni mwake na ndio maana bado wanamkubali, usingojee kuelezwa nenda mwenyewe vijijini utapata jibu la kukubalika au kutokubali kwake.

Suala wa vijana kukaa vijiweni na Kyela kulishwa na Rungwe ni ufinyu wa kufikiri, hivi Rungwe wanalima mpunga na mchele wanaokula unatoka wapi? Ni uchambuzi rahisi tu wa uchumi kwamba hakuna aliyekamilika kila mmoja anamtegemea mwenzake, Rungwe wanapeleka ndizi Kyela na wao wanachukua mchele na matunda, ajabu iko wapi hapo. Hivi Unaelewa kwamba mahindi yaliyojazana pale kwenye soko la Tukuyu ni kutoka Mbeya?

Kyela waling'oa migomba wakapanda cocoa ambayo inawapa pesa zaidi ya ndizi, na ushahidi wa hilo ni makusanyo ya halmashauri hizo mbili, yale ya Rungwe yako chini sana, uasikini Rungwe uko juu, tatizo mnaangalia barabarani, nendeni ndani vijijini mkajionee. Na hilo sio tatizo la Kyela, Rungwe au Mbeya ni tatizo la nchi nzima, Kyela wanasikika kwa sababu ni wazungumzaji. Hivi vijiwe vilivyoko pale Ushirika, Tukuyu Mjini, Katumba, KK, Mwakaleli ni vijana kutoka Kyela!!

Engineer haukuwa mkweli kuhusu waandishi kuzuiwa, hakuna aliyezuiwa, waandishi walikuwa huru kukusanya na kutoa habari. Kwanza ni lini hao waandishi Kyela walimwandika vibaya Dr Mwakyembe, sijawahi soma popote. Kilichopo ninachokifahamu mimi ni kwamba pale Kyela mjini walikuwa wakimtania mmoja wa hao waandishi kwamba ni mtoto wa kwanza wa DC Mashimba kutokana na jinsi alivyokuwa amejisogeza kwake kiasi cha kushinda naye muda wote hadi kuweka kijiwe chao nyumbani kwake DC!
 
Mtanzani, umeongea mengi kuhusu siasa za kyela. Ninachokiona katika maelezo yako mengi ni uegemezi wako upande usiokubaliana na Dr Mwakyembe. Hilo ni jambo la kawaida, lakini tatizo nilionalo ni kuegemea habari za kuelezwa na upande mmoja, hivi nani alikweleza kwamba Prof Mwandosya ni miongoni mwa kingmakers wa siasa za Kyela, na kwamba Dr. Mwakyembe anaitegemea nguvu ya Profesa kushinda jimboni kwake?

Kama ulikuwa huelewi Profesa hakumuunga mkono Dr Mwakyembe 2005, yeye aliegemea kwa Mwakipesile pamoja na kusaidiwa sana na Mwakyembe kwenye harakati zake za kugombea Urais. Hata Mbeya Mjini Profesa alimpigania sana Thom na kumshughulikia Mpesya. Sababu kubwa aliamini Mwang'onda na kundi lake la kina Mwakipesile walikuwa upande wake kwenye Urais. Uteuzi wa JK ndio uliomfadhaisha Profesa kwani ndipo alipobaini kuwa jamaa hawakuwa upande wake na walimchuuza.

Kwenye kinyang'anyoro cha NEC kilichomuokoa ni wabunge wa mkoa huo wakiwemo alowapiga vita, kina Mwakyembe na Mpesya, kupigania heshima ya mkoa wao kwa kutoruhusu watu wa nje kuwaamulia mambo yao, na hiyo ndiyo inayoelezwa kuwa moja ya sababu za Dr Siame kutemwa kwenye uwaziri kwa sababu alieleza wazi msimamo wake.

Dr Mkwayembe amefanya kazi jimboni mwake na ndio maana bado wanamkubali, usingojee kuelezwa nenda mwenyewe vijijini utapata jibu la kukubalika au kutokubali kwake.

Suala wa vijana kukaa vijiweni na Kyela kulishwa na Rungwe ni ufinyu wa kufikiri, hivi Rungwe wanalima mpunga na mchele wanaokula unatoka wapi? Ni uchambuzi rahisi tu wa uchumi kwamba hakuna aliyekamilika kila mmoja anamtegemea mwenzake, Rungwe wanapeleka ndizi Kyela na wao wanachukua mchele na matunda, ajabu iko wapi hapo. Hivi Unaelewa kwamba mahindi yaliyojazana pale kwenye soko la Tukuyu ni kutoka Mbeya?

Kyela waling'oa migomba wakapanda cocoa ambayo inawapa pesa zaidi ya ndizi, na ushahidi wa hilo ni makusanyo ya halmashauri hizo mbili, yale ya Rungwe yako chini sana, uasikini Rungwe uko juu, tatizo mnaangalia barabarani, nendeni ndani vijijini mkajionee. Na hilo sio tatizo la Kyela, Rungwe au Mbeya ni tatizo la nchi nzima, Kyela wanasikika kwa sababu ni wazungumzaji. Hivi vijiwe vilivyoko pale Ushirika, Tukuyu Mjini, Katumba, KK, Mwakaleli ni vijana kutoka Kyela!!

Engineer haukuwa mkweli kuhusu waandishi kuzuiwa, hakuna aliyezuiwa, waandishi walikuwa huru kukusanya na kutoa habari. Kwanza ni lini hao waandishi Kyela walimwandika vibaya Dr Mwakyembe, sijawahi soma popote. Kilichopo ninachokifahamu mimi ni kwamba pale Kyela mjini walikuwa wakimtania mmoja wa hao waandishi kwamba ni mtoto wa kwanza wa DC Mashimba kutokana na jinsi alivyokuwa amejisogeza kwake kiasi cha kushinda naye muda wote hadi kuweka kijiwe chao nyumbani kwake DC!

Nsesi,

Sitaki kuendeleza malumbano. Ni ukweli mtupu kwamba Prof. alimuunga mkono Dr. Mwakyembe 2005. Lakini pia ni ukweli mtupu kwamba prof. sio mjinga hakutumbukiza kichwa kichwa kwenye siasa za Kyela kama ambavyo hakufanya kwenye siasa za Mbeya. Pia ni ukweli mtupu kwamba Prof. Mwandosya ni kingmaker wa siasa za mkoa wa Mbeya.

Pia ni ukwelui mtupu kwamba Kyela inategemea baadhi ya mambo toka Rungwe wakati ilitakiwa kuwa kinyume. Hali ya hewa ya Kyela ni nzuri zaidi lakini hata mboga za majani zinaletwa toka Rungwe.

Hapo mjini penyewe, biashara zimeshikwa na wageni wakati sisi wenyeji tunapiga domo. Hayo ndio mambo ya kushughulikia na sio kuelezea mapato ya halmashauri. Hayo mapato si yanaletwa na watu wanaochapa kazi wakiwemo wengi kutoka nje ya Kyela?

