GOOD: DK Slaa atibua mambo kwa Wassira

nngu007

JF-Expert Member
Aug 2, 2010
15,862
5,797
Sunday, 27 February 2011 21:04 0diggsdigg

_dk%20wilbord%20slaa.jpg
Katibu mkuu wa Chadema,Dk Wilbroad Slaa

Anthony Mayunga, Bunda na Frederick Katulanda, Butiama
ALIYEKUWA mgombea ubunge wa ubunge kwa tiketi ya Chadema jimbo la Bunda Elias Maarugu ametimuliwa kwenye mkutano wa hadhara wa chama hicho uliohutubiwa na katibu mkuu Dk Wilbroad Slaa baada ya kukataliwa
na wananchi kwa madai kuwa alihongwa na kumwachia Stephen Wasira.

Dalili za kumkataa Maarugu zilianza mapema mara baada ya kuitwa asalimie wananchi mjini Bunda, umati mkubwa wa wananchi ulipiga kelele na kudai hawataki kumsikiliza kwa kuwa aliwasaliti na kuuza haki zao.

Wananchi hao walipiga kelele wakisema hawako tayari kumsikiliza huku wakimtaka atoke jukwaani kwa kuwa hafai, "hatumtaki huyo mtoeni hapo aliuza kura, alihongwa msaliti hafai mtoeni hatutaki kumsikiliza.”

Kelele hizo zilisikika sauti kwa nguvu za wananchi waliojaza uwanja wa stendi ya zamani.

Licha ya Maarugu kujikakamua na kusema Peoples, wananchi walipaza sauti na kumtaka atoke haraka sana," hatutaki kumsikiliza huyo mtoeni huyo hafai msaliti alikuwa wapi kwanini amekuja leo siku zote alikuwa
wapi?”walihoji.

Kutokana na kelele na wananchi kugoma kumsikiliza Dk Slaa alilazimika kuingilia kati na kusema kuwa, "sauti ya wengi ni sauti ya Mungu, hivyo kama umma wote huu unakukataa ndugu yangu Maalugu kuna kitu naomba utueleze kwa nini watu hawa wanakukataa.”

Hata hivyo katibu mkuu huyo kuwataka wananchi wawe na subira wananchi waliendelea kugoma na kusema kuwa hawako tayari kumwona wala kumsikiliza hivyo wakamtaka atoke eneo hilo.

“Maarugu Chadema inapinga ufisadi ndani na nje ya chama kama unatuhumiwa wewe ni mtu mzima na kuheshimu sana nakuomba uamke taratibu uage uende kwako na sisi tunakuchunguza, natamka kuanzia sasa
kuwa nakufutia ugombea wa miaka mitano ijayo kwa kuwa hufai maana nakataliwa na wananchi, nitatoa taarifa kwenye kamati tendaji ya chama,”alisema.

Kutokana na kauli hiyo Maarugu ambaye aliwahi kuwa mkuu wa wilaya ya Magu na Misenyi alilazimika kushuka taratibu huku akizomewa na maelfu ya wananchi waliokuwa wamefurika hapo,huku Dk Slaa akiwasihi wananchi
wasimpige,kumtukana kwa kuwa suala lake bado linachunguzwa na wananchi watapewa majibu.

Aliagiza kamati tendaji ya chama wilaya kuketi haraka kujadili kisha kutoa taarifa kwake ndani ya wiki mbili, na kama wataridhika nayo wataifanyia kazi,vinginevyo watalazimika kuunda kamati maalumya kufuatilia kwa kuwahoji wananchi wa jimbo hilo.

Mapema Mkurugenzi wa mambo ya Bunge na halmashauri wa chama hicho John Mrema alisema kitendo hicho hakipaswi kuvumiliwa hata kwa viongozi wengine wa chama hicho na kuwa chadema mambo yao yako wazi.

Wakati huo huo Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe amekataa madai ya wakazi wa Tarime kudai kuwa kura zao zilichakachuliwa na CCM kushinda Ubunge katika jimbo hilo.

Akizungumza jana katika uwanja wa mpira wa barabara ya Nyamwaga, mwenyekiti wa Chadema, alisema hakubaliani na hoja za watu kusingizia chama chake kilishindwa uchaguzi kutokana na kuchakachuliwa kura bali mgawanyiko wa ndani.

Alisema katika kipindi cha uchaguzi alifika Tarime na kukaa kikao na viongozi wa chama chake Tarime na kubainisha kuwa katika kikao hicho aliwaeleza wazi kama hawajui kushindwa uchaguzi na kama wamesahau kutawaliwa na CCM basi wajue kuwa watajifunza pale ambapo kiti cha ubunge kitakapo ondoka.

“Niliwaeleza katika kikao cha ndani kama hawajui hathari za ubinafsi basi watajifunza pale watakapopoteza kiti cha Ubunge, niliwaeleza kuwa mtajifunza pale mtakapotawaliwa na CCM. Sasa kuniambia kuwa kura zilichakachuliwa nakataa…sababu naijua,” alieleza Mbowe ambaye alionekana kukasirika.

Mwenyekiti huyo ambaye ni kiongozi wa kambi ya upinzani Bungeni, alisema ingawa alitambua mpasuko huo, yeye akiwa kiongozi wa chama mwenye dhamana ya kupitisha majina ya wagombea, walipoletwa waliogombea waliwapima kwa vigezo na kuamua kulirudisha jina la Waitara Chacha.

“Leo nalisema hili ili mjue kuwa pale ubinafsi unapotawala katika harakati za ukombozi ni hatari sana…, Mwera alikuwa anataka kuwa mbunge, Waitara, Heche na Matage, wote hawa waliutaka ubunge lakini hawawezi kuwa wote ni lazima ashinde mmoja,” alifafanua.

Alisema kuwa kila mmoja anayo haki ya kugombea ubunge lakini inapofikia kila mmoja anataka kushinda hapo ndipo inapokuwa ngoma.

“Nasema tulirudisha jina la Waitara, hatujutii hilo na wala watitajutia. Mwera anaona ahaa…, nadhani hakuridhika, siwezi kujadili mtu hapa na Mwera namheshimu. Basi hapa ndipo ukatokea mgawanyiko na ninyi mkawashabikia mkasahau tatizo siyo mtu bali ni kushinda ubunge,” alisema Mbowe.

Alisema lakini tokea kumalizika kwa uchaguzi huo watu wakawa wanasema kuwa walisalitiwa na wao kwa wao na wengine kwenda nje ya wilaya kusaidia kampeni jambo ambalo alisema siyo kweli na kusema kwa vile uchaguzi umekwisha sasa ni zamu ya kujipanga na kuangalia walipokosea na kujiandaa kwa uchaguzi.

“Sitaki kusikia hili la kuchakachuliwa kura Tarime, kama mnadai kuwa mlichakachuliwa kura mlikuwa wapi? Ukerewe ambao walikuwa wakiambiwa mambo kama tarime wameshinda, mabomu yalipigwa lakini wakerewe walikomaa na matokeo yakatangazwa, Mwanza risasi za moto zilipigwa na mabomu usiku kucha siku tatu lakini wakaona looo watangaze sasa Tarime mlikuwa wapi?” alihoji Mbowe.
 
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Uratibu na Uhusiano), Steven Wassira, amemtaka Katibu Mkuu wa Chadema, DK Willibrod Slaa, kutumia elimu yake ya udaktari kuzumgumza mambo ya kitaalamu badala ya kutaka kusikika.

Wassira alisema kinachofanywa na Dk Slaa ni kutaka kusikika. "Kitendo cha Dk Slaa kupita jimboni kwangu Bunda na kuwaambia wananchi kwamba mimi sifai kwa kuwa nimewasababishia njaa, kinaonyesha anavyoshindwa kutumia taaluma yake kujenga hoja za msingi" alisema Wassira.

Kwa mujibu wa Wassira, Dk Slaa aliwaeleza wananchi hao kuwa amewaletea njaa licha ya kwamba alikuwa Waziri wa Kilimo na Umwagiliaji. "Simwelewi DK Slaa, siasa sio kuzumgumza zungumza tu hata kama huna hoja za msingi, kwanza yeye ni Daktari halafu ni mtu mzima, anawaambia wananchi wangu kule Bunda kwamba mimi nimeleta njaa" alisema Wassira na kuhoji:

"Amefanya utafiti akabaini njaa ya Bunda sababu ni mimi? sasa kuna Jumanne Magembe na Mwanga kuna ukame, je yeye ndio kasababisha?

Mwananchi Machi 16 2011
 
Inaelekea huyu Wassira ni zuzu kwelikweli. Hata anavyongoea inaelekea anafikiri Dr. Slaa ni daktari wa watu!!!
 
Kama kuna binadamu anayeichukia CHEDEMA kwa moyo wake wote ni huyu baba! Yani anatamani turudi enzi za TANU lol!
 
Wassira..acha hasira..sababu hasira ni hasara...slaa ni noma...na chadema ni balaaa..watanzania tunaitaka..madaraka tunawapa.:fencing

Nawasilisha
 
Wasiira,tuache porojo. Hoja ya msingi hapa ni kilimo cha kisasa kinachopenya season zote na kinachomnufaisha mkulima hata kama mvua haitanyesha.

Kilio cha nini wakati tuna mito kibao? Hapo ndipo ilipolala hoja ya dkt slaa. Amkeni jamani kumekucha.
 
Sunday, 27 February 2011 21:04 0diggsdigg

_dk%20wilbord%20slaa.jpg
Katibu mkuu wa Chadema,Dk Wilbroad Slaa

Anthony Mayunga, Bunda na Frederick Katulanda, Butiama
ALIYEKUWA mgombea ubunge wa ubunge kwa tiketi ya Chadema jimbo la Bunda Elias Maarugu ametimuliwa kwenye mkutano wa hadhara wa chama hicho uliohutubiwa na katibu mkuu Dk Wilbroad Slaa baada ya kukataliwa
na wananchi kwa madai kuwa alihongwa na kumwachia Stephen Wasira.

Dalili za kumkataa Maarugu zilianza mapema mara baada ya kuitwa asalimie wananchi mjini Bunda, umati mkubwa wa wananchi ulipiga kelele na kudai hawataki kumsikiliza kwa kuwa aliwasaliti na kuuza haki zao.

Wananchi hao walipiga kelele wakisema hawako tayari kumsikiliza huku wakimtaka atoke jukwaani kwa kuwa hafai, "hatumtaki huyo mtoeni hapo aliuza kura, alihongwa msaliti hafai mtoeni hatutaki kumsikiliza."

Kelele hizo zilisikika sauti kwa nguvu za wananchi waliojaza uwanja wa stendi ya zamani.

Licha ya Maarugu kujikakamua na kusema Peoples, wananchi walipaza sauti na kumtaka atoke haraka sana," hatutaki kumsikiliza huyo mtoeni huyo hafai msaliti alikuwa wapi kwanini amekuja leo siku zote alikuwa
wapi?"walihoji.

Kutokana na kelele na wananchi kugoma kumsikiliza Dk Slaa alilazimika kuingilia kati na kusema kuwa, "sauti ya wengi ni sauti ya Mungu, hivyo kama umma wote huu unakukataa ndugu yangu Maalugu kuna kitu naomba utueleze kwa nini watu hawa wanakukataa."

Hata hivyo katibu mkuu huyo kuwataka wananchi wawe na subira wananchi waliendelea kugoma na kusema kuwa hawako tayari kumwona wala kumsikiliza hivyo wakamtaka atoke eneo hilo.

"Maarugu Chadema inapinga ufisadi ndani na nje ya chama kama unatuhumiwa wewe ni mtu mzima na kuheshimu sana nakuomba uamke taratibu uage uende kwako na sisi tunakuchunguza, natamka kuanzia sasa
kuwa nakufutia ugombea wa miaka mitano ijayo kwa kuwa hufai maana nakataliwa na wananchi, nitatoa taarifa kwenye kamati tendaji ya chama,"alisema.

Kutokana na kauli hiyo Maarugu ambaye aliwahi kuwa mkuu wa wilaya ya Magu na Misenyi alilazimika kushuka taratibu huku akizomewa na maelfu ya wananchi waliokuwa wamefurika hapo,huku Dk Slaa akiwasihi wananchi
wasimpige,kumtukana kwa kuwa suala lake bado linachunguzwa na wananchi watapewa majibu.

Aliagiza kamati tendaji ya chama wilaya kuketi haraka kujadili kisha kutoa taarifa kwake ndani ya wiki mbili, na kama wataridhika nayo wataifanyia kazi,vinginevyo watalazimika kuunda kamati maalumya kufuatilia kwa kuwahoji wananchi wa jimbo hilo.

Mapema Mkurugenzi wa mambo ya Bunge na halmashauri wa chama hicho John Mrema alisema kitendo hicho hakipaswi kuvumiliwa hata kwa viongozi wengine wa chama hicho na kuwa chadema mambo yao yako wazi.

Wakati huo huo Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe amekataa madai ya wakazi wa Tarime kudai kuwa kura zao zilichakachuliwa na CCM kushinda Ubunge katika jimbo hilo.

Akizungumza jana katika uwanja wa mpira wa barabara ya Nyamwaga, mwenyekiti wa Chadema, alisema hakubaliani na hoja za watu kusingizia chama chake kilishindwa uchaguzi kutokana na kuchakachuliwa kura bali mgawanyiko wa ndani.

Alisema katika kipindi cha uchaguzi alifika Tarime na kukaa kikao na viongozi wa chama chake Tarime na kubainisha kuwa katika kikao hicho aliwaeleza wazi kama hawajui kushindwa uchaguzi na kama wamesahau kutawaliwa na CCM basi wajue kuwa watajifunza pale ambapo kiti cha ubunge kitakapo ondoka.

