Ghasia aagiza Fataki huyu abanwe mbavu....................

Rutashubanyuma

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
219,470
911,173
Ghasia aagiza anayeambukiza Ukimwi abanwe


Na Martha Fataely, Moshi

MWENYEKITI wa baraza la wafanyakazi wa ofisi ya taifa ya takwimu ameagizwa kumchukulia hatua za kisheria mtumishi mmoja ambaye anadaiwa kuwaambukiza Ukimwi kwa makusudi watumishi wa taasisi hiyo. Waziri wa Nchi, Ofisi ya
Rais, Menejment ya Utumishi, Bi. Hawa Ghasia alitoa agizo hilo katika ufunguzi wa kikao cha tatu cha wafanyakazi wa ofisi ya takwimu ya taifa ikiwa ni baada ya kupata taarifa za mtumishi huyo. Kutokana na malalamiko ya watumishi wengi na ukweli wa mambo yenyewe, namuachia mwenyekiti wa baraza wenu alishughulikie haraka iwezekanavyo ili kunusuru nguvu kazi ya taifa isiendelee kuteketea na ili iwe fundisho kwa wengine,� alisema.

Waziri Ghasia alisema amepokea malalamiko mengi juu ya tabia mbaya za mtumishi huyo ambaye inasemekana kutokana na uwezo wa kifedha alionao amekuwa akiwarubuni wasichana wafanye naye mapenzi huku akijua ni muathirika.
Hii sio tabia ya kiungwana lakini kwa kuwa kuna sheria za nchi ambazo zinaelekeza cha kufanya kwa watu kama hawa, hakuna haja ya kumfumbia macho, kwani huu ni mchezo mbaya,� alisema.

Alisema ni vyema kwa mwenyekiti huyo Dkt. Albina Chuwa kutomuonea haya mtumishi huyo kwa kuwa taifa litaendelea kupoteza nguvu kazi na wazazi wametumia fedha nyingi kuwaelimisha watoto wao.

 
Waziri Ghasia alisema amepokea malalamiko mengi juu ya tabia mbaya za mtumishi huyo ambaye inasemekana kutokana na uwezo wa kifedha alionao amekuwa akiwarubuni wasichana wafanye naye mapenzi huku akijua ni muathirika.
Hii sio tabia ya kiungwana lakini kwa kuwa kuna sheria za nchi ambazo zinaelekeza cha kufanya kwa watu kama hawa, hakuna haja ya kumfumbia macho, kwani huu ni mchezo mbaya,� alisema.

Alisema ni vyema kwa mwenyekiti huyo Dkt. Albina Chuwa kutomuonea haya mtumishi huyo kwa kuwa taifa litaendelea kupoteza nguvu kazi na wazazi wametumia fedha nyingi kuwaelimisha watoto wao.
Easier said than done.............ushahidi kuupata ndiyo noma inapoanzia...............................

Inabidi uthibitishe ya kuwa hao waathirika kweli walipata vvu kutoka kwa mshukiwa wa fataki....................kuthibitisha ya kuwa ni kweli alitembea nao.......hapo unahitaji shahawa zake zikutwe kwenye uke zao....................na zipimwe zionekane zina vvu na watuhumu wao hawana vvu hivyo kuthibitisha mtuhumiwa wa fataki kweli ana nia ya kuwaambukiza wahusika...............

kuthibitisha nia ya kuwaambukiza watuhumu nayo ni mtihani mwingine.............................inabidi uthibitishe ya kuwa anaijua hali yake ya kiafya.....kwa maana alishawahi kupimwa na kuonekana ana vvu.kama hajawahi kupimwa inamaanisha ya kuwa hajijui afya yake na hivyo hawezi kupatikana na hatia ya kuambukiza wengine kwa kukusudia................................

Hivi haya Mheshimiwa Ghasia anayajua au ni mwepesi wa kusukumia majukumu mazito hao wengineo.....ambao wamemlalamikia.............
 
kwanini hajamtaja kama anamjua? liyumba si yuko jela au kuna mwingine?
 
kwanini hajamtaja kama anamjua? liyumba si yuko jela au kuna mwingine?
Wanajua athari za kisheria ambazo zinaweza kuwakumba ukizingatia wanafanyia kazi majungu ya mitaani na hayajathibitishwa na madaktari................waathirika hao utawakuta nao ni njiwa tu na hawashikiki sasa wanamtafuta wakumlaumu tu......................
 
Wanajua athari za kisheria ambazo zinaweza kuwakumba ukizingatia wanafanyia kazi majungu ya mitaani na hayajathibitishwa na madaktari................waathirika hao utawakuta nao ni njiwa tu na hawashikiki sasa wanamtafuta wakumlaumu tu......................
kuna haja ya kurudi na mambo ya mze punch hadi maofisini sasa

huyo jamaa atajwe bana
 
kuna haja ya kurudi na mambo ya mze punch hadi maofisini sasa

huyo jamaa atajwe bana

Yaweza kusaidia.........ingawaje tangia watu wamegundua mahakama na msamiati wa kuchafuliwa jina...................basi ipo kazi katika kuwashughulikia hapo.............
 
Easier said than done.............ushahidi kuupata ndiyo noma inapoanzia...............................

Inabidi uthibitishe ya kuwa hao waathirika kweli walipata vvu kutoka kwa mshukiwa wa fataki....................kuthibitisha ya kuwa ni kweli alitembea nao.......hapo unahitaji shahawa zake zikutwe kwenye uke zao....................na zipimwe zionekane zina vvu na watuhumu wao hawana vvu hivyo kuthibitisha mtuhumiwa wa fataki kweli ana nia ya kuwaambukiza wahusika...............

kuthibitisha nia ya kuwaambukiza watuhumu nayo ni mtihani mwingine.............................inabidi uthibitishe ya kuwa anaijua hali yake ya kiafya.....kwa maana alishawahi kupimwa na kuonekana ana vvu.kama hajawahi kupimwa inamaanisha ya kuwa hajijui afya yake na hivyo hawezi kupatikana na hatia ya kuambukiza wengine kwa kukusudia................................

Hivi haya Mheshimiwa Ghasia anayajua au ni mwepesi wa kusukumia majukumu mazito hao wengineo.....ambao wamemlalamikia.............

Ruta:

Kiutaalamu hiyo ni easy kesi. Virus wa HIV wana DNA markers. Hivyo ni rahisi kutambua ni nani ameambukiza.
 
Back
Top Bottom