Habari za afya ya Dr. Harrison Mwakyembe

Wakuu kwa kitendo cha Chenge na hatimaye Mwakyembe kuugua nimeingiwa na wasi wasi kwamba vijisenti vimefanya kazi Russia na kupata yale magadi ya KGB na mtu wao London na sasa yanaweza yakawa ndiyo yatakayo mkutaka Mwakyembe .A thotough investigation is needed na Mwakyembe need to be tested kwa kila namna .
 
yale Madini Ya Kgb..ukitumia Kwa Kumimina Kila Kiti Na Ukizingatia Lile Jengo Lina Centralised Ac...ingekuwa Balaa ...lazima Wabunge Asilimia Kubwa Wangezurika Akiwemo Mnyunyizaji......kazi Kama Ile Hufanywa Na Majasusi Waliokubuhu...kwa Direct Application Tena Dose Lazima Iwe Ndogo Sana..kadiri Dosage Inapozidi Kifo Hutokea Haraka Zaidi Tena Kwa Dalili Za Moja Kwa Moja,kama Yule Nwandishi Wa Russia Alipewa Dozi Kubwa Kiasi Hakukatiza Wiki Na Hata Mtoto Mdogo Alijua Ni Sumu,dosage Ikiwa Ndogo Mdhurika Hufa Softly Such That Its Hardly Kuhusisha Na Mauwaji Ya Kijasusi...because Otherwise Kwa Kupaka Kila Kiti Ingeweza Kuwauwa Wasiohusika....so Guys Rule Out Kama Walikuwa Wanapaka Vitu Kwenye Viti..basi Hizo Ni Imani Za Kishirikina!

...kama jasusi angetaka kumdhuru mwakyembe kwa sumu njia rahisi ingekuwa kupaka kwenye shuka kwenye gest aliyofikia au kwenye chombo ,kifaa anachotumia...and these is confined to handful known people within the system......sasa kama nafikia mahali kundi la kisiasa linakuwa na chemikali za kuuwa wenzao ambazo kwa kawaida humilikiwa na serikali..basi watanzania tutakuwa tumefikishana mahali pabaya...na kwa namna MTANDAO walivyo basi ,viongozi watamalizana wote!
 
Hakuna cha madini ya KGB wala nini, huo ni ushirikina wa mswahili ambao umekuwa ukitukwamisha kwa miaka kuleta maendeleo.

Madini ya KGB au hata sumu huwezi kuweka kwenye viti vya wabunge ukitegemea eti kesho yake yafanye kazi, kama ni kufanya kazi basi kila mtu kwenye hilo jengo angelidhurika.

Tunalipa nguvu mno suala la uchawi wakati kiukweli hao wachawi hawana lolote zaidi ya vichwa vyao kuwa na matatizo.

Mimi nimejitolea kuwa guinea pig, kama kuna mtu ana huo uchawi basi aje anyunyizie nyumbani kwangu na kama kuna mtu atadhurika basi tutamlipa.

Kwa yanayoongelewa sasa Tanzania, tunawatisha hata wabunge wazalendo ambao wanataka kupambana na mafisadi.
 
Heshima mbele wakuu, kwanza mimi nalaani vikali kitendo hiki kutokea katika sehemu yetu tukufu,maana mambo haya tumezoea kusikia yakitokea huku uswahilini tunakoishi,ni aibu kubwa kwa bunge,halafu kitu kingine jamani hivi huyu Chenge ana fanya nini bungeni mpaka sasa?? KWANINI asijiuzulu?? huyu ni FISADI inatakiwa afukuzwe haraka sana la sivyo ataharibu kila kitu maana alikua wa kwanza kupinga vikali ripoti ya Richmond ndani ya bunge tena kwa jeuri wakati alipokua waziri
 
Chenge msomi wa Havard University.

Hana uchawi wowote, anatishia tu, waoga wakapata mshutuko, wanaojiamini hakuna kitu.

Wait a minute!!!! naomba ufafanuzi, Chenge ametajwa hapa kuwa anausika na hayo mauzauza au ametajwa hapa kwa kuwa amesona Havard? Ufafanuzi Please
 
Wait a minute!!!! naomba ufafanuzi, Chenge ametajwa hapa kuwa anausika na hayo mauzauza au ametajwa hapa kwa kuwa amesona Havard? Ufafanuzi Please

Mkuu,

Chenge ndiye anahusika kunyunyizia juju viti vya waheshimiwa.
 
