Kichwa Ngumu
JF-Expert Member
- Nov 6, 2010
- 1,726
- 312
PAYE inalipwa na mwajiri ila anakata kwenye mshahara wa mtumishi wakeSijaelewa hapa. Wana JF naomba mnieleweshe. Yaani hajalipa kodi tangia mwaka 1992, wakati yeye amejiunga na CHADEMA 1995, na amekuja kuwa katibu mkuu baadaye sana. Au wanamaanisha mshahara wake wa tangu November mwaka jana alipogombea urais? Lakini pia, hivi kati ya mwajiri na mwajiliwa, je ni nani anayetakiwa kubanwa kuhusu kama mwajiriwa analipa kodi au la? Kwa mfano, mimi huwa nakatwa kodi, lakini sijawahi kwenda TRA kubisha hodi ili nilipe kodi, huwa inakatwa automatically tu kabla hata mimi sijaugusa mshara wangu. Au wanamaanisha CHADEMA kama chama ndo hailipi kodi? Na kama ndio hilo wao TRA wanawajibikaje kwa kutokusanya kodi tangia mwaka 1992 kwene chama ambacho kina usajili na kinafanya kazi kila siku? Na je hali ikoje vyama vingine vya siasa?
Dr. mpaka mwaka karibu mwishoni mwa 2010 alikuwa mbunge kama hakalipa sio kosa lake ni kosa la utendaji mbovu wa Serikali
Mimi ninapiki piki yangu inafanyakazi ya boda boda mpaka mwishoni mwa Machi inabidi uwe umelipa mapato fail to do that Aprili piki piki itakamatwa utalipa TZS 65,000 ( 35,000 mapato, 20,000 fine na 10,000 gharama za kukushika) kwa ninin hawakufanya hinyo kwa CDM? waanze wao kuwajibishwa kabla ya CDM.