Gharama za matibabu ya viongozi wastaafu ni kufuru

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,790
288,007
Gharama za matibabu ya viongozi wastaafu ni kufuru
Thursday, 05 July 2012 20:39
Mwananchi

Bunge linaloendelea na kikao chake mjini Dodoma, juzi liliambiwa kwamba Serikali imetenga Sh9 bilioni kwa ajili ya kugharamia matibabu ya viongozi wakuu wastaafu. Akihitimisha mjadala wa hotuba yake, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais anayeshughulikia Menejimenti na Utumishi wa Umma, Celina Kombani alisema fedha hizo ni kwa ajili ya wastaafu wanaopaswa kutunzwa na Serikali.

Bila kuelezea suala hilo kwa undani, Waziri Kombani alisema tu kwamba kiwango hicho kimepungua mwaka huu kutoka Sh10 bilioni zilizotengwa mwaka jana hadi Sh9 bilioni mwaka huu kutokana na idadi ya viongozi wastaafu wanaopaswa kuhudumiwa na Serikali kupungua. Wastaafu wanaoangukia katika fungu hilo ni marais Ali Hassan Mwinyi na Benjamin Mkapa.

Mawaziri wakuu wastaafu ni Joseph Warioba, Samuel Malecela, Cleopa Msuya, Salim Ahmed Salim na Edward Lowasa. Waziri Kombani hakuwataja viongozi wastaafu waliopungua, lakini sote tunafahamu fika kwamba Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere na Mzee Rashid Mfaume Kawawa tayari wametangulia mbele ya haki.

Bila shaka takwimu hizo zitakuwa zimewashangaza wengi kutokana na wingi wa fedha zinazotengwa kila mwaka kugharamia tu matibabu ya viongozi, bila kutilia maanani fedha nyingine nyingi zinazotengwa kama mafao ya viongozi hao wastaafu. Kwa akili ya kawaida, fedha hizo ni nyingi mno kulinganisha na idadi ya viongozi waliokusudiwa na takwimu hizo zinaacha maswali mengi kuliko majibu.

Tunasema hivyo kwa sababu hatuoni jinsi kiasi hicho kikubwa cha fedha kinaweza kugharamia matibabu ya idadi ndogo sana ya viongozi wetu wastaafu, kwani siyo siri pia kwamba wastaafu wetu wengi wamekuwa wakipatwa na maradhi ya kawaida ambayo siyo tu hayahitaji fedha nyingi kuyatibu, bali pia yangeweza kupata tiba hapa nchini. Ndiyo maana tunasema vifungu vikubwa vya fedha zinazotengwa kila mwaka kwa shughuli hiyo siyo tu vinatia shaka, bali pia vinaacha ukungu na kiza kinene vikiwa vimetanda.

Sisi hatusemi kwamba viongozi wetu hao wastaafu hawastahili kupata matibabu kwa kodi zetu. Tunachosema hapa ni kwamba gharama za matibabu yao hazipaswi kuwa siri au kuacha shaka hata kama wastaafu hao walitutumikia vizuri wakati wa utawala wao. Ni sahihi kabisa kwamba walipakodi wangetaka kujua kodi zao zinavyotumika kuwagharimia viongozi wao.

Bado tunasisitiza kwamba Sh9 bilioni kwa matibabu ya viongozi hao wastaafu siyo tu ni nyingi mno, bali pia ni kufuru na za kufikirika. Takwimu hizo hazijumliki hata kidogo. Ni matibabu yapi yenye gharama hata robo ya kiasi hicho kilichotengwa, hata ukiweka usafiri, malazi na gharama nyingine? Ni kichekesho kwamba fedha hizo zimepitishwa na Bunge.

