Nsaji Mpoki
JF-Expert Member
- Nov 5, 2007
- 396
- 65
Wakuu Mlekwa & Ngongo
Nakubaliana na hoja zenu za umoja ni nguvu.Lakini katika umoja huo, tukubaliane kuwa wakati mwingine tupanue wigo wa uchaguzi wa sera badala ya personalities au itikadi za vyama.Najua watz wengi wapenda demokrasia mna hamu sana ya kuona opposition inaongeza idadi ya viti bungeni.Mimi kwa upande wangu napenda tuwafundishe na kuwazoesha wapiga kura kuchagua ubora wa sera na mgombea.Naunga mkono CHADEMA wagombee, ili sera zao zitambulike kwa wapiga kura wa Tanzania hiyo ndio nafasi pekee ya kujitangaza.Ninachotaka kushauri hapa si vizuri,incase mgombea wao hauziki waanze kumkandia mgombea wa chama kingine cha upinzani.
Tofauti ya uchaguzi wa Tarime vyama vingine vya upinzani vilikuwa vinaonyesha kukipiga vita vya wazi CHADEMA.Hali hiyo isirudiwe,chama kishiriki kueleza sera na mikakati yake ya kuboresha na kutetea walipa kodi wa Taifa letu.
Mkuu Gembe, si kweli kuwa sisi watu wa Mbeya tuna ukabila.Nitakupa mfano wa madiwani wawili wa kyela na nitaonyesha mabano ya kata wanazowakilisha.Kuna Visky Mahenge ambaye ni mkinga(Kyela) na Mh.Chrissy ambaye ni mkulya(Ipinda).Vilevile kule mbozi wenyeji wa wilaya ni Wanyiha na Wanyamwanga, lakini Mwenyekiti wa Council ni mnyakyusa.Huyu marehemu Nyaulawa,alikuwa mkinga ambao kule Mbeya vijijini ni wachache na walio wengi ni Wasafwa na Wamalila(kabila la Mboma).Huu mkoa wa Mbeya sasa hivi una wahamiaji wengi kutoka sehemu mbalimbali ya nchi yetu na nchi jirani na wanaishi vizuri na kushiriki kwenye chaguzi mbalimbali za uongozi.Nakumbuka hata uchaguzi mkuu wa 2005,NCCR-Mageuzi walimsimamisha Temigunga Kisonga(mhehe) na alivutia wapiga kura wengi licha ya kwamba matokeo yalitoka kinyume na ilivyotegemewa.Mimi kama mchunguzi kilichowaangusha wapinzani ni kukosa network ya mawakala wa dhati kama wale wa Tarime.Kipindi kile mchuano ulikuwa mkali kati ya Mwakagenda(CHADEMA) na Kisonga(NCCR-Mageuzi),lakini matokeo yakawa landslide victory kwa mgombea wa CCM akisaidiwa na nguvu ya EPA.
Ninachokijua mimi ni kwamba wananchi wa Mbeya wana permanent interest,wanataka miundo-mbinu kama vile International Airport,Tarmac road mbeya-chunya-itigi,Chuo Kikuu cha sayansi na Teknolojia n.k.Mbeya hawana chuki na mtu yeyote anayejali maslahi yao na wala hawawezi kulambishwa pipi ya kupewa vyeo kwa sababu vyeo hivyo vinakuwa kwa waliopewa sio mkoa wote.Hawapendi kuzugwa!
Nakubaliana na hoja zenu za umoja ni nguvu.Lakini katika umoja huo, tukubaliane kuwa wakati mwingine tupanue wigo wa uchaguzi wa sera badala ya personalities au itikadi za vyama.Najua watz wengi wapenda demokrasia mna hamu sana ya kuona opposition inaongeza idadi ya viti bungeni.Mimi kwa upande wangu napenda tuwafundishe na kuwazoesha wapiga kura kuchagua ubora wa sera na mgombea.Naunga mkono CHADEMA wagombee, ili sera zao zitambulike kwa wapiga kura wa Tanzania hiyo ndio nafasi pekee ya kujitangaza.Ninachotaka kushauri hapa si vizuri,incase mgombea wao hauziki waanze kumkandia mgombea wa chama kingine cha upinzani.
Tofauti ya uchaguzi wa Tarime vyama vingine vya upinzani vilikuwa vinaonyesha kukipiga vita vya wazi CHADEMA.Hali hiyo isirudiwe,chama kishiriki kueleza sera na mikakati yake ya kuboresha na kutetea walipa kodi wa Taifa letu.
Mkuu Gembe, si kweli kuwa sisi watu wa Mbeya tuna ukabila.Nitakupa mfano wa madiwani wawili wa kyela na nitaonyesha mabano ya kata wanazowakilisha.Kuna Visky Mahenge ambaye ni mkinga(Kyela) na Mh.Chrissy ambaye ni mkulya(Ipinda).Vilevile kule mbozi wenyeji wa wilaya ni Wanyiha na Wanyamwanga, lakini Mwenyekiti wa Council ni mnyakyusa.Huyu marehemu Nyaulawa,alikuwa mkinga ambao kule Mbeya vijijini ni wachache na walio wengi ni Wasafwa na Wamalila(kabila la Mboma).Huu mkoa wa Mbeya sasa hivi una wahamiaji wengi kutoka sehemu mbalimbali ya nchi yetu na nchi jirani na wanaishi vizuri na kushiriki kwenye chaguzi mbalimbali za uongozi.Nakumbuka hata uchaguzi mkuu wa 2005,NCCR-Mageuzi walimsimamisha Temigunga Kisonga(mhehe) na alivutia wapiga kura wengi licha ya kwamba matokeo yalitoka kinyume na ilivyotegemewa.Mimi kama mchunguzi kilichowaangusha wapinzani ni kukosa network ya mawakala wa dhati kama wale wa Tarime.Kipindi kile mchuano ulikuwa mkali kati ya Mwakagenda(CHADEMA) na Kisonga(NCCR-Mageuzi),lakini matokeo yakawa landslide victory kwa mgombea wa CCM akisaidiwa na nguvu ya EPA.
Ninachokijua mimi ni kwamba wananchi wa Mbeya wana permanent interest,wanataka miundo-mbinu kama vile International Airport,Tarmac road mbeya-chunya-itigi,Chuo Kikuu cha sayansi na Teknolojia n.k.Mbeya hawana chuki na mtu yeyote anayejali maslahi yao na wala hawawezi kulambishwa pipi ya kupewa vyeo kwa sababu vyeo hivyo vinakuwa kwa waliopewa sio mkoa wote.Hawapendi kuzugwa!