Habari njema kwa chadema

kvelia

JF-Expert Member
Jun 24, 2009
246
44
Kada wa CCM Arumeru atimkia CHADEMA

MAMBO ndani yaChama Cha Mapinduzi (CCM) yameendelea kuwa tete baada ya mmoja kati yawalioshiriki kinyang’anyiro cha kuomba kuteuliwa kugombea ubunge wa Jimbo laArumeru Mashariki kwa tiketi ya chama hicho, Anthony Musami, kutimkia Chama chaDemokrasia na Maendeleo (CHADEMA).
Mgombea huyoambaye ni mkuu wa Shule ya Sekondari ya Leguruki inayomilikiwa na Jumuiya yaWazazi wa CCM alijiunga na CHADEMA juzi, ambapo alichukua fomu za kuombakuteuliwa kugombea ubunge kupitia CHADEMA.
Musamiakiongea na mwandishi wa habari hizi kwa njia ya simu alikiri kujiunga naCHADEMA na kuongeza kuwa atazungumza na waandishi wa habari leo (Jumapili)kuelezea sababu za kujitoa kwenye chama hicho tawala.
Kada huyo waCCM aliweza kurejesha fomu hizo ambapo alifuata taratibu kwa kujaza nahivyo kuwahi kuzirejesha jana ambayo ndiyo ilikuwa siku ya mwisho yakuzirejesha.
Katibu waCHADEMA wilayani Arumeru, Totinan Ndonde, aliwaonyesha waandishi wa habari fomuza mgombea huyo ambaye alisema kuwa kama chamawalimpokea na wanaamini atafuata na kukubaliana na taratibu za CHADEMA, ikiwamokuheshimu maamuzi ya vikao halali vya chama.
Kwa upandewake, Katibu wa CCM wilayani Arumeru, Edson Lihweuli, alipopigiwa simu yake yakiganjani na kuulizwa endapo chama chake kina taarifa za kukimbiwa na kadahuyo, katibu huyo alikata simu mara moja na alipopigiwa tena simu hiyo iliitabila kupokewa.
Musami alikuwamiongoni mwa wagombea sita walioshiriki kinyang’anyiro cha kura za maoni ndaniya CCM na kuambulia kura 22 kati ya kura 1,134 zilizopigwa.
Mgombea huyoalishika nafasi ya tano kwenye uchaguzi huo ambao mtoto wa aliyekuwa mbunge wajimbo hilo, marehemu Jeremiah Sumari, Sioi Sumari, aliongoza kwa kupata kura361 akifuatiwa na William Sarakikya aliyepata kura 259, Elirehema Kaayakura 205, Elishilia Kaaya 176 na Rishankira Urio aliyeambulia kura 11.
Hata hivyokura hizo za maoni ndani ya CCM zilipigiwa kelele za kuwapo kwa vitendo vyarushwa, hali iliyosababisha mmoja wa wana CCM aliyekuwa amechukua fomu yakuomba kuteuliwa ambaye ni Rais wa Mtandao wa Maendeleo ya Vijana nchini (YDN),Elipokea Urio, kujitoa kwenye kinyang’anyiro hicho akipinga vitendo hivyo vyarushwa.
Aidha,mchakato huo wa kupata mteule wa kupeperusha bendera ya CCM umesababishamvutano mkali ndani ya Jumuiya ya Vijana ya chama hicho (UV CCM) kiasi chakutolewa kwa tamko la kumzuia mjumbe wa Baraza la UVCCM mkoani Arusha, KenedyMpumilwa, kujihusisha na kampeni kwenye jimbo hilo.
Mpumilwa nimmoja kati ya viongozi wa chama hicho waliojitokeza hadharani kupinga vikalimatokeo ya uchaguzi huo kwa madai kuwa yalitokana na ushawishi wa rushwa,kwamba mmoja wa wagombea hao kwa kushirikiana na wapambe wake waligawa fedhakwa wajumbe wa mkutano mkuu maalumu uliompitisha mgombea, hivyo akautakauongozi wa chama kuyabatilisha.
Hata hivyomwishoni mwa wiki Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, John Tendwa, akiongea na waandishi wa habari jijini Arusha alielezea kushangazwa nawale wanaolalamikia kuwapo kwa vitendo vya rushwa kwenye kinyang’anyiro hicho,kwa madai kuwa havikuwapo na akawataka wakubaliane na matokeo.

Alisema kuwa rushwa inayodaiwa kutolewa haikuwapo, kwani kiongozi wa kimila wa ukoo wa Sumari alitaka kuandaa chakula kwa ajili ya kutoa sadaka ya shukurani kutokana na msiba wa aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo, marehemu Jeremiah, lakini Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa nchini (TAKUKURU) walimfuata wakamshauri sadaka hiyo akaitoe kanisani.


