Haaaa Mzee Mengi!!

Status
Not open for further replies.
Umeona kwa Mengi tu? Hiyo barabara inakwenda kwenye nyumba za kuishi watumishi wa serikali akiwepo Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mawaziri, Wakurugenzi n.k. Hivyo inatakiwa serikali itengeneze. Huwezi kulinganisha na TBC kwani TBC wanatumia kodi zetu ambazo ni pamoja na anazolipa Mengi. Hata hivyo kila mtu ana mipango ya biashara yake na inawezekana parking kutengenezwa ipi kwenye process. Mengi anafanya kazi kubwa sana hasa ya kusaidia jamii yenye mahitaji. Ofisi zake zinafikika na hata parking gari zina park lakini kumbuka kuna watu wenye mahitaji muhimu zaidi ya kujenga parking. Barabara ni ya serikali na hilo eneo ni industrial area.
 
Luku bado haijaisha? Naona unajambo ambalo unataka kusema ila unatafuta jinsi ya kuliingiza.Kinachokupeleka kwenye parking ya wenzako ni ni hasa, au ulikwepa kulipia parking fee za jiji?
 
Kwani hiyo parking ikoje mpaka inashupaliwa kihivyo?. Mi navyojua Bwana Mengi ana majukumu makubwa na mengi sana kiasi kwamba kushughulikia vitu vidogo kama parking ya magari ni kumwonea bure. Vitu vidogo kama hivyo viko ndani ya uwezo wa kina Joyce Mhavile. Mengi aanze kushughulikia parking ya Bonite Bottlers, kisha IPP Media, then Body Care halafu sijui wapi tena, kina Mhavile na wenzake watafanya kazi gani? Msimwonee bure mzee wa watu.
 
Ishu inabaki palepale, ungetegemea kwa mtu wa hadhi nchini ambaye anajihusisha na ishu za mazingira ya jamii angeonyesha mfano kwenye mazingira yanayomzunguka.

Hivi umeshawahi kuona jinsi kulivyokuwa na vumbi pembezoni mwa ofisi zake? Only kama wafanyakazi wake wangekwenda kwenye chest x-ray exam ndivyo ingedhibitisha ni jinsi gani mazingira ya ofisi za mwanamazingira maarufu nchini yalivyokuwa.

Ofisi ngapi za SERIKALI zina vumbi sembuse huyu mtu binafsi? Usione hapo alipo amesaidia kuwapa ajira hao watanzania wenzie na pia kugawa misaada kwa taasisi na yatima ukafikiri anazo za kumwaga ni kwasababu anakwenda kimahesabu sana: Parking sio issue sana kama kuna watu wanapokea mshahara kutunza familia zao, tunapata habari mbalimbali kupitia TV na magazeti yake, tunasaidiwa kulea yatima na wasiojiweza ktk jamii zetu etc.
Tungekuwa na kina Mengi watano hivi Tz lol mbona kusingekuwa na ukosefu wa ajira, lakini hao wengine wankwenda kufukia hela zao bank za nje, tena za wizi basi, mumtie moyo badala ya kumkatisha tamaa. Keep it up Mengi, you make a good role model for any Tanzanian with a good will to their country.
 
Kwa nini Mengi tu? Hiyorabara haiendi kwake peke yake. Kwa taarifa hata mashine za kufulia nguzo za Alpha Dry Cleaner zipo huko huko. Ofisi za kampuni hiyo zipo hukohuko, mbona wao hawatajwi kuhusu hiyo barabara?
 
Nakubaliana na mzee mtoa hoja kwamba kuna tatizo! Vile vibanda vya mama ntilie vichafu na vibaya bado viko kwenye ile barabara.

Kwa m2 wa Mazingira kama mzee Mengi.... ile barabaa inayoelekea kwake inatia kichefu chefu.

kwa hiyo ulitaka mengi awafukuze mama ntilie na vibanda vyao....
lowasa ofisi zake ziko kwenye ile barabara na alikuwa pm mbona umtaji
chuki binafsi....
anyway siyo chuki bali uko kazini
 
Ndo maanake mbona sisi kwetu huko kwenye mashimo tunafukia wenyewe tunakodi lori na kushusha mzigo kisha tunasawazisha.

