Losambo
JF-Expert Member
- Nov 8, 2011
- 2,612
- 864
ccm
Kuzaliwa 1977
Kufa 2015
Duuuuh kweli unamaono ya mbali sana.
ccm
Kuzaliwa 1977
Kufa 2015
​r.i.p chichiemccm
kuzaliwa 1977
kufa 2015
ukifikiri kwa kina utagundua hili gazeti la ccm linataka kukuza mgogoro,read between the lines you will realize this
Gazeti la RAI linalomilikiwa na Habari Cooperation limefichua njama kubwa zilizoandaliwa na Chama cha Mapinduzi dhidi ya Chama kikuu cha upinzani Tanzania CDM.Gazeti hilo toleo la leo alhamisi limedai mkakati huo kabambe uliosukwa kwa muda mrefu na kwa ustadi mkubwa tayari umeiva na hatua ya kwanza imeanza kwa kuwatumia baadhi ya makada walioko ndani ya CDM ambao ni mbunge wa Maswa Mashariki John Shibuda na Makamu Mwenyekiti wa Baraza la Vijana CDM-BAVICHA Bi Juliana Shonza.Gazeti hilo limezidi kudai kwamba mkakati wa CCM ni kuhakikisha inawatumia makada hao kuisambaratisha CDM.
Ku-deal na Shibuda ni rahisi sana, viongozi wa CHADEMA hawatakiwi kuumiza kichwa. Dawa yake ni kum-ignore.
Viongozi wa CHADEMA wakianza kujibizana na Shibuda atawatoa kwenye hoja za msingi na hivyo kupoteza focus ya 2015.
Hizo ndio gharama za zoa zoa, maana wakati mwingine unaweza kuzoa hata nyoka ukidhani umenasa samaki!
Gazeti la RAI linalomilikiwa na Habari Cooperation limefichua njama kubwa zilizoandaliwa na Chama cha Mapinduzi dhidi ya Chama kikuu cha upinzani Tanzania CDM.Gazeti hilo toleo la leo alhamisi limedai mkakati huo kabambe uliosukwa kwa muda mrefu na kwa ustadi mkubwa tayari umeiva na hatua ya kwanza imeanza kwa kuwatumia baadhi ya makada walioko ndani ya CDM ambao ni mbunge wa Maswa Mashariki John Shibuda na Makamu Mwenyekiti wa Baraza la Vijana CDM-BAVICHA Bi Juliana Shonza.Gazeti hilo limezidi kudai kwamba mkakati wa CCM ni kuhakikisha inawatumia makada hao kuisambaratisha CDM.
CCM inadhihirisha ni kiasi gani imezeeka na kwamba inashindwa ku-focus kwenye mambo ya msingi yanayolikabili taifa kwa sasa na kupeleka nguvu zake nyingi kuwaza na kujipanga namna ya kuendelea kutawala. Ni viongozi wenye mawazo MGANDO kama akina Nape na Wassira ndio ambao wanaona kuwa CHADEMA ni tatizo kwa ccm kuendelea kutawala nchi hii. Lakini kwa sisi ambao tunafahamu mambo yanavyokwenda, tunaamini kuwa tatizo kubwa na ambalo linaingusha sisiem, siyo Chadema, Ni ccm yenyewe kushindwa kutatua matatizo ya MSINGI ya wananchi kama, KUPAA KWA B
Watapanga mipango yote, lakini mwisho wa siku watashindwa kwa sababu kuibomoa CHADEMA, hakurudishi imani ya wananchi kwa CCM, ila kuongeza chuki dhidi ya viongozi wake. Kuiongea CHADEMA kila siku, ni kuingezea umaarufu na kuifanya izidi kupendwa zaidi. Hata mwalimu alisema, CCM HAIKUMZAA, na wala ccm haijamzaa Mtanzania yoyote yule...! Kama bado wanatumia mbinu za 1947 katika dhama hizi za sayansi na teknolojia, ni aibu.
Washauri na viongozi wakuu wa ccm wameishia, hawana maono tena, hawana dira wala mwelekeo kama chama chenyewe. Yaani akili zao zimezeeka kama chama chenyewe. Mwalimu aliwaambia, "wananchi wataendelea kuichagua ccm na mabaya yake, kama hakutakuwa na chama kingine cha upinzani ambacho kinaweza kutatua matatizo yao!!!" Sasa hivi kuna mbadala, kama ccm ina mpango wa kuua upinzani Tanzania, Watanzania tutakuwa tayari kuongozwa na jeshi, kuliko kuicha ccm madarakani kwa miaka mingine mitano, ni kifo chetu na vizazi vyetu.
Lakini, kikubwa na kizuri, ccm wamechoka kufikiri na akili zao zimedumaa, nashukuru kuwa tumeanza kuzifahamu mbinu zao mapema, hii ni katikati ya 2012, bado tuna miaka karibu mitatu na nusu kufika uchaguzi 2015, tunajipanga zaidi kukabiliana na mbinu zao, na tunazidi kutangaza sera zetu kwa wananchi hadi vijijini. Kasi hii ya elimu kwa umma ikiendelea hadi 2015, hakuna ubishi kuwa ccm haitashinda uchaguzi wowote ule ki halali, na ni imani yangu kuwa, hata polisi na wanajeshi watatuunga mkono, kwani ni askari wachache sana ambao wananufaika na uongozi wa ccm, wengi ni walalahoi tu kama waalimu, madaktari na watumishi wengine wa umma, tatizo ni kwamba wao hawawezi kugoma.
STK ONE,
TOGETHER WE CAN BRING THE CHANGES WE NEED.....YES WE CAN, GOD BLESS CDM!!!!
[/SIZE yanayofanywa yote na ccm kwa cdm ni kukikomaza chama
ccm
Kuzaliwa 1977
Kufa 2015