cheusimangala
JF-Expert Member
- Feb 27, 2010
- 2,585
- 497
wasichana wenzangu amani ya Mungu iwe juu yenu.
Kuna habari fulan mtu kanieleza imepelekea niamue kuwashauri juu ya hili.
Ni hivi,
Nawashauri kama una rafiki yako mnapendana kiasi cha kuwa kama ndugu mnaoshirikiana na kusaidiana katika mambo mabalimbali,usihamie na kukaa naye nyumba moja sababu utampoteza.
Najua wengi wanafikiri itakua raha zaidi kama yeye na rafiki yake wanayependana watakaa katika nyumba moja lakini wanakua wanakosea sababu uchunguzi wangu unaonesha wengi wanaishia kugombana.
Hii ni kwa wale wenzangu na mie ambao bado hawajaolewa,wanaoishi peke yao.
SABABU ZA MIM KUPINGA MARAFIKI KUISHI NYUMBA MOJA NI HIZI;
..mkiishi mbalimbali mtakua mna hamu yakukutana kila mara lkn mkiishi pamoja mtagunduana madhaifu yenu hivyo kufanya mkinahiane.
..kila binadamu ana utashi wake,wewe unaweza kuwa uko very organized lkn mwenzio akawa haoni hatari kutotandika kitanda au kutupatupa nguo kila mahali jambo ambalo litakua litakua linakukera na kwa vile yeye ndio tabia yake hata ukimweleza anaweza akarudia hivyo lazima tu mwishowe utakua unanuna nuna na yeye ataona unamfanyia visa kwa kununanuna bila sababu na hapo upendo wenu utakua umepungua.
..mkihamia pamoja mtachanganya vitu venu,hapa kuna hatari ya mmoja wenu kuona vitu vyake mwenzie havithamini vinaharibika.Hii nishasikia watu
wengi wakilalamikia.
.
..Mkiamua kukaa pamoja lazima mtataka kushare gharama za kula na vitu kama hygienic materials,hapa kuna mmoja anaweza kuona yeye anagharamia zaidi ya mwenzake na kwa kuwaza hivi upendo utapungua.
..Pili wewe unaweza kuwa mtu wa kutumia vitu kwa ubahili kwa lengo la kusave pesa kwa maendeleo yako,mwenzio anaweza kuwa ni yule sabun anamimina kwenye mashine hadi nguo haziishi povu hapo lazima wazimu ukupande kichwani.
..mkiishi pamoja lazima msaidiane kazi kama vyombo na kusafisha nyumba lakini mwenzio anaweza kukutegea na hutafurahia au wewe unaweza ukawa majukumu yamekuzidi ukashindwa kumsaidia kama sio muelewa hatafurahia.
..ikitokea mmoja pesa zimekata kwa muda ndio hapo utata unapozidi maana yule anayegharamia ataanza kuona kama vile anakulea japo wakati mlipokua mkiishi mbalimbali alikua hasiti kukukopesha au hata kukusaidia bure.
..nyote ni watu wazima hivyo kila siku kumrekebisha mwenzio ni jambo ambalo hatalifurahia,au kama ni wewe kila siku unaambiwa sipendi ufanye hivi sipendi ufanye vile lazima utajiona huna uhuru.
Kwa kweli nimeshuhudia marafiki wengi waliokuwa wakipendana sana wakiishia kukorofishana baada ya kuwa wanaishi pamoja,kila mmoja anaondoka akimuona mwenzie mbaya lkn ukweli ni kwamba hakuna mbaya kati yao ni hali halisi tu.
Wenzetu wanaume naona wanaurahisi wakuishi pamoja na kuelewana lakini sisi katika hili asilimia kubwa linatushinda.
Halafu kama mmoja ana mtoto mmoja hana ndio inakua balaa lkn kama nyote mna watoto ndio balaa zaidi.
Ni rahisi kwa mwanamke kuishi na mwanaume 8mume)hadi kifo kiwatenganishe na wakaelewana japo kutoelewana kwa hapa na pale kupo lkn mwanamke kuishi na mwanamke mwenzie(rafiki) inaishiaga vibaya LKN PIA NAFAHAMU MARAFIKI WALIOFANIKIWA KUISHI PAMOJA NA WAKAZIDI KUPENDANA NA LEO WAMEOLEWA HAWAITANI MARAFIKI BALI WANAITANA SISTERS
HIVYO USHAURI WANGU NI KWAMBA MSIISHI NYUMBA MOJA NA MARAFIKI ZENU MTAWAPOTEZA.
with love.:A S-rose:
Kuna habari fulan mtu kanieleza imepelekea niamue kuwashauri juu ya hili.