Kinachosikitisha ni Bunge kutohoji fedha zote hizo zinakwenda wapi. Bunge lisiloona umuhimu wa kuibana Serikali iboreshe mazingira na huduma katika hospitali zetu ili viongozi na wananchi watibiwe katika hospitali hizo badala ya kupeleka fedha zetu nje na kujenga uchumi wa nchi nyingine. Ebu fikiria hili: Mwaka uliopita, wagonjwa waliopelekwa India kutibiwa mwaka wa fedha uliopita walitumia Sh7 bilioni zikiwa kodi za wananchi.

Kwa nini tusitumie fedha hizo kuleta vifaa na wataalamu kutoka nje kwa lengo la kuimarisha hospitali zetu na wataalamu hao kutusaidia kujenga uwezo wa wafanyakazi katika hospitali zetu na sekta ya afya kwa jumla? Lengo la kuweka sheria ya mafao ya viongozi ilikuwa njema ili viongozi wetu wasiishi maisha ya mashaka baada ya kustaafu.

Bahati mbaya hakuna aliyejua kwamba baada ya kuzikwa kwa Azimio la Arusha viongozi wetu wangetupilia mbali maadili ya uongozi na kuwa matajiri wakubwa, wengine wakifanya biashara na kuanzisha makampuni hata wakiwa bado katika ofisi za umma. Ndiyo maana tunalazimika kusema kuwa, huko tuendako tutalazimika kuangalia upya mafao ya viongozi, hasa suala hili la kutumia mabilioni ya fedha kila mwaka kwa matibabu ya kufikirika ya viongozi wetu.
 
hivi kwa mfano kwenye hizo bil 9 walizotengewa waki2mia bil 5 ,hizo bil 4 zinarudishwa?
 
hivi kwa mfano kwenye hizo bil 9 walizotengewa waki2mia bil 5 ,hizo bil 4 zinarudishwa?

Kwa ufisadi ulivyokithiri ndani ya Serikali sidhani kama zinarudishwa bali huwa zinaingia mifukoni mwa wajanja wachache. Wakiambiwa watoe details ni kiasi gani kilichotumika katika miaka mitano iliyopita na payment receipts husika za matibabu ya Mwinyi na Mkapa basi wataanza kung'aa macho.
 
Sumaye amesahaulika akawekwa Lowasa?Kumbe Lowasa ni Waziri Mkuu Mstaafu!!!
Hizo hela zitakuwa za kuwatibu wao,wake zao,watoto wao,ndugu zao mpaka na mifugo yao!!
Kweli mwenye shibe hamjui mwenye njaa!!!
 
Kiukweli Tanzania mambo ni magumu na yanatia hasira mpaka basi. Uvumilivu utaja fika mwisho tuu!!!
 
Hii aibu halafu hakuna hata mmoja anayetibiwa ndani ya nchi

Ndio maana hawaoni umuhimu wa kuboresha sekta ya afya nchini maana wanajua watapelekwa nje kwa gharama za pesa za walipa kodi. Pesa za kuwalipia wao kutibiwa nje siku zote hazikosekani ila wakiulizwa pesa za kuboresha sekta ya afya nchini hawakawii kung'aka, "Serikali haina uwezo."
 
Huku wakipitia wale wakaguzi wa matumizi ya serıkali si itakuwa aibu tupu.
 
kweli tanzania italiwa na wenye meno, Drs wana watete wananchi sababu wanajua madudu haya, watu wanawaona wasaliti, haya siku moja mtawakmbuka.
 
Naona kama wizi au kulipana fadhili. Lowassa anaingiaje wakati hakustaafu? Walaji wastaafu au?
 
Pamoja na gharama hizi za matibabu hawa viongozi wastaafu huwa wanabadilishiwa gari kila mwaka. Pia wanalipiwa dreva, gardener, mpishi na walinzi na pesa za chakula. Kwa kifupi ni kwamba wanatunzwa na pesa za walipa kodi kwa asilimia 100 mpaka watakapoondoka hapa duniani. Cha kushangaza ni kuwa pamoja na hayo yote jamaa hawaridhiki na wanaiba na kuiuza nchi. Hii nafikiri ni laana isiyo na mfano.
 
hivi kwa mfano kwenye hizo bil 9 walizotengewa waki2mia bil 5 ,hizo bil 4 zinarudishwa?

