moto ya mbongo
JF-Expert Member
- Sep 9, 2009
- 476
- 326
GERALD HANDO ANATUMIA VIBAYA NAFASI YAKE YA UTANGAZAJI WA KIPINDI CHA POWER BREAKFAST CHA CLOUDS FM:
Katika kumsikiliza Gerald Hando jana 03/JULAI/2012 na leo 04/JULAI/2012 katika segment yao ya JICHO LA NG'OMBE saa 12:55 asubuhi mtangazaji huyu anaonesha kabisa anaeneza propaganda na anatumika kusafisha njia kwa manufaa ya wachache badala ya kutumia nafasi ya chombo cha habari kwa manufaa ya umma.
Jana akizungumzia ishu ya jaribio la kumuua Dr. Stephen Ulimboka alijaribu kuhamisha muelekeo wa jinsi jambo lilivyo kwa kusema kuwa kuchukuliwa kwake (Dr) na kwenda kupigwa kule alikopelekwa msitu wa Pande kuna watu wengine au madaktari wengine walikuwepo kwa hiyo lawama isielekezwe kwa serikali.Jambo hili linahiataji uchunguzi huru ili kuupata ukweli halisi wa jambo hili.
Leo pia katika jicho la ng'ombe ameongea kwa vijembe kuwa katika bunge la bajeti wabunge hawazungumzii masuala ya bajeti na badala yake wanaingiza hoja za kibinafsi(personal) akitolea mfano kuwa mamabo ya mitaani kama kufumaniwa mwishoe yataongelewa bungeni.Jambo hili limeniacha na mshangao mkubwa kwani siku ya jana Bungeni Mbunge wa Ubungo kupitia CHADEMA Mheshimiwa John Mnyika alimtaja Mbunge wa Iramba Magharibi kupitia CCM Mheshimiwa Mwigulu Nchemba kuwa alihusika katika wizi wa EPA wa bilioni 133.Nchemba alikanusha na Mnyika amepewa siku 7 za kuthibitisha kauli yake hiyo.
Kitu kinachostaajabisha kwa hawa jamaa akina Gerald Hando na wanaowatumia ni kupinga kitu kama hicho kwa sababu dhaifu eti si muda muafaka kuzungumzia mambo kama hayo napenda kuwauliza wao na wadau wote mnaoisoma thread hii je wananchi wa Tanzania waliobiwa na mafisadi kwa miaka mingi na kudanganywa kuwa masuala hayo ni ishu za usalama wa taifa watatetewa na nani?????Je kuna muda gani muafaka wa kuzungumzia iwapo mambo hayo yameshughulikiwa kwa udhaifu mkubwa na miaka inazidi kuyoyoma jamaa wakiendelea kuzalisha faida na kuficha mapesa katika akaunti za siri ng'ambo?
Baada ya kampuni ya ukaguzi wa mahesabu ya Delloite & Touche kugundua mwaka ule wanasiasa kwa kushirikiana wafanyabiashara na mabenki ya hapa nchini kupitia benki kuu waliiba mabilioni ya pesa katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA).
Kampuni ile ilizuiwa kuendelea na kazi na mambo yalipokuwa moto serikali iliunda tume ya watu watatu Ludovick Utouh Mkaguzi Mkuu wa Mahesabu wa Serikali ,Saidi Mwema Mkuu wa Jeshi la Polisi na mwendesha mashtaka wa serikali Johnson Mwanyika aliyestaafu kwa sasa.
Jambo lilelifanywa katika kununua muda(buying time)ili wananchi wasahau na watulie ili mambo yao yaende vizuri.
Matokeo yake wachache walitolewa mhanga kama akina Rajabu Maranda na Farijala Hussein wakati wale wengine waliambiwa warudishe wengine waasia,mtanzania mwenye asili ya Irani na jamaa zake,wanasheria na wazawa wengine waliachiwa wale keki ya taifa dhidi ya wanyonge wengi wa Tanzania.
Kukafuatia kauli za mara mafisadi hawakamatiki ni wajanja sana.Nyaraka za usajili wa makampuni yale bandia zilipotea kule BRELA na mabenki kama CRDB,Akiba Commercial Bank yaliyotoa pesa zile hayajatoa majina na ni akina nani walichukua pesa zile usanii uliendeshwa hapo hakuna cha maana kilichopatikana ili kusaidia wananchi na nchi yetu.
Kitu hiki wananchi wengi wanaosikiliza radio hii ya Clouds FM na wenye upeo mdogo wanaona Hando kusema kitu kama hiki ni sawa tu bila kujua kuwa kuna wachache wanaofaidi nchi tena kwa njia haramu na kwa kukandamiza wananchi walio wengi.
WATANZANIA TUAMKE ILI TUKOMBOKE TUKIRUHUSU WANYONYAJI WEUSI WENZETU KUTUIBIA UTAJIRI WA NCHI NA MEDIA ZINAZOSET AGENDA PIA KUTUMIKA KUTUDANGANYA TUTAISHIA PABAYA.