Unaweza kuukataa ukweli lakini ndio hivyo. Kyela tuko nyuma sana mkuu. Mimi naijua Kyela kuliko unavyodhani na inanisikitisha sana kuona huo umaskini wa kutisha huko vijijini wakati resources zipo kibao. Ninawaelewa vijana wa Kyela hapo mjini, ni maneno tu na majungu mengi ya kisiasa badala ya kuchangamkia kazi. Afadhali hata dada zetu angalau wameanza kuamka na kujifunza toka kwa wenzao wa Rungwe na kuanza kufanya vibiashara vyao.

Concern yangu Kyela ni maendeleo na wala sio mwanasiasa mmoja mmoja. Sio rafiki wa mwanasiasa yeyote lakini pia si adui wa mwanasiasa yeyote. Kwangu mimi Kyela ni kubwa kuliko mimi au kuliko mtu mwingine yeyote. Yeyote ambaye yuko tayari kukemea ujinga huo, mimi nitamuunga mkono.
 
Nsesi,Concern yangu Kyela ni maendeleo na wala sio mwanasiasa mmoja mmoja. Sio rafiki wa mwanasiasa yeyote lakini pia si adui wa mwanasiasa yeyote. Kwangu mimi Kyela ni kubwa kuliko mimi au kuliko mtu mwingine yeyote. Yeyote ambaye yuko tayari kukemea ujinga huo, mimi nitamuunga mkono.

- Mkuu Mtanzania, hapa tupo pamoja sana, siasa za Tanzania sasa zinaanza kuwa mimi mimi, na sio sisi tena, hii sio Kyela tu hata kwenye taifa na kwa kweli linatupeleka pabaya sana hili as a nation, ni vyema huko Kyela mmshaliona mapema, tulikatae kwa nguvu zote hili la umimi na ubinafsi mbele.

FMES!
 
Mtanzania na Nsesi,

Mie naona nyie mnaweza hata kuwa MNAFAHAMIANA. Maana nyote mwaifahamu sana Kyela. Ila Kyela ni kubwa na nafikiri Mtanzania ana habari kutoka kwa jamaa zake XXX na YYY ambao waliona SIKIO la tembo. Nsesi naye pia alikuwepo hapo na akaona mgongo wa Tembo. Sasa hapa niseme kuwa nakubaliana na Mtanzania. Hamna haja ya marumbano. Cha muhimu ni kuwasaidia wananchi. Kama RA angelikuja na kusema ataacha ufisadi wake na awatumikie watu wa Kyela, huku akitoa ushirikiano wa nguvu na viongozi wengine, basi angelifaa zaidi ya huyo mbunge wenu Mwakyembe ambaye hadi leo bado anaendeleza ugomvi wa uchaguzi wa mwaka 2005 na mkuu wa Mkoa.

Mwakyembe alifanya kosa kuwa mara baada ya kuchaguliwa, hakuwaunganisha adui zake wote na kuwaleta kwake kama Obama alivyofanya. Sasa wakati akipita akicheka kuwa "boss ni nani?" anakuta mbaya wake kapewa UKUU WA MKOA. Lohh, kama ya kile kisa cha Rashid Makame na Meena(??) aliyemuacha pale JKT Ruvu na kwenda kuwa mkuu wa mkoa Mbeya. Jamaa akatukana sana sana. Makame kaitwa Dar, akapitia pale JKT Ruvu kwenda KUFISADI mayai kidogo, basi nasikia jamaa kuona gari akauliza nani huyo wakamjibu ni Makame, akaita MPs wamfukuze. Jamaa akatolewa mkuku. Akaenda Dar, kufuka huko anaambiwa, kuaniza leo wewe ndiyo unakuwa mkuu wa JKT. Simu ya kwanza ya Makame ilienda RUVU JKT.

Hivyo wandugu, ukipanda juu, usiwasau waliokupandisha na ukaanza kujiona kama Mungu fulani hivi. Utajikuta uko mlima Meru, wakati mwinzio kabebwa na kuwekwa mlima Kilimanjaro........... Hii ni kwa Mwakyembe na Mwakipesile. Malizeni maugomvi yenu na muanze kuisaidia jamii. Ugomvi wenu zinaumia NYASI.
 
Mtanzania na Nsesi,

Mie naona nyie mnaweza hata kuwa MNAFAHAMIANA. Maana nyote mwaifahamu sana Kyela. Ila Kyela ni kubwa na nafikiri Mtanzania ana habari kutoka kwa jamaa zake XXX na YYY ambao waliona SIKIO la tembo. Nsesi naye pia alikuwepo hapo na akaona mgongo wa Tembo. Sasa hapa niseme kuwa nakubaliana na Mtanzania. Hamna haja ya marumbano. Cha muhimu ni kuwasaidia wananchi. Kama RA angelikuja na kusema ataacha ufisadi wake na awatumikie watu wa Kyela, huku akitoa ushirikiano wa nguvu na viongozi wengine, basi angelifaa zaidi ya huyo mbunge wenu Mwakyembe ambaye hadi leo bado anaendeleza ugomvi wa uchaguzi wa mwaka 2005 na mkuu wa Mkoa.

Mwakyembe alifanya kosa kuwa mara baada ya kuchaguliwa, hakuwaunganisha adui zake wote na kuwaleta kwake kama Obama alivyofanya. Sasa wakati akipita akicheka kuwa "boss ni nani?" anakuta mbaya wake kapewa UKUU WA MKOA. Lohh, kama ya kile kisa cha Rashid Makame na Meena(??) aliyemuacha pale JKT Ruvu na kwenda kuwa mkuu wa mkoa Mbeya. Jamaa akatukana sana sana. Makame kaitwa Dar, akapitia pale JKT Ruvu kwenda KUFISADI mayai kidogo, basi nasikia jamaa kuona gari akauliza nani huyo wakamjibu ni Makame, akaita MPs wamfukuze. Jamaa akatolewa mkuku. Akaenda Dar, kufuka huko anaambiwa, kuaniza leo wewe ndiyo unakuwa mkuu wa JKT. Simu ya kwanza ya Makame ilienda RUVU JKT.

Hivyo wandugu, ukipanda juu, usiwasau waliokupandisha na ukaanza kujiona kama Mungu fulani hivi. Utajikuta uko mlima Meru, wakati mwinzio kabebwa na kuwekwa mlima Kilimanjaro........... Hii ni kwa Mwakyembe na Mwakipesile. Malizeni maugomvi yenu na muanze kuisaidia jamii. Ugomvi wenu zinaumia NYASI.

Sikonge,

Nimecheka kweli kweli hiyo ya Makame.

Utafikiri unajua yaani Mwakipesile alipoapishwa tu kuwa RC, kituo cha kwanza kilikuwa Kyela na gari lake la RC. Ikabidi wale wole waliokuwa wanamzomea wakae kimya, maana sasa kapewa na nyundo kabisa ya polisi.

Na yeye RC alifanya makosa sana maana JK angeweza kumteua Mwakyembe kuwa waziri ofisi ya waziri mkuu anayeshughulikia serikali za mitaa, sijui ingelikuwaje.

Wenzetu akina Obama, Clinton, wametuacha mbali sana. Ukiona mama Clinton anavyomwaga sifa sasa kuhusu Obama au Obama anavyomwaga sifa kuhusu mama Clinton. Utadhani sio wale ambao walikuwa wanarushiana vijembe.