Kujibu swali lako, hazibaki, na kila mwaka inabidi ziongezwe kwani hazitoshi, hasa ifikapo mwezi wa Ogasti.
 
Gharama za matibabu ya viongozi wastaafu ni kufuru
Thursday, 05 July 2012 20:39
Mwananchi

Bunge linaloendelea na kikao chake mjini Dodoma, juzi liliambiwa kwamba Serikali imetenga Sh9 bilioni kwa ajili ya kugharamia matibabu ya viongozi wakuu wastaafu. Akihitimisha mjadala wa hotuba yake, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais anayeshughulikia Menejimenti na Utumishi wa Umma, Celina Kombani alisema fedha hizo ni kwa ajili ya wastaafu wanaopaswa kutunzwa na Serikali.

Bila kuelezea suala hilo kwa undani, Waziri Kombani alisema tu kwamba kiwango hicho kimepungua mwaka huu kutoka Sh10 bilioni zilizotengwa mwaka jana hadi Sh9 bilioni mwaka huu kutokana na idadi ya viongozi wastaafu wanaopaswa kuhudumiwa na Serikali kupungua. Wastaafu wanaoangukia katika fungu hilo ni marais Ali Hassan Mwinyi na Benjamin Mkapa.

Mawaziri wakuu wastaafu ni Joseph Warioba, Samuel Malecela, Cleopa Msuya, Salim Ahmed Salim na Edward Lowasa. Waziri Kombani hakuwataja viongozi wastaafu waliopungua, lakini sote tunafahamu fika kwamba Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere na Mzee Rashid Mfaume Kawawa tayari wametangulia mbele ya haki.

Bila shaka takwimu hizo zitakuwa zimewashangaza wengi kutokana na wingi wa fedha zinazotengwa kila mwaka kugharamia tu matibabu ya viongozi, bila kutilia maanani fedha nyingine nyingi zinazotengwa kama mafao ya viongozi hao wastaafu. Kwa akili ya kawaida, fedha hizo ni nyingi mno kulinganisha na idadi ya viongozi waliokusudiwa na takwimu hizo zinaacha maswali mengi kuliko majibu.

Tunasema hivyo kwa sababu hatuoni jinsi kiasi hicho kikubwa cha fedha kinaweza kugharamia matibabu ya idadi ndogo sana ya viongozi wetu wastaafu, kwani siyo siri pia kwamba wastaafu wetu wengi wamekuwa wakipatwa na maradhi ya kawaida ambayo siyo tu hayahitaji fedha nyingi kuyatibu, bali pia yangeweza kupata tiba hapa nchini. Ndiyo maana tunasema vifungu vikubwa vya fedha zinazotengwa kila mwaka kwa shughuli hiyo siyo tu vinatia shaka, bali pia vinaacha ukungu na kiza kinene vikiwa vimetanda.

Sisi hatusemi kwamba viongozi wetu hao wastaafu hawastahili kupata matibabu kwa kodi zetu. Tunachosema hapa ni kwamba gharama za matibabu yao hazipaswi kuwa siri au kuacha shaka hata kama wastaafu hao walitutumikia vizuri wakati wa utawala wao. Ni sahihi kabisa kwamba walipakodi wangetaka kujua kodi zao zinavyotumika kuwagharimia viongozi wao.

Bado tunasisitiza kwamba Sh9 bilioni kwa matibabu ya viongozi hao wastaafu siyo tu ni nyingi mno, bali pia ni kufuru na za kufikirika. Takwimu hizo hazijumliki hata kidogo. Ni matibabu yapi yenye gharama hata robo ya kiasi hicho kilichotengwa, hata ukiweka usafiri, malazi na gharama nyingine? Ni kichekesho kwamba fedha hizo zimepitishwa na Bunge.

Kinachosikitisha ni Bunge kutohoji fedha zote hizo zinakwenda wapi. Bunge lisiloona umuhimu wa kuibana Serikali iboreshe mazingira na huduma katika hospitali zetu ili viongozi na wananchi watibiwe katika hospitali hizo badala ya kupeleka fedha zetu nje na kujenga uchumi wa nchi nyingine. Ebu fikiria hili: Mwaka uliopita, wagonjwa waliopelekwa India kutibiwa mwaka wa fedha uliopita walitumia Sh7 bilioni zikiwa kodi za wananchi.

Kwa nini tusitumie fedha hizo kuleta vifaa na wataalamu kutoka nje kwa lengo la kuimarisha hospitali zetu na wataalamu hao kutusaidia kujenga uwezo wa wafanyakazi katika hospitali zetu na sekta ya afya kwa jumla? Lengo la kuweka sheria ya mafao ya viongozi ilikuwa njema ili viongozi wetu wasiishi maisha ya mashaka baada ya kustaafu.

Bahati mbaya hakuna aliyejua kwamba baada ya kuzikwa kwa Azimio la Arusha viongozi wetu wangetupilia mbali maadili ya uongozi na kuwa matajiri wakubwa, wengine wakifanya biashara na kuanzisha makampuni hata wakiwa bado katika ofisi za umma. Ndiyo maana tunalazimika kusema kuwa, huko tuendako tutalazimika kuangalia upya mafao ya viongozi, hasa suala hili la kutumia mabilioni ya fedha kila mwaka kwa matibabu ya kufikirika ya viongozi wetu.

OH Yeah Sikujua kuwa FREDRICK SUMAYE hakuwa Waziri Mkuu kwa Miaka 10 alikuwa nani then?

Hizi Habari zetu zinaandikwa bila kufuatilia zinaondoa umaridadi wa kuzisoma kweli; too many

mistakes
 
Majenerali wa jeshi wastaafu wote wanatibiwa nje, ni marehemu kyaro alikataa akabaki bugando hadi kifo chake.
 
[h=2]kikwete ni mnafiki no 1[/h]
Tangu tupate maraisi hatujawahi kuwa na rais mnafiki, mzembe,dhaifu na ndumila kuwili kama kikwete uendeshaji serikali yake umejaa fitina dhihaka na upuuzi mwingi anyemshabikia huyu naomba aweke haya maelezo kwa kuprint au kucopy na baa ya 2015 mtaona kwa nini tz imefika hapa ilipo ni sababu ya huyu mr dhaifu hakuna alichowahi kuongoza kikafanikiwa zaidi ya kutengeneza makundi ndani ya chama na nchini ili awe madarakani kirahisi mungu ibariki tanzania kwa haraka sana tuondokane na huyu mnafiki
 
Yaani matibabu tu kila mtu ana wastani kama wa bilioni moja na usheeeee! Ndo maana kila mtu anataka awe rais ndani ya magamba wanajua utaishi kama malkia wa nyuki pindi madaraka yakiisha, hapo mbali na mali za kifisadi ambazo tayari wanazo, aiseeeee!
 
ndio maana kuepusha haya matatizo ndio maana kwa wenzetu huko Marekani Rais analipwa mafao kwa miaka 10 baada ya kustaafu na baada ya hapo anaweza kuongezewa miaka 5 kwa executive order ya sitting president. Hii ni kuzuia mtu kutumikia urais kwa miaka 8 halafu alipwe mafao miaka 20! Hivyo ukiamua kugombea Urais ukiwa na umri mdogo ni juu yako. Mfano mwaka jana nakumbuka Rais Carter aliibiwa baiskeli yake alipoenda dukani kwa vile kwa sasa hana ulinzi wa aina yeyote ingawa FBi wanaendela kumfuatilia kwa extra security lakini sio kama huku kwetu.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Back
Top Bottom