General Tyre: Is it a slow death to a once an East Africa Giant??

Wizara ya fedha inaendelea kumlipa mshahara wa tsh 30 milion kwa mwezi meneja kuu wa General Tyre bwana Devendra Lohani ambaye amegoma kurudi Tanzania kwa kuhofia kukamatwa na kuhojiwa na vyombo vya dola kwa kuifilisi General Tyre.

Bwana Devendra Lohani aliletwa nchi na Continetal ya Ujerumani ambao pia waliwajibika kumlipa mshahara laikini Continental ujerumani walimfukuza kazi Devendra Lohani mara baada ya kubaini uendeshaji mbovu mwaka 2007. Mwenyekiti wa bodi na wajumbe wote wa bodi waliamua kumwajiri bwana Devendra kinyume na ushauri wa Continental ujerumani waliotaka mtanzania mzawa aajiriwe ili kupunguza gharama kubwa za kumwajiri mgeni. Uamuzi wa bodi kumwajiri bwana Devendra Lohani umeendelea kuliletea taifa hasara kubwa kwasababu mpaka sasa wizara ya fedha imeshamlipa tsh360,000,000/= bila kufanyakazi pia ikumbukwe bwana Devendra ni muhusika mkuu kwenye sakata la kuifilisi General Tyre.

Bwana Devendra Lohani kwa sasa ameajiriwa na kiwanda cha kutengeneza matairi India Appolo. Appolo ya India nao walihusika sana kuhijumu General tyre kwa kuchukua kinyemela specification za utengenezaji wa Tubes baada ya uzalishaji wa tubes kusimamishwa kuzalishwa.

Hizi ni tuhuma kubwa Ngogo. Ni vema ukaanika data hapa JF si wajua Wakulu huchota evidences hapa? Kama ni kweli basi naamini huo mshahara unagawanywa kwa wajumbe wa Bodi ya Genaral Tyre na Wizara ya Fedha maana mwenye akili timamu hawezi kufanya hivyo.

Hata hivyo uwezekano huo upo si imeandikwa RUSHWA HUPOFUSHA MACHO!
 
Hizi ni tuhuma kubwa Ngogo. Ni vema ukaanika data hapa JF si wajua Wakulu huchota evidences hapa? Kama ni kweli basi naamini huo mshahara unagawanywa kwa wajumbe wa Bodi ya Genaral Tyre na Wizara ya Fedha maana mwenye akili timamu hawezi kufanya hivyo.

Hata hivyo uwezekano huo upo si imeandikwa RUSHWA HUPOFUSHA MACHO!

Mkuu Ibrah,

Kwanza hatukujua kwamba Bwana Devendra Lohani katemwa na mwajiri wake Continental, ni muda si mrefu tulifanikiwa kuiona email kutoka kwa Business Manager Ujerumani kwenda kwa mwenyekiti wa bodi Mheshimiwa Shelukindo na nakala kwa CEO kumjulisha jamaa si mwajiriwa tena wa Continental na wanashangaa ni kwanini bado yuko Tanzania. (NB email ya mwaka 2007 Juni)

Baada ya kuisoma email na kutafakari kwa kina tukaanza kujiuliza Bwana Devendra alikuwa anaishije hapa Tanzania tangu mwaka 2007 bila salary? Tunajua kweli huyu jamaa alikuwa mwizi lakini wakati tunahangaika tulibahatika kuona mkataba kati yake na bodi tena umekuwa signed na mwenyekiti na mjumbe anaitwa Ndunguru.

Wizara ya fedha inawalipa wafanyakazi wote wa General Tyre wanaostahili, wastaafu, waliokufa, walioajiriwa sehemu nyingine through bank A/C kwa kifupi hakuna uhakiki unaofanyika. Kwakuwa Bwana Devendra Lohani anao mkataba ulioridhiwa na bodi ya mheshimiwa William Shelukindo wizara ya fedha imekuwa ikimlipa kama wanavyofanya kwa wafanyakazi wengine.

Mambo haya yamewezekana kwasababu bodi na manager mkuu Bwana Devendra Lohani walikuwa wanafanya mambo yao kwa siri. Ni bahati nzuri sasa mambo mengi yanaanza kuvuja baada ya baadhi ya wapambe wa manager mkuu kuanza kubaini wameingizwa mjini / wameachwa kwenye mataa.

