Government to sue NorConsult

FM,

Najua Kifukwe sio mzungu (namfahamu yeye binafsi kwa karibu mno)ila hiyo ni kampuni ya Wazungu na ndio maana ilifanikiwa kufanya kazi kubwa kubwa miaka kumi bila hata kuguswa.

Ingelikuwa kampuni ya mswahili ungeona wasingemaliza hata mwezi.

Middle class ya Watanzania ndio wasaliti wakubwa wa nchi. Wanaweza kuja hapa JF kulaani viongozi mafisadi lakini kama ni mtu clean na umewahi kufanya biashara TZ, utajua ninasema nini. Hao hao walioko Brela, TRA, banks, ardhi nk. wanaihujumu TZ kwa njia chungu nzima. Kibaya zaidi wanakwamisha Watanzania wenzao, wakati wakija Wazungu wanalegea, shame on them!

Ndio maana watu kama akina Kifukwe kwa kutumia ukaribu wao na Wazungu wakaweza kupeta miaka yote hiyo bila kuguswa wala kulipwa kodi.

Na hili ndilo tatizo kubwa sana huko serikalini no wonder kina Rostam wanaiba na kupeta bila kujali hata kidogo. Ukitaka kufanya mambo yako kwa halali unazungushwa kama mjinga wakati wenye dola tano mifukoni toka nje wanapata mabilioni!
 
Kwa kufunga kazi zao zote Tanzania baada ya miaka 30 nchini, wafanyakazi kama 60 hivi wa NORCONSULT TANZANIA LTD watakuwa hawana kazi, yote sababu ya bosi wao F. Kifukwe kukaidi maagizo mahususi kutoka ofisi kuu ya NORCONSULT kuwa afuate maadili ya biashara ya kampuni na asitoe wala kupokea rushwa.

Achilia mabli hizo bilioni 2.4 za kodi NORCONSULT TANZANIA LTD wanazotuhumiwa kudaiwa. Inawezekana kabisa uongozi wa NORCONSULT TANZANIA LTD wametia ndani pesa za kodi wakishirikiana n vogogo wa TRA na kwingineko huku ofisi kuu Norway wakijua kuwa kodi inalipwa. Wanorwei ni taifa la wafuata sheria na siyo watu wa njaa njaa.

La msingi hapa ni kwamba jamii ya Tanzania kwa ujumla itaumia vibaya kwani watapoteza sifa nzuri waliyokuwa nayo kwa Wanorwei pamoja na misaada ya fedha, teknolojia na ujenzi wa miundombinu. Yote sababu ya uroho na ufisadi wa vichwa maji wachache.
 
Mh!! Hivi ni kwamba tumelala au kuna watu wanatuzunguka??? I don't believe this humu humu Tz haya mambo yanafanyika?? Lazimam itakuwa watu wamekula ganji watulie...sasa huyu kifukwe ni huyu huyu wa akina nsajigwa na Ivo au mwingine??? Nchi imeoza kudadadeki lakini tutaenda nao sambamba!!!
 
Pundit
irregardless ya huyo Mu-Australia..............kinachosikitisha zaidi ni hao watanzania wahandisi na supporting staff wanaofanya kazi hapo diligently.......sijui ajira yao itakuwa vipi,

.....maana kama jamaa ndio walikuwa major share holder......na mikataba ya kazi (waliyonayo) zinazoendelea waliingia wao.....sasa kama wame-cease siju utaratibu unakuwaje?......Fundi Mchundo/Mtanzania/Morani/Mwendapole hebu tupeni shule hapo

Mkuu Ogah, hapo mkubwa nadhani ni zaidi kwenye sheria manake kuna mambo matatu ambayo kwa kweli sina ujuzi nayo kabisaaa:
1. Fate ya wale staff wazawa na maybe waliotoka nje - Hapa ni Labour laws and contractual matters

2. Corruption charges as accused by WB - Hapa nadhani kuna watu wa PCCB na hao WB wenyewe kuangalia what really happened, na mwisho

3. Kufanya kazi bila kibali - Hapa kuna professional bodies na other registration bodies vikiwemo BRELA, ERC, ACET nk.... Humu pia wanaweza wakaingia hata TRA kwenye maswala ya kodi nk....

Pamoja na kusema hayo hapo ju, mimi kuna kakitu kananishangaza kidogo. Unajua ukisoma zile tender documents wanaandika kabisa lazima uwe a registered company ili uweze ku bid.... Sasa hawa jamaa wamekuwa wanapiga miradi mikubwa mikubwa kule na huko throughout Bongo bila vibali, je wale wanaofanya evaluation walikuwa hawalioni hili?? Lets assume kumetokea a claim in any of the projects done by this firm, je nani watambana kwenye mambo ya "Professional Indemnity???".....