TAFAKARI.
Katika kumsikiliza Gerald Hando jana 03/JULAI/2012 na leo 04/JULAI/2012 katika segment yao ya JICHO LA NG'OMBE saa 12:55 asubuhi mtangazaji huyu anaonesha kabisa anaeneza propaganda na anatumika kusafisha njia kwa manufaa ya wachache badala ya kutumia nafasi ya chombo cha habari kwa manufaa ya umma.
Jana akizungumzia ishu ya jaribio la kumuua Dr. Stephen Ulimboka alijaribu kuhamisha muelekeo wa jinsi jambo lilivyo kwa kusema kuwa kuchukuliwa kwake (Dr) na kwenda kupigwa kule alikopelekwa msitu wa Pande kuna watu wengine au madaktari wengine walikuwepo kwa hiyo lawama isielekezwe kwa serikali.Jambo hili linahiataji uchunguzi huru ili kuupata ukweli halisi wa jambo hili.
Leo pia katika jicho la ng'ombe ameongea kwa vijembe kuwa katika bunge la bajeti wabunge hawazungumzii masuala ya bajeti na badala yake wanaingiza hoja za kibinafsi(personal) akitolea mfano kuwa mamabo ya mitaani kama kufumaniwa mwishoe yataongelewa bungeni.Jambo hili limeniacha na mshangao mkubwa kwani siku ya jana Bungeni Mbunge wa Ubungo kupitia CHADEMA Mheshimiwa John Mnyika alimtaja Mbunge wa Iramba Magharibi kupitia CCM Mheshimiwa Mwigulu Nchemba kuwa alihusika katika wizi wa EPA wa bilioni 133.Nchemba alikanusha na Mnyika amepewa siku 7 za kuthibitisha kauli yake hiyo.
Kitu kinachostaajabisha kwa hawa jamaa akina Gerald Hando na wanaowatumia ni kupinga kitu kama hicho kwa sababu dhaifu eti si muda muafaka kuzungumzia mambo kama hayo napenda kuwauliza wao na wadau wote mnaoisoma thread hii je wananchi wa Tanzania waliobiwa na mafisadi kwa miaka mingi na kudanganywa kuwa masuala hayo ni ishu za usalama wa taifa watatetewa na nani?????Je kuna muda gani muafaka wa kuzungumzia iwapo mambo hayo yameshughulikiwa kwa udhaifu mkubwa na miaka inazidi kuyoyoma jamaa wakiendelea kuzalisha faida na kuficha mapesa katika akaunti za siri ng'ambo?
Baada ya kampuni ya ukaguzi wa mahesabu ya Delloite & Touche kugundua mwaka ule wanasiasa kwa kushirikiana wafanyabiashara na mabenki ya hapa nchini kupitia benki kuu waliiba mabilioni ya pesa katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA).
Kampuni ile ilizuiwa kuendelea na kazi na mambo yalipokuwa moto serikali iliunda tume ya watu watatu Ludovick Utouh Mkaguzi Mkuu wa Mahesabu wa Serikali ,Saidi Mwema Mkuu wa Jeshi la Polisi na mwendesha mashtaka wa serikali Johnson Mwanyika aliyestaafu kwa sasa.
Jambo lilelifanywa katika kununua muda(buying time)ili wananchi wasahau na watulie ili mambo yao yaende vizuri.
Matokeo yake wachache walitolewa mhanga kama akina Rajabu Maranda na Farijala Hussein wakati wale wengine waliambiwa warudishe wengine waasia,mtanzania mwenye asili ya Irani na jamaa zake,wanasheria na wazawa wengine waliachiwa wale keki ya taifa dhidi ya wanyonge wengi wa Tanzania.
Kukafuatia kauli za mara mafisadi hawakamatiki ni wajanja sana.Nyaraka za usajili wa makampuni yale bandia zilipotea kule BRELA na mabenki kama CRDB,Akiba Commercial Bank yaliyotoa pesa zile hayajatoa majina na ni akina nani walichukua pesa zile usanii uliendeshwa hapo hakuna cha maana kilichopatikana ili kusaidia wananchi na nchi yetu.
Kitu hiki wananchi wengi wanaosikiliza radio hii ya Clouds FM na wenye upeo mdogo wanaona Hando kusema kitu kama hiki ni sawa tu bila kujua kuwa kuna wachache wanaofaidi nchi tena kwa njia haramu na kwa kukandamiza wananchi walio wengi.
WATANZANIA TUAMKE ILI TUKOMBOKE TUKIRUHUSU WANYONYAJI WEUSI WENZETU KUTUIBIA UTAJIRI WA NCHI NA MEDIA ZINAZOSET AGENDA PIA KUTUMIKA KUTUDANGANYA TUTAISHIA PABAYA.
TAFAKARI.