Sijui kwanini sisi Afrika tunaweka hasira kwa muda mrefu sana. Hata Zimbabwe pale unaona kabisa yule Mugabe bado hajasamehe na kusema yameisha. Ukienda kwa Odinga na Kibaki naona kama bado hasira haijaisha. Mimi naamini tatizo kubwa ni wapambe. Hao wanaofaidika kunapokuwa na makundi au majungu. Yote ni umaskini ule ule, mtu anaona wakipatana yeye atakosa kwa kula.
 
Bubu,

Labda tuambie nini maana ya matusi. Wengine watu wa bara, neno matusi lina maana nyingi sana. Je maneno kama haya kwa mawazo yako sio matusi?

Rostam ni fisadi namba moja
Rostam ni mbumbumbu na hajui kitu
Rostam ni mchafu
Rostam ni bubu hata bungeni hawezi kufungua mdomo wake nk.

Sija quote exactly, lakini maneno karibu na hayo kama sio matusi utaita ni nini?

Maana ya tusi kwa kiingereza imetafsiriwa kama insult, swear word, abusive behaviour.

Unamwita mtu fisadi ambaye hajahukumiwa na mahakama, kama sio insult ni nini?Nafikiri taarifa ya engineer ilikuwa sahihi kabisa. Labda kama watu mnaona matusi ni mpaka ya nguoni.

Kwa habari mimi nilizozipata Kyela, taarifa ya Engineer ilikuwa sahihi kwa asilimia kubwa sana. Of course kila mtu anaandika kwa namna anayoijua yeye hivyo kunaweza kuwa na tofauti ya tafsiri ya hapa na pale, lakini karibu kila alichoandika Engineer kilitokea siku hiyo.

Fisadi Rostam si lazima apelekwe Mahakamani tuelezwe kuwa ni fisadi. Huyu jamaa ni fisadi completely, akipita njiani anatoa harufu ya kifisadi, akikohoa anatoa harufu ya kifisadi, akitoa jasho harufu ni ufisadi tupu. Watanzania hawahitaji mahakama kuwaambia RA ni fisadi, watanzania wanataka huyo fisadi apelekwe anakostahili either Ukonga akanyee debe au afilisiwe kisha arudishwe kwao Iran.
Ndiyo nimesema kuwa RA ni fisadi anayehitaji kushughulikiwa ipasavyo. Serikali ikishindwa basi wananchi wanaweza kuifanya hiyo shughuli vilevile tena kwa ufanisi wa hali ya juu.
 
Samahani Mkuu Bubu just curiosity! Mwandishi wa habari hii ni miongoni wa wale wateule wa DR Mwakyembe?
Mkuu, una introduce a very interesting element katika suala zima la uandishi na michango yetu wanaJF. Hivi asiye mteule wa Dr. Mwakyembe anatakiwa aandike vipi, na wewe mwenzetu ni mteule wa nani? Fataki
 
Masahihisho hapo, Kyela iligawanyika katikati kati ya Dr. na Mwakipesile. Baada ya uchaguzi wa CCM ni kama Dr. hakuwa na upinzani tena.

Hilo la asilimia 93 japo ni sahihi lakini kwa mazingira ya Kyela nafikiri haina maana hiyo mwandishi anayotaka kuonyesha.

Hata mwaka 2010 Kyela itagawanyika katikati na tegemeeni mapambano makali sana kutokea huko.

Dr. Mwakyembe ana advantage kwasababu ni mbunge na anaweza kuzunguka jimboni bila kuambiwa anafanya kampeni. Tatizo kubwa zitakuwa zile ahadi zake za 2005 ambazo kwa sehemu kubwa hakuna kilichofanyika. Pia ni kama Dr. hajui kutengeneza marafiki, maana watu wengi waliomuunga mkono 2005, sasa wamejikata taratibu kwa sababu mbalimbali ikiwemo ya dharau (elimu), kutokushaurika na kukosa uongozi wa pamoja. Kiujumla dharau ndio weakness kubwa ya Dr. Kuna jamaa aliwahi kuniambia, inatosha kukaa na Dr. wiki moja tu kuweza kugundua weaknesses zake nyingi sana hasa dharau na usanii wa kusema mambo ambayo anajua wazi hawezi kufanya.

Kwa habari tulizo nazo wengine, jimbo la Kyela litakuwa gumu sana 2010 tofauti na watu walioko mbali na Kyela wanavyofikiri. Nafikiri hata Dr. kalitambua hili na mambo mengi yanayotokea sasa kwa sehemu kubwa ni siasa za Kyela. Dr. kafanikiwa kupitia magazeti ya Dar kuwafanya wengi walioko mbali na Kyela waamini atashinda kirahisi Kyela. Ukweli wa kule wilayani unaonyesha atakuwa na kazi ngumu sana.

Muda wote watu walidhani ni mpambano mwingine kati ya Dr na mwakipesile, lakini kwa taarifa za uhakika ni kwamba ni kama 100% Mwakipesile hatagombea ubunge Kyela. Hiyo inatoa nafasi kwa sura mpya kuingia kwenye ulingo. Dr angeweza kumshinda Mwakipesile kirahisi sana maana angemhusisha na ufisadi wa akina Lowassa na Rostam.

Kingmaker wa siasa za Kyela ni pamoja na prof. Mwandosya. Ila prof ni mjanja sana, hawezi kutumbukiza kichwa chake moja kwa moja. Anashirikiana na makundi yote hata kama ni kwa maneno tu. Naamini hataweza kumuunga mkono Dr moja kwa moja na atawaachia wana Kyela waamue. Anachoweza kufanya ni kumsaidia resources na kisha kuwaacha wana Kyela waamue.

Dr. Mwakyembe ana wafuasi wengi miongoni mwa wana Kyela wenye uwezo wanaoishi Dar, wakiongozwa na Kifukwe, yule aliyekuwa Yanga. Kule Kyela wanaitwa mafia wa Dar, hao ndio tegemeo kubwa la Dr. Wana mbinu nyingi, wana pesa, wana uhusiano wa karibu na Mengi. Kundi hilo hilo ndilo lilisaidia kwenda kuficha wajumbe kule Rungwe mwaka 2005 kabla ya mkutano mkuu wa uchaguzi. Kuna uvumi hili kundi ndilo limesababisha DC wa Kyela kuondolewa. Hivyo nategemea Dr. atakuwa na access ya pesa ma media ili kushinda Kyela. Tatizo lake ni kwamba wengi wa watu kwenye hili kundi hawajafanya chochote cha maana Kyela. Kwa Kyela ni kama watalii tu wanaofika Kyela na magari yao makubwa na wapambe lakini hawana muda kabisa na matatizo ya Kyela isipokuwa pale wanapokuwa na interests zao. Pia wameanza kugawanyika maana kwa mfano Mwanjala ambaye ndiye alikuwa kinara wa kubeba na kuhonga wajumbe kwa ajili ya Dr. sasa kakosana naye na ameamua yeye mwenyewe kugombea ubunge 2010. Hili kundi linakumbukwa kwa kusaidia kuanza kwa kanisa la Morovian la Kyela. Waliweza kuua njama za Rungwe kuzuia Kyela wasianzishe kanisa lao. Kuna watu bado wanawakumbuka vizuri kwa hilo.

Kundi lingine lenye nguvu ni la wale wastaafu mbalimbali ambao sasa wamejenga Kyela na kuishi Kyela. Hawa hawana uhusiano mzuri na Dr. Hili lina watu waliokuwa kwenye nafasi za juu upande wa jeshi la wananchi na polisi na foreign. Kundi hili ni pamoja na Apson mwenyewe, lina uhusiano wa karibu sana na Mwakipesile. Ni katika watu waliomshauri vizuri Mwakipesile kwamba asigombee maana ataadhirika vibaya. Hawa wanaijua Kyela vizuri sana ila sidhani kama wana influence kubwa vijijini. Wao wanaona wana influence lakini mimi nina wasiwasi kama influence yao itakuwa kubwa. Wakiungana kumuunga mtu mwingine basi atakuwa na advantage ya pesa na ushauri lakini pia atakuwa na disadvantage ya kuwa linked na mafisadi ili hata kama yeye hana uhusiano wowote na ufisadi, bado aunganishwe na Rostam kupitia hao wastaafu.

Ikifika 2010 kumbuka maneno ya hapo juu. Kyela ni katika majimbo ya kuyaangalia sana 2010. Watu wanaweza kuja kuwa shocked kuona Dr. kaangushwa na watafikiri Rostam kafanya kazi yake, kumbe ni mambo ya Kyela na siasa za Kyela.

Mkuu Mtanzania, ni rahisi sana kuiinamia kompyuta yako na kumwaga analysis ya kila aina kutokana na simulizi kwa njia ya simu za mikononi na magazeti aina ya Nyundo, lakini kwa wanaokivaa hicho kiatu na kujua panapouma, unachofanya si huduma ni ubishi wa kijiweni usio na tija kwa ndugu zako wana-Kyela. Wote tuliokwenda Kyela kwa ajili ya maadamano hayo hatukushuhudia Mwandishi yoyote akizuiwa kwenda Kyela. Kwanza, kwa akili ya kawaida tu, utamzuia mtu kwa kutumia nini? Polisi, Usalama wa Taifa au JWTZ? Mimi ninachojua ni kuwa baadhi ya waandishi wenzetu walitaka waalikwe ili baada ya kazi wapewe "bahasha"! Wanaojua kujituma, walikwenda Kyela "bahasha or no bahasha".

Umetoa simulizi ndefu za akina Kifukwe, Mwanjala, Apson, Mwakipesile, wastaafu n.k. Very interesting reading, indeed. Hata sisi tunazisikia sana simulizi hizo ukiwa nje ya Kyela na ukiwa Kyela ukaishia kunywa pombe Pataya. Ushahidi wa hili ni pale unaposema Dk. Mwakyembe anaweza kumshinda Mwakipesile uchaguzi ujao kwa urahisi sana kwa kumhusisha na mafisadi akina Rostam. Kwa sisi tunaoivinjari Kyela na wilaya zote za Mbeya kwa karibu, Dk. hahitaji kata kufungua mdomo kuhusu Mwakipesile kwani Mkuu wa Mkoa huyo alishakufa kisiasa siku nyingi! Twende kwa data:

Uchaguzi Mkuu wa 2000, Mwakipesile alichaguliwa kuwa Mbunge kwa 52% as against 48% votes za wapinzani, pamoja na heavy rigging kufanyika in Mwakipesile's favour. Tatizo la watu wa Kyela mnaoishi nje ya wilaya yenu, kama ninavyoamini kuwa Mkuu Mtanzania na wewe ni mmoja wao, mnaweka mbele sana ubinafsi ambao hauisaidii wilaya yenu tajiri kwa kila kitu iweze kwenda mbele. Mmgeuzwa na akina Lowassa kuwa recruitmernt ground ya kumalizana nyie wenyewe. Wewe fikiria, how on earth can one imagine today that Mwakipesile can defeat an opponent like Dr. Mwakyembe who polled 93% clear votes in 2005? Najua utakimbilia kuwa "alihonga" kwa kutumia wapambe wake wakati huo, akina Mwanjala na Kifukwe kama unavyotueleza. To me that is cheap conjecture inayowamaliza Wanyakyusa na itaendelea kuwatafuna.

Sitetei mtu just for the sake of it. Natetea Mtanzania halisi aliyejitahidi kuleta mabadililo katika kipindi hiki kifupi. Kyela ya 2005 ya Mwakipesile si Kyela ya 2009 ya Dk. Mwakyembe. Imebadilika. Jifunzeni kutembelea kwenu, msiwe mabingwa wa kumwaga sera kwenye mitandao tu! Analysis yako Mkuu, ni nzuri tu kwa wasomaji wa forum hii, lakini haikubaliani kabisa na assessment ya watu wa kawaida kabisa wa Kyela kuhusu Dk. Mwakyembe. Nilikuwa mmoja wa waandishi tuliofuatana na Katibu Mkuu wa CCM Makamba, katika ziara yake ya Kyela. Aliingia Kyela na mtazamo kama wako Mkuu Mtanzania, lakini akabadilika ghafla na kuanza kumpigia debe Dk. Mwakyembe baada ya kuona wananchi wa kawaida wakigombania kumshika mkono Mbunge wao na kumshangilia kila tulipopita. NJOO 2010, UTUMALIZIE UBISHI
 
Mkuu Ijabu Issa

Hapo umenena, asiyekubaliana na nawe yuko katika kufurahisha baraza la JF. Tangu kuingia kwa huyo jamaa kuna mabadiliko makubwa sana ya kifikra na kimaendeleo. Ila kwa wanaoishia pale Pataya ni kweli Kyela inarudi nyuma kwa sababu wanachokiona pale ni pombe na baadhi ya marafiki zao kutoonekana tena mjini baada ya mirija kutoweka. Si Makamba pekee, hata Lowasa mwenyewe alipofika kwenye mkutano wa hadhara alisoma haraka haraka hadhara iliyokuwepo pale na kubaini kwamba akipeleka zile ngonjera zake zaMwanza na Kigoma angeumbuka, naye akajikuta akimfagilia.

Wananchi wa Kyela sio wajinga kumkumbatia mtu asiye na tioja kwao, ni kwamba wameona kazi yake. Hata hao vijana wanaodaiwa kuwa wapambe wake wa vijiweni, jamani ni vijana wasiomtegemea Dr. Mwakyembe, wanapesa zao na hawafanyi vile kupata favour kwani wanazo shughuli zinazowaingizia vipato kuliko huo ubunge wa Dr. Wasomi wa Kitanzania tuache porojo kujifanya tunayaelewa sana masuala ya wananchi waishio vijijini wakati wenyewe tunaishia mijini.

Pili bado nataka Mtanzania asipotoshe watu kuhusu Prof Mwandosya na siasa za Mbeya. Huyu sio kingmaker wa siasa za Mbeya, na ukweli hakumuunga mkono Dr Mwakyembe na Mpesya kwa sababu aliamini kina Abson watampatia urais, na alipobaini kachuuzwa alirudi mwenyewe kwa kina Mpesya na Mwakyembe, na amshukuru mbunge mmoja viti maalumu.