Mkuu,

Chenge ndiye anahusika kunyunyizia juju viti vya waheshimiwa.

Asante mkuu kwa ufafanuzi. Sasa naamini maneno niliyowahi kuambiwa na mtu mmoja ambaye aliwahi kuwa mbunge na kwa sasa ni mstaafu pia mwingine ambaye aliwahi kugombea ubunge kuwa "aslimia 95 -98 ya wabunge wote wanaamini ushirikina" nikamuuliza kwa nini? akasema sometimes wapambe wao wanawalazimisha kufanya hivyo hata kama wao wenyewe hawapo willing. Na kama hutaki basi wanakuacha na hawaendelei na kampeni.

Mimi Binafsi siamini uchawi ndio maana sitaweza kugombea nafasi kwenye siasa. Ninachojiuliza mimi ina maana huo uchawi unafanya kazi kikubwa hivyo? ina maana wanaweza hata kuwaloga wapiga kura wetu badala ya kuwapigia kura watu walio wazuri wanaendelea kuwapigia wale wale? Kama haya kweli yanawezekana basi Tanzania kuna kazi kubwa sana ya kumkomboa mtanzania kutoka kwenye wimbi la umaskini kwani nguvu za giza ndio zinafanya kazi badala ya akili za kawaida za binadamu.

Mama Getrude Lwakatare Mbunge wa kuteuliwa tunamuomba kesho jumatatu kabla ya kuanza kikao cha bunge apige maombi ya kutosha kabisa, waalikwe pia Mashehe, maaskofu mbalimbali iwe ni kuomba tuu na kufukuza nguvu zote za giza ndani ya bunge ili liweze kuwa huru kuijadili hii budget, EPA, Richmond, KIWIRA, na mengineyo ambayo ni muhimu sana kwa Mustakabali wa taifa letu lenye raslimali nyingi sana kila upande lakini wananchi wetu wanazidi kuwa maskini wa kutupwa.

MUNGU IBARIKI TANZANIA, WABARIKI WATU TULIOWAPA DHAMANA YA KUIONGOZA HII NCHI, PIA WALAANI WALE WOTE WALIOPATA DHAMANA KUTOKA KWA SHETANI
 
Kwa hiyo Muhusika Mkuu wa hili Sakata zima ni Chenge... maana nimefuatilia sana na mpaka mda huu nilikuwa sijapata jina la Muhusika. kama ni kweli tunahitaji kuAngalia na kupambanua kujua ni nini mwelekeo wa Serikali ya Tanzania...Serikali ya Muungwana.

Nchi yetu ni ya
 
Tanzania, serikali ya awamu ya nne ya mauza uza na mazingaombwe! hvi jambo moja la kushangaza husiana na hawa mafisadi....wanapojiuzuru uwaziri huwa katika mtazamo wao ni kwamba wanakuwa wametakasika?

muungwana nae kila wakati ooh nimesikitishwa na kushtushwa na taarifa za kwamba fisadi amejiuzulu...ni kwa nini? kwa nini waendelee kung'ang'ania ubunge?

Nadhani its about time tuanze wabonda mawe hawa mafisadi mpaka wafe!

given a chance ntaanza na Visenti.!
 
Mbeya wamtahadharisha Kikwete

Mwandishi Wetu Aprili 1, 2009

Raia Mwema~Muungwana ni Vitendo

KUNA kila dalili ya historia kujirudia kwa wakazi wa Wilaya ya Kyela mkoani Mbeya. Ni ile historia inayohusu yaliyomsibu aliyekuwa Makamu wa Rais, Aboud Jumbe alipotembelea wilaya hiyo mwaka 1984 na wananchi kuamua kuanika uozo, unafiki na ufisadi wa viongozi wa wakati ule wilayani hadi mkoani kuhusu maendeleo ya maduka ya Ujamaa wilayani humo.

Wananchi wale waliwaumbua viongozi wa serikali kwenye mkutano wa hadhara kwa kuweka wazi kwamba taarifa alizokuwa akipewa kusifia maendeleo ya maduka hayo zilikuwa za kupikwa, na kwamba hayakuwa maduka ya wananchi bali ya viongozi, kwamba bidhaa alizoonyeshwa zilijazwa usiku wa kuamkia ziara yake.

