wende
JF-Expert Member
- Sep 6, 2009
- 714
- 65
IBM yafungua ofisi Tanzania
na Irene Mark
na Irene Mark
KAMPUNI ya IBM imefungua tawi lake jijini Dar es Salaam ili kurahisisha upatikanaji wa huduma zake barani Afrika na Dunia nzima.
Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Meneja wa IBM hapa nchini David Sawe, alisema uzinduzi huo ni sehemu ya mpango wa kusambaza huduma za kampuni hiyo duniani.
Alisema licha ya IBM kuwepo Afrika Mashariki kwa zaidi ya miaka 50 sasa imefungua ofisi zake nchini ili kuwafikia wateja wake kipindi hiki cha kusherehekea miaka 100 tangu kuanzishwa kwake.
Tunazo sababu nyingi za kufungua ofisi Tanzania, tunaamini ipo fursa ya kupata soko la uhakika, imara, sawia na Teknolojia ya Mawasiliano (TEHAMA) pia kuna uchumi na siasa isiyoyumba.
Sababu hiyo na nyingine nyingi zimetulazimu kufungua ofisi ya IBM hapa hivi sasa, katika miaka ya hivi karibuni tumejenga uwezo wa kibiashara hapa nchini, alisema Sawe na kuongeza kwamba wameanzisha makundi ya kusambaza huduma za kibiashara kwenye sekta ya utalii, elimu na TEHAMA.
Kwa upande wake Meneja Mkuu wa IBM Afrika Mashariki, Tony Mwai, alisema hadi sasa zipo ofisi 20 za kampuni hiyo kwenye nchi mbalimbali Afrika ikiwemo Tanzania, Kenya, Misri, Afrika Kusini, Senegal na Tunisia.
Nyingine ni Ghana, Morocco, Nigeria, Algeria na kwamba mpango wa IBM ni kuwa na ofisi 40 barani Afrika ifikapo mwaka 2015 huku ikijivunia kuongeza ajira kwa nchi husika.
Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Meneja wa IBM hapa nchini David Sawe, alisema uzinduzi huo ni sehemu ya mpango wa kusambaza huduma za kampuni hiyo duniani.
Alisema licha ya IBM kuwepo Afrika Mashariki kwa zaidi ya miaka 50 sasa imefungua ofisi zake nchini ili kuwafikia wateja wake kipindi hiki cha kusherehekea miaka 100 tangu kuanzishwa kwake.
Tunazo sababu nyingi za kufungua ofisi Tanzania, tunaamini ipo fursa ya kupata soko la uhakika, imara, sawia na Teknolojia ya Mawasiliano (TEHAMA) pia kuna uchumi na siasa isiyoyumba.
Sababu hiyo na nyingine nyingi zimetulazimu kufungua ofisi ya IBM hapa hivi sasa, katika miaka ya hivi karibuni tumejenga uwezo wa kibiashara hapa nchini, alisema Sawe na kuongeza kwamba wameanzisha makundi ya kusambaza huduma za kibiashara kwenye sekta ya utalii, elimu na TEHAMA.
Kwa upande wake Meneja Mkuu wa IBM Afrika Mashariki, Tony Mwai, alisema hadi sasa zipo ofisi 20 za kampuni hiyo kwenye nchi mbalimbali Afrika ikiwemo Tanzania, Kenya, Misri, Afrika Kusini, Senegal na Tunisia.
Nyingine ni Ghana, Morocco, Nigeria, Algeria na kwamba mpango wa IBM ni kuwa na ofisi 40 barani Afrika ifikapo mwaka 2015 huku ikijivunia kuongeza ajira kwa nchi husika.