Habari Mbaya kwa Watu Wote kama ilivyoandikwa na 'Raia Fulani'

Vilio vya manabii, na machozi ya "Raia Fulani": Unafikiri Mwenye Enzi kalala usingizi..hata siku moja!! Atawalipa accordingly.
 
Jama ni hodari sana maana amenirudisha enzi za vitabu vya hadithi na stori za wafalme wa enzi hizo zilizokuwa zikisisimua nakuweza kujenga picha akilini ya tukio lilivyokuwa linatendeka. Wewe utakuwa ni wazamani mpenda kusoma. All the best nakuomba nikukaribishe kwenye page ya uongozi na siasa , fb n twitter
 
Nao wana wa nchi wakiwa hawaamini kwa kile kinachotokea mbele ya macho na masikio yao, ndipo Yule mwana mpendwa wa mkulima, mkuu wa mawaziri aliposimama na kuijongelea mimbari kwa ajili ya kutoa neno la hitimisho. Nayo maneno mengi yakamtoka kinywani. Maneno yaliyoandikwa juu ya gome. Naam, maneno mengi.

Hapo ilikuwa yapata saa moja usiku, nae alikuwa Akiendelea kushukuru na kupongeza na kushauri na kukemea na kusisitiza na kusihi, wala asijue kuwa wana wa nchi walikuwa na kiu nyingine. Kiu ya kusikia jambo jipya. Kiu ya kusikia habari njema.

Hata alipofikia tamati, hapakuwako na neno lolote la kuwafariji wana wa nchi kwa maana walitamani mioyoni mwao kusikia, "Yanipasa kujivua gamba", wala wasisikie.

Naye akiisha kusema hayo, akahitimisha kwa kuahirisha Baraza la saba hadi mwezi wa Juni wa mwaka bila kwa neno la matumaini kwa wana wa nchi. Ndipo waliposema, "Hakika mwana wa mkulima mwoga!"

Yaani siku ya jana si Wananchi tu walikuwa wanasubiri kauli yake.

Hata Wabunge wote waliisubiri kwa hamu sana. Sijawahi kushuhudia Hotuba Fake kama ile ya jana, hata Wabunge walikuwa wanaomba amalize tu ili waende kula DINNER maana alikuwa anachosha tu. Na mishipa imemsimama bila ya aibu.

Hotuba yake yote ilitawaliwa na ukimya tu toka kwa wabunge, hakuna aliyethubutu kupiga hata Makofi kwa jinsi walivyomchoka.

Sijashuhudia PM akitoa hotuba ya kufunga Vikao vya Bunge na Wabunge pale mwishoni HAWAPIGI MAKOFI.

Kwa dalili za Jana; hakika nimeamini kuwa PINDA AMEKALIA TAWI LA MPAPAI kwani ni heri ya Kuti kavu atafika nalo chini salama.

CCM NIMEIONA IPO WARD YA ICU MUHIMBILI. SIDHANI KMA ITAPONA MWAKA HUU. TUJIANDAE KUICHIMBIA KABURI.



MIZAMBWA
NABII MTARAJIWA!!!
 
MNYISANZU. Popote pale penye mapinduzi ya kijeshi, wanajeshi wa kawaida ndiyo wahusika wakuu. Tena wenye vyeo kama kapteni na luteni ndiyo wafanya mapinduzi,kwani wao ndiyo wenye wanajeshi,kupitia vikosi.

Hivyo wanajeshi wetu hawana ujasiri kama tulivyo sisi raia wa kawaida.
Thanks for your clarification mkuu. Wanajeshi wetu nao wamekuwa corrupted na system so wanachokifanya ni ku-preserve status quo.
 
Well said. Viongozi wa majeshi ndio kikwazo cha mapinduzi nchini. Wanajeshi wa kawaida wanataka sana kuipindua serikali ila viongozi wao ndio stumbling blocks.

...Mbona hata EL alishajaribu na Akashindwa! Au hamjui kwa nini J aliamua
 
Kumradhi... Namaanisha ndo maana J aliamua kumtoa sadaka baada ya EL kushindwa kwa kusalitiwa na baadhi ya makamanda wanaofaidika na ufalme wa JK. Chunguzeni.. ( just tetesi)
 
Viongozi wa jeshi hawawezi , siunajua mpunga wanaovuta na marupurupu kibao na tena CAG huwa hakagui huko kwao , ila wanajeshi wakawaida ngazi ya macaptain ,kanali wanaweza wakiamua
 
raia fulan si kama jina lako lilivyofichika, "raia fulani" unakipaj kilichofichuka. Great, great article mkuu. Nimeisoma kwa ladha ya aina yake.
 


Ee mkuu mfalme wa kisasi
Mfalme wa kisasi uangaze!
Mwenye kuhukumu nchi, ujitukuze
Uwape wenye kiburi stahili zao.

Mkuu hata lini wasio haki,
Hata lini wasio haki watashangilia?
Ee mkuu wanawaseta watu wako
Wanawatesa warithi wako

Nao husema, mkuu haoni
Mfalme wa wote hafikiri
Enyi wajinga miongoni mwa watu, fikirini
Enyi wapumbavu, lini mtakapopata akili?

Aliyelitia sikio mahali pake asisikie?
Aliyelifanya jicho asione?
Awaadhibuye mataifa asikemee?
Amfundishaye mwanadamu asijue?

Lakini mkuu amekuwa ngome kwetu
Na Mfalme wetu mwamba wetu wa kukimbilia
Naye atawarudishia uovu wao
Atawaangamiza katika ubaya wao
Naam, mkuu, Mfalme wetu atawaangamiza.
:violin::violin::violin::violin::violin:
NI UPEPO TU, UTAPITA

Mnajua Watanzania, JK katutukana.
"Ukiona Lusinde, na JK yuko mbele"
 
Hata mfamaji hutapatapa huku akikusanya kila takataka iliyo mbele yake
ndivyo kwa watawala wetu wanavyo tapatapa.
Hongera raia fulani
 
Kwani nchi kupinduliwa nani kakuambia ni habari mbaya?
Nchi kupinduliwa ni hatua moja kuelekea kwenye ukombozi.
Duniani kote, pale jeshi linapogundua serikali imeshindwa kuwatumikia wananchi, na kuna chama ambacho kinatetea maslahi ya umma lakini inashindwa kutokana na utawala wa mabavu, linaipindua hiyo serikali kandamizi, na kuikabidhi kwa wananchi kwa njia ya haki, kwa maana ya kufanya uchaguzi wa kidemokrasia, ambapo taratibu zote za uchaguzi unaratibiwa na jeshi.
Kwa mfano jeshi letu ukiacha Shimbo na Mwamunyange wakiwemo wafuasi wachache, wanaelewa jinsi serikali yetu ilivyoshindwa kuwatumikia wananchi, wanaelewa jinsi serikali yetu inavyowakumbatia waizi.

Kakwambia nani jeshi limeona hilo ? unajua hapa kwetu watu watapiga keleleeeee mwisho yatapita kama alivosema UPEPO UTAPITA !
 
Hata mfamaji hutapatapa huku akikusanya kila takataka iliyo mbele yake
ndivyo kwa watawala wetu wanavyo tapatapa.
Hongera raia fulani
 
Back
Top Bottom