Nyie Wapambe wa Mengi,
Haya yambo kayapigia sana kelele humu ndani Mzee Mwanakijiji. Haya mambo ya ohh mbona siko peke yangu, ohh ni jukumu la serikali, ohhh kifo cha wengi harusi, ndiyo yanayotufanya milele tubaki palepale.

Mengi ni mtu maarufu sana na milele popote alipo ataonekana yeye. Kusema kuna wengine pale basi si awaite na kuwaambia wachangie kujenga hiyo barabara? Anasubiri na yeye kila kitu maana kashalipa kodi?

Nikiwa naishi Ilala Flats, tulikuwa na jirani yetu mmoja Mhandisi, Mzee Ngonyani. Kutokana na mabomba ya maji machafu kuziba, maji taka yalikuwa yakimwagika nje na kutoa harufu mbaya sana, wenyewe wakisema MAFURIKO. Yakitokea kinachofanywa mnafunga madirisha ya upande huo. Mhandisi huyo alifika point akachoka, akaja kuitisha mkutano kuwa ataenda kununua mabomba na kugharamia ujenzi wake. Wanaotaka kumsaidia wamsaidie na wasiotaka waache. Huwezi amini, wote walitoa hela. Tatizo dogo lipo kwa Msomali, yeye siku zote anasema "hana muda, wampe gharama na yeye atatoa pesa - Yes alitoa hela..." Wakati mwingine ni vitu viko ndani ya uwezo wetu ila tunakosa KIONGOZI. Kila mtu au anaona hilo HALIMHUSU au anasubiri FULANI aanze.

Tusiwe waoga namna hiyo. Mwambieni Mzee ashirikiane na jirani zake hao wenye mashine za kufulia sijui, na wenye viwanda wengine, unaweza kukuta wakapata hata msaada kutoka EU kama wao ni masikini saana na ile barabara ikajengwa kwa Zege ili kuhimili mizigo mizito kutoka kiwandani. Cement Tanzania ipo, mawe na mchanga upo, shida iko wapi? Ni pesa tu. Hao watu kama wameweza kuwa na Viwanda, kinawashinda nini kujenga barabara au Parking?
Mnaweza kumtetea sana ila ukweli ni kuwa UJUMBE UMEMFIKIA. Na kama nyie ni Wapambe wake basi MFIKISHIENI. Siku anafungua na aseme kuwa wameijenga kwa ushirikiano na wenzake. Labda itakuwa mfano kwa watu wengi huko mitaani kushirikiana na kuweka mazingira yao katika hali safi. Tunaisubiri saana serikali wakati serikali yenyewe ni ya CCM (Chama Cha Mafisadi).
 
kwa hiyo ulitaka mengi awafukuze mama ntilie na vibanda vyao....
lowasa ofisi zake ziko kwenye ile barabara na alikuwa pm mbona umtaji
chuki binafsi....
anyway siyo chuki bali uko kazini

Semilong,

Ninaipenda sahihi yako.
You can not keep 40m people quite forever....
one year one month one day they will wake up..........


Hawa 40m wamelala usingizi wa pono na sijui wataamka lini.
Kama watu wataanza kuonyesha mfano wa kubadili mazingira, amini hata wabunge itabidi waje na GIA mpya maana ya kusema "nitawaletea maji, umeme na barabara" watu hawatanunua. Na sanasana watachagua mtu ambaye amekuwa akishirikiana nao katika kubadili mazingira yao. Haya mambo ya Wabunge kuchaguliwa na kuhamia Dar, ni upuuzi wa waziwazi. Na bado mtu kama huyo mnamchagua tena.
Kama wajanja wasipoanza kuwaamsha, basi kwa akili za sisi MIPINGO, milele hawataamka.
Kitu kibaya cha kufanyiwa ni kwamba hata hao wanaofaidika sasa kwa kuwa Kikwete ni Rais, siku akiondolewa, kila kitu kitaanza kuharibika. Watashindwa kuweka hata kibao cha barabarani kinachocost kama sh 5,000.
 
