Habari muhimu kuhusu mgomo wa wanafunzi wote wa vyuo vikuu tanzania

unahamasisha mgomo halafu unafanya kosa kama hapo kwenye red!!!
nakushauri wewe na wenzako wa mwaka wa tatu muanzishe mfuko wa kusomesha wadogo zenu,kama mwaka watatu katika fani zote na vyuo vyote nchini wakichangia huu mfuko mtaweza kusomesha japo mwanafunzi mmoja na baada ya miaka mitano mtaweza kusomesha wanafunzi 30.ili mfuko uwe endelevu basi wanaokopeshwa watarejesha kwa riba nafuu.tuache kufikiria maandamano kila siku tuchangamshe vichwa hasa sisi wasomi.maandamano tuwaachie wamachinga na wanaappolo.

umeanza kuchangia kwa kichwa ila mwisho umemalizia kwa masaburi,maandamano ndio fimbo ya mnyonge ya kudai haki,haijalishi ni msomi,mmachinga au nani,hata huko kwenye nchi zlizoendelea mfano uingereza,wanafunzi na wasomi toka vyuo vyenye heshima kama oxford huwa wanaandamana pindi wanapoona serikali inafanya mambo ya ajabu ambayo yanalenga kuhatarisha wao kupata fursa muhimu kama elimu.so jiangalie mkuu,sio unakurupuka tu kama hawa watawala wa magamba.over
 
we ni mbaguzi mwazisha mada anaunganisha nguvu wewe unavunja acha hizo.

Sijavunja maada ila ni ukweli kuwa wana UDOM mmejidhalilisha sana kuwatelekeza Viongozi wenu ambao walikuwa wanapigana mpate hizo field zenu za macourse yenu mapya.MPO WENGI KAMA INZI LAKINI HAMNA IMPACT YOYOTE KATIKA MAPINDUZI YA MAMBO YA WANACHUO.Au kwa kuwa mmeambiwa chuo mmejengewa na Serikali ya CCM (ile ni kodi zenu na makato ya wazazi wenu HAMKENI VILAZA WAKUBWA NYIE)
 
Sina ham na wana udom, 2megoma wote thn leo wako chuo cc hm afu no othr reaction
 
Nyie c ndo mnaomzomeaga rais...kuleni kelele zenu sasa!Na hatushindwi kuwatimua wote..muanze tena application hatuna shda sisi...wasom wa cku hz ovyoo kabisa,,,yoo


leo unaongea umekaa tena kwa kuzungukwa na Malaika huko Mbinguni ila maamuzi yetu na laana za walipa kodi walio masikini huku Duniani pamoja na kulima kuwalisha mlioko mbinguni, mtalia machozi ya Usaa mkiwa Jehanamu. Pu**...f.uuuuu
 
Badili kuhamasishana msome kwa bidii mje kulikomboa taifa mnahamasishana kwenye maandamano.

Kama mmechoka na kusoma rudini kijijini mkalime.
 
UDOM,MZUMBE,ARU,SUA ndo nliko apa ndo madudu kwanzia chuo adi uongozi wa wanafunzi wote hususani mwaka wa kwanza hawajapata hela na ni wiki ya nne ao ni wale ambao hawajapata saivi ndo wanajiuza na kulazwa kwenye majani!kwa upande wa wasiokua nao wamekaririshwa SUA amnaga mgomo wala uwez kuchange system chakula 1000 kivp akati mjin dar 800 au UDSM wanamashamba?hostel zko mbali naul 1200 AKATI KUNA MAGARI YA CHUO yamepark cjui wanafugia PANYA em jumatatu 2gome*kama libya walichange system kwa miez kwa ishindweje SUA tusitishiwe na mtu*
 
Mimi ni MTANZANIA niliyefanikiwa kujiunga na chuo kikuu cha dodoma (udom) mwaka juzi kwa bahati nzuri nimefanikiwa kupata mkopo 100% ni kweli fedha imeongezeka lakini haitakuwa vizuri mimi niongezewe na wengine wakose kabisa haikuwa dhamira yetu.Sisi ndiyo tumesababisha wadogo zetu wa mwaka wa kwanza kukosa kabisa mikopo wakati serikali yetu inafedha nyingi tu za kutusomesha wote,sasa tuamueni moja tuwasaidie wadogo zetu ili nao waweze kupata elimu,ebu fikiria zaidi ya wanafunzi 1000 wamekosa mikopo wengine tunaosoma nao wanarudi nyumbani kwa sababu hawana fedha za kujikimu..Tuacheni unafiki, kuna watu hawana mikopo jaman isiwe kigezo cha kuongezewa sisi hela ndio inatuvunja nguvu ya kudai haki za wengine,isije ikathibitisha kauli kuwa "mwenye nacho anaongezewa asiye nacho anajimwa"kwel hata ALAH anakataa.Tusije tukaonekana ni WANAFIKI mbele ya jamii na ahera pia kisa tumeongezewa bumu kumbukeni hata wao wanatutega kwa hili.SASA tuungane vyuo vyote TANZANIA kupinga hili swala kwa sababu kila chuo kuna watu hawakupata mikopo,UDSM wameanza,tuungane jamani ili hata alah asituone wanafiki pia kuongezeka kwa bumu isiwe sababu ya kutowasaidia wenzetu.SISI NDIO VIONGOZI WA NCHI YETU.Nasisitiza kuanzia jumatatu tarehe 15/11/2011 vyuo vyote TANZANIA tuungane kupinga hili swala kwa kutoingia darasani.Kila mtu anaongozwa na nafsi yake pamoja na mungu mmoja.

tatizo ni kua kati yenu kuna wanafiki wanakuja kufanya mipango ya kugoma ila mkitoka wanaenda dodoma hoteli kukutana na mlacha au kikula,nakumbuka nimeshaitwa ofisini mara nying mpk vuvuzela langu akatumwa police kuja rum kuchukua,mkiamua mnaweza ila lazima mjue kuna wanafiki wakati wa kupanga mipango,
 
Kati ya vyuo ambavyo kuna mazezeta wengi ni UDOM maana nilitegemea wingi wa wao ungewafanya watoe shinikizo juu ya matatizo ya wanafanzi wenzao warudi yamekaa kama mazezeta alafu cha kushangaza nusu yao kati ya wanafunzi wenye mkopo hawakupewa hadi muda huu na haijulikani watapewa lini.kingine ni kuwa yameongezewa bei ya chakula kwa asilimia 50 eti kwa ajili ya compasation za inflation ya asilimia 16.7.ndio maana watu wengi wanawaita Chuo cha vilaza wa Tanzania.BIG UP my camp UDSM kwa kuwa mkombozi wa kila jambo linalohusu maslahi ya wanachuo nchini ikiwemo ongezeko la feza za boom. Na maliza kwa kusema "WATAGOMA WOTE ILA SIO HAO MAZEZETA WA UDOM".

we ndo zezeta na ****** cijawahi kuona,hivi we una habari uongoz wa CHSS ulifukuzwa wote baada ya ule mgomo,hvi unajua wanafunzi waliorudishwa wamerudishwa kwa hati za viapo,hvi unajua saivi college ya CHSS wanafunz hawana uongoz,.we acha kuropoka ka unawashwa tigo,.UDDHM Ki2 gan mbona mmepgwa mabom kmya.mwaka mzma wa masomo uliopta udom Kulikuwa na migomo kudai haki afu unaleta mipasho,.
 
ni kweli kaka lakini jaribu kuangalia hata tukigoma kila kona kuna ffu,tutafika wapi?ata maandamano ya amani hawataki unadhani migomo itakuaje!! la msingi viongozi wetu walioko vyuoni wafanye harakati za kuwanusuru wenzetu hasa kwa kushinikiza bodi na serikali kutuangalia kwa jicho la pili vinginevyo tutalalamika na mwiso wa siku tutaumia bure.
 
aSISI ni wazazi
ulichosema ni sahii lakini ni kweli mnao uwezo wa kuungana mkaufanikisha MGOMO? we umepata 100%na mwingine kakosa kabisa utakuwa na machungu naye kweli? inatia uchungu kuona Yatima wa kweli anarudi nyumbani na mtoto wa kigogo akiwa na 100%
Hii ndo tanzania yetu wote
 
Nafikiri mnapogoma lazima mjipange vyema. Mimi ninafanya utafiti wa crisis managemnet in higher learning institutions. Kwa miakamitano sasa UDSM hakuna mgomo hata mmoja uliofanikiwa na kila mwaka kuna mmgomo kama siyo mmoja ni miwili. Kisa ni ni ni? Hakuna mipango thabiti ya migomo hiyo. Kwanza lazima ujue unagomea nini? (hapa uwe specific kama ni mikopo kwa waliokosa uwe na data kamili ya ambao hawajaweza kujipia kabisa kati ya hao 14,000/= na pia mnataka wawe means tested kivipi?), Kwa faida ya nani?(ya unao watetea? ya kwako kwa mgongo ya hao mnao watetea? "isije kuwa wale waosema kina fulani walifanya hivi au vile leo ni wabunge" kama mmoja wa viongozi wa kunji la UDSm alivyosema pale rev square, ni kwa faida ya kundi au makundi fulani? ni ya shinikizo jingine zaidi ya lengo linalotamkwa?), Upepo wa kusikiliza ukoje huko kwa tunaowashinikiza? wako tayari kutoa pesa kwa shinikizo la migomo? wanahusisha migomo yoyote na maswala ya kisiasa au kidini au kikabila?), Je kuna mtu au kundi la watu ambalo limeshaanza mchakato wa madai husika(ni kwa staili gani na imefanikiwa au haijafanikiwa kwa kiwangoa gani?), Je mikakati yenu imepangikaje(hakuna double face "wenye nia tofauti na inayokusudiwa", haiingiliani na mipango mingine ambayo imeshaanza? mipango ya wawli haiwezi kuwa kikwazo?). Mwisho lazima ujiulize kama mkakati mliousuka ukishindikana nini kitafuata?

Ushauri wangu ni huu: (siyo lazima ufuatwe ila naangalia uzoefu na utafiti ambao bado naendelea kuufanya.

Ni vyema kushinikiza wabunge kujadili swala husika na kufikia maafikiano ya nini hasa kifanyike ili hata kama ni kuandika barua ifuate utaratibu unaokubaliwa kama taarifa za awali ili baadae isisemwe hawa ni wahuni kwa kuwa hawajaleta taarifa yoyote kuhusu madai yao. Barua itaandikwa na katibu wa bunge na kupata signature za wabunge wote badala ya kusainiwa kwa jina la "MWANAHARAKATI" bila kueleza hata mwanaharakati wa wapi!!! lazima tujue hata wanaopigania haki za mashoga ni wanaharakati za ushoga, wanaharakati za waabudu shetani, wanaharakati za kisiasa n.k. pili lazimabaada ya barua kwenda kwa mamlaka husika na kutopata majibu iandikwe nyingine na mwisho ya tatu huku mkimobilize mabunge ya vyuo vingine kufanya hivyo ili mwisho wa siku isionekane ni chuo fulani tu!! Ikifikia hapo kila mtu atakua anajua nini kinachoendelea na watu wa usalama na wanahabari wengine watapeleka ujumbe sahihi kwa kadiri iwezekanavyo. Mwisho mabunge ya vyuo vyote yatapitisha mgomo wa kutoingia madarasani bila propaganda zinazotumiwa na wanasiasa kwa kusaini petition kubariki mgomo husika. Kwa kutumia rev square hata kwa ugomvi wa kisiasa ndani ya association za wanafunzi hakuna atakaye wasikiliza. Enzi za kina kina samweli sita, kina bashiru ali, kina kitilla mkumbo, kina mkenda ukisikia rev square ni bunge au rais wa DAURSO anaongea kwa jambo lenye mvuto na kama ni mgomo hata Rais wa Nchi anatoa majibu au mkwara muda mfupi baada ya rev. Waongoza migomo na maandamano wa sasa wamepotelea kusikojulikana walikua wanang'ata na kupuliza wakigoma leo chuo kikifungwa ndiyo wakwanza kuandika barua za kuomba kurudi kwa uapa kuwa hawatahusika na migomo tena labda niulize watu wengi wanasififia watu kadhaa waligoma na kufukuzwa miaka kadhaa iliyopita bila kujiuliza kina machibya wako wapi nani aligoma warudishwe? UDOM watu mia kadhaa nani anataarifa zao? ana hata amedhiriki kufungua kesi kushinikiza warudi? Ninachomaanisha hapa ni kwamba ukiendesha migomo kiuanharakati usiojulikana uanaharakati upi mwishowe utabaki na begi lako kama ulivyoingia chuo na hutakua umemsaidia uliyetamani kumsaidia.

Tujipange upya, vyema, kuiokomboa nchi kutoka mikononi mwa walafi wachache au tuanze mpango wa Haraambeee ya kenya ile 7500 tunayopewa ya chakula tuimege kama 2500 tusaidie waliokosa mikopo kabisa ili angalau wapate ada,(2500x100000=250,000,000/=) itawaokoa wengi sana. au tuanzishe scholaship funds kama za baadhi ya wabunge kama godbless lema na wengine wengi kupitia mfuko wa wabunge inayowasomesha wanafunzi wa shule za kata.

Mwisho ushauri kwa serikali. 1. TCU iondolewe mamlaka ya kudahi wanafunzi kama inavyota kwanza shughuli ya kudahili siyo kazi yake ni kazi ya vyuo iache tamaa ya kupata pesa za admission. Kazi hiyo viachiwe vyuo vya elimu ya juu ili mwanafunzi aamue aende wapi vyu vipeleke majina TCU kwaajili ya cceditation tu. 2. Serikali itoe elimu ya umma kuhusu mikopo ya elimu ya juu ili ieleweke kuwa ni mkopo na siyo hisani. 3. Serikali ishinikize vyuo viwe na ushirikiano wa karibu na TCU na Bodi ya mikopo ili wanafunzi wanodahiliwa wapate mikopo stahiki badala ya serikali kuangalia idadi ya wanafunzi kuwa kubwa badala ya kuangalia pia adha wanayoipata wazazi na wanafunzi wanao pata mikopo nusu au waliokosa kabisa ha hapa kigezo kiwe ufaulu mkubwa na siyo uwezo wa mtu kifedha maana ni ngumu kuutambua(hili nasema kwa kuwa kila mtu ni maskini anposikia fedha inatoka serikalini hata mkulima mwenye ng'ombe 100 shamba hekari 50 na zaid atajiita mkulima mchanga) na wale watakaokosa basi waombe vyuo kama private candidates kulingana na uwezo wao.

Naomba kupewa michango ya ziada na kukosolewa ili ninacho kifanya kiwe strong na kwaajili ya kuliendeleza taifa na kuondokana na migogoro isiyo ya msingi vyuoni.
 
History inaonyesha kila tatizo lilitokea chuoni especially hapa udsm watu wakagoma,mabom yakapigwa, changes zilionekana, hvyo basi hakuna jambo lililosikilizwa bila kugoma.
 
Badili kuhamasishana msome kwa bidii mje kulikomboa taifa mnahamasishana kwenye maandamano.

Kama mmechoka na kusoma rudini kijijini mkalime.

Siku utakapowaza kwa kutumia akili ndo utaelewa kinachowasibu wanafunzi sio unaropoka tu masaburi we
 
Back
Top Bottom