Kama ambavyo wanaJamvi wengi wamekuwa wakisema, IT CAN ONLY HAPPEN IN TANZANIA........ Sasa naanza kukubaliana nalo.... Hivi mnakumbuka kwenye case ya Richmond (report ya Mwakyembe et al), jamaa waliweka kwenye reference kuwa walifanya ujenzi wa 60,000seat stadium in Dar, and guess what evaluators never noticed that!!!!!!

Mungu Ibariki Tanzania...........
 
Hivi thinking about it, ina maana hawa jamaa hawana kazi hapa mjini at this moment?? Manake lazima kuna watu wanaweza wakalizwa na what about ongoing projects au zile completed na bado zipo kwenye "Defect liability Period".... Assets zao (if they have any) bado hazijakamtwa tu????????

Its hard to believe such a scenario can actually happen in a country like ours jamani*&^%$#@
 
Morani75,

Mzee shukrani kwa maoni yako........hii issue inaonekana si rahisi kama inavyofikiriwa...........ume-raise a VER GOOD POINT........evaluation team/s hawakuliona hili ktk miradi ambayo hawa jamaa wanayo in hand na hata iliyokwisha?

....je inawezekana Norconsult ilikuwa na registration certificate feki!??.........hii issue naona itaondoka na wengi, kuanzia TRA, BRELA na TANROADS............

well,...............its high time now hata hivi vyombo vyetu vya usalama i.e. TISS na PCCB vikawa vinahusishwa (kama vilikuwa vinahusika.....basi na wao....wawajibishwe i.e the officers involved) katika mchakato wa kutoa kazi kwa makampuni yote iwe ya ndani na nje pia..........
 
Jamaa hawana kazi and that is that.Norconsult walikuwa na contractors, wengine walikuwa wanaajiliwa seasonally na kukiwa na msimu hawana deal sana, au kama hawakutaki tu wanakupiga stop.Thats how these contracts are structured and people in need of a job did not bother to think about such consequences.

Kwa hiyo sijui kama hii kesi inaweza kubadilisha sana hili.Wataambiwa tu tunafunga ofisi ya Tanzania kutokana na corruption charges, at best kama vipi ulijiandikisha unatoka Mpanda huko unakatiwa nauli and thats that.Sijui hata kama contracts zao zina severance payments au kama hii inaweza ku qualify as a condition to get severance payment.

Lakini Norwegians si watu wabaya na ni wasoshalisti wazuri tu (ingawa Norconsult has a pretty much capitalistic and international face) wanaweza kuwapa kifuta jasho (my worry is the difference between the status of contractor and employee, unaweza kukuta Kifukwe na ma director watatu wanne peke yao ndiyo employees na wengine ni contractors wasio hna haki zozote!)
 
Angalieni gazeti lao Norwegian wakati waziri mkuu wao alipokuja TZ

Stoltenberg confronts problems in Africa
Prime Minister Jens Stoltenberg was greeted by a cannon salute and waving Norwegian flags when he arrived in Tanzania on Monday, but plenty of problems lay lurking below the festive surface.

Tanzania is one of the lands that have receive most aid from Norway over the years, and the warm welcome to Stoltenberg and his wife, Ingrid Schulerud, was therefore not unexpected, writes newswire NTB.

Environment and Development minister Erik Solheim was also among the Norwegian visitors and it was announced that Norway has set aside NOK 500m (USD 100m) to be used over a five-year period in a partnership agreement with Tanzania for forests and the climate.

Deforestation in Tanzania is among the largest in Africa measured in terms of area, only surpassed by Sudan and Zambia. Emissions from deforestation are thought to be around 100 million tons per year, about double the total emissions from Norway, according to the Norwegian Foreign Ministry.

The run-up to the Tanzania visit has been far from problem-free, however, with a lot of media focus on corruption in foreign aid and very questionable Norwegian investments in mines in Africa.

A Norwegian accounting firm recently claimed that around NOK 150m (USD 30m) in foreign aid earmarked for tree-planting projects in Tanzania had probably ended up in the pockets of corrupt officials and politicians.

The matter is still under investigation, but the development minister has admitted that Norway has been naïve at times.