SOURSE: TANZANIA DAIMA
 
Kumbe kupokea makapi ni habari njema?!. Alikuwa CCM akaomba kugombea akashika nafasi ya pili kutoka mwisho!, ameihama CCM na kuomba kugombea Chadema!, subirini kitakachofuata baada ya kutopitishwa Chadema!.
 
kwani CHADEMA wao hawana utaratibu wa kupata mgombea wao mpaka wasubiri nani atakimbia toka chama kingine ndiyo akabidhiwe fomu bila hata ya proper internal vetting?
 
hakuna cha habari njema hapo sana sana ni mzigo tu: hao ni mamluki, anakuja baada ya kubemendwa!!!! siku zote alikua wapi.
 
Huyu jamaa namfahamu kinyang'anyiro cha 2010 alikuwepo haohao ccm mpaka walichoma moto ndani ya nyumba yake bahati nzuri viliungua tu vitu vichache.
Toka hapo alikuwa njia panda hata hivyo nashangaa alijitokeza tena safari hii lazima kuna vita amefanyiwa tena na ccm wakati ni mfanyakazi katika shule Yao.
 
huyo jamaa asubili inaonekana ana uchu wa madaraka, lkn tusubuli demokrasia ya kwer ndani ya cdm, nina imani haki itatendeka na ata akikosa lkn ataridhika tu,
 
CDM wanapaswa kuwa makini na watu wa namna hiyo, wasipitishwe bila kuchunguzwa kwanza. Wasije kukusanya vibaraka wanakuja kuvuruga chama kama yule jamaa wa Shinyanga!!!!!
 
Nadhani ushindi wa CHADEMA arumeru hautegemei udhaifu wa CCM tena....hata kama waende chama kizima pale Arumeru,sasa ni mwisho.
 
Source: TANZANIA DAIMA a.k.a Gazeti la CHADEMA

Unafikili habari itakuwa fair? na chadema atatimka tena maana hatochaguliwa kupeperusha bendera! kama unataka kukubaliana na mimi angalia kauli hii "chama walimpokea na wanaamini atafuata na kukubaliana na taratibu za CHADEMA, ikiwamokuheshimu maamuzi ya vikao halali vya chama" Chama kina wenyewe hicho bora ungebaki na Uwalimu mkuu wa shule ya CCM
 
Je, kwenye kundi la wazee wetu maarufu kama Washili huko, mpaka hivi sasa watakua watakua wamepuputika na kubakia idadi gani ya wale 'Washili wa Tendwa', wenye kutishia watu vifo hapo vijijini, ukilinganisha na wale 'Washili Orijino' wale wazee wa ukweli wa kudumisha mila na amani kwa wote bila kufuata itikadi za kisiasa nchini?
 
kupotea njia kujua njia, kama kajiunga na chama mara moja anakuwa na haki ya kugombea lakini wajibu wa kupitisha mgombea ni la chama kama kitaona huyo aliyepata kura 22 za ccm atakiletea ushindi atateuliwa huyohuyo lakini ajue wagombea ni wengi na huku hakuna rushwa ndiyo raha ya CHADEMA
CDM wanapaswa kuwa makini na watu wa namna hiyo, wasipitishwe bila kuchunguzwa kwanza. Wasije kukusanya vibaraka wanakuja kuvuruga chama kama yule jamaa wa Shinyanga!!!!!
 
Kumbe kupokea makapi ni habari njema?!. Alikuwa CCM akaomba kugombea akashika nafasi ya pili kutoka mwisho!, ameihama CCM na kuomba kugombea Chadema!, subirini kitakachofuata baada ya kutopitishwa Chadema!.

Mkuu Pasco,
Mtu kuondoka chama kimoja kwenda kingine haimaanishi ni makapi.Watu walio upinzani they were one time CCM.Hata hapo katika swala la makapi kidogo nadhani unahitaji kueleza ni makapi kivipi kwa sababu unaweza kutuaminisha kila aliyeshindwa basi ni makapi.Katika mazingira ya kidemokrasia hio sio sahihi.

Kumbuka huyu msami amechukua maamuzi magumu sana ya kuondoka CCM wakati huu,yeye mwenyewe ni mkuu wa shule ya wazazi ya CCM,Kwa hio hilo swala lina implication katika ajira yake.Kwamba ameondoka CCM kwa sababu ya rushwa kutawala,ameenda CDM anapoamini hakuna rushwa hivyo ameenda katika chama ambacho watu wanashindanishwa kwa haki.Naamini akishindwa kwa haki atakuwa comfortable.I stand to defend the guy.
 
In a way ni habari yakufurahisha na kusikitisha kwamba tayari process za kuchakachua mambo zimeanza,na sijui huyu jamaa anayehama chama kitu gani kinachomshangaza mpaka anahama alipaswa kufahamu utaratibu wa chama chake 'kuridhi vyeo'
 
Back
Top Bottom