Hivi kuna mtu alishindwa kupata parking kwenye hizo ofisi? Kama vumbi ni swala la muda tu kwani elinino inakuja!(jokes)
 
Nyie Wapambe wa Mengi,
Haya yambo kayapigia sana kelele humu ndani Mzee Mwanakijiji. Haya mambo ya ohh mbona siko peke yangu, ohh ni jukumu la serikali, ohhh kifo cha wengi harusi, ndiyo yanayotufanya milele tubaki palepale.

Mengi ni mtu maarufu sana na milele popote alipo ataonekana yeye. Kusema kuna wengine pale basi si awaite na kuwaambia wachangie kujenga hiyo barabara? Anasubiri na yeye kila kitu maana kashalipa kodi?

Nikiwa naishi Ilala Flats, tulikuwa na jirani yetu mmoja Mhandisi, Mzee Ngonyani. Kutokana na mabomba ya maji machafu kuziba, maji taka yalikuwa yakimwagika nje na kutoa harufu mbaya sana, wenyewe wakisema MAFURIKO. Yakitokea kinachofanywa mnafunga madirisha ya upande huo. Mhandisi huyo alifika point akachoka, akaja kuitisha mkutano kuwa ataenda kununua mabomba na kugharamia ujenzi wake. Wanaotaka kumsaidia wamsaidie na wasiotaka waache. Huwezi amini, wote walitoa hela. Tatizo dogo lipo kwa Msomali, yeye siku zote anasema "hana muda, wampe gharama na yeye atatoa pesa - Yes alitoa hela..." Wakati mwingine ni vitu viko ndani ya uwezo wetu ila tunakosa KIONGOZI. Kila mtu au anaona hilo HALIMHUSU au anasubiri FULANI aanze.

Tusiwe waoga namna hiyo. Mwambieni Mzee ashirikiane na jirani zake hao wenye mashine za kufulia sijui, na wenye viwanda wengine, unaweza kukuta wakapata hata msaada kutoka EU kama wao ni masikini saana na ile barabara ikajengwa kwa Zege ili kuhimili mizigo mizito kutoka kiwandani. Cement Tanzania ipo, mawe na mchanga upo, shida iko wapi? Ni pesa tu. Hao watu kama wameweza kuwa na Viwanda, kinawashinda nini kujenga barabara au Parking?
Mnaweza kumtetea sana ila ukweli ni kuwa UJUMBE UMEMFIKIA. Na kama nyie ni Wapambe wake basi MFIKISHIENI. Siku anafungua na aseme kuwa wameijenga kwa ushirikiano na wenzake. Labda itakuwa mfano kwa watu wengi huko mitaani kushirikiana na kuweka mazingira yao katika hali safi. Tunaisubiri saana serikali wakati serikali yenyewe ni ya CCM (Chama Cha Mafisadi).
Huyu mzee anapoona sehemu atapata sifa basi yeye ndo yupo mbele lkn si kwa sababu ya maslahi ya taifa. kwanza angewalipa wafanyakazi wake mishahara mizuri na kwa wakati kama kweli ana uchu na raia wa nchi hii,wafanya kazi wanalalamika sana tu,ninaye sahiba yangu mmoja analalamika kutolipwa kwa wakati,na sahiba yangu mwengine alikuwa pale lkn alishindwa kukaa,aliacha kazi kwa mambo hayo hayo ya kuwabana watu. Nina sahiba yangu mwengine ambaye ni mlemavu ambaye yumo ktyk kamati za walemavu aliwahi kuniambia huyu jamaa anachukua misaada nje ya walemavu ili atuletee akifika hapa anatuandalia chakula kizuri ktk hoteli kubwa,tukimaliza hicho tunachopewa ktk barua huwezi kuamini wakati amepewa fedha nyingi kwa ajili awape walemavu. Yupo kwa ajili ya Faida yake tu huyu mzee.
 
Semilong,

Ninaipenda sahihi yako.
You can not keep 40m people quite forever....
one year one month one day they will wake up..........