Huyo Mwakipesile anayeteka Mtanzania tuamini kwamba Profesa bado anashirikiana naye ndiye aliyeongoza mambano ya kumng'oa kwenye NEC akiwatumia ma DC na viongozi wa CCM, ushirikiano huo uko wapi! Profesa sio mtoto kwamba atayarudia tena makosa ya 2005, tena hafichi chuki yake dhidi ya huyo jamaa, na ajapo Mbeya hupitiliza Rungwe hapitii kwenye ofisi ya RC. Kama hiyo haitoshi, Profesa anafahamu fika kazi anayoifanya RC kwa kumtumia yule kijana wa BOT ya kumng'oa. Na watu wanamhurumia huyo kijana kwani kubebwa na RC pale Mbeya ni kujipa nuksi kwenye siasa za Mbeya, yatamkuta yaliyomkuta Thom.

Kingine Mkuu Mtanzania hao wastaafu na huyo jamaa RC hawana nguvu yoyote Mbeya, kwani pamoja na pesa zote zilizomwagwa kwao kuvuruga mkoa wa Mbeya wameshindwa na kina bwana mkubwa sasa wanawageuka, alibaki Makamba, juzi kawaeleza ukweli.
 
Kwi kwi kwi!!! sawa wakuu, naona mmeongozana kuandika kitu kitu kimoja na kubadili fonts? Utamdanganya mjinga, mwerevu hung'amua.

Kwa taarifa tu prof. Mwandosya alishindwa urais kabla hata haijajulikana nani watagombea ubunge. CCM walimchagua Kikwete tarehe 4 May 2005, hiyo ni kabla hata ya bunge la budget. Mpaka hata June 2005 ilikuwa haijulikani kama Dr. Mwakyembe atagombea ubunge Kyela. Kwahiyo kusema aliwaunga Mwakipesile na Mwang'onda kwa mategemeo kwamba Apson angempatia urais ni makosa makubwa. Uko wrong kwenye facts na pia uko wrong kwenye timeline.

Wacha nikubali kutofautiana na tusubiri hiyo 2010. Pia wacha niwaachie wananchi wa Kyela waendelee kufaidi hayo maendeleo makubwa mnayosemwa mbunge wao kawaletea. Kama kuna mtu analeta maendeleo Kyela, nitakuwa wa kwanza kuunga mkono, maendeleo ya kweli, sio maendeleo ya ya wanasiasa kwenye majukwaa.
 


Jifunzeni kutembelea kwenu, msiwe mabingwa wa kumwaga sera kwenye mitandao tu! Analysis yako Mkuu, ni nzuri tu kwa wasomaji wa forum hii, lakini haikubaliani kabisa na assessment ya watu wa kawaida kabisa wa Kyela kuhusu Dk. Mwakyembe. Nilikuwa mmoja wa waandishi tuliofuatana na Katibu Mkuu wa CCM Makamba, katika ziara yake ya Kyela. Aliingia Kyela na mtazamo kama wako Mkuu Mtanzania, lakini akabadilika ghafla na kuanza kumpigia debe Dk. Mwakyembe baada ya kuona wananchi wa kawaida wakigombania kumshika mkono Mbunge wao na kumshangilia kila tulipopita. NJOO 2010, UTUMALIZIE UBISHI

Ijabu Issa,

Labda hapa nimtete Mtanzania ili isijekuwa ikaonekana anajitetea mwenyewe. Mie ni wa Sikonge ila ni kipindi sasa nafahamiana na Mtanzania pamoja na ndugu zake wengi. Kutokana na matatizo ya forrum, nieshindwa kuutafuta ujumbe wake alionitumia mwaliko tuonane Kyela summer hii. Ntajitahidi nikiweza ili summer nifike hapo Kyela kwa mara ya kwanza.

Mtanzania ni mtu aliyekaribu sana na Kyela. Kwenye uchaguzi wa ubunge, ndugu zake walikuwa kila siku na Mwakyembe na yeye kufahamu kila siku kinachoendelea huko. Kimradi chake kinamfanya kuwa mtu wa kufahamu kinachoendelea huko kila siku. Kila umeme ukikatika, utamsikia hapa akilia kwani ni gharama zinaongezeka.

Kwa hiyo akikuambia uchaguzi wa Mwakyembe ulikuwa hivi basi anafahamu au moja kwa moja kutoka kwa wapambe wa Mkwayembe na au hata kutoka kwake mwenyewe Mwakyembe.

Tatizo la ugomvi wa viongozi mara nyingi huwa kuna kukomoana. Unaweza kukuta Mwakipesile kwa makusudi kabisa analegeza kamba za kiatu ili umeme usiwepo Kyela, ili barabara zisijengwe Kyela nk ili mradi ni kukomoana tu. Hili nafikiri ndilo ambalo Mtanzania hataki. Kama Mwakyembe angeliwaunganisha viongozi wote, basi leo hii Mbeya/Kyela ingelikuwa kama Obama na Clinton wakiwa katika team moja. Ila wao hadi kesho ni kukomoana tu.

Issa, unaweza kuwa kwenye kikao au mkutano na kuonyeshwa picha fulani. Ila mara nyingi hiyo inakuwa ni trail tu na picha lenyewe hasa linachezwa chinichini. Mie nilikuwa mtu kuamini picha hilo unaloliona. Lazima niseme kuwa JF imenifanya kufungua macho mambo mengi sana ya Tanzania. FMes, Mtanzania, Mwanakijiji, Invisible, Kishoka, na wengine wengi wamesaidia sana kufahamu hilo. Hiyo inatokana na kwamba, wanahabari za ndani wa picha kamili na siyo trail ambayo wengine huwa tunaonyeshwa. Hivyo, na wee unapokuwa kwenye mkutano kama mwaandishi/mwana habari basi nenda zaidi. Chimba hasa kujua nini kinaendelea maana hapo unaonyeshwa trail tu na picha kamili limeshachezwa na wafahamu wa mambo wanafahamu muda huo nini kinauzwa (uongo gani unatangazwa kwa wananchi). Ukifanya hivyo basi utakuwa mwaandishi mzuri sana maana utaandika hadi kile ambacho mtu wa kawaida huwa hakioni akiwa kwenye mkutano. Ningelikuwa mie, ningelimdodosa zaidi Mtanzania kupata mambo mengi na si kusema "ohh wewe uko mbali na Kyela, wajua mambo kwa simu..." Yes, kumbuka anaweza kuwa mbali ila analijua picha lote, na wewe uko pale kila siku waona trail tu.
 
Nsesi,
Mwanzo nilikuwa nakuaminia. Ila unaanza kunipa wasiwasi kuwa wee ni mpambe wa Mwakyembe. Usitake kutuambia kuwa Mkwakyembe ni "Mtakatifu" namna hiyo. Huyo ni mwanasiasa tu. Unatuwekea picha ya mwakyembe kama vile ni mtu anayeitwa 'midas touch', everthing he touch, turns gold. Hapa ndiyo naona unaanza kunifunga kamba. Kitu kama hicho dunia ya leo hakipo.