In addition, Kirkens Nødhjelp (KN) (Norwegian Church Aid) has claimed the Norwegian Oil Fund has invested over NOK 2bn (USD 400m) in three gold-mining companies that are stripping Tanzania's local people of their land and natural resources.

Before he travelled to Tanzania, Stoltenberg held a speech on Sunday, at the SADC Summit in Mauritius, in which he criticized the situation in Zimbabwe following recent elections there.
NTB/Aftenposten English Web Desk
Catherine Stein

Lakini kumbe ndio wao wanazichukua hizo fedha back halafu waja kutudai na interest kubwa....HYPOCRITES

Kina Kifukwe waliwekwa tu pale kama frontman na nadhani jamaa hata qualifation za management hana... si huyu jamaa alikuwaga utalii college NBI?

Hapo ndipo mtu unajiuliza kweli tutafika? nimeona vijana wengi ambao wana damu za kizalendo waliosoma nje na ndani na wanapotaka kufanya kitu kuendeleza maisha yao na yetu jinsi wanavyo kwamisha na urasimu uliojaa pale BRELA,,TRA..PORT mpaka wanaishiwa na inabaki nao waaanze kukata kona na kufuata nyayo zao hao mafisadi


POLE SANA TANZANIA.....LAKINI USIJALI IKO SIKU NA SIO MBALI SANA....(i hope)
 
Angalieni gazeti lao Norwegian wakati waziri mkuu wao alipokuja TZ



Lakini kumbe ndio wao wanazichukua hizo fedha back halafu waja kutudai na interest kubwa....HYPOCRITES

Kina Kifukwe waliwekwa tu pale kama frontman na nadhani jamaa hata qualifation za management hana... si huyu jamaa alikuwaga utalii college NBI?

Hapo ndipo mtu unajiuliza kweli tutafika? nimeona vijana wengi ambao wana damu za kizalendo waliosoma nje na ndani na wanapotaka kufanya kitu kuendeleza maisha yao na yetu jinsi wanavyo kwamisha na urasimu uliojaa pale BRELA,,TRA..PORT mpaka wanaishiwa na inabaki nao waaanze kukata kona na kufuata nyayo zao hao mafisadi


POLE SANA TANZANIA.....LAKINI USIJALI IKO SIKU NA SIO MBALI SANA....(i hope)

Just to set the record straight, Kifukwe anatakiwa kuwa Engineer aliyesoma India na Norway.
 
Just to set the record straight, Kifukwe anatakiwa kuwa Engineer aliyesoma India na Norway.

Ni kweli Kifukwe alisoma Norway, akaoa mama wa Norway. Baada ya muda mama
akaja TZ kama Tx, kisha akamvuta Kifukwe naye kuja kama TX wakati ni Mtanzania.

Wakazizoa za kuwa TX miaka mingi tu. Nafikiri baadaye ndio wakafanya mabadiliko kwenye mfumo wa kampuni yao.

Mkewe ambaye kama sikosei sasa wameachana ni balozi/mfanyakazi (sina uhakika 100%, ila nafikiri ni balozi) wa ubalozi wa Norway huko Uganda.
 
Haya ndiyo niliyoyandika jana, tunakimbilia kusema kampuni za Watanzania zina wababaishaji, kumbe wanashindana na majambazi ya kimataifa.

Kampuni ya Mswahili itachunguzwa na papers kufunguliwa mara 20, anakuja mzungu, ni pita tu bwana mkubwa.

Hao hao BRELA au TRA ndio tukipita wengine na kufuata kila sheria wanatuona
kama takataka, hii nchi yetu imejaa Wajinga na Wapumbavu wengi sana serikali, itakuwa ngumu mno kuendelea.

Nina mengi sana ya kuandika kuhusu ujinga na ubwege wa Watanzania inapokuja kwenye masuala yanayohusu Watanzania wenzao na wageni. Nitasubiri mpaka nije niweke kwenye kitabu kwi kwi kwi!!!

Hapa mkuu umenena.

Unajua hata ubalozi wa TZ London wageni huwa wanachukua dakika zisizopungua 20 kukamilisha shughuli zote za kupata viza ya kuingia Tanzania.

Hapo huwa wanakuwa na pasi zao mikononi na hulipa hio ada ya viza ambayo kwa siku nafikiri nchi yetu inaingiza sana.

Nilipigwa na butwaa pale nilipoona msururu wa wageni kuonekana kwisha mapema kuliko msururu wa watanzania.

Naisifia sana nchi ya Brazil ambao nao wameweka mtindo wa kuchukua alama za vidole kwa mgeni yeyote yule kutoka USA.
 