Hawa 40m wamelala usingizi wa pono na sijui wataamka lini.
Kama watu wataanza kuonyesha mfano wa kubadili mazingira, amini hata wabunge itabidi waje na GIA mpya maana ya kusema "nitawaletea maji, umeme na barabara" watu hawatanunua. Na sanasana watachagua mtu ambaye amekuwa akishirikiana nao katika kubadili mazingira yao. Haya mambo ya Wabunge kuchaguliwa na kuhamia Dar, ni upuuzi wa waziwazi. Na bado mtu kama huyo mnamchagua tena.
Kama wajanja wasipoanza kuwaamsha, basi kwa akili za sisi MIPINGO, milele hawataamka.
Kitu kibaya cha kufanyiwa ni kwamba hata hao wanaofaidika sasa kwa kuwa Kikwete ni Rais, siku akiondolewa, kila kitu kitaanza kuharibika. Watashindwa kuweka hata kibao cha barabarani kinachocost kama sh 5,000.
sikonge
kuna politics nyingi zina juu ya huyu mzee yani anashambuliwa kutoka kila kona, yaani hata ile barabara inaweza ikawa haitengenezwi kwa ajili ya politics..
embu fikiria mtu anadiriki kusema pembeni kuna mama ntilie wengi unataka mengi awafukuze hao mama ntilie kwani yeye ndio mwenye mji au yeye ndio halmashauri ya jiji
ningependa kurejea kwenye sahihi yako
"mitanzania mingine ina wivu wa kijinga"

kwa watu wanaolalamika mishahara ile ni biashara na watu wanalipwa mishahara ambayo ni market rate...
mengi anafanya ile biashara ili apate faida na akishapata faida jinsi ya kuitumia ile hela ni maamuzi yake, kinachoniuzi ni pale wafanyakazi wanapokuwa na chuki na kutaka hela wapewe wao na wakati wameshalipwa mishahara
 
Sasa na wewe mbona unaanguka kwenye msemo wako maarufu (Miafrika Ndivyo Tulivyo). Yaani huoni kabisa (kwa hadhi yake na jinsi alivyokuwa mtari wa mbele kwenye shughuli za kijamii) mazingira ya ofisi zake yanavyomsuta?

Jamani yule ni role model kwa watu wengi tu (mimi mmoja wao). Kwa hiyo kila anachojihusisha kwenye jamii kinatugusa kwa namna moja au nyingine. Isitoshe, tunaainisha mazingira yanayomzunguka na na kile anachofanya kwenye jamii. Ndio maana ya kuwa "mfano" wa kuigwa huko...au?


Akijenga hiyo parking nzuri mtaanzisha la kuanzisha tena!

Ndugu yangu Quemu ujue kila mtu ana vipaumbele vyake, na malengo ya kutimiza, huku akibanwa na muda!

Mi sioni shida na parking, ni suala la muda , huenda atalishughulikia.
 
Mh hizi thread zingine jamani; Sasa kazi ya Kujenga barabara tangu lini ikawa ya Mzee Mengi? Na hata kama akijitolea kujenga kwa fedha zake itabidi apate kibali toka serikali kuu na jiji ikiwa ni pamoja na kueleza nia na madhumuni ya kufanya hivyo.

Pale ambapo mtu huna cha kusema au hoja ya msingi, kaa kimya soma za wenzako na ikibidi changia.
 
...mbele ya ofisi yangu ambayo inatembelewa na watu wengi kutokana na shughuli ninazofanya, kuna mtaro wa kupitisha maji ya mvua. kwa vile hii ni bongo mtaro huu mara nyingi unakuwa umejaa uchafu wa mifuko ya rambo ambayo mingine ina vinyesi vya binadamu. kwa mawazo ya watu wengi hapa ni kwamba sina sababu ya kuingia gharama za ziada kuuweka mtaro ule katika hali ya usafi (na bila shaka katika kufanya hivyo kuongeza intergrity ya biashara yangu!) kwa vile tu ninalipa kodi na wenye jukumu la kuhakikisha kuwa mtaro huo unakuwa safi ni serikali ya mtaa wangu!
Haishangazi basi kila tatizo linapotokea mahali na wananchi husika wakahojiwa na redio ama televisheni kilio chao kikubwa kuwa "Tunaiomba serikali itufanyie...bla bla bla"! potelea mbali kwamba tatizo hilo wakilishughulikia kwa umoja wao halitachukua hata saa moja kulimaliza! mwenye maneno yake, samahani.....Miafrika Ndivyo Tulivyo!
 