Yaliyofuatia katika mkutano ule ni vurugu zilizosababisha wananchi kadhaa kukamatwa na kupelekwa kwenye mahabusu ya Tukuyu wilayani Rungwe, hatua ambayo simulizi zake zimewafanya wananchi wa wilaya hiyo leo hii kulinganishwa na wale wa Tarime mkoani Mara kwa misimamo yao isiyotetereka.

Baada ya wenzao kukamatwa, makundi ya wananchi kutoka wilayani humo walikwenda kwenye mahabusu hiyo ya Tukuyu wakidai kuwa siku ya hizo fujo nao walikuwapo hivyo wakamatwe, inaelezwa kuwa serikali ilisalimu amri; kwani ililazimika kuwaachia wote kwa hofu ya uwezekano wa wilaya nzima kuhamia kwenye mahabusu hiyo.

Leo, wananchi wa wilaya hiyo wanaamini kuwa wamefikishwa katika hali ile ile ya mwaka 1984 kutokana na vitendo vya unyanyasaji unaofanywa na Polisi mkoani humo kila wanapopanga mambo yao ya kisiasa yanayomhusisha mbunge wao, kwa sababu tu hayawafurahishi wakubwa mkoani humo.

Safari hii ishara zimeanza kujionyesha katika malumbano yaliyoibuka hivi karibuni kati ya Mbunge wa Jimbo hilo la Kyela, Dk. Harrison Mwakyembe na Mbunge wa Igunga, Rostam Aziz yenye mizizi yake kwenye sakata la ununuzi wa mitambo chakavu ya Dowans.

Sakata hilo sasa linasambaa kama moto wa nyika na tayari limewafikia wapigakura wa wilaya hiyo ya Kyela, ambao wameamua kuvunja ukimya na kujitokeza kusimama na mbunge wao, Dk. Mwakyembe.

Wananchi hao, wakiongozwa na viongozi wao wa jadi na wazee waliandaa maandamano makubwa mjini Kyela, Jumapili iliyopita, maandamano ambayo katika dakika zake za mwisho yalizuiwa kwa amri ya Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mbeya, Zelothe Stephen. Hatua hiyo imeacha maswali mengi yasiyo na majibu.

Lakini swali ambalo linaendelea kuwasumbua wananchi wa Kyela kutokana na amri hiyo ni kuhusu nafasi ya jeshi hilo katika kulinda demokrasia nchini. Wananchi hao walisikika wakiulizana: “Hivi Jeshi la Polisi mkoani Mbeya liko kwa ajili ya nani hasa, wananchi au wakubwa pale mkoani?”

“Tunakoelekea ni kubaya na wa kulaumiwa ni Rais Jakaya Kikwete mwenyewe kwani; ameigawa Kyela,” alisikika mwananchi mmoja akizungumza baada ya polisi kuwaamuru wananchi hao kuondoka eneo la Community Center ambako ndiko maandamano hayo yalikuwa yaanzie.

Alipobanwa na waandishi wa habari waliofika eneo hilo kutoa ufafanuzi wa hatua hiyo ya kuzuia maandamano hayo ya wananchi, kiongozi mmoja wa ngazi ya juu wa jeshi hilo wilayani Kyela alibainisha kwamba wameamriwa na Kamanda wao wa Mkoa kuzuia kufanyika kwa maandamano hayo kwa sababu za kiusalama.

Sababu zilizotolewa ni pamoja na kuwapo kwa Naibu Waziri wa Fedha na Uchumi wilayani humo, ambaye hata hivyo hakuonekana mjini Kyela siku hiyo.

Kiongozi huyo alidai zaidi kwamba wakubwa kule mkoani wameyazuia maandamano hayo eti yangewabughudhi watu waliokuwa makanisani na wafanyabiashara wa mji huo wa Kyela!


Ni wazi zilikuwa sababu za kitoto ambazo ziliwaudhi zaidi wananchi; kwani waliichukulia hatua hiyo kuwa ni uvunjaji wa Katiba kwa wakubwa hao wa mkoani kuwaingilia mno katika masuala yao ya ndani.

Hata hivyo, busara ya mbunge huyo, kwa kufika eneo hilo la Community Center pale alipopata taarifa za waandamanaji kugoma kutii amri ya Polisi, iliepusha madhara ambayo yalikuwa yatokee; kwani aliwasihi kuachana na maandamano na badala yake waende moja kwa moja uwanjani walikopanga kukutana naye.

