Roughly sh. laki sita inatosha.
Laki 6? Hapa kuna vitu viwili. Kwanza kufanya wiring, pili kuingiza umeme. Kuhusu wiring bei inategemea material unayotumia (quality ya nyaya), quality ya fundi, main switch, sockets etc. Kwa mfano switch za taa zipo za tsh 2000, 3500 na 6000. Nyaya ndo zinatofuti kibwa sana ya bei. Nafikiri budget ya 1.5m ni ideal.
Kuingiza umeme inategemea pia nguzo ngapi. Kama ni nguzo moja ni Tsh 1.4m. ongeza laki 7 kwa kila nguzo inayoongezeka. Punguzo lililotangazwa bungeni halijaanza kutumika hado Jan
Labda nieleweshe zaidi.Nyumba ni vyumba vitatu vya kulala dining sitting room na choo size wastani.
Kuna kuweka wiring pamoja na kuvuta umeme.Umeme upo si zaidi ya mita 15, yaani upo kwa jirani next ya nyumba yangu.je nitahitaji nguzo?breakdown ya gharama za kuvuta umeme na Kuweka wiring kwenye nyumba ndio natafuta.
Ahsanteni kwa wale walionipa majibu ya awali.