Nimekuwa muumini mkubwa wa gazeti la Raia Mwema kutokana na ukweli kwamba ni moja ya magazeti yanayoandika habari kwa weledi mkubwa.
Waandishi wa gazeti hili nimekuwa nikiwaona ni miongoni mwa waandishi wenye weledi mkubwa na wasioyumbishwa. Hata waandishi wa kujitegemea wanaotuma taarifa kwenye gazeti hili ni wa kutiliwa mfano.
Nimeanza kuwa na mashaka baada ya kufanya tathmini kwa muda wa miezi kama mitatu hivi kama bado baadhi ya waandishi wa gazeti hili wanatilia maanani kiapo chao cha uandishi.
Nakumbuka Katibu wa Itikadi na uenezi wa CCM, Nape Nnauye alitembelea vyombo karibu vyote vya habari na gazeti Raia mwema likiwa mojawapo. Tangu wakati huo nimekuwa siridhishwi na habari zinazoongoza kwenye gazeti hilo ukurasa wa mbele. Ni habari ambazo ni tofauti sana na zilivyokuwa zinaripotiwa mwanzo.
Wadau mtanisaidia lakini mwenye kufanya tathmini alinganishe habari zinazoongoza ukurasa wa mbele kwa muda niliotaja na jinsi ilivyokuwa inaripotiwa kabla.
Utafiti wangu umejionyesha dhahiri baada ya hekaheka za kampeni za Igunga kuanza.Gazeti hili likiripoti habari ya Igunga limekuwa likionyesha waziwazi kwamba CCM itashinda. Tafuta nakala ya wiki iliyopita.
Gazeti la leo limetoa taarifa kwamba Chadema na CUF watashindwa kwa sababu watagawana kura za upinzani,na habari hii imewekwa ukurasa wa mbele kwa makusudi na naamini imepangwa.
Sasa nikajiuliza kwanini gazeti hili liseme eti CUF na Chadema watagawana kura? Ina maana kura za kugawanyika ni za CUF na Chadema tu?
Ningependa kuwashauri wahariri wa gazeti hili watambue kwamba imani kubwa wananchi waliyokuwa wanaonyesha kwa gazeti hili inaanza kufifia na hakika mimi ni miongoni mwa watu watakaokuwa wanafikiri mara mbilimbili wakati wa kununua gazeti hili.
Nawasilisha.
Waandishi wa gazeti hili nimekuwa nikiwaona ni miongoni mwa waandishi wenye weledi mkubwa na wasioyumbishwa. Hata waandishi wa kujitegemea wanaotuma taarifa kwenye gazeti hili ni wa kutiliwa mfano.
Nimeanza kuwa na mashaka baada ya kufanya tathmini kwa muda wa miezi kama mitatu hivi kama bado baadhi ya waandishi wa gazeti hili wanatilia maanani kiapo chao cha uandishi.
Nakumbuka Katibu wa Itikadi na uenezi wa CCM, Nape Nnauye alitembelea vyombo karibu vyote vya habari na gazeti Raia mwema likiwa mojawapo. Tangu wakati huo nimekuwa siridhishwi na habari zinazoongoza kwenye gazeti hilo ukurasa wa mbele. Ni habari ambazo ni tofauti sana na zilivyokuwa zinaripotiwa mwanzo.
Wadau mtanisaidia lakini mwenye kufanya tathmini alinganishe habari zinazoongoza ukurasa wa mbele kwa muda niliotaja na jinsi ilivyokuwa inaripotiwa kabla.
Utafiti wangu umejionyesha dhahiri baada ya hekaheka za kampeni za Igunga kuanza.Gazeti hili likiripoti habari ya Igunga limekuwa likionyesha waziwazi kwamba CCM itashinda. Tafuta nakala ya wiki iliyopita.
Gazeti la leo limetoa taarifa kwamba Chadema na CUF watashindwa kwa sababu watagawana kura za upinzani,na habari hii imewekwa ukurasa wa mbele kwa makusudi na naamini imepangwa.
Sasa nikajiuliza kwanini gazeti hili liseme eti CUF na Chadema watagawana kura? Ina maana kura za kugawanyika ni za CUF na Chadema tu?
Ningependa kuwashauri wahariri wa gazeti hili watambue kwamba imani kubwa wananchi waliyokuwa wanaonyesha kwa gazeti hili inaanza kufifia na hakika mimi ni miongoni mwa watu watakaokuwa wanafikiri mara mbilimbili wakati wa kununua gazeti hili.
Nawasilisha.