Nyie Wapambe wa Mengi,
Haya yambo kayapigia sana kelele humu ndani Mzee Mwanakijiji. Haya mambo ya ohh mbona siko peke yangu, ohh ni jukumu la serikali, ohhh kifo cha wengi harusi, ndiyo yanayotufanya milele tubaki palepale.

Mengi ni mtu maarufu sana na milele popote alipo ataonekana yeye. Kusema kuna wengine pale basi si awaite na kuwaambia wachangie kujenga hiyo barabara? Anasubiri na yeye kila kitu maana kashalipa kodi?

Nikiwa naishi Ilala Flats, tulikuwa na jirani yetu mmoja Mhandisi, Mzee Ngonyani. Kutokana na mabomba ya maji machafu kuziba, maji taka yalikuwa yakimwagika nje na kutoa harufu mbaya sana, wenyewe wakisema MAFURIKO. Yakitokea kinachofanywa mnafunga madirisha ya upande huo. Mhandisi huyo alifika point akachoka, akaja kuitisha mkutano kuwa ataenda kununua mabomba na kugharamia ujenzi wake. Wanaotaka kumsaidia wamsaidie na wasiotaka waache. Huwezi amini, wote walitoa hela. Tatizo dogo lipo kwa Msomali, yeye siku zote anasema "hana muda, wampe gharama na yeye atatoa pesa - Yes alitoa hela..." Wakati mwingine ni vitu viko ndani ya uwezo wetu ila tunakosa KIONGOZI. Kila mtu au anaona hilo HALIMHUSU au anasubiri FULANI aanze.

Tusiwe waoga namna hiyo. Mwambieni Mzee ashirikiane na jirani zake hao wenye mashine za kufulia sijui, na wenye viwanda wengine, unaweza kukuta wakapata hata msaada kutoka EU kama wao ni masikini saana na ile barabara ikajengwa kwa Zege ili kuhimili mizigo mizito kutoka kiwandani. Cement Tanzania ipo, mawe na mchanga upo, shida iko wapi? Ni pesa tu. Hao watu kama wameweza kuwa na Viwanda, kinawashinda nini kujenga barabara au Parking?
Mnaweza kumtetea sana ila ukweli ni kuwa UJUMBE UMEMFIKIA. Na kama nyie ni Wapambe wake basi MFIKISHIENI. Siku anafungua na aseme kuwa wameijenga kwa ushirikiano na wenzake. Labda itakuwa mfano kwa watu wengi huko mitaani kushirikiana na kuweka mazingira yao katika hali safi. Tunaisubiri saana serikali wakati serikali yenyewe ni ya CCM (Chama Cha Mafisadi).
kama umeona serikali imeuza loliondo na watu wanachomewa nyumba hawana pa kukaa na iko kimya?huna haja ya kuongea kuhusu parking ya mengi,inadhuru au kuhusiana vipi na mahitaji ya wananchi?licha ya hivyo MZEE MENGI ni msaada na ni mtu mzuri sana katika kusaidia na kujali ubinadamu unapomfikia,kusema kweli jamani mi kuhusu huyu mzee nampa heshima yake,ni tofauti kabisa na hao watu mnawaita viongozi.kuhusu ufisadi na kilakitu nani si fisadi tanzania?MWACHENI MZEE APUMZIKE,ANA THAWABU NYINGI KULIKO LAANA MNAZOMTUPIA,NA NI MFANO KATIKA JAMII
 