Hivi jamani kuna yoyote ajuae kama sheria za utoaji tenda iwe serikalini au katika makampuni na mashirika ya umma inasemaje?

Kukiwa na Legislation katika sekta kama haya ya ujenzi nafikiri watanzania watanufaika zaidi.

Kipaumbele kiwe kwa waTZ kwanza halafu ndio wanaangaliwa ma-expert ambao watakuwa wanakuja kwa muda maalum.
 
Hivi jamani kuna yoyote ajuae kama sheria za utoaji tenda iwe serikalini au katika makampuni na mashirika ya umma inasemaje?

Kukiwa na Legislation katika sekta kama haya ya ujenzi nafikiri watanzania watanufaika zaidi.

Kipaumbele kiwe kwa waTZ kwanza halafu ndio wanaangaliwa ma-expert ambao watakuwa wanakuja kwa muda maalum.

Rich,

Resource nzuri ya sheria za Tanzania hii hapa chini, I am not sure kuhusu hiyo unayotafuta lakini ina documents za sheria nyingi sana.

http://www.lexadin.nl/wlg/legis/nofr/oeur/lxwetan.htm
 
Why did Norconsult AS left in a hurry ......


1. Assumption moja ni kuwa wamevunja cardinal rule ya serikali yao (Sheria kwao ni msumeno na wanafahamu what will be next) hivyo faini yao itakuwa kubwa na huenda wakapoteza billions sio Tanzania bali kokote wanakofanya kazi ulimwenguni.

2. Ili kutokuipaka matope serikali yao wameona bora wakimbie, Je ubalozi wa Norway wanasemaje pale Dar? Je, walikuwa hawalijui hili?

3. Wasingeweza kujikosha kwa maajabu yao na ni lazima Norwegian Embassy know what is cooking (I presume)

4. Je serikali ya JK itachukua hatua gani kwa kampuni hii (Norconsult AS ambayo kutokana na vitendo vyake inakubali kuvunja sheria) na zile ambazo hazikusajiliwa kihalali?



Je, Kampuni zingine kama Konoike, Cowiconsult, H. P. Gauff GmbH, Carbro na nyinginezo hawana matatizo kama yaliyowakumba Norconsult?
 
Kuna argument kuwa Norconsult AS na Norwegian Embassy walikuwa hawajui kitu, hii isue ilikuwa ya Kifukwe na ma-goons wake pale Norconsult.
 
Kuna tendency ya watanzania kuamini kuwa watu au kampuni za kutoka nchi za Scandinavia ni waaminifu kwa sababu ya misaada wanayotupa. Lakini na wao wana wajanja wao ambao hawachelewi kunyonya au kupindisha sheria. Nakumbuka kuna waliowai kuwekeza katika nchi moja lakini kiwanda kilikuwa cha madawa ya kulevya.
 
Kuna argument kuwa Norconsult AS na Norwegian Embassy walikuwa hawajui kitu, hii isue ilikuwa ya Kifukwe na ma-goons wake pale Norconsult.

Mkuu,
Huo hauwezi kuwa utetezi hata siku hasa kwenye haya makampuni makubwa. Ndio maana vitu kama code of conducts ni muhimu kweli kweli kwenye haya mashirika makubwa.

Miaka kumi walikuwa hawajui matatizo kwenye subsidiary yao? Hiyo sababu sio utetezi wa kutosha kabisa.

Nafikiri wameamua kutoka clean na ndio maana wameamua kufunga virago mapema kama njia ya kuanza kujisafisha na kuokoa miradi yao ya sehemu zingine.
 
Why did Norconsult AS left in a hurry ......


1. Assumption moja ni kuwa wamevunja cardinal rule ya serikali yao (Sheria kwao ni msumeno na wanafahamu what will be next) hivyo faini yao itakuwa kubwa na huenda wakapoteza billions sio Tanzania bali kokote wanakofanya kazi ulimwenguni.

2. Ili kutokuipaka matope serikali yao wameona bora wakimbie, Je ubalozi wa Norway wanasemaje pale Dar? Je, walikuwa hawalijui hili?

3. Wasingeweza kujikosha kwa maajabu yao na ni lazima Norwegian Embassy know what is cooking (I presume)

4. Je serikali ya JK itachukua hatua gani kwa kampuni hii (Norconsult AS ambayo kutokana na vitendo vyake inakubali kuvunja sheria) na zile ambazo hazikusajiliwa kihalali?