Ni hivi,
Nawashauri kama una rafiki yako mnapendana kiasi cha kuwa kama ndugu mnaoshirikiana na kusaidiana katika mambo mabalimbali,usihamie na kukaa naye nyumba moja sababu utampoteza.
Najua wengi wanafikiri itakua raha zaidi kama yeye na rafiki yake wanayependana watakaa katika nyumba moja lakini wanakua wanakosea sababu uchunguzi wangu unaonesha wengi wanaishia kugombana.
Hii ni kwa wale wenzangu na mie ambao bado hawajaolewa,wanaoishi peke yao.
SABABU ZA MIM KUPINGA MARAFIKI KUISHI NYUMBA MOJA NI HIZI;
..mkiishi mbalimbali mtakua mna hamu yakukutana kila mara lkn mkiishi pamoja mtagunduana madhaifu yenu hivyo kufanya mkinahiane.
..kila binadamu ana utashi wake,wewe unaweza kuwa uko very organized lkn mwenzio akawa haoni hatari kutotandika kitanda au kutupatupa nguo kila mahali jambo ambalo litakua litakua linakukera na kwa vile yeye ndio tabia yake hata ukimweleza anaweza akarudia hivyo lazima tu mwishowe utakua unanuna nuna na yeye ataona unamfanyia visa kwa kununanuna bila sababu na hapo upendo wenu utakua umepungua.
..mkihamia pamoja mtachanganya vitu venu,hapa kuna hatari ya mmoja wenu kuona vitu vyake mwenzie havithamini vinaharibika.Hii nishasikia watu
wengi wakilalamikia.
.
..Mkiamua kukaa pamoja lazima mtataka kushare gharama za kula na vitu kama hygienic materials,hapa kuna mmoja anaweza kuona yeye anagharamia zaidi ya mwenzake na kwa kuwaza hivi upendo utapungua.
..Pili wewe unaweza kuwa mtu wa kutumia vitu kwa ubahili kwa lengo la kusave pesa kwa maendeleo yako,mwenzio anaweza kuwa ni yule sabun anamimina kwenye mashine hadi nguo haziishi povu hapo lazima wazimu ukupande kichwani.
..mkiishi pamoja lazima msaidiane kazi kama vyombo na kusafisha nyumba lakini mwenzio anaweza kukutegea na hutafurahia au wewe unaweza ukawa majukumu yamekuzidi ukashindwa kumsaidia kama sio muelewa hatafurahia.
..ikitokea mmoja pesa zimekata kwa muda ndio hapo utata unapozidi maana yule anayegharamia ataanza kuona kama vile anakulea japo wakati mlipokua mkiishi mbalimbali alikua hasiti kukukopesha au hata kukusaidia bure.
..nyote ni watu wazima hivyo kila siku kumrekebisha mwenzio ni jambo ambalo hatalifurahia,au kama ni wewe kila siku unaambiwa sipendi ufanye hivi sipendi ufanye vile lazima utajiona huna uhuru.
Kwa kweli nimeshuhudia marafiki wengi waliokuwa wakipendana sana wakiishia kukorofishana baada ya kuwa wanaishi pamoja,kila mmoja anaondoka akimuona mwenzie mbaya lkn ukweli ni kwamba hakuna mbaya kati yao ni hali halisi tu.
Wenzetu wanaume naona wanaurahisi wakuishi pamoja na kuelewana lakini sisi katika hili asilimia kubwa linatushinda.
Halafu kama mmoja ana mtoto mmoja hana ndio inakua balaa lkn kama nyote mna watoto ndio balaa zaidi.
Ni rahisi kwa mwanamke kuishi na mwanaume 8mume)hadi kifo kiwatenganishe na wakaelewana japo kutoelewana kwa hapa na pale kupo lkn mwanamke kuishi na mwanamke mwenzie(rafiki) inaishiaga vibaya LKN PIA NAFAHAMU MARAFIKI WALIOFANIKIWA KUISHI PAMOJA NA WAKAZIDI KUPENDANA NA LEO WAMEOLEWA HAWAITANI MARAFIKI BALI WANAITANA SISTERS
HIVYO USHAURI WANGU NI KWAMBA MSIISHI NYUMBA MOJA NA MARAFIKI ZENU MTAWAPOTEZA.
with love.:A S-rose: