BULOLE BUKOMBE
JF-Expert Member
- Apr 7, 2011
- 488
- 109
Wana jf leo asubuhi kulikuwa na vurugu katika mji wa geita iliyosababishwa na wachimbaji wadogo waliokataa amri ya serikali kuondoka maeneo wanayochimba dhahabu na kuwaachia wawekezaji waliopewa eneo hilo katika vurugu hizo baadhi ya magari yamechomwa moto na mengine kuvunjwa vioo. Hali ilkuwaa mbaya zaidi pale mabomu ya machozi yalipokuwa yakipigwa pembeni kabisa uzio wa hospitali ya wilaya ya Geita kwani hofu ilitanda kwa wagonjwa lakini walitulizwa na wauguzi ambao wanaonekana kuizoaea hali hiyo, kuwa hiyo ni kelele tu haina madhara kwao moja kwa moja, kabla sijaondoka mjini hapo kuelekea Bukoba nilipata tetesi kuwa wachimbaji wawili wameuawa kwa kupigwa risasi na polisi.