Mikael Aweda
JF-Expert Member
- Dec 17, 2010
- 2,973
- 3,901
Wakuu, gazeti la raia mwema la leo limeujadili ktk ukurasa wa pili hali ya kisiasa ya mwaka 2011 na kusema kuwa ulikuwa ni mwaka wa kisiasa zaidi kutokana na matukio kadhaa yaliyoorodheshwa ambayo ni katiba mpya, Sakata la Arusha, Wabunge wa chadema kususia hotuba ya Rais, maandamano ya chadema nk. Matukio yote yalimweka DR Slaa kuwa ktk ya matukio hayo hasa suala la katiba mpya ambalo ni agenda ya chadema na ilipata msukumo kutokana na Dr Slaa kudai kuibiwa kura na kususia kuhudhuria kuapishwa kwa Rais Kikwete. Likaja sakata la wabunge wa chadema kudai katiba mpya nje na ndani ya Bunge.
Gazeti limewaorodhesha viongozi wengi wa kisisasa wa vyama vya ccm, Chadema na CUF Kila mmoja kwa jinsi alivyopanda au kushuka kisiasa. Lipumba na Maalim wanaonekana kushuka Hamad Rashid akionekana kuja juu zaidi. Kwa upande wa Chadema wengi kwa kuwa ndio wanachipukia wameonekana kupanda zaidi.
Lakini kubwa kuliko zote ni pale gazeti linaposema, ninanukuu;
KATIBU MKUU WA CHADEMA DR W Slaa amezidi kungara kwa umaarufu wa kisiasa pengine kuliko wanasiasa wengine ndani ya Chadema , huku akionekana kuwa kiongozi wa kitaifa zaidi, na baadhi ya watu waliamini kuwa kuanguka kwake kisiasa (urais 2010) kungeweza kuwa ni ishara ya chadema kupoteza umaarufu.
Viongozi wengine waliofanya vizuri ni kila mmoja ktk nafasi yake Mbowe, Lisu, Zitto, nk
My take; Hayo ni maoni ya gazeti niliyoya paraphrase naomba maoni yenu
Gazeti limewaorodhesha viongozi wengi wa kisisasa wa vyama vya ccm, Chadema na CUF Kila mmoja kwa jinsi alivyopanda au kushuka kisiasa. Lipumba na Maalim wanaonekana kushuka Hamad Rashid akionekana kuja juu zaidi. Kwa upande wa Chadema wengi kwa kuwa ndio wanachipukia wameonekana kupanda zaidi.
Lakini kubwa kuliko zote ni pale gazeti linaposema, ninanukuu;
KATIBU MKUU WA CHADEMA DR W Slaa amezidi kungara kwa umaarufu wa kisiasa pengine kuliko wanasiasa wengine ndani ya Chadema , huku akionekana kuwa kiongozi wa kitaifa zaidi, na baadhi ya watu waliamini kuwa kuanguka kwake kisiasa (urais 2010) kungeweza kuwa ni ishara ya chadema kupoteza umaarufu.
Viongozi wengine waliofanya vizuri ni kila mmoja ktk nafasi yake Mbowe, Lisu, Zitto, nk
My take; Hayo ni maoni ya gazeti niliyoya paraphrase naomba maoni yenu