Maandamano hayo yaliandaliwa na wananchi wa kawaida kabisa wa wilaya hiyo wakiongozwa na viongozi wao wa jadi kwa maana ya machifu na mafumu pamoja na wazee, na kupata baraka kutoka uongozi wa Jeshi la Polisi wilayani humo.

Lengo la wananchi hao kuandaa maandamano hayo ambayo walipanga yapokewe na mbunge wao mwenyewe ilikuwa kumshinikiza awafafanulie ukweli wa habari iliyoandikwa na gazeti moja litolewalo kila wiki (sio Raia Mwema), likidai Dk. Harrison Mwakyembe atavuliwa ubunge.

Baada ya habari hiyo kuchapishwa, wananchi hao walitaka kufahamu mwenye mamlaka na nguvu ya kumvua ubunge mbunge wao waliyemchagua kwa asilimia 93, kwamba ni wabaya wake, Rais, Spika au wapiga kura wake ambao ni wao wananchi wa jimbo la Kyela?

Hatua ya polisi mkoani Mbeya haikuwaudhi wananchi tu; bali hata mbunge wao huyo ambaye wakati akijibu hoja za wapiga kura wake, kama walivyozibainisha katika risala yao kwake, alisema amechoshwa na manyanyaso mara kwa mara anayofanyiwa pamoja na wananchi wake na uongozi wa mkoa huo; hivyo kuelezea dhamira yake ya kulifikisha suala hilo kwa Rais Kikwete.

Sehemu ya risala ya wananchi hao kwa mbunge inasema: “Madhumuni ya maandamano haya ni kuelezea hisia zetu na kupata maelezo yako kuhusu maana na lengo la kampeni ya chuki inayoendeshwa dhidi yako na baadhi ya magazeti. Mbali na kuonyesha dhahiri nia ya kutaka kukuchafua tu kisiasa, magazeti hayo sasa yanadai mbunge wetu uondolewe ubunge.”

Wapiga kura hao wametangaza rasmi kumpigania mbunge wao; kwa sababu wanaamini kwamba chuki dhidi ya mbunge wao huyo mizizi yake ni kamati ya kuchunguza zabuni ya kufua umeme wa dharura ambayo taarifa yake iliwang’oa mawaziri kadhaa.

“Tangu muda huo, siku haipiti bila habari au maoni au makala moja au zaidi inayomshambulia mbunge wa Kyela. Mara kaiba maji ya DAWASCO, mara yeye na wenzake waliandika taarifa yao baada ya muda kupita, mara si mwana mtandao, mara anatumiwa na mambo mbalimbali ya kipuuzi..,” inasema sehemu ya risala hiyo.


Lakini kinachowafadhaisha zaidi wananchi hao wa Kyela ni jinsi Chama cha Mapinduzi (CCM) kinavyolishughulikia jambo hilo kwamba pamoja na kuwapo mkakati huo wa wazi, chama hicho hukaa kimya hadi pale watu wanapomnyooshea kidole bwana mkubwa huyo.

Wananchi hao wanahitimisha risala yao kwa kusema kwamba Dk. Mwakyembe alichaguliwa kwa asilimia 93 ya wapigakura wa Kyela na kwamba hata mwakani watampa ushindi huo huo. “Mwakani wana-Kyela tunasema: Rais ni Jakaya Mrisho Kikwete na mbunge ni Harrison George Mwakyembe.


Katika hili Rais Jakaya Kikwete anapaswa kuelewa kwamba anapolea uozo kama huo wa kudumaza demokrasia na kuwanyima wananchi haki yao ya msingi na kikatiba, anazidisha hasira ya wananchi dhidi yake yeye na wala si hao wasaidizi wake.

Wananchi wa Kyela wanaamini kwamba Rais wao ndiye chanzo cha matatizo yote ya kisiasa yanayowasibu wilayani humo pamoja na mbunge wao.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu ngoja ngoma izidi kunoga. Kwa sasa tunaanza kuvuta pumzi ili tujiandae kucheza. Yetu Macho!!
 
Samahani Mkuu Bubu just curiosity! Mwandishi wa habari hii ni miongoni wa wale wateule wa DR Mwakyembe?
 
Masanilo, hulali tu saa hizi? Au ndiyo mwatengeneza dawa na Mwalimu Juma?

Mie ngoja nilale kidogo maana macho yanafumba yenyewe..... hii JF ni kama unabwia unga maana ukishaianza, hamna cha bia wala ............... Ngoja niote MANUMBU!!!
 