Je, Kampuni zingine kama Konoike, Cowiconsult, H. P. Gauff GmbH, Carbro na nyinginezo hawana matatizo kama yaliyowakumba Norconsult?

Mkuu, inaelekea uliondoka zamani! Konoike ni contractors na sio consultants. H.P.Gauff GmbH, Carl Bro, Sweco waliishaondoka zamani! Nadhani makampuni ya kigeni ya uhandisi yaliyobaki ni Howard Humphreys na Cowi Consult.

Mazingira ya kufanya kazi nyumbani kwa makampuni ya kigeni ni magumu mno tofauti na tunavyodhania.
Kwanza, registration fees na subscription fees za consultancy firms za kigeni katika professional bodies ni kubwa mno.
Pili, wataalamu wa kigeni individually nao wanatakiwa kuwa registered na wao nao fees zao ni za juu sana ukilinganisha na zile kwa raia wa Tanzania.
Tatu, makampuni mengi haya yalikuja ili kutekeleza miradi inayofadhiliwa na nchi zao. Kwa muelekeo wa ufadhili umebadilika na kuwa multi-lateral (EU, World Bank etc) inakuwa vigumu kwa nchi moja moja kupigia debe kampuni zake.
Nne, baada ya soko kufunguliwa pamekuwa na ushindani mkubwa kutoka makampuni ya nyumbani (TanConsult, M-Konsult etc) ambayo wakati mwingine yanashirikiana na makampuni mengine ya nje.
Tano, mdudu rushwa umeingia mno katika utoaji wa contracts, eneo ambalo haya makampuni mengine yanabanwa na sheria za kwao.

Ili kuepuka mengi ya haya , makampuni mengine yamekuwa localised. Hii inawapunguzia mzigo wa fees maana as a local company fees ni ndogo na vile vile kuruhusu washirika wao wabongo kucheza mchezo tunavyojua wenyewe. Mara nyingi u'foreign company' unakuwa token tu, ili kuwawezesha kupata miradi michache inayotoka kwao na kubakiza veneer ya kuwa bado ni clean.

Kuhusu wafanyakazi katika makampuni kama haya yanayofunga virago, naamini kuwa wanalipwa terminal benefits zao vizuri tu. Na tusisahau kuwa kama kuna ulaji mara nyingi hata wale watendaji wasimamizi nao wananufaika! Wafanyakazi wakisha jua bosi kuwa ni mwizi basi nao huwa hawasiti kujichukulia pensheni yao mapema.

haya yote niliyoyazungumzia hapa ni general na si lazima kuwa NorConsult ikawa na yenyewe imo katika kundi hili. Siwajui kwa hiyo siwezi kuwazungumzia. Kinachoniuma mimi ni kuwa hawa mabwana kama sikosei ndiyo waliyotayarisha Environmental Impact Assessment report kuhusu mradi wa Soda Ash lake natron na kudai kuwa flamingoes hawatadhurika! kama kweli ni wachafu, na makampuni kutoka India tunayajua, nina wasi wasi hasa na genuineness ya hiyo assessment. kwangu mimi, mengine yote tisa ila kwenye hili kama walihusika inabidi washughulikiwe KIKAMILIFU.

Amandla!
 
Wakuu well put.... Hivi tukirudi ile miaka ya mwishoni mwa 90 (nadhani ilikuwa around 1998/9) mnakumbuka kuwa CarlBro walifunga ofisi kwa kashfa karibu sawa na hii?? Just to refresh our memories ni kuwa kilichotokea then ndicho kinachotokea sasa na pia wale jamaa walifunga duka wakati wana kazi kubwa nyingi tu, pamoja na kwamba kuna walioponea kwa kitendo kile kwa kupata magari etc lakini nakumbuka kuna ambao walienda kwenye a total/silent death wakati ule.......

So hii si kitu kigeni kutokea na wala haitakuwa mwisho kutokea, swali ni kwamba tutaendelea kuona haya mpaka lini?? CarlBro did the same crap and now wamerudi kuanzia miaka ya 2005ish through their office in Uganda, je tumeweza kuwa scrutinize kuona kilichotokea 1998 hakitajirudia tena?? Au wamerudi sasa kama CarlBro International tunaamini kuwa wamekuwa wasafi?? Au kule kwenye registration bodies hawana records kuwa the firm was once registered in Tz as a foreign consulting firm but walifunga duka katika mazingira yasioyoeleweka pamoja na kwamba walikuwa na good jobs as well as reputation then??

Naomba kuwakilisha...........
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom