All in all he is ahead of them if at all they had any plans to expel him fro the party
Mzee, mchezaji akimpiga kanzu golikipa anakuwa anaelekea golini, sasa akipiga tena na tobo si atakuwa anarudisha mpira uwanjani badala ya kufunga !?Mwingine anaweza kusema kapigwa kanzu halafu akapigwa tobo.
Mimi mwenyewe nina wasiwasi jamaa wasijekuharibu mchakato wa kutoa usajili wa kudumu kwa CCJ.Kuna habari kuwa msajili wa vyama vya siasa ana maagizo kutoka kwa mkulu kuwa asikipe CCJ usajili wa kudumu mpaka baada ya uchaguzi. Na ukizingatia kuwa hataki kuruhusu suala la mgombea binafsi bado CCM wataendelea kupeta
Mrema katika zama za mwanzo za siasa za upinzani ni tofauti na mPENDAZOE wa zama hizi za kisiasa.Mpendazoe F. wa 2010 ninamfananisha na Mrema A. L. wa 1995.
Tusubiri matokeo.
Mzee, mchezaji akimpiga kanzu golikipa anakuwa anaelekea golini, sasa akipiga tena na tobo si atakuwa anarudisha mpira uwanjani badala ya kufunga !?
Leo nilisikia kauli ya Tambwe Hiza kuhusu kuhama kwa Mpendazoe
Alisema yeye amefurahi sana kuona Mpenda zoe amehama CCM kwani alikuwa anaibana sana CCM na amesema atafurahi akisikia wale wote waliokuwa kundi moja wapinga ufisadi wakihama Chama Hicho, kwani chama kitakuwa salama na hakitakuwa na migogoro. lakini hakusema endapo wanaotuhumiwa ufisadi nao wahame. jee Tambwe anafurahia Ufisadi ndani ya CCM? jee kiongozi anafaa kuwa Mbunge? anafaaa kutuongoza?Jeee akipata nafasi hizo hatozila Fedha zetu kwa kuwa wote wataobaki CCM watakuwa kimya baada kundi ambalo Tambwe halipendi likiondoka?
na wenyewe wana vituko.. sasa kama alikuwa mzigo kwanini hawakumtua au wao ndio walikuwa mzigo yeye kawatua..
Mimi mwenyewe nina wasiwasi jamaa wasijekuharibu mchakato wa kutoa usajili wa kudumu kwa CCJ.
Lazima maumivu wanayasikilizia. ukiachana na hilo huyu Mh. kawamaliza sana manake ni kama timu mnaongoza mpaka dakika ya 90 then kwenye majeruhi jamaa wanarudisha na kuongeza bao. Natumaini CCM watakuja na hoja za msingi. Subiri siku moja ambapo vijana wa kitanzania watakapoamua kukipa talaka chama hiki hilo litakuwa sio tena bao bali gharika.