Samahani Mkuu Bubu just curiosity! Mwandishi wa habari hii ni miongoni wa wale wateule wa DR Mwakyembe?

Hilo miye silijui maana siwajui waandishi wa Raia Mwema hata wale ambao wanaweka majina yao kwenye articles zao, lakini CCM wasipokuwa makini wataupoteza mkoa wa Mbeya kama ambavyo walivyoupoteza Kilimanjaro.

Tuliambiwa hapa kwamba Mwakyembe katika mkutano ule alitumia muda mwingi kumtukana fisadi Rostam na mpaka sasa hivi sijaona pengine popote pale matusi hayo kama ilivyodaiwa na engineer. Kwa maoni yangu kama Mwakyembe angekuwa ametumia matusi basi wabaya wake ndani ya CCM wangeshalizungumza hilo la uvurumishaji matusi, lakini hadi hii leo hatujasikia lolote. Je, kulikuwa na matusi kweli yaliyotolewa na Mwakyembe ama engineer aliandika kishabiki ili kumpaka matope Mwakyembe?
 
Samahani Mkuu Bubu just curiosity! Mwandishi wa habari hii ni miongoni wa wale wateule wa DR Mwakyembe?

Hawa ndio ma-great thinkers wa JF bwana.... Mwakyembe akiumbuliwa wanafurahi na wanachangia.... akisifiwa wanakasirika na wanazira... ufuuuu
 
Mbeya wamtahadharisha Kikwete


Baada ya habari hiyo kuchapishwa, wananchi hao walitaka kufahamu mwenye mamlaka na nguvu ya kumvua ubunge mbunge wao waliyemchagua kwa asilimia 93, kwamba ni wabaya wake, Rais, Spika au wapiga kura wake ambao ni wao wananchi wa jimbo la Kyela?

Masahihisho hapo, Kyela iligawanyika katikati kati ya Dr. na Mwakipesile. Baada ya uchaguzi wa CCM ni kama Dr. hakuwa na upinzani tena.

Hilo la asilimia 93 japo ni sahihi lakini kwa mazingira ya Kyela nafikiri haina maana hiyo mwandishi anayotaka kuonyesha.

Hata mwaka 2010 Kyela itagawanyika katikati na tegemeeni mapambano makali sana kutokea huko.

Dr. Mwakyembe ana advantage kwasababu ni mbunge na anaweza kuzunguka jimboni bila kuambiwa anafanya kampeni. Tatizo kubwa zitakuwa zile ahadi zake za 2005 ambazo kwa sehemu kubwa hakuna kilichofanyika. Pia ni kama Dr. hajui kutengeneza marafiki, maana watu wengi waliomuunga mkono 2005, sasa wamejikata taratibu kwa sababu mbalimbali ikiwemo ya dharau (elimu), kutokushaurika na kukosa uongozi wa pamoja. Kiujumla dharau ndio weakness kubwa ya Dr. Kuna jamaa aliwahi kuniambia, inatosha kukaa na Dr. wiki moja tu kuweza kugundua weaknesses zake nyingi sana hasa dharau na usanii wa kusema mambo ambayo anajua wazi hawezi kufanya.

Kwa habari tulizo nazo wengine, jimbo la Kyela litakuwa gumu sana 2010 tofauti na watu walioko mbali na Kyela wanavyofikiri. Nafikiri hata Dr. kalitambua hili na mambo mengi yanayotokea sasa kwa sehemu kubwa ni siasa za Kyela. Dr. kafanikiwa kupitia magazeti ya Dar kuwafanya wengi walioko mbali na Kyela waamini atashinda kirahisi Kyela. Ukweli wa kule wilayani unaonyesha atakuwa na kazi ngumu sana.

Muda wote watu walidhani ni mpambano mwingine kati ya Dr na mwakipesile, lakini kwa taarifa za uhakika ni kwamba ni kama 100% Mwakipesile hatagombea ubunge Kyela. Hiyo inatoa nafasi kwa sura mpya kuingia kwenye ulingo. Dr angeweza kumshinda Mwakipesile kirahisi sana maana angemhusisha na ufisadi wa akina Lowassa na Rostam.

Kingmaker wa siasa za Kyela ni pamoja na prof. Mwandosya. Ila prof ni mjanja sana, hawezi kutumbukiza kichwa chake moja kwa moja. Anashirikiana na makundi yote hata kama ni kwa maneno tu. Naamini hataweza kumuunga mkono Dr moja kwa moja na atawaachia wana Kyela waamue. Anachoweza kufanya ni kumsaidia resources na kisha kuwaacha wana Kyela waamue.

Dr. Mwakyembe ana wafuasi wengi miongoni mwa wana Kyela wenye uwezo wanaoishi Dar, wakiongozwa na Kifukwe, yule aliyekuwa Yanga. Kule Kyela wanaitwa mafia wa Dar, hao ndio tegemeo kubwa la Dr. Wana mbinu nyingi, wana pesa, wana uhusiano wa karibu na Mengi. Kundi hilo hilo ndilo lilisaidia kwenda kuficha wajumbe kule Rungwe mwaka 2005 kabla ya mkutano mkuu wa uchaguzi. Kuna uvumi hili kundi ndilo limesababisha DC wa Kyela kuondolewa. Hivyo nategemea Dr. atakuwa na access ya pesa ma media ili kushinda Kyela. Tatizo lake ni kwamba wengi wa watu kwenye hili kundi hawajafanya chochote cha maana Kyela. Kwa Kyela ni kama watalii tu wanaofika Kyela na magari yao makubwa na wapambe lakini hawana muda kabisa na matatizo ya Kyela isipokuwa pale wanapokuwa na interests zao. Pia wameanza kugawanyika maana kwa mfano Mwanjala ambaye ndiye alikuwa kinara wa kubeba na kuhonga wajumbe kwa ajili ya Dr. sasa kakosana naye na ameamua yeye mwenyewe kugombea ubunge 2010. Hili kundi linakumbukwa kwa kusaidia kuanza kwa kanisa la Morovian la Kyela. Waliweza kuua njama za Rungwe kuzuia Kyela wasianzishe kanisa lao. Kuna watu bado wanawakumbuka vizuri kwa hilo.

Kundi lingine lenye nguvu ni la wale wastaafu mbalimbali ambao sasa wamejenga Kyela na kuishi Kyela. Hawa hawana uhusiano mzuri na Dr. Hili lina watu waliokuwa kwenye nafasi za juu upande wa jeshi la wananchi na polisi na foreign. Kundi hili ni pamoja na Apson mwenyewe, lina uhusiano wa karibu sana na Mwakipesile. Ni katika watu waliomshauri vizuri Mwakipesile kwamba asigombee maana ataadhirika vibaya. Hawa wanaijua Kyela vizuri sana ila sidhani kama wana influence kubwa vijijini. Wao wanaona wana influence lakini mimi nina wasiwasi kama influence yao itakuwa kubwa. Wakiungana kumuunga mtu mwingine basi atakuwa na advantage ya pesa na ushauri lakini pia atakuwa na disadvantage ya kuwa linked na mafisadi ili hata kama yeye hana uhusiano wowote na ufisadi, bado aunganishwe na Rostam kupitia hao wastaafu.

Ikifika 2010 kumbuka maneno ya hapo juu. Kyela ni katika majimbo ya kuyaangalia sana 2010. Watu wanaweza kuja kuwa shocked kuona Dr. kaangushwa na watafikiri Rostam kafanya kazi yake, kumbe ni mambo ya Kyela na siasa za Kyela.
 
Hawa ndio ma-great thinkers wa JF bwana.... Mwakyembe akiumbuliwa wanafurahi na wanachangia.... akisifiwa wanakasirika na wanazira... ufuuuu

Ndio raha ya Demokrasia na kutumia akili, kila mtu anatetea anachokiona sawa kwake au sivyo jamaa yangu?
 
Hilo miye silijui maana siwajui waandishi wa Raia Mwema hata wale ambao wanaweka majina yao kwenye articles zao, lakini CCM wasipokuwa makini wataupoteza mkoa wa Mbeya kama ambavyo walivyoupoteza Kilimanjaro.


Mkuu as long as Mwakyembe atabaki sisiemu, hawatapoteza hilo jimbo; labda wasimpitishe tu!!! lakini hata aje nani pale atapigwa chini na kajamaa kale. Na sisiemu si wajinga kiasi cha kutompitisha kwenye chaguzi za awali

Dont think all CCM members are stupid, ni wachache kama Mwakipesile ndio wenye matatizo, lakini matatizo yao yanaeleweka... kuzui masikio yasipite kichwa maana mbeya kuna watu wakiachiwa wanakuwa na vichwa kupita wakulu wao, nadhani umenielewa
 
Back
Top Bottom