Sijui umelipwa au umeahidiwa kiasi gani? Au ni mapenzi tu? Pulizii nyie watu. Mnalaani wanasiasa kwa ufisadi wakati nyie wenyewe mnashindwa kuandika ukweli. Dunia hii siyo black or white only. Wee uandishi wako unaanza kutupa hiyo sura. Sijawahi kufika Kyela ila sihitaji kufika huko kujua nini kinapikika. Mwakyembe anaweza/atashinda uchaguzi ujao. Hiyo siyo big deal. Kinachosemwa hapa ni kuwa viongozi waungane nguvu ili kusaidia wananchi na siyo kufanya kazi na kusubiri, akija kwenye anga zangu basi namlipua ili wananchi waone ubovu wake.

Mie naungana na wanaosema kuwa kiongozi anaweza kuwa Mhindi, Mwanamke, Albino, Kilema, kipofu, mfupi, Mrefu, Mkala, Mgogo, nk nk nk. Cha muhimu ni kuwa ile last product yaani maendeleo kwa wananchi yafike, basi. Hivyo, mwambie Mwakyembe a-solve ugomvi wake na RC na wawe team moja kwa ajili ya maendeleo na maisha ya kila siku ya watu wa Kyela, Mbeya na Tanzania kwa ujumla.
 
Asante Mkuu Sikonge,

Ukitaka kujua ukweli utaupata tu, bora uliza maswali ya ziada. Kwa mfano mtu anakuja na kusema alishinda kwa asilimia 93, wewe mwulize alimshinda nani? Utakuja gundua alikishinda kivuli. Dr. Mwakyembe alipata ushindani upande wa CCM lakini sio kwenye uchaguzi wa jimbo maana upinzani hawakuweka mtu wa maana yeyote. Hata ukiangalia matokeo ya Kyela anatajwa Dr peke yake.

Anasema 2000 Mwakipesile alishinda kwa asilimia 52, ni kweli lakini alimshinda nani? Utakuta kulikuwa na mchuano mkali kati ya Mwakipesile na jamaa ambaye sasa ndiye mwenyekiti wa CCM wa wilaya, enzi hizo akiwa chini ya Mrema.

Simtetei Mwakipesile na in fact nilimpinga kwa nguvu zote 2005 na kumuunga mkono Dr. Mwakyembe lakini ni muhimu kuweka facts sawa.

Hayo ya kwamba mtu hayuko sehemu basi hajui kitu, ndio weakness yetu. Kuna wazungu wako Ulaya, wanaijua Tanzania kuliko sisi Wazaramo wa kariakoo.

Ukiona mtu anakataa hata kwamba prof. Mwandosya ni kingmaker wa siasa za Mbeya, utasema huyo anajua ya Mbeya kweli?

Rudia maandishi ya Nsesi kuhusu diwani wa Kyela mjini, utagundua ni ubaguzi tu kwasababu huyo jamaa ni Mkinga. Anaandika majungu kibao ambayo hayana ukweli wowote. Juzi kwenye kura za wanaoua Albino, hao wapambe wameenda kupiga kura kibao kuonyesha huyo diwani ni jambazi. Sioni sababu yoyote ya kufanya hivyo kwa mtu ambaye ameishi Kyela miaka na miaka, kawekeza Kyela na sasa anaongoza kusukuma mbele maendeleo ya kata yake. Kwasababu haelewani na baadhi ya waheshimiwa basi imekuwa balaa. Vitu kama hivyo ndivyo vinatuudhi sisi wengine.

Wacha tuendelee kuelemishana.
 
I dont vote for CCM & whoever votes for them must be counted as Fisadi mpaliliaji, hivyo ikiwa wananchi wa Kyela wanatoa sapoti kwa mfuasi yeyote yule wa Sultani CCM awe Mwakiembe au Mwakibibo huyo haitakii mema Tanzania ,CCM ni Chama ambacho kinambadilisha mtu mwema na kuwa muovu tena muovu wa kupindukia maana kama ni mpya basi atawashinda aliowakuta kwa uovu na yupo tayari kuua.

Ujumbe kwa wanachi wa Kyela msukumo wa Mtanzania kwa sasa si kuikumbatia au kumkumbatia mtu yeyote yule aliekuwemo ndani ya CCM, juhudi za nguvu zinazotakiwa kufanywa ni kumuondosha Sultani CCM na mayai yake popote yawapo ,haya mambo ya kusema mbunge wetu,sijui wananchi au wapiga kura wake haya ni mapandikizi ya maneno yanayopandwa pasipo ukweli kutokana na hisia za wananchi zilivyo ukichanganya na ukali wa maisha ,siamini kabisa kama wengi wa Watanzania wanawaona viongozi waliomo ndani ya CCM kama ni wa maana au ni wa kutiliwa maanani sana hasa ukipima hakuna maendeleo aliyoyapata Mtanzania chini ya Serikali ya CCM ambayo inawajumuisha viongozi wake wote wakiwemo akina Mwakiyembe na Rostamu matatizo waliyonayo ni kugombania ulaji na hakuna jingine.

Maana haya makelele wanayopigiana sio kujivutia kwa wananchi kwamba kila mmoja aonekane ni msafi bali ni kujivutia ndani ya mitandao ya Chama chao, mwananchi kwao si lolote si chochote.
 
NAAM! NI Wale wasiomwandika vibaya na akaamuwa wao tu wahudhurie kwenye mkutano wake huo.

Mkuu mkutano wa wazi huwezi kuchagua wahudhuliaji. Yeyote atakaejisikia kuhudhuria atahudhuria. Isitoshe mkutano wa Dr. Mwakyembe kila paparazi atataka kushiriki
 
Mbeya wamtahadharisha Kikwete

Mwandishi Wetu Aprili 1, 2009

Raia Mwema~Muungwana ni Vitendo

KUNA kila dalili ya historia kujirudia kwa wakazi wa Wilaya ya Kyela mkoani Mbeya. Ni ile historia inayohusu yaliyomsibu aliyekuwa Makamu wa Rais, Aboud Jumbe alipotembelea wilaya hiyo mwaka 1984 na wananchi kuamua kuanika uozo, unafiki na ufisadi wa viongozi wa wakati ule wilayani hadi mkoani kuhusu maendeleo ya maduka ya Ujamaa wilayani humo.

Wananchi wale waliwaumbua viongozi wa serikali kwenye mkutano wa hadhara kwa kuweka wazi kwamba taarifa alizokuwa akipewa kusifia maendeleo ya maduka hayo zilikuwa za kupikwa, na kwamba hayakuwa maduka ya wananchi bali ya viongozi, kwamba bidhaa alizoonyeshwa zilijazwa usiku wa kuamkia ziara yake.

Yaliyofuatia katika mkutano ule ni vurugu zilizosababisha wananchi kadhaa kukamatwa na kupelekwa kwenye mahabusu ya Tukuyu wilayani Rungwe, hatua ambayo simulizi zake zimewafanya wananchi wa wilaya hiyo leo hii kulinganishwa na wale wa Tarime mkoani Mara kwa misimamo yao isiyotetereka.

