Huu msigano wa wanamtandao itakuwa neema kwa watanzania kama rais atakuwa na ujasiri wa kuwatosa. Vinginevyo itakuwa balaa kwa taifa. Lowasa alipokwenda kwao alipokelewa kama shujaa. Jana Chenge si tu kapokelewa kama shujaa, lakini alipata ujasiri wa kusema kuwa mnyantuzu hawezi kunywa sumu afe na kuacha vijisenti vyake. Nashindwa kuamini kuwa ujasiri wao hautokani na ukweli, kama ilivyoandikwa na mwanahalisi, kuwa mambo haya ya ufisadi waliyafanya pamoja au alijua kuwa waliyafanya na yalimnufaisha. Mwalimu alikuwa rafiki mkubwa wa Kambona lakini walipo part njia ilibidi Kambona akimbie nchi. Nashindwa ku imagine kuwa Kambona angekwenda kwao Manda na kutamba mbele ya wananchi. Call it dictatorship or anything.