Mkuu Ibrah, wakubwa walishaanza mchakato wa kuinunua General Tyre kwa bei poa hivyo waliandaa utaratibu wa kukichukua kiwanda bila kelele. Walimwandaa Bwana Devendra kufanikisha malengo yao hii ni pamoja na kumpatia mshahara mzuri. Mabadiliko ya baraza la mawaziri yalichangia kwa kiasi kikubwa mpango wote kuvurugika.

Bwana Hans mmliki wa kiwanda cha Fibre Board na kiwanda cha mbolea Minjingu tayari alishaanza mkakati wa kuinunua General Tyre kwa msaada wa wanasiasa waliotemwa kwa skendo za ufisadi.
 
Bwana Hans mmliki wa kiwanda cha Fibre Board na kiwanda cha mbolea Minjingu tayari alishaanza mkakati wa kuinunua General Tyre kwa msaada wa wanasiasa waliotemwa kwa skendo za ufisadi.
Hans? Huyu ni yule Singa wa Arusha? Wow, haya wale viongozi wa kuwekwa mifukoni na mafisadi toka India kazi wanayo mwaka huu!

Jamani nchi yetu imemalizwa na mafisadi, watoto na wajukuu wetu wataishia kutulaani kwa kuwaachia nchi "uchi"
 
Hans? Huyu ni yule Singa wa Arusha? Wow, haya wale viongozi wa kuwekwa mifukoni na mafisadi toka India kazi wanayo mwaka huu!

Jamani nchi yetu imemalizwa na mafisadi, watoto na wajukuu wetu wataishia kutulaani kwa kuwaachia nchi "uchi"
Mkuu Morani 75, heshima mbele.

Hans amekuwa akilitumia kundi la wanasiasa wezi tangu enzi za awamu ya pili kujipatia rasilimali za taifa kwa njia za kifisadi. Fibre Board sina hakika sana lakini nasika kiliuzwa tsh 400m tu halafu akauza eneo kubwa la kiwanda kwa tsh 500m.

Kiwanda cha Fibre Board kilikuwa kinatengeneza faida kubwa, waliokuwa wafanyakazi wa Fibre Board mpaka leo bado wanahangaika kudai mafao yao. Nina hakika hata Minjingu ikifuatiliwa lazima utakuta na madudu ya ufisadi.
 
Mkuu Ngongo, kwa vile tumeanza kufuatilia wale so-called makambale nadhani huu uchafu na upuuzi wote utasafishwa!!

Nina imani kubwa sana na Mhe JK kuwa pamoja na vihunzi na vizuizi vyote mbele yake, ataweza kufanya atleast 10% ya masafisho haya!!!

Mungu Ibariki Tanzania, Mungu tubariki waTanzania!!
 
Tanzania Investment Bank wamtimua kazi Bi Rose Soloka baada ya kupata habari za ufisadi alioufanya wakati akiwa financial manager General Tyre.

Napenda kuchukua nafasi hii kuipongeza TIB kwa uamuzi wa busara walioufanya. Binafsi nilichukua jukumu la kufuatilia ajira ya Rose Soloka TIB na kuhakikisha anaondolewa mara moja kazini.

Wakati umefika watanzania kuhakikisha hawa wezi wanaiba fedha kutoka shirika moja la umma hadi lingine hawafanikiwi kupata ajira sehemu nyingine.
 
Wakati umefika watanzania kuhakikisha hawa wezi wanaiba fedha kutoka shirika moja la umma hadi lingine hawafanikiwi kupata ajira sehemu nyingine.

Mkuu Kabonde, kwa kweli nisiposema kwamba umefanikisha kazi kubwa nitakuwa sikutendei haki. Kazi nzuri sana mkuu tukiangalia kwamba ulifanya mambo kiufanisi (rudia email yako uliyowapelekea TIB kwenye posti zako huko nyuma).

Ndugu zanguni wanajamvi, kuna mtu alisemaga humu ndani kwamba tunapiga makelele wakati mwenye nyumba amelala, hili la TIB linadhihirisha ukweli kwamba kama mwenye nyumba alikuwa amelala, usingizi umeanza kuisha!!