Baada ya wenzao kukamatwa, makundi ya wananchi kutoka wilayani humo walikwenda kwenye mahabusu hiyo ya Tukuyu wakidai kuwa siku ya hizo fujo nao walikuwapo hivyo wakamatwe, inaelezwa kuwa serikali ilisalimu amri; kwani ililazimika kuwaachia wote kwa hofu ya uwezekano wa wilaya nzima kuhamia kwenye mahabusu hiyo.

Leo, wananchi wa wilaya hiyo wanaamini kuwa wamefikishwa katika hali ile ile ya mwaka 1984 kutokana na vitendo vya unyanyasaji unaofanywa na Polisi mkoani humo kila wanapopanga mambo yao ya kisiasa yanayomhusisha mbunge wao, kwa sababu tu hayawafurahishi wakubwa mkoani humo.

Safari hii ishara zimeanza kujionyesha katika malumbano yaliyoibuka hivi karibuni kati ya Mbunge wa Jimbo hilo la Kyela, Dk. Harrison Mwakyembe na Mbunge wa Igunga, Rostam Aziz yenye mizizi yake kwenye sakata la ununuzi wa mitambo chakavu ya Dowans.

Sakata hilo sasa linasambaa kama moto wa nyika na tayari limewafikia wapigakura wa wilaya hiyo ya Kyela, ambao wameamua kuvunja ukimya na kujitokeza kusimama na mbunge wao, Dk. Mwakyembe.

Wananchi hao, wakiongozwa na viongozi wao wa jadi na wazee waliandaa maandamano makubwa mjini Kyela, Jumapili iliyopita, maandamano ambayo katika dakika zake za mwisho yalizuiwa kwa amri ya Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mbeya, Zelothe Stephen. Hatua hiyo imeacha maswali mengi yasiyo na majibu.

Lakini swali ambalo linaendelea kuwasumbua wananchi wa Kyela kutokana na amri hiyo ni kuhusu nafasi ya jeshi hilo katika kulinda demokrasia nchini. Wananchi hao walisikika wakiulizana: "Hivi Jeshi la Polisi mkoani Mbeya liko kwa ajili ya nani hasa, wananchi au wakubwa pale mkoani?"

"Tunakoelekea ni kubaya na wa kulaumiwa ni Rais Jakaya Kikwete mwenyewe kwani; ameigawa Kyela," alisikika mwananchi mmoja akizungumza baada ya polisi kuwaamuru wananchi hao kuondoka eneo la Community Center ambako ndiko maandamano hayo yalikuwa yaanzie.

Alipobanwa na waandishi wa habari waliofika eneo hilo kutoa ufafanuzi wa hatua hiyo ya kuzuia maandamano hayo ya wananchi, kiongozi mmoja wa ngazi ya juu wa jeshi hilo wilayani Kyela alibainisha kwamba wameamriwa na Kamanda wao wa Mkoa kuzuia kufanyika kwa maandamano hayo kwa sababu za kiusalama.

Sababu zilizotolewa ni pamoja na kuwapo kwa Naibu Waziri wa Fedha na Uchumi wilayani humo, ambaye hata hivyo hakuonekana mjini Kyela siku hiyo.

Kiongozi huyo alidai zaidi kwamba wakubwa kule mkoani wameyazuia maandamano hayo eti yangewabughudhi watu waliokuwa makanisani na wafanyabiashara wa mji huo wa Kyela!


Ni wazi zilikuwa sababu za kitoto ambazo ziliwaudhi zaidi wananchi; kwani waliichukulia hatua hiyo kuwa ni uvunjaji wa Katiba kwa wakubwa hao wa mkoani kuwaingilia mno katika masuala yao ya ndani.

Hata hivyo, busara ya mbunge huyo, kwa kufika eneo hilo la Community Center pale alipopata taarifa za waandamanaji kugoma kutii amri ya Polisi, iliepusha madhara ambayo yalikuwa yatokee; kwani aliwasihi kuachana na maandamano na badala yake waende moja kwa moja uwanjani walikopanga kukutana naye.

Maandamano hayo yaliandaliwa na wananchi wa kawaida kabisa wa wilaya hiyo wakiongozwa na viongozi wao wa jadi kwa maana ya machifu na mafumu pamoja na wazee, na kupata baraka kutoka uongozi wa Jeshi la Polisi wilayani humo.

Lengo la wananchi hao kuandaa maandamano hayo ambayo walipanga yapokewe na mbunge wao mwenyewe ilikuwa kumshinikiza awafafanulie ukweli wa habari iliyoandikwa na gazeti moja litolewalo kila wiki (sio Raia Mwema), likidai Dk. Harrison Mwakyembe atavuliwa ubunge.

Baada ya habari hiyo kuchapishwa, wananchi hao walitaka kufahamu mwenye mamlaka na nguvu ya kumvua ubunge mbunge wao waliyemchagua kwa asilimia 93, kwamba ni wabaya wake, Rais, Spika au wapiga kura wake ambao ni wao wananchi wa jimbo la Kyela?

Hatua ya polisi mkoani Mbeya haikuwaudhi wananchi tu; bali hata mbunge wao huyo ambaye wakati akijibu hoja za wapiga kura wake, kama walivyozibainisha katika risala yao kwake, alisema amechoshwa na manyanyaso mara kwa mara anayofanyiwa pamoja na wananchi wake na uongozi wa mkoa huo; hivyo kuelezea dhamira yake ya kulifikisha suala hilo kwa Rais Kikwete.

Sehemu ya risala ya wananchi hao kwa mbunge inasema: "Madhumuni ya maandamano haya ni kuelezea hisia zetu na kupata maelezo yako kuhusu maana na lengo la kampeni ya chuki inayoendeshwa dhidi yako na baadhi ya magazeti. Mbali na kuonyesha dhahiri nia ya kutaka kukuchafua tu kisiasa, magazeti hayo sasa yanadai mbunge wetu uondolewe ubunge."

Wapiga kura hao wametangaza rasmi kumpigania mbunge wao; kwa sababu wanaamini kwamba chuki dhidi ya mbunge wao huyo mizizi yake ni kamati ya kuchunguza zabuni ya kufua umeme wa dharura ambayo taarifa yake iliwang'oa mawaziri kadhaa.

"Tangu muda huo, siku haipiti bila habari au maoni au makala moja au zaidi inayomshambulia mbunge wa Kyela. Mara kaiba maji ya DAWASCO, mara yeye na wenzake waliandika taarifa yao baada ya muda kupita, mara si mwana mtandao, mara anatumiwa na mambo mbalimbali ya kipuuzi..," inasema sehemu ya risala hiyo.


Lakini kinachowafadhaisha zaidi wananchi hao wa Kyela ni jinsi Chama cha Mapinduzi (CCM) kinavyolishughulikia jambo hilo kwamba pamoja na kuwapo mkakati huo wa wazi, chama hicho hukaa kimya hadi pale watu wanapomnyooshea kidole bwana mkubwa huyo.

