Gazeti Uhuru-Siyoi hakuwa chaguo la CCM na wana-Arumeru!

C.C.M. Wanaugulia kipigo. Huyo Mhariri atakuwa ameagizwa na Nape kuandika hayo. Mkumbuke Nape hukupenda Siyoi apitishwe.
 
Kwa kweli kama kuna tahariri za uhuru ambazo ziliwahi kunishangaza ni ya toleo la leo jumanne

Mhariri ametoa tahariri ndefu na kuhitimisha kwa madai kuwa mgombea wa CCM hakuwa chaguo la CHAMA na wana arumeru na kwamba ndiyo sababu wameambulia nafasi ya pili.

kama gazeti la chama linaandika haya,tambua wao jikononi mambo yanakwenda ndivyo siyvo

Kinachokushangaza nini au ulevi tu wa ushindi,mbona hili liko wazi sana na tokea mwanzo lilisemwa kwamba jamaa hakua chaguo la wengi chamani na pia watu wa arumeru hawkupenda kurithiwa kama mali za marehemu mzee sumari.

SOMA HIYO HABARI HAPO CHINI BEFORE UCHAGUZI...


HALI ndani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Jimbo la Arumeru Mashariki, bado si swari baada ya mchakato wa kura za maoni kumpata mgombea wa chama hicho katika kinyang'anyiro cha ubunge kukamilika, Raia Mwema.
Ingawa mshindi katika kinyang'anyiro hicho amepatikana ambaye ni mtoto wa Mbunge aliyetangulia, marehemu Jeremiah Sumari, Sioi Sumari, wenzake wamelalamikia ushindi wake wakidai umetokana na matumizi ya fedha na si kukubalika kwake kisiasa wakionya kwamba, ameshinda ndani ya chama kwa nguvu ya fedha, lakini nje ya chama hicho, hali itakuwa ngumu kwake kushinda.

Katika hatua nyingine baadhi ya washindani wake wamedai kuwa hata kanuni za CCM hazijazingatiwa ambazo zinataka mshindi wa kura za maoni apate zaidi ya asilimia 50 ya kura zote lakini kwa upande wa Arumeru Mashariki, ameshinda kwa asilimia Kama mgombea huyo atapitishwa katika vikao vingine vya juu vya CCM ambavyo ni Kamati Kuu na Halmashauri Kuu (NEC) ya chama hicho 34.91, ambayo ni sawa na kura 361 (34.91).


Kijana huyo wa marehemu Sumari ambaye pia kwa sasa ni Mkwe wa Waziri Mkuu aliyejiuzulu kwa kashfa ya kampuni ya kufua umeme ya Richmond, ambaye pia ni Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa, alifuatiwa kwa idadi ya kura na William Sarakikya aliyepata kura 259 ambazo ni sawa na asilimia 25.


Wengine waliofuatia katika kinyang'anyiro hicho ndani ya CCM ni pamoja na Elirehema Kaaya aliyepata kura 205 sawa na asilimia 19.82; Elishilia Kaaya kura 176 sawa na asilimia 17.02, Antony Musani kura 22 sawa na asilimia 2.12 na Rashiankira Urio aliyeambulia kura 11 ambazo ni sawa na asilimia 1.06.


Kwa upande mwingine, wepesi wa kampeni za mgombea huyo wa CCM kama atapitishwa na vikao vya juu vya chama hicho utategemea zaidi na ushirikiano kutoka kwa washindani wake hao kwenye kinyang'anyiro hicho ambao baadhi wamesikika wakisema mwenzao huyo alitumia fedha kupata ushindi huo.


Uchaguzi wa Arumeru Mashariki utarajiwa kufanyika mapema Aprili, kuziba nafasi iliyoachwa wazi na Jeremiah Sumari, ambaye alifariki dunia kutokana na maradhi ya saratani yaliyokuwa yakimsumbua.


Wakati wa awamu ya kwanza ya ubunge wake, Sumari alipata kushika wadhifa wa Naibu Waziri hadi Serikali ya awali chini ya Waziri Mkuu, Lowassa, ilipovunjwa mwaka 2008 na kuundwa nyingine chini ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.
 
mzee una roho ngumu..kwani najiuliza umevutiwa na nini mpaka ununue gazeti la uhuru...mimi mara ya mwisho nimelisoma ilikuwa mwaka 1994
 
Gazeti la uhuru lipo chini ya wahariri MBUMBUMBU.
CHADEMA 4 LIFE
SOLIDARITY FOREVER
 
Wanasheria watusaidie, Sio anaweza kulishitaki gazeti za Uhuru kwa deformation?

Kama kuna kutokubaliana kati ya wajumbe wa CCM hilo ni tatizo la ndani lakini kwenye official level CC ya CCM ilimptisha Sioi. Sasa kwa mhariri wa UHURU kuharamisha maamuzi ya CC ambayo mwenyekiti wake ni Kikwete ni kituko. Hivi kama Sioi angeshinda Uhuru wangesema hakuwa chaguo la CCM?

Minyukano ya CCM inatia kinyaa!
Mkuu FJM hiki ni kituko cha mwaka. Sioi alipitishwa kwa kufuata taratibu zote za chama cha CCM,sasa gazeti la chama linapotoka na madai kama haya linataka kumhadaa nani? Hii ndiyo shida ya wana CCM kuiona nchi yetu ni yao tu. Na wao ndiyo wenye akili ya kufanya jambo lolote kwa nchi hii! Ndiyo maana wenye akili tumeishabaini kwamba CCM haitoachia madaraka kwa njia za kidemokrasia kwasababu haijui kushindwa ktk uchaguzi,itaondoka kwa nguvu ya umma!
 
Kikao halali cha chama kinatoa chaguo la chama, tena chini ya mwenyekiti wa chama. Wacheni kudhalilishana, Sababu sio mgombea, ila ni chama kupoteza mvuto kwa wananchi. Msitafute kondoo wa sadaka.

Leave them alone mkuu...Usitoe mbinu za ushindi kwa adui.
 
Kwani uhuru nalo gazeti au kijarida cha waganga njaa waliokosa ajira kwenye vyombo vya habari na kubaki kujikomba kwa CCM? Kama hakuwa chaguo la CCM kulikuwa na mantiki gani vigogo karibu wote akiwamo Mkapa kwenda Arumeru? Je Sioi alikuwa chaguo la nani kama siyo la CCM? La Lowassa, Mafisadi au wasanii na watukanaji?
 
Kampeni za Mvua njoo Katarina usije.. Ziishe sasa

Mnamo September 1928, kwenye kitongoji cha Leeward Mji mdogo Wa Puerto Rico, ndani ya mji wa Florida nchini Marekani ulikumbwa na upepo mkali ulioambatana na mvua kubwa uliojulikana kama hurricane Katrina. Kimbunga hicho kilileta vifo Na uharibifu wa Mali kiasi ambacho hakikuwahi kurekodiwa nchini humo. Basi serikali ya Marekani ikatishika Na kuwasihi watu wamuombe Mola kwamba Mvua Ije Lakini Katrina no... Na Msemo huo ukaenea sana. Wazee wetu wakashindwa kutafsiri neno Katrina badala yake wakasema Katarina.. Wakatenda mbali Na kupotosha uhalisia kwamba Katrina ni Katarina(Jina la Kike) Na kutukaririsha kwamba tuimbe mvua njoo katarina (Mke) usije wakimaanisha Bora mvua kuliko mwanamke.

Nadhani ndio Fikra za Chama Letu CCM, Kampeni Na sera za kuwarubuni wadanganyika ambao sasa wameshagundua Ni Katrina sio Katarina...
 
Back
Top Bottom