"Niliwaeleza katika kikao cha ndani kama hawajui hathari za ubinafsi basi watajifunza pale watakapopoteza kiti cha Ubunge, niliwaeleza kuwa mtajifunza pale mtakapotawaliwa na CCM. Sasa kuniambia kuwa kura zilichakachuliwa nakataa…sababu naijua," alieleza Mbowe ambaye alionekana kukasirika.

Mwenyekiti huyo ambaye ni kiongozi wa kambi ya upinzani Bungeni, alisema ingawa alitambua mpasuko huo, yeye akiwa kiongozi wa chama mwenye dhamana ya kupitisha majina ya wagombea, walipoletwa waliogombea waliwapima kwa vigezo na kuamua kulirudisha jina la Waitara Chacha.

"Leo nalisema hili ili mjue kuwa pale ubinafsi unapotawala katika harakati za ukombozi ni hatari sana…, Mwera alikuwa anataka kuwa mbunge, Waitara, Heche na Matage, wote hawa waliutaka ubunge lakini hawawezi kuwa wote ni lazima ashinde mmoja," alifafanua.

Alisema kuwa kila mmoja anayo haki ya kugombea ubunge lakini inapofikia kila mmoja anataka kushinda hapo ndipo inapokuwa ngoma.

"Nasema tulirudisha jina la Waitara, hatujutii hilo na wala watitajutia. Mwera anaona ahaa…, nadhani hakuridhika, siwezi kujadili mtu hapa na Mwera namheshimu. Basi hapa ndipo ukatokea mgawanyiko na ninyi mkawashabikia mkasahau tatizo siyo mtu bali ni kushinda ubunge," alisema Mbowe.

Alisema lakini tokea kumalizika kwa uchaguzi huo watu wakawa wanasema kuwa walisalitiwa na wao kwa wao na wengine kwenda nje ya wilaya kusaidia kampeni jambo ambalo alisema siyo kweli na kusema kwa vile uchaguzi umekwisha sasa ni zamu ya kujipanga na kuangalia walipokosea na kujiandaa kwa uchaguzi.

"Sitaki kusikia hili la kuchakachuliwa kura Tarime, kama mnadai kuwa mlichakachuliwa kura mlikuwa wapi? Ukerewe ambao walikuwa wakiambiwa mambo kama tarime wameshinda, mabomu yalipigwa lakini wakerewe walikomaa na matokeo yakatangazwa, Mwanza risasi za moto zilipigwa na mabomu usiku kucha siku tatu lakini wakaona looo watangaze sasa Tarime mlikuwa wapi?" alihoji Mbowe.

Nimefurahishwa sana na hii kitu, kama watu hawakupendi unaachia ngazi mwenyewe, na kama watu wamefahamu kuwa uliuza haki yao huna haki ya kuwa mmoja wao.
 
Wasira unatakiwa uone aibu. Eneo kubwa la bunda liko mita 5 kutoka usawa wa ziwa victoria lakini wana bunda hawana maji. Kuna sababu ya kuwa na njaa bunda kweli. Shame on you.
 
Wasira anakasirika nini si ndio yeye alikuwa anauza sera ya Kilimo Kwanza sasa kilimo kwanza ni kilimo cha kungoja msimu wa mvua kweli naye awe mkweli alipokosea akubali ili afanya bidii wananchi Bunda wafanye kilimo cha umwagiliaji
 
Habari murua kabisa.

Nadhani Slaa atume watu wa makao makuu ilikuokoa hilo jimbo, maana hilo jimbo si la CCM siku zote ilifikia hatua wakaligawa kwa sababu ya Pressure ya upinzani nilishangaa sana kuona CCM wanalichukua mara mbili wakati hata Wassira aliwai kulipata kwasababu ya Upinzani!
 
Nimechoka kweli kweli na ujinga wa huyu Wassira hivi anadhani hiki bado ni kizazi cha "zidumu fikra za mwenyekiti na mapinduzi nitakulinda mpk kufa"?!!!!................. haki ya Mungu CCM inaumbukaje mwaka huu? navutiwa na kufurahishwa sana na huu mwamko wa watanzania............ lets go guys ............ lets go......................
 
NIDHAMU YA WOGA
Waswahili hutafsiri nidhamu ya woga kama - UNAFIKI. Hili ndio tatizo kubwa la viongozi wetu pamoja na kundi kubwa la wananchi wa Tanzania.

Habari hii nitakuja itafutia mida niandike kitu safi kuhusiana na na somo hilo hapo juu. Nidhami ya Woga.
 
Alikuwa Upinzani kwanini Alirudi Chama Tawala? Umaarufu wake uliisha???
 
Back
Top Bottom