Wananchi hao wanahitimisha risala yao kwa kusema kwamba Dk. Mwakyembe alichaguliwa kwa asilimia 93 ya wapigakura wa Kyela na kwamba hata mwakani watampa ushindi huo huo. "Mwakani wana-Kyela tunasema: Rais ni Jakaya Mrisho Kikwete na mbunge ni Harrison George Mwakyembe.


Katika hili Rais Jakaya Kikwete anapaswa kuelewa kwamba anapolea uozo kama huo wa kudumaza demokrasia na kuwanyima wananchi haki yao ya msingi na kikatiba, anazidisha hasira ya wananchi dhidi yake yeye na wala si hao wasaidizi wake.

Wananchi wa Kyela wanaamini kwamba Rais wao ndiye chanzo cha matatizo yote ya kisiasa yanayowasibu wilayani humo pamoja na mbunge wao.
kwani kuwa mwanasiasa mwenye kumweka masilahi ya umma mbele unahitajika kuwa ndani ya CCM???

MWAKYEMBE acha unafikii, komaa kiakili na kimawazo na ufuate moyo wakooo...HAMA CCM utetee masilahi ya ummaa...

wapo waliohama na mchango wao kwenye utetezi wa taifa ni kupigiwa mfanooo..(dr slaa)

Jifunze na fanya maamuzii...CCM haikuhitajiiii kwa sasa (soma alama za nyakati)
 
Nsesi,
Mwanzo nilikuwa nakuaminia. Ila unaanza kunipa wasiwasi kuwa wee ni mpambe wa Mwakyembe. Usitake kutuambia kuwa Mkwakyembe ni "Mtakatifu" namna hiyo. Huyo ni mwanasiasa tu. Unatuwekea picha ya mwakyembe kama vile ni mtu anayeitwa 'midas touch', everthing he touch, turns gold. Hapa ndiyo naona unaanza kunifunga kamba. Kitu kama hicho dunia ya leo hakipo.

Sijui umelipwa au umeahidiwa kiasi gani? Au ni mapenzi tu? Pulizii nyie watu. Mnalaani wanasiasa kwa ufisadi wakati nyie wenyewe mnashindwa kuandika ukweli. Dunia hii siyo black or white only. Wee uandishi wako unaanza kutupa hiyo sura. Sijawahi kufika Kyela ila sihitaji kufika huko kujua nini kinapikika. Mwakyembe anaweza/atashinda uchaguzi ujao. Hiyo siyo big deal. Kinachosemwa hapa ni kuwa viongozi waungane nguvu ili kusaidia wananchi na siyo kufanya kazi na kusubiri, akija kwenye anga zangu basi namlipua ili wananchi waone ubovu wake.

Mie naungana na wanaosema kuwa kiongozi anaweza kuwa Mhindi, Mwanamke, Albino, Kilema, kipofu, mfupi, Mrefu, Mkala, Mgogo, nk nk nk. Cha muhimu ni kuwa ile last product yaani maendeleo kwa wananchi yafike, basi. Hivyo, mwambie Mwakyembe a-solve ugomvi wake na RC na wawe team moja kwa ajili ya maendeleo na maisha ya kila siku ya watu wa Kyela, Mbeya na Tanzania kwa ujumla.

Mkuu Sikonge, hii tabia ya sisi Waswahili kukimbilia conclusion kwamba "mtu kalipwa" simply because hukubaliani naye au anajenga hoja tofauti na wewe, inatokana na nini? Kasumba, ushamba, historia yetu ndefu ya utumwa na ya kutawaliwa? Pamoja na hoja zako nzuri, una haribu unapokimbilia dhana hiyo ya kitoto ya kwamba mwenzio kalipwa! If that is the rule, wewe umelipwa na nani - Kapuya, Kaboyonga, Rostam au Ntimizi?
 
Dr Mkwayembe amefanya kazi jimboni mwake na ndio maana bado wanamkubali, usingojee kuelezwa nenda mwenyewe vijijini utapata jibu la kukubalika au kutokubali kwake.

Suala wa vijana kukaa vijiweni na Kyela kulishwa na Rungwe ni ufinyu wa kufikiri, hivi Rungwe wanalima mpunga na mchele wanaokula unatoka wapi? Na hilo sio tatizo la Kyela, Rungwe au Mbeya ni tatizo la nchi nzima, Kyela wanasikika kwa sababu ni wazungumzaji. Hivi vijiwe vilivyoko pale Ushirika, Tukuyu Mjini, Katumba, KK, Mwakaleli ni vijana kutoka Kyela!!

Lazaro, hadi hapo utaona kuwa kijana anajikanyaga mwenyewe. Kwanza anasema vijana wa Kyela kijiweni ni ufinyu wa kufikiri. Na chini zaidi anaandika vijiwe vya ushirika Tukuyumjini, Katumba, KK, Mwakaleli ni vijana kutoka Kyela. Hawa kama kwao ni poa na kazi za kufanya kibao, kwa nini wawe kijiweni? Tena hadi wana ushirika, sijui wa nini?


Nsesi,
Mwanzo nilikuwa nakuaminia. Ila unaanza kunipa wasiwasi kuwa wee ni mpambe wa Mwakyembe. Usitake kutuambia kuwa Mkwakyembe ni "Mtakatifu" namna hiyo. Huyo ni mwanasiasa tu.
Sijui umelipwa au umeahidiwa kiasi gani? Au ni mapenzi tu? Pulizii nyie watu.

Lazaro, nimeandika SIJUI na nimei-underline. Wewe wasema nimekimbilia conclusion...... Ok, umeuliza sababu ya kufanya hivyo. Sababu ni moja tu ambayo wewe umeshai-conclude, nayo ni USHAMBA. Wee ulitegemea nini kutoka kwa mtu anayeishi Sikonge??

Mkuu Sikonge, hii tabia ya sisi Waswahili kukimbilia conclusion kwamba "mtu kalipwa" simply because hukubaliani naye au anajenga hoja tofauti na wewe, inatokana na nini? Kasumba, ushamba, historia yetu ndefu ya utumwa na ya kutawaliwa? Pamoja na hoja zako nzuri, una haribu unapokimbilia dhana hiyo ya kitoto ya kwamba mwenzio kalipwa! If that is the rule, wewe umelipwa na nani - Kapuya, Kaboyonga, Rostam au Ntimizi?


Nimeipenda hii ya UTUMWA. Inawezekana nayo imechangia. Halafu hao walipaji mbona umeweka wa Tabora tu? Hivi huyo Kaboyanga ndiyo nani? Mwenzio Mshamba wa SIKONGE siwafahamu wengi.

Asante kwa maneno yako. Nilikuwa sijui kama nina dhana ya kitoto. Nitajitahidi sana siku nyingine kuicha. Lazima nikiri maneno yako mazito na ya busara nzito. Maneno kama haya sijawahi kuyasikia katika maisha yangu yote. Ujaliwe kwa busara zako nzito, na kwa uhakika utafika mbali kwa busara zako hizo. Watu kama nyie mngelikuwepo wengi basi Tanzania tungelikuwa mbali sana. Ubarikiwe.
 
Last edited:
Back
Top Bottom