Gazeti la RAI linalomilikiwa na Habari Cooperation limefichua njama kubwa zilizoandaliwa na Chama cha Mapinduzi dhidi ya Chama kikuu cha upinzani Tanzania CDM.Gazeti hilo toleo la leo alhamisi limedai mkakati huo kabambe uliosukwa kwa muda mrefu na kwa ustadi mkubwa tayari umeiva na hatua ya kwanza imeanza kwa kuwatumia baadhi ya makada walioko ndani ya CDM ambao ni mbunge wa Maswa Mashariki John Shibuda na Makamu Mwenyekiti wa Baraza la Vijana CDM-BAVICHA Bi Juliana Shonza.Gazeti hilo limezidi kudai kwamba mkakati wa CCM ni kuhakikisha inawatumia makada hao kuisambaratisha CDM.