sikonge
kuna politics nyingi zina juu ya huyu mzee yani anashambuliwa kutoka kila kona, yaani hata ile barabara inaweza ikawa haitengenezwi kwa ajili ya politics..
embu fikiria mtu anadiriki kusema pembeni kuna mama ntilie wengi unataka mengi awafukuze hao mama ntilie kwani yeye ndio mwenye mji au yeye ndio halmashauri ya jiji
ningependa kurejea kwenye sahihi yako
"mitanzania mingine ina wivu wa kijinga"

kwa watu wanaolalamika mishahara ile ni biashara na watu wanalipwa mishahara ambayo ni market rate...
mengi anafanya ile biashara ili apate faida na akishapata faida jinsi ya kuitumia ile hela ni maamuzi yake, kinachoniuzi ni pale wafanyakazi wanapokuwa na chuki na kutaka hela wapewe wao na wakati wameshalipwa mishahara

Semilong,
Hayo ya Mama Ntilie na Mishahara wala sikutaka kuyaelezea. Ni UPUPU wa hali ya juu ambao mtu wala huwezi kuujibu maana itakuwa kama vile mtu kaiba nguo zako wakati unaoga na wewe unaanza kumfukuza nje huku ukiwa uchi. Yes, ukiwa uchi wa mnyama. Sasa please, usikwepeshe habari kwa kuipeleka huko. Mie hapa naongelea ni BARABARA tu na si kwa Mengi peke yake ila watu wote wenye viwanda/wanaishi huko. Mengi kwa kutumia umaarufu wake, angeliweza kuwangunisha watu wote pale na wote wachangie kwa kiwango fulani ujenzi wake. Kama wakiwa kundi, itabidi City watowe kibali au hata kusaidia kujenga. Haya mambo ya kusubiri fulani aanze yametufkisha hapa tulipo. Ndiyo maana nikaandika mfano huu hapa chini, NAURUDIA:

Nikiwa naishi Ilala Flats, tulikuwa na jirani yetu mmoja Mhandisi, Mzee Ngonyani. Kutokana na mabomba ya maji machafu kuziba, maji taka yalikuwa yakimwagika nje na kutoa harufu mbaya sana, wenyewe wakisema MAFURIKO. Yakitokea kinachofanywa mnafunga madirisha ya upande huo. Mhandisi huyo alifika point akachoka, akaja kuitisha mkutano kuwa ataenda kununua mabomba na kugharamia ujenzi wake. Wanaotaka kumsaidia wamsaidie na wasiotaka waache. Huwezi amini, wote walitoa hela. Tatizo dogo lipo kwa Msomali, yeye siku zote anasema "hana muda, wampe gharama na yeye atatoa pesa - Yes alitoa hela..." Wakati mwingine ni vitu viko ndani ya uwezo wetu ila tunakosa KIONGOZI. Kila mtu au anaona hilo HALIMHUSU au anasubiri FULANI aanze.
 
Huyu mzee anapoona sehemu atapata sifa basi yeye ndo yupo mbele lkn si kwa sababu ya maslahi ya taifa. kwanza angewalipa wafanyakazi wake mishahara mizuri na kwa wakati kama kweli ana uchu na raia wa nchi hii,wafanya kazi wanalalamika sana tu,ninaye sahiba yangu mmoja analalamika kutolipwa kwa wakati,na sahiba yangu mwengine alikuwa pale lkn alishindwa kukaa,aliacha kazi kwa mambo hayo hayo ya kuwabana watu. Nina sahiba yangu mwengine ambaye ni mlemavu ambaye yumo ktyk kamati za walemavu aliwahi kuniambia huyu jamaa anachukua misaada nje ya walemavu ili atuletee akifika hapa anatuandalia chakula kizuri ktk hoteli kubwa,tukimaliza hicho tunachopewa ktk barua huwezi kuamini wakati amepewa fedha nyingi kwa ajili awape walemavu. Yupo kwa ajili ya Faida yake tu huyu mzee.[/QUOTEkuna mshahara mzuri bongo?hata uwape milioni ngapi kesho watalia kutaka nyongeza,basi kama hao rafiki zako wanaona wanaonewa waache kazi basi kwani wamelazimishwa?mi nachukia sana unafkinafki huu
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom