kwa hiyo ulitaka mengi awafukuze mama ntilie na vibanda vyao....
lowasa ofisi zake ziko kwenye ile barabara na alikuwa pm mbona umtaji
chuki binafsi....
anyway siyo chuki bali uko kazini
Nyie Wapambe wa Mengi
kama umeona serikali imeuza loliondo na watu wanachomewa nyumba hawana pa kukaa na iko kimya?huna haja ya kuongea kuhusu parking ya mengi,inadhuru au kuhusiana vipi na mahitaji ya wananchi?licha ya hivyo MZEE MENGI ni msaada na ni mtu mzuri sana katika kusaidia na kujali ubinadamu unapomfikia,kusema kweli jamani mi kuhusu huyu mzee nampa heshima yake,ni tofauti kabisa na hao watu mnawaita viongozi.kuhusu ufisadi na kilakitu nani si fisadi tanzania?MWACHENI MZEE APUMZIKE,ANA THAWABU NYINGI KULIKO LAANA MNAZOMTUPIA,NA NI MFANO KATIKA JAMII
Mkuu Sikonge mie sio mpambe kabisaaa wa mzee Pua ndo maana katika thread ile nimesema matajiri wa Kibongo wanajisikia ufahari wanapo toa michango yao public lakini mfuate kwa pembeni kuwa unashida unauguliwa kama utapewa thubutu hapo hapo utakuta mtu katoka kutoa 150mil lakini unashida ya 100000 unanyimwa.
Ile barabara kwani inaenda kwa Mzee Mengi peke yake? Kule chini kuna akina Subbash Patel na watu influential kibao. Lakini kwa kuwa watu wamezoea Mengi huwa anajitolea basi wanataka ajenge. Hata kama hamumpendi huyu mzee tumtendee haki kidogo,kazi ya barabara ni ya wakusanya kodi,otherwise mtu ajitolee mwenyewe siyo tuanze kuleta siasa hapa eti ajenge.
Mkuu Fidel nilikuwa namaanisha kweli WAPAMBE na siyo wewe. Ukisoma vizuri utaona kuwa NAKUBALIANA NA WEWE na si NAKUPINGA. Tupo pamoja kwa hilo.
Hivi kuna mtu alishindwa kupata parking kwenye hizo ofisi? Kama vumbi ni swala la muda tu kwani elinino inakuja!(jokes)
Nyani Ngabu uko sawa "MIAFRIKA NDIVYO TULIVYO"
NN,Hivi kwani Mecco kazi yao nini? Kama Mecco hawawezi kazi si wapewe Kajima au Konoike....
Mzee anahisi anawajibika zaidi kwa jamii. anawajibika kwa wanaohitaji, wanaohitaji zaidi ya barabara na parking nzuri. kwake hivyo haviongezi lolote kama kumsaidia anaehitaji Tsh. 60,000 pale nzega ili aweze anzisha japo biashara ya vitymbua pale nzega.
Nadhani na wewe una ajenda yako. Ulitaka Mengi awafanyie kazi jiji wao waendelee kuponda raha wanakusanya kodi na kutafuna bata. Yeye alipe kodi, alafu ajenge barabara kwa kumfurahisha nani??
Wewe umejenga chochote wapi???
Lakini maeneo anayoyazungumzia si miliki yake, japo kuna wakati wenye viwanda maeneo hayo walikusanya nguvu na kugharimia uwekaji wa kokoto ktk barabara kuu iendayo huko, baada ya halm. kutotoa kipaumbele. Huyo Bw. Acheki pia na parking ya Alfa dry cleaners ya mzee wa kazi hapohapo jirani
Kwa nini usiseme basi washirikiane na wale wenye viwanda maeneo yale na kuna shwahiba wa SSM na kiwanda cha Nondo halafu unataka Mengi ajenge peke yake???