Ntemi Kazwile
JF-Expert Member
- May 14, 2010
- 2,182
- 307
Leo ni takribani wiki mbili sasa tangu wanafunzi zaidi ya 1,000 wa kitivo cha taaluma ya habari na mawasiliano cha UDOM wafukuzwe chuoni kutokana na sababu za kitoto...
Kitivo hiki ni miongoni mwa vitivo ambavyo wanafunzi wake wanasomeshwa bure (hawakopeshwi) na ni moja wapo ya matarajio tuliyonayo kama taifa kutuwezesha kushiriki kwenye kijiji cha ulimwengu katika kipindi hiki cha teknolojia ya mawasiliano na habari, ajabu ni kwamba kwa uzembe wa watu wachache ambao wanaamini kuwa maamuzi yao kamwe hayatakiwi kuhojiwa na kupingwa wamesababisha wataalamu wetu hawa watarajiwa wafukuzwe na serikali iendelee kuingia gharama kubwa ya kulipa watumishi ambao hawafanyi kazi. Taasisi kama UDOM naamini inaajiri watu wengi wanaolipwa pesa nyingi, achilia mbali gharama zingine za uendeshaji kama umeme, maji,muda unaopotea kwa wanafunzi hawa, n.k.
Ifike wakati sasa tukatae kuingizwa kwenye gharama zisizostahili kama hizi na watu wachache wanaodhani ni miungu watu, ifike wakati wazazi tupinge kwa nguvu zetu zote watoto wetu kunyanyaswa na kunyimwa haki zao za msingi kama watanzania. Tusiwaruhusu watendaji wasiowajibika kutuingiza kwenye hasara kama ilivyotokea kwenye mikataba feki na ya kifisadi ambayo wametuingiza na bado wanakula kuku kwa mrija.... INATOSHA!
Kitivo hiki ni miongoni mwa vitivo ambavyo wanafunzi wake wanasomeshwa bure (hawakopeshwi) na ni moja wapo ya matarajio tuliyonayo kama taifa kutuwezesha kushiriki kwenye kijiji cha ulimwengu katika kipindi hiki cha teknolojia ya mawasiliano na habari, ajabu ni kwamba kwa uzembe wa watu wachache ambao wanaamini kuwa maamuzi yao kamwe hayatakiwi kuhojiwa na kupingwa wamesababisha wataalamu wetu hawa watarajiwa wafukuzwe na serikali iendelee kuingia gharama kubwa ya kulipa watumishi ambao hawafanyi kazi. Taasisi kama UDOM naamini inaajiri watu wengi wanaolipwa pesa nyingi, achilia mbali gharama zingine za uendeshaji kama umeme, maji,muda unaopotea kwa wanafunzi hawa, n.k.
Ifike wakati sasa tukatae kuingizwa kwenye gharama zisizostahili kama hizi na watu wachache wanaodhani ni miungu watu, ifike wakati wazazi tupinge kwa nguvu zetu zote watoto wetu kunyanyaswa na kunyimwa haki zao za msingi kama watanzania. Tusiwaruhusu watendaji wasiowajibika kutuingiza kwenye hasara kama ilivyotokea kwenye mikataba feki na ya kifisadi ambayo wametuingiza na bado wanakula kuku kwa mrija.... INATOSHA!