Sisi wanaJF tutaendelea kusema ukweli mpaka aibu na nafsi zao ziwasute na kutekeleza jema kwa waTanzania wote! Mungu Ibariki Tanzania, Mungu tubariki waTanzania!!
 
NDIVYO TULIVYO!..
Hii ndiyo ilikuwa hofu kubwa ya mwalimu, hata chini ya Ubepari tumeshindwa kuendesha miradi ya uzalishaji isipokuwa tumefanikiwa kuunda tabaka la Mafisadi...

Watanzania inabidi tuamke. hatuna wa kutetea, hatuna mjomba wa kutugombania kila mtu anatukamua, hata wale waliotakiwa wapiganie kulinda maslahi ya umma, ndio hao wa kwanza kuitafuna nchi.
 
Shelukindo mbunge wa Bumbuli siku hizi ndio anajifanya kuwa ni mmoja wa vinara wa kuwaumbua mafisadi lakini kumbe kwa kufanya hivyo anaficha madhambi yake lukuki aliyofanya kama Mwenyekiti wa kampuni ya General Tyre; huyu bwana akishirikiana na Mramba na CEO {NEPALESE} wameiba sana fedha za kampuni ; Mpaka Mramba akiwa waziri wa fedha alisitisha kampuni ya TAC ASSociates wasiende kufanya audit baada ya kugundulika kuwa $milloni 10 kampuni ilizopewa na serikali kununulia mali ghafi hazikutumika kwa shuhuli hiyo!!

Ni dhahili kuwa Mramba na Shelukindo ndio wauaji wakuu wa kampuni ya General Tyre!!
 
Duh, finaly naona wameanza kukiongelea.... sasa hii ni ishara ya kuwa na matumaini au pia ni njia nyingine ya kutafta pesa za kampeni ya 2010 manake kwa kweli Tz usanii ndio tija....

Serikali yaahidi kufufua General Tyre

Na John Ngunge

Serikali imesema kwamba itahakikisha kuona kiwanda cha kutengeneza magudurudumu cha General Tyre kilichoko Arusha kinafufuliwa haraka na kuwa soko la mpirara unaolimwa Tanzania.

Kauli hiyo ilitolewa bungeni jana na Waziri Viwanda, Biashara na Masoko, Dk. Mary Nagu, wakati akihitimisha hotuba ya makadirio ya wizara yake kwa mwaka 2009/10.

Alielekeza lawama kwa mwekezaji ambaye alisema ameshindwa ama hana nia ya kufufua kiwanda hicho.

Awali, kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda na Biashara, iliishangaa serikali kuendelea kulipa Sh. milioni 120 kila mwezi kwa wafanyakazi 318 wa kiwanda cha hicho ambao wako nyumbani baada ya kiwanda hicho kusitisha uzalishaji.

Akitoa maoni hayo kwa niaba ya mwenyekiti wake, Abdisalaam Issa Khatib, mjumbe wa kamati hiyo ambaye ni Mbunge wa Magomeni, Mohammed Chomboh, (CCM), alisema kila mwezi wafanyakazi hao wanalipwa kiasi hicho cha fedha bila kufanya kazi.

Pia alisema kuna mashine 79 zenye uwezo wa kufanya kazi, ambazo zimesimama kutokana na kufungwa kwa kiwanda hicho.

‘Serikali ikiwa na hisa asilimia 76, ni jambo la kusikitisha sana kuona kwamba rasilimali kama hii haina tija katika kuchangia pato la taifa na wakati huo huo ujuzi wa wafanyakazi ukitoweka," alisema.

Alisema kufungwa kwa kiwanda hicho kumekuwa chanzo cha wafanyakazi kujiona yatima, hawana baba wala mama na kwamba ili kunusuru teknolojia, mitambo na watalaam waliopo, kamati inaishauri serikali kuharakisha ufufuaji wa kiwanda hicho kwa maslahi ya nchi.

Kwa upande wake, Msemaji wa Kambi ya Upinzani bungeni kuhusu wizara hiyo, Lucy Owenya (Viti Maalum Chadema), aliitaka serikali kutoa maelezo ya kina kuhusu hatima ya kiwanda hicho, la sivyo, anatarajia kuleta hoja binafsi ili iundwe tume kuchunguza matatizo ya kiwanda hicho kuona kama kuna hujuma ama la.

"Kiwanda hiki kimezungumziwa katika bajeti zote lakini serikali imeziba masikio kwanini? Na je, tutaendelea kuagiza mpira kutoka Malasia na Brazil na kuacha mashamba yetu ya mpira yavunwe kwa ajili ya Big-G zinazotengenezwa Kenya mpaka lini?" alihoji.

CHANZO: NIPASHE, 29 July 2009
 
Heshima mbele wanajamvi.

SEREKALI YASITISHA AJIRA YA WATUMISHI 300 WA GENERAL TYRE LTD.

Serekali imetangaza rasmi kusitisha ajira za wafanyakazi wote zaidi ya 300 wa kilichokuwa kiwanda cha kutengeneza matairi [General Tyre ea ltd]kilichoko mkoani Arusha.

Tamko la kusitisha ajira za wafanyakazi wa General Tyre limetolewa na naibu katibu mkuu wa wizara ya viwanda ,biashara na masoko Dr Shabani Mjaka baada ya kukitembelea kiwanda hicho na kuzungumza na waliokuwa wafanyakazi wa GTEA.


Dr Mjaka alisema hatua ya serekali kukifunga kiwanda imetokana na kubaini ubadhirifu wa zaidi ya sh 10 bilioni ilizokuwa imezitoa kwaajili ya kukijengea uwezo wa kuzalisha.


Dr Mjaka alisema kuwa uongozi uliokuwepo madarakani ulidai kutumia kiasi cha sh 3.4 bilioni kununulia malighafi ambazo hata hivyo hazina vielelezo vya manunuzi na hazijulikani vilipo hadi sasa.


Kuhusu hatma ya mafao ya wafanyakazi, Dr Mjaka alisema serekali itahakikisha wanalipwa kabla ya tarehe 8 August mwaka huu.


Chanzo: Nipashe 01 August 2009.
 
Serikali kupitia naibu katibu mkuu wa wizara ya viwanda,biashara na masoko Dr Mjaka imebaini pasipo shaka kwamba uongozi umetafuna kiasi cha sh 3.4 bilioni kununua malighafi hewa.

Serikali hiyohiyo inakubali kuwalipa wafanyakazi [uongozi] waliokwapua fedha badala ya kuwapeleka mahakamani kwa kosa la kuiba na kulisababishia taifa hasara kubwa ikiwa ni pamoja na wafanyakazi zaidi ya 300 kukosa ajira.

Wanajamvi tulipiga kelele sana kuhusu ubadhirifu uliokuwa ukifanyika lakini kuanzia serikali ya Mheshimiwa Mkapa na hata hii ya Mheshimiwa Kikwete hawakuchukua hatua stahiki badala yake wanautangazia umma wameamua kufunga kiwanda mpaka atakapo patikana mwekezaji.

Mheshimiwa Kikwete wakati wa kampeni zake alituambia ataongeza ajira milioni 1 lakini ameshindwa kulinda ajira 325 alizozikuta.
 
Mfanyabiashara na mjasiliamali makini ni yule asiyechoka kufuatilia sera mbalimbali za serikali ili apange mambo yake ya kibiashara vizuri.

Mathalani, endapo program za nchi hii ingekuwa zinatekelezwa, basi bila shaka wafanyabiashara waagizao nafaka toka nje wangeanza kufanya uagizaji huo kwa umakini zaidi kuliko ilivyokuwa hapo kabla!

KILIMO KWANZA + BIG 7 (from BIG 4) ingekuwa ni alert tosha kabisa kwao!

Aidha, kwa upande mwingine, wafanyabiashara wanao-deal na pembejeo ingekuwa ni opportunity kwao ya kujipanga vizuri zaidi!! So, what about General Tyre?

Sio siri, nilikuwa sifahamu kabisa kwamba kiwanda hiki kishatangulia kuzimu zamani !!! Inakuwaje ktk mazingira kama ya sasa kiwanda kama hiki kishindwe kufanya kazi? Kama kiliweza kufanya kazi wakati ule wa magari kudumu kwenye namba za TZ kwa miaka na miaka (narrow market) ilikuwaje kikashindwa kudumu sasa ambapo mamia kwa mamia ya mitumba ya magari yanaagizwa (soko la matairi nalo linatanuka) kila mwezi?!

Tatizo nini wadau? Inauma sana!

Hivi kweli katika cars/vehicles flooding iliyopo nchini hivi sasa isingetosha kuifanya General Tyre kuwa among the biggest employer? Au kuna ufisadi uliofanyika katika kuwanufaisha waagiza matairi ya gari?! Matairi ya gari ni complementary goods, kila idadi ya magari inapoongezeka mahitaji ya matairi nayo huongezeka at least twice!

Sio siri, kushindwa kufanya kazi kwa General Tyre kunatakiwa kuangaliwe kwa jicho la pili!!
 
General Tyre imefuata mkondo wa viwanda vingine vyoote vya serikali, kama ambavyo imetokea kwa mashirika kibao ya umma.

Ufisadi upo saana, maana nasikia nchi ya Jirani hapa inayoanzia na herifi K wanazalisha matairi kwa kasi ya ajabu na kuna tetesi kwamba nchi hiyo ilifurahia sana kuchechemea, na hatimaye kufa kwa GT!
 
General Tyre imefuata mkondo wa viwanda vingine vyoote vya serikali, kama ambavyo imetokea kwa mashirika kibao ya umma.

Ufisadi upo saana, maana nasikia nchi ya Jirani hapa inayoanzia na herifi K wanazalisha matairi kwa kasi ya ajabu na kuna tetesi kwamba nchi hiyo ilifurahia sana kuchechemea, na hatimaye kufa kwa GT!

Any serious competitor lazima angefurahia upuuzi huu!! Kwa upuuzi huu unaoendelea nchini hata kama dunia nzima ikakumbwa na ukame wa miaka kadhaa huku tanzania tukiwa na mvua za kutosha, bado hatutaweza ku-trap such opportunity! Hakika inauma sana!!
 
Hapo ndio ujue upumbavu wa serikali yetu, ikiwa na mkono mahali inanyonya hadi kuua mtaji, ni jambo la kukiboresha na kuweka viwango vikubwa vya imports ili kuwezesha kiwanda hiki, isitoshe hadi used tires in best roads in abroad zinakuja kutumika kwa worse roads in tz, duh? Tunasubiri kuzikwa mi naona.

General Tyre wangeingia uwakala na woote, dunlop, westland, firestone, wrangler and the rest, lakini tuna uvivu saaana, tunataka kununua na kuuza basi, hii nchi nilishasema ni ya WAMACHINGA, no production, no manufacturing ni upupu mtupu ukitaka kuyafikiria ya nchi yetu.

Lakini ni viongozi wanapelekea hayo yote, why MATAIRI yashindwe kufanya biashara tz? Haingii akilini!!
 
Historia yake ni ngumu na nzito kidogo,kuna siri nyingi sana pale.

Naona mambo mengi sana yalifanywa na uongozi wa juu wa kiwanda hichi,serikali kwa kupitia kamati za bunge walishatembelea na wakajionea wenyewe hali ilivyokuwa, ila kitu kimoja ambacho hawakujua, ni kuwa yule MD alikuwa mjanja sana, kwani wafanyakazi walikuwa wanapewa msosi mchana na jioni na kila siku wanapelekwa na kurudishwa nyumbani na mshahara wanapata, hata kama kiwanda hakifanyi kazi, ndio maana hujawahi sikia wafanyakazi wakigoma seriously kwa muda wote mpaka kimefungwa.

Kwa upande mwingine uongozi wa nyuma kabisa ndio ulianzisha issue kwa kuuza mashamba, nyumba na kuweka madeni makubwa sana ambayo ndio yameigharimu general tyre mpaka sasa.
 
Kuna mada moja ilishachambuliwa hapa kwa undani sana ,ipo under international forum

Unaweza tuma link ya hiyo thread?

Me huwa najiuliza Watanzania ni watu wa aina gani? Sisi ni wajanja sana usoni, lakini kwenye ubongo ni wapuuzi watupu.
 
Katika mambo ambayo nilishajikatia tamaa nayo ni General Tyre,serikali iko kama haioni yanayoendelea,kuna kichaa mmoja alijisemea bora nchi iuzwe kila mtu apewe hela yake.Sa sijui tungeenda wapi lakini ingekua afadhali mi naona.
 
Back
Top Bottom