BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,789
- 288,011
Gharama za kuhifadhi makontena bandarini zapanda
Mwandishi Wetu
Daily News; Thursday,January 01, 2009 @20:00
MAMLAKA ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) imeongeza gharama ya kuhifadhi makontena bandarini kwa asilimia 100 kuanzia jana. Vilevile TPA imetangaza kwamba itapiga mnada makontena yaliyokaa kwa muda mrefu bandarini bila ya kuchukuliwa na wahusika.
Ofisa Mawasiliano Mwandamizi wa Bandari, Peter Milanzi alitoa taarifa hiyo wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Dar es Salaam jana. Milanzi alisema hatua hiyo imefikiwa baada ya wateja kutochukua makontena kwa wakati na kusababisha msongamano wa meli nje ya mlango wa bandari.
"Kuanzia leo Januari mosi (jana) gharama ya kuhifadhi makontena bandarini imeongezeka na kwamba kontena litakalokaa bandarini baada ya siku 21, gharama yake itakuwa dola za Marekani 40 (zaidi ya Sh 51,000) kwa kontena la futi 20 na dola 80 kwa kontena la futi 40, alisema Milanzi.
Aidha, alisema makontena yote yaliyokaa kwa muda mrefu bandarini zaidi ya siku 21 kama hayatachukuliwa ifikapo Januari 15 mwaka huu, yatakabidhiwa kwa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kwa ajili ya kupigwa mnada. Milanzi alisema upigaji mnada makontena hayo utafanyika kwa haraka na hatua hiyo itakuwa endelevu.
Aliwataka wateja kwenda kuyaondoa makontena hayo haraka kabla ya kazi hiyo kuanza. Alisema TPA pamoja na wadau wake wataendelea kufanya kazi kwa saa 24 kila siku ili kuwezesha wateja wao kuchukua mizigo muda wote wanapotaka kufanya hivyo.
Hata hivyo, aliwataka wateja kutambua kuwa bandari ni mlango wa biashara na siyo sehemu ya kuhifadhia mizigo. Alisisitiza kwamba wateja wanatakiwa kuheshimu taratibu kwa kufuata muda unaofaa kuchukua mizigo yao.
Kwa mujibu wa ofisa huyo, awali makontena ya wateja wa ndani ya nchi kuanzia siku moja hadi siku saba, yalikuwa yakihifadhiwa bure, na kuanzia siku ya nane hadi 30, kontena la futi 20 lilikuwa likitozwa dola za Marekani 20 kwa siku na la futi 40 lilikuwa likitozwa dola 40 kwa siku.
Hata hivyo, alisema kuanzia siku ya 30 hadi kontena linapotolewa na mhusika, kontena la futi 20 lilikuwa likitozwa dola za Marekani 27 kila siku na la futi 40 lilikuwa likitozwa dola za Marekani 54 kwa siku.
Kwa makontena ya nje ya nchi yanayotumia bandari ya Dar es Salaam, awali yalikuwa yanahifadhiwa bure kwa siku 15 tangu siku ya kwanza. Kuanzia siku ya 16, kwa siku 30 baada ya hapo, kontena la futi 20 lilikuwa likitozwa dola za Marekani 20 kwa siku na la futi 40 lilikuwa likitozwa dola 40 kwa siku.
Hata hivyo, alisema kuanzia hapo baada ya kipindi cha siku 30 kwa makontena ya nje ya futi 20, yalikuwa yakitozwa dola za Marekani 27 kila siku na dola 54 kwa kontena la futi 40 kila siku
Mwandishi Wetu
Daily News; Thursday,January 01, 2009 @20:00
MAMLAKA ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) imeongeza gharama ya kuhifadhi makontena bandarini kwa asilimia 100 kuanzia jana. Vilevile TPA imetangaza kwamba itapiga mnada makontena yaliyokaa kwa muda mrefu bandarini bila ya kuchukuliwa na wahusika.
Ofisa Mawasiliano Mwandamizi wa Bandari, Peter Milanzi alitoa taarifa hiyo wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Dar es Salaam jana. Milanzi alisema hatua hiyo imefikiwa baada ya wateja kutochukua makontena kwa wakati na kusababisha msongamano wa meli nje ya mlango wa bandari.
"Kuanzia leo Januari mosi (jana) gharama ya kuhifadhi makontena bandarini imeongezeka na kwamba kontena litakalokaa bandarini baada ya siku 21, gharama yake itakuwa dola za Marekani 40 (zaidi ya Sh 51,000) kwa kontena la futi 20 na dola 80 kwa kontena la futi 40, alisema Milanzi.
Aidha, alisema makontena yote yaliyokaa kwa muda mrefu bandarini zaidi ya siku 21 kama hayatachukuliwa ifikapo Januari 15 mwaka huu, yatakabidhiwa kwa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kwa ajili ya kupigwa mnada. Milanzi alisema upigaji mnada makontena hayo utafanyika kwa haraka na hatua hiyo itakuwa endelevu.
Aliwataka wateja kwenda kuyaondoa makontena hayo haraka kabla ya kazi hiyo kuanza. Alisema TPA pamoja na wadau wake wataendelea kufanya kazi kwa saa 24 kila siku ili kuwezesha wateja wao kuchukua mizigo muda wote wanapotaka kufanya hivyo.
Hata hivyo, aliwataka wateja kutambua kuwa bandari ni mlango wa biashara na siyo sehemu ya kuhifadhia mizigo. Alisisitiza kwamba wateja wanatakiwa kuheshimu taratibu kwa kufuata muda unaofaa kuchukua mizigo yao.
Kwa mujibu wa ofisa huyo, awali makontena ya wateja wa ndani ya nchi kuanzia siku moja hadi siku saba, yalikuwa yakihifadhiwa bure, na kuanzia siku ya nane hadi 30, kontena la futi 20 lilikuwa likitozwa dola za Marekani 20 kwa siku na la futi 40 lilikuwa likitozwa dola 40 kwa siku.
Hata hivyo, alisema kuanzia siku ya 30 hadi kontena linapotolewa na mhusika, kontena la futi 20 lilikuwa likitozwa dola za Marekani 27 kila siku na la futi 40 lilikuwa likitozwa dola za Marekani 54 kwa siku.
Kwa makontena ya nje ya nchi yanayotumia bandari ya Dar es Salaam, awali yalikuwa yanahifadhiwa bure kwa siku 15 tangu siku ya kwanza. Kuanzia siku ya 16, kwa siku 30 baada ya hapo, kontena la futi 20 lilikuwa likitozwa dola za Marekani 20 kwa siku na la futi 40 lilikuwa likitozwa dola 40 kwa siku.
Hata hivyo, alisema kuanzia hapo baada ya kipindi cha siku 30 kwa makontena ya nje ya futi 20, yalikuwa yakitozwa dola za Marekani 27 kila siku na dola 54 kwa